Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

SURA YA KUMI NA SITA


Giza lilikuwa limekwisha ingia siku ya tatu tulipofika mahali pa kupiga kambi chini ya ‘Vichawi Vitatu’ yaani ile milima mitatu iliyokuwa mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani.

Katika safari yetu tulikuwa sisi watatu, na Foulata, na Infadus, na Gagula aliyechukuliwa katika machela, ambaye daima tulimsikia akitukana na kuguna, na askari wachache pamoja na viongozi na watumishi.

Siwezi kusahau milima ile namna ilivyokuwa katika mwangaza wa jua la asubuhi; ilikwenda juu sana hata kufika mawinguni.


Tulipotazama juu tuliona Njia Kuu ya Sulemani inakwenda moja kwa moja mpaka kilele cha katikati, mwendo wa kiasi cha saa mbili.


Afadhali nisijaribu kueleza mambo tuliyokutana nayo katika safari hii, msomaji na akisie mwenyewe.

Lakini sasa tunakaribia mashimo yale ya ajabu ambayo ndiyo sababu aliyofia Yule mzee Mreno zama za miaka mia tatu nyuma, na tena Yule mjukuu wake aliyekuwa rafiki yangu, na tena, labda hata na ndugu yake Bwana Henry.


Je, ajali yetu itakuwa ya namna hiyo hiyo? Wao walipatwa na maovu kama alivyosema Yule kichawi Gagula; na sisi je? Tulipokuwa tukienda katika ile njia nzuri sikuweza kujizuia nisiwe na hofu. Na tena nadhani Bwana Good na Bwana Henry vile vile walikuwa na hofu.


Kwa muda wa saa moja na nusu tulikwenda kwa miguu upesi upesi tukivutwa na tamaa, hata wale waliochukua machela waliona shida kufuatana nasi, na Gagula akatoa kichwa chake katika machela akasema, ‘Nendeni pole pole nyinyi watu weupe, nyinyi mtafutao hazina, mbona mnakwenda mbio kuonana na maovu ?’

Akacheka kicheko cha uhabithi kilichochukiza sana na kufanya mwili kunisisimka, na kwa muda kidogo tulipunguza mwendo wetu.


Basi tuliendelea kwenda mpaka tuliona shimo kubwa lililokwenda chini sana mbele yetu, katikati ya mahali tulipo na kile kilele. Nikamuuliza Bwana Henry, ‘Je, unajua shimo hili ni la nini?’

Yeye na Bwana Good wakatikisa vichwa vyao. Nikawaambia, ‘Ni dhahiri kuwa hamjapata kuona mahali panapochimbwa almasi.


Nadhani shimo hili ni shimo la kuchimba almasi.’
Basi tulifuata njia ili tupate kutazama vitu vitatu tulivyoona kutoka mbali kidogo, na tulipokaribia tuliona kuwa ni Wale Watatu Walio Kimya, wanaoogopwa na Wakukuana. Lakini hatukutambua vema ukubwa wao mpaka tulipofika karibu kabisa.


Hapo tuliona masanamu matatu, na baina ya kila sanamu na mwenzake ilikuwa nafasi ya hatua ishirini, na wote wanatazama uwanda wa Loo. Masanamu mawili yalikuwa ya wanaume na lile la tatu lilikuwa la mwanamke.


Basi tulisimama tukatazama sana masanamu yale, na baadaye kidogo Infadus akatujia, akainua mkuki wake kuyaamkia yale masanamu, akatuuliza kama tunataka kuingia Mahali pa Mauti sasa hivi, au tutangoja mpaka kwisha chakula cha mchana.
 
Ikiwa tunataka kwenda sasa hivi, basi Gagula yu tayari kutuongoza.

Kwa kuwa ilikuwa saa tano tu, nasi tulikuwa na hamu sana kupatazama mahali penyewe, tulisema kwamba tunataka kwenda sasa hivi, nami nikatoa shauri kama afadhali tuchukue chakula pamoja nasi, maana labda tutakawia katika mahali penyewe.
Basi machela ya Gagula ikaletwa, akatoka ndani.


Huko nyuma Foulata aliweka nyama na vibuyu viwili vya maji katika kikapu. Gagula alipotoka katika machela akacheka na akajikongoja kushika njia. Sisi tulimfuata, mpaka kwenye mlango wa pango.


Hapo Gagula akasimama akatungojea, na hata hivi sasa akicheka kicheko cha uhabithi. Akasema, ‘Sasa watu weupe waliotoka katika nyota, mashujaa wenye busara, mtayari?


Tazama mimi nipo hapa kufanya aliyoniamuru bwana wangu mfalme, yaani kuwaonyesheni hazina na mawe meupe yanayong’aa.Ha!Ha!Ha!’
Nikajibu, ‘Sisi tu tayari.’


Akasema, ‘Vema! Vema! Jipeni moyo mpate kuvumilia mtakayo yaona. Nawe Infadus, utakuja, wewe uliye mhaini bwana wako?’


Infadus akakunja uso kwa hasira, akajibu, ‘La, mimi siji, hayanihusu. Lakini wewe, Gagula, utawale ulimi wako, wangalie pia mabwana zangu.


Mimi ninawatia katika mikono yako, na ukiudhuru hata unywele mmoja, wewe Gagula, utakufa, hata ukiwa mchawi wa namna gani! Umisikia?’


Gagula akajibu, ‘Nasikia Infadus. Lakini usiogope, mimi maisha nafuata amri za mfalme tu. Mimi nimefuata amri za wafalme wengi Infadus, lakini mwisho wao walifuata amri zangu mimi.

Ha!Ha! Nakwenda kutazama nyuso zao mara moja tena, na vile vile nitatazama uso wa Twala. Haya twendeni, twendeni.’


Akachukua kibuyu cha mafuta akatia utambi kama taa. Bwana Good akamuuliza Foulata, ‘Unakuja, Foulata?’ Akajibu, ‘Naogopa, bwana wangu.’ Akasema, ‘Basi nipe kikapu.’

Akajibu, ‘La, bwana wangu, uendako nami nitakwenda.’ Basi Gagula hakungoja zaidi, akaingia katika ule mlango, tukaona kuwa ni kinjia cha kutosha watu wawili kwenda pamoja, tena giza tupu.

Tukamfuata Gagula huku tukiogopa na kutetemeka; tukasikia kishindo cha mbawa, na mara Bwana Good akauliza, ‘Je, nini kile, kitu kimenipiga usoni?’ Nikasema, ‘Haya twendeni, alikuwa ni popo tu.’


Basi tukaenda mbele na tulipokuwa tumekwisha kwenda kadiri ya hatua hamsini tuliona kuwa giza linapungua, na halafu tukajiona katika mahali pa ajabu.
 
Tumo katika pango kubwa lililo kwenda juu sana, hata kwa juu lilikuwa kadiri ya hatua mia moja. Kutoka pango hilo mapango madogo yaliingia katika mlima.

Basi tulitaka kutazama kila mahali, lakini Gagula hakutupa nafasi, yeye alikwenda mbele mpaka mwisho wa pango kubwa, tukamfuata.

Tulipofika huko tuliona mlango mwingine na Gagula akatugeukia akauliza, ‘Mko tayari kuingia katika Mahali pa Mauti?’

Tukajibu, ‘Haya tu tayari.’
Bwana Henry akasema, Mambo yanaanza kutisha sasa.’ Basi wakanipa nafasi mimi nitangulie, lakini katika roho yangu niliogopa, mpaka Bwana Good aliposema, ‘Haya, twende rafiki, au kiongozi wetu mzuri atatupoteza.’


Basi kuambiwa haya, nikaanza kuingia katika kinjia, na baada ya hatua ishirini hivi, nilijiona katika pango lingine.

Lilikuwa giza kidogo, lakini nilipozoea giza niliona meza ndefu na mwisho wa meza sanamu jeupe kubwa imekaa, na kuzunguka meza masanamu meupe mengine yenye kimo cha mtu.

Tena nikaona katikati sanamu jingine jeusi kidogo, na macho yangu yalipozoea giza nilitambua masanamu yale ni nini, nikageuka nikakimbia kutoka pango lile kadiri nilivyoweza kwenda mbio.


Kwa kawaida mimi siyo muoga sana, wala siogopi mambo ya kishetani, lakini nakiri kuwa niliyoyaona yalinitisha sana, na Bwana Henry asingalinizuia ningetoka pangoni upesi, na nisingekubali kuingia tena, hata kwa almasi zote zilizopo duniani.


Lakini Bwana Henry alinikamata baraabara, na kwa hivyo nilisimama, Lakini, mara na yeye macho yake yalizoea giza na yeye aliona yale niliyoyaona mimi, mara akaniacha akaanza kujifuta jasho usoni.


Bwana Good akashangaa kabisa, na Foulata akamkumbatia huku akilia tu. Gagula tu ndiye aliyecheka sana.

Mambo tuliyoyaona yakawa ya kutisha mno. Maana mwisho wa meza ile ndefu tuliona mifupa ya mtu mrefu sana, urefu wa futi kumi na tano au zaidi, naye ameshika mkuki mkononi, akawa kama sanamu za hayo Mauti yenyewe.

Nikasema, ‘Je, hi! Ni nini?’ Na Bwana Good akaonyesha wale waliokuwa wamekaa mezani akasema, ‘Na hawa ni nani?’


Na Bwana Henry akaonyesha Yule mweusi kidogo akauliza, ‘Na huyu ni nani?’
Gagula akacheka, ‘Hee!Hee!Hee! Maovu yanawajia wote waingiao Mahali pa Mauti. Hee! Hee!Hee!Ha!Ha! Njoo Ndovu, wewe uliye shujaa katika vita, njoo mtazame Yule uliyemuua.’


Na kizee huyu akamshika kwa vidole vyake vyembamba akamwongoza kwenye meza. Sisi tukafuata. Alipofika akasimama akamwonyesha Yule mweusi kidogo, Bwana Henry akastuka akarudi nyuma.

Maana pale mezani maiti yaTwala ilikuwepo, mfalme wa hivi karibuni wa Wakukuana, alikaa na kichwa chake amekipakata.

Na maiti huyo alifunikwa chumvi; tukasikia matone ya maji yakidondoka, tukafahamu kuwa maiti ya Twala inageuzwa kuwa jiwe, yaani kwa dawa iliyomo katika yale maji yanyodondoka.


Tukatazama masanamu yale mengine na tukafahamu Maiti za wafalme wa zamani zimekaa kuzunguka meza, na maiti ya mfalme Twala imekaa juu ya meza imepakata kuwa wale ni maiti wafalme wa zamani, na sasa wamekwisha geuka kuwa masanamu ya mawe kwa ile dawa.

Tukahesabu masanamu ishirini na saba, na ile ya mwisho ilikuwa sanamu ya baba yake Ignosi, na kila moja limegeuka jiwe.

Tukaona kuwa desturi hii ya kuweka maiti za wafalme hapa ni ya zamani sana. Lakini sanamu ile kubwa iliokaa mwisho wa meza tuliona kuwa ni kazi ya mikono ya watu wale waliochonga Wale Watatu Walio Kimya.
 
Tumo katika pango kubwa lililo kwenda juu sana, hata kwa juu lilikuwa kadiri ya hatua mia moja. Kutoka pango hilo mapango madogo yaliingia katika mlima.

Basi tulitaka kutazama kila mahali, lakini Gagula hakutupa nafasi, yeye alikwenda mbele mpaka mwisho wa pango kubwa, tukamfuata.

Tulipofika huko tuliona mlango mwingine na Gagula akatugeukia akauliza, ‘Mko tayari kuingia katika Mahali pa Mauti?’

Tukajibu, ‘Haya tu tayari.’
Bwana Henry akasema, Mambo yanaanza kutisha sasa.’ Basi wakanipa nafasi mimi nitangulie, lakini katika roho yangu niliogopa, mpaka Bwana Good aliposema, ‘Haya, twende rafiki, au kiongozi wetu mzuri atatupoteza.’


Basi kuambiwa haya, nikaanza kuingia katika kinjia, na baada ya hatua ishirini hivi, nilijiona katika pango lingine.

Lilikuwa giza kidogo, lakini nilipozoea giza niliona meza ndefu na mwisho wa meza sanamu jeupe kubwa imekaa, na kuzunguka meza masanamu meupe mengine yenye kimo cha mtu.

Tena nikaona katikati sanamu jingine jeusi kidogo, na macho yangu yalipozoea giza nilitambua masanamu yale ni nini, nikageuka nikakimbia kutoka pango lile kadiri nilivyoweza kwenda mbio.


Kwa kawaida mimi siyo muoga sana, wala siogopi mambo ya kishetani, lakini nakiri kuwa niliyoyaona yalinitisha sana, na Bwana Henry asingalinizuia ningetoka pangoni upesi, na nisingekubali kuingia tena, hata kwa almasi zote zilizopo duniani.


Lakini Bwana Henry alinikamata baraabara, na kwa hivyo nilisimama, Lakini, mara na yeye macho yake yalizoea giza na yeye aliona yale niliyoyaona mimi, mara akaniacha akaanza kujifuta jasho usoni.


Bwana Good akashangaa kabisa, na Foulata akamkumbatia huku akilia tu. Gagula tu ndiye aliyecheka sana.

Mambo tuliyoyaona yakawa ya kutisha mno. Maana mwisho wa meza ile ndefu tuliona mifupa ya mtu mrefu sana, urefu wa futi kumi na tano au zaidi, naye ameshika mkuki mkononi, akawa kama sanamu za hayo Mauti yenyewe.

Nikasema, ‘Je, hi! Ni nini?’ Na Bwana Good akaonyesha wale waliokuwa wamekaa mezani akasema, ‘Na hawa ni nani?’


Na Bwana Henry akaonyesha Yule mweusi kidogo akauliza, ‘Na huyu ni nani?’
Gagula akacheka, ‘Hee!Hee!Hee! Maovu yanawajia wote waingiao Mahali pa Mauti. Hee! Hee!Hee!Ha!Ha! Njoo Ndovu, wewe uliye shujaa katika vita, njoo mtazame Yule uliyemuua.’


Na kizee huyu akamshika kwa vidole vyake vyembamba akamwongoza kwenye meza. Sisi tukafuata. Alipofika akasimama akamwonyesha Yule mweusi kidogo, Bwana Henry akastuka akarudi nyuma.

Maana pale mezani maiti yaTwala ilikuwepo, mfalme wa hivi karibuni wa Wakukuana, alikaa na kichwa chake amekipakata.

Na maiti huyo alifunikwa chumvi; tukasikia matone ya maji yakidondoka, tukafahamu kuwa maiti ya Twala inageuzwa kuwa jiwe, yaani kwa dawa iliyomo katika yale maji yanyodondoka.


Tukatazama masanamu yale mengine na tukafahamu Maiti za wafalme wa zamani zimekaa kuzunguka meza, na maiti ya mfalme Twala imekaa juu ya meza imepakata kuwa wale ni maiti wafalme wa zamani, na sasa wamekwisha geuka kuwa masanamu ya mawe kwa ile dawa.

Tukahesabu masanamu ishirini na saba, na ile ya mwisho ilikuwa sanamu ya baba yake Ignosi, na kila moja limegeuka jiwe.

Tukaona kuwa desturi hii ya kuweka maiti za wafalme hapa ni ya zamani sana. Lakini sanamu ile kubwa iliokaa mwisho wa meza tuliona kuwa ni kazi ya mikono ya watu wale waliochonga Wale Watatu Walio Kimya.
Umetisha Mkuu... Umetisha sana
 
Lakini niliona kuwa siha zake kwa Bwana Henry zilikithiri, baadaye tulikuja kujua kuwa askari hawakumfananisha Bwana Henry na mwanadamu wa kawaida.

Walisema kuwa hapana mwanadamu aliyeweza kupigana na Twala kama yeye alivyopigana naye, na hasa baada ya siku ya vita kama vile, maana Twala alisifiwa kuwa si mfalme tu lakini ni askari shujaa kupita wote.

Na pigo lile alilompiga hata kumkata kichwa likawa kama methali, yaani pigo lolote lililozidi nguvu likiitwa, Pigo la Ndovu.


Infadus akatuarifu kuwa askari wote wa Twala wamejiweka chini ya amri ya Ignosi, na wale waliokaa mbali wanafika sasa kujitoa. Kufa kwake Twala kwa mkono wa Bwana Henry kumemaliza kabisa vita katika nchi, maana Skraga aliyekua mrithi hata yeye amekufa.


Baadaye Ignosi akaja kutuamkia amevaa ile almasi ya kifalme juu ya kipaji cha uso. Nikamtazama alipokuwa akija, nikajaribu kumfananisha na Yule aliyekuja kwetu, akiomba tumpe kazi miezi michache nyuma.


Basi alipokaribia nikanyanyuka nikasema, ‘Hujambo, Ewe mfalme!’
Akajibu, ‘Sijambo, Makumazahn, mimi ni mfalme kwa nguvu za mikono yenu.’ Akatuarifu kuwa mambo yote yanaendelea vizuri, naye alitumaini kufanya karamu baada ya juma mbili apate kuonekana mbele ya watu wake.


Nikamuuliza atamfanya nini Yule Gagula, akajibu, ‘Yeye ni kama waziri mwovu katika nchi, na lazima nimuue, pamoja na wachawi wote.


Ameishi sana duniani, hata hapana anayejua miaka mingapi, naye ndiye aliyewafundisha wachawi wote na kufanya nchi iwe mbaya mbele ya Mungu.’
Nikajibu, ‘Kweli, lakini anayo maarifa mengi, na ni rahisi kuharibu maarifa kuliko ‘kuyapata!’


Akajibu, ‘Kweli, ni yeye peke yake ajuaye siri ya Wale Watatu Walio Kimya, na palipozikwa wafalme.’ Nikasema, ‘Ndiyo, na usisahau kuwa almasi zipo. Usisahau, Ignosi, yale uliyoahidi kuwa utatuongoza mpaka mashimo ya almasi, hata kama itakulazimu umwache Gagula aishi.’ Akajibu, ‘Mimi siwezi kusahau, Makumazahn, nami nita yafikiri maneno uliyosema.’


Ignosi alipoondoka nilikwenda kumtazama Bwana Good, nikamkuta ameshikwa na homa kali sana. Kwa siku mbili tulifikiri kuwa lazima atakufa, tukawa na mioyo mizito sana, lakini Foulata hakukubali, akasema kuwa lazima atapona.


Usiku wa tano wa ugonjwa wake nilikwenda kumtazama usiku kabla ya kwenda kulala, nikaingia chumbani pole pole sana, na kwa mwangaza wa taa nilimwona Bwana Good, lakini hakuwa akigaagaa kama siku zote, alilala kimya kabisa. Basi nilifikiri huu ndio mwisho, na nilikaribia kulia kwa uchungu.


Mara nilisikia sauti, ‘Sh! Sh!’ Nikatambua nikaenda karibu nikaona kuwa amelala usingizi wala hakufa, Alilala hivyo kwa muda wa saa kumi na nane, na wakati huo wote ameshika mkono wa Foulata, naye hakuweza kuondoka kwa sababu aliogopa atamwamsha.

Akakaa hivi bila kujinyosha na bila kula; lakini kwa kweli alipoamka ikawa lazima kumchukua, maana hakuweza kwenda kwa sababu viungo vyake vilikufa ganzi.
Bwana Good alilala masaa 18 [emoji23] [emoji23] [emoji23], noma ssna Makumazahn
 
Baada ya hivi, hakukawia kupona, lakini Bwana Henry hakumwambia habari za vitendo vya Foulata mpaka alipokuwa karibu ya kupona. Bwana Good akasema, ‘Mwambie kuwa ameniokoa, nami sitasahau kabisa wema wake.’


Nikamwambia Foulata maneno aliyosema Bwana Good na Foulata akafurahi sana, akamtazama kwa macho ya mapenzi akasema, ‘Sivyo, bwana, labda bwana wangu amesahau kuwa yeye ndiye aliyeokoa maisha yangu, na mimi ni kijakazi wa Bwana.’


Baada ya siku chache Ignosi akafanya baraza kuu akakubaliwa na wakubwa wote wa nchi. Ikawa sherehe kubwa sana, na askari wale waliobaki katika jeshi lile la Wajivu waliwekwa mbele wakapewa shukrani za mfalme kwa kazi nzuri na ushujaa waliofanya katika vita.

Kila mtu alipewa zawadi ya ng’ombe na wote wakapandishwa kuwa wakubwa katika jeshi jipya ambalo vile vile liliitwa kwa jina la Wajivu.


Tena Ignosi alithibitisha maneno yale aliyotuahidi, mbele ya watu wote, yaani, watu hawatauawa tena bila ya kuhukumiwa, naya kuwa desturi ile ya kuwafichua wachawi itakoma mara moja.


Baraza ilipovunjika tulimsuburi Ignosi tukamwambia kuwa sasa tuna hamu ya kuzifichua siri zile za Mashimo yale ya Sulemani ambayo yalikuwepo mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani; tukamuuliza kama amekwisha pata habari yoyote, akajibu, ‘Rafiki zangu, nimepata habari kuwa ni pale wanapokaa Wale Watatu Walio Kimya, ambao Twala alitaka kumuua Foulata awe ndiye mhanga wao.


Tena ni pale katika shimo kubwa wafalme wanapozikwa; ndipo mtakapoona maiti ya Twala amekaa pamoja na wale waliomtangulia. Na hapo lipo shimo lililokwenda chini sana lililochimbuliwa na watu wa zamani sana, labda kwa makusudio ya kutafuta mawe ya thamani uliyotaja.


Hapo ndipo Mahali pa Mauti, na humo kuna chumba ambacho hakijulikani. Ila na mfalme na Gagula. Twala alikijua lakini sasa amekufa, nami sikijui, wala sijui nini kilichomo.

Lakini imesimuliwa kuwa zamani mtu mweupe alivuka milima, akaongozwa na mwanamke mmoja, akaonyeshwa chumba kile cha siri, akaonyeshwa hazina.


Lakini kabla hawajaweza kuzichukua, akampitia kinyume na kuwaambia adui zake, akafukuzwa na mfalme wa wakati ule, na tangu siku ile hapana mtu aliyeingia katika mahali hapo.’


Nikasema, ‘Hadithi hiyo ni ya kweli Ignosi, maana tuliona maiti ya huyo mtu katika milima.’ Akajibu, ‘Ndiyo, tulimwona, na sasa nimeahidi kuwa kama mnaweza kukifikia chumba hicho, mna ruhusa kuchukua mawe yale ikiwa yapo.’

Nikasema, ‘Hicho kito unachovaa juu ya kipaji cha uso kila siku chathibitisa kuwa yapo.’ Akasema, ‘Labda, kama yapo mnayo ruhusa kuchukua kadiri mnayotaka, yaani ikiwa ni lazima mniache, ndugu zangu.

’Nikasema, ‘Lazima, lazima tukitafute hicho chumba .’ Akajibu, ‘Yupo mtu mmoja tu anayeweza kutuonyesha, naye ni Gagula.’

Nikasema, ‘Na kama hatakubali kutuonyesha itakuwaje?’
Akasema, ‘Basi atakufa. Nimemwacha hai kwa kusudio hilo tu. Tumwite tuone kama atakubali.’

Akatuma mtu kumwita. Baada ya kitambo akaletwa na askari huku akiwatukana. Mfalme akamwambia askari wamwache, na mara alipoachiliwa akakaa chini, na macho yake yakang’aa kama kito, akasema, ‘Wataka nini kwangu, Ignosi? Huthubutu kunigusa, ukinigusa nitakuua papo hapo ulipokaa. Jihadhari na uchawi wangu.’

Ignosi akajibu, ‘We mbwa jike, uchawi wako haukumwokoa Twala, wala hauwezi kunidhuru mimi.

Sikiliza, nataka utwambie habari za siri za mawe yale yanayong’aa’.
Gagula akacheka, akasema, ‘Ha!Ha! Hapana ajuaye ila mimi nijuaye siri hizo, nami sitakwambia kamwe.

Mashetani weupe hawa watakwenda zao mikono mitupu.’
Ignosi akasema, ‘Lazima utaniambia. Nitakushurutisha.’ Akajibu, ‘Kwa namna gani, Ewe mfalme? Wewe kweli ni mkubwa mwenye nguvu lakini nguvu zako zinawezaje kuukamua ukweli kutoka kwa mwanamke?’


Ignosi akajibu, ‘Najua ni vigumu, lakini nitafanya.’ Gagula akasema, ‘Ndiyo, lakini kwa namna gani?’ Ignosi akasema, ‘Hivi, ikiwa huniambii, utakufa kwa mateso ya pole pole.’
Gagula akalia, akasema, ‘Kufa? Hutothubutu kunigusa; wewe hujui mimi ni nani.


Umri wangu wadhani ni miaka mingapi? Mimi niliwajua baba za baba za baba zako. Nchi ilipokuwa mpya, mimi nilikuwapo; nchi itakapokuwa imechakaa mimi nitakuwapo. Siwezi kufa ila kuuawa kwa ajali, maana hapana anayethubutu kuniua.’


Ignosi akajibu, ‘Ndiyo, lakini nakwambia kuwa mimi nitakuua.’ Akashika mkuki wake akamsimamia juu tayari. Yule kizee akasema, ‘Sitakuonyesha kabisa; huwezi kuthubutu kuniua, huwezi kabisa. Atakayeniua mimi atalaaniwa milele.’


Pole pole Ignosi akashusha mkuki hata ncha yake ilimchoma kidogo, na mara Gagula akaruka juu kwa sauti kali, kisha akaanguka chini akagaagaa, huku akisema, ‘Basi, basi, niachilie niishi nami nitakuonyesha.’


Ignosi akasema, ‘Vema. Nilihisi’ kuwa nitapata njia ya kukufanya ukubali. Kesho utafuatana na Infadus na ndugu zangu weupe, kuwaonyesha hapo mahali, na uangalie sana usifanye makosa, maana usipowaonyesha, hakika utakufa.’


Yule kizee akajibu, ‘Sitakosa, Ignosi. Ni desturi yangu kutimiza niliyoahidi. Ha!Ha!Ha! Zamani mwanamke mmoja alimwonyesha mtu mweupe kile chumba na tazama! Alipatikana na maovu. Jina lake lilikuwa Gagula vile vile.


Labda mimi na huyo mwanamke ni mmoja.’ Na mcho yake maovu yalizidi kung’aa.
Nikasema, ‘Mwongo, hayo yalitokea zamani vizazi kumi nyuma.’


Akasema, ‘Labda, labda; mtu akiishi miaka mingi pengine husahau. Labda lilikuwa jina la mama yangu nayeye aliniambia, kwa hakika jina lake lilikuwa Gagula vie vile. Lakini, angalieni, nawaambia ya kuwa katika chumba kile yalipo hayo mawe, mtaona kifuko cha ngozi kimejaa mawe meupe.


Huyo mtu alijaza kifuko hicho, lakini hakuwahi kukichukua. Alipatikana na maovu , nasema alipatikana na maovu! Labda aliyeniambia alikuwa mama wa mama yangu! Itakuwa safari ya furaha.


Tutapita katika mahali walipopigana askari juzi, tutaona maiti waliokufa katika vita. Macho yao yatakuwa yamekwisha pofuka sasa, na mbavu zao zitakuwa zimekwisha bonyeka. Ha! Ha!Ha!’
[emoji39] [emoji119] [emoji119]
 
Back
Top Bottom