Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

SURA YA KUMI NA NANE

Siwezi kabisa kueleza vitisho na taabu za usiku uliofuata. Zilipunguzwa kidogo kwa usingizi, maana hata katika hatari kama ile tuliyokuwa nayo, usingizi ulitujia kwa jinsi tulivyochoka.

Lakini sikuweza kulala sana, maana niliona mauti yananikaribia, kimya kikawa kingi hata sikuweza kupata usingizi. Tumezikwa ndani ya mlima wa theluji, na hata vishindo vya mizinga yote ya dunia haviwezi kutufikia.


Tumetengwa kabisa na kila sauti ya duniani, tumekuwa kama watu waliokwisha kufa. Ndipo nilipokumbuka mambo yote yaliyotupata. Hapo karibu nasi ziko fedha za kutosha kulipia madeni ya watu wote duniani, na kuunda meli zilizo bora, lakini hazitufai kabisa. Kweli, mali ambayo watu wengi huitafuta maisha yao yote, mwisho wake haina thamani hata kidogo.


Usiku ulipita. Baadaye, Bwana Henry akauliza, ‘Je, Bwana Good, unazo chembe ngapi za kibiriti?’ Akajibu, ‘Vijiti vinane tu.’


Akasema, ‘Vema, afadhali washa kimoja sasa tupate kujua ni saa ngapi.’
Akawasha kimoja, na kulikuwa giza totoro, hata alipokiwasha macho yaliingiwa na kiwi. Ilikuwa saa kumi na moja.


Akasema, ‘Afadhali na tule kidogo sasa tupate nguvu kidogo.’ Na Bwana Good akauliza, ‘Ya nini kula, si afadhali tukihimize kifo?’

Bwana Henry akajibu, ‘Kama maisha yapo, basi na tamaa ipo.’ Basi tukala, tukanywa maji kidogo; tukangoja. Kisha Bwana Good akasema, ‘Afadhali na tukae karibu na mlango tupate kumsikia atakayekaribia.’

Basi akakaribia mlangoni akaanza kupiga kelele, lakini wapi! Alifanya kelele nyingi sana, lakini zilitufaa nini? Baadaye akaacha kupiga kelele, maana tuliona kuwa zinatuzidishia kiu tu.

Basi tulikaa tena juu ya makasha yale ya almasi yaliyokuwa na hazina za thamani nyingi, na mimi nilikata tamaa nikaweka kichwa changu kwenye bega la Bwana Henry nikalia na kutokwa na machozi; na nadhani nilimsikia Bwana Good akilia vile vile.


Bwana Henry alikuwa mtu mwema sana! Hata tungalikuwa watoto wawili naye ni mlezi wetu, nadhani asingaliweza kutufanyia wema zaidi.

Alisahau sehemu yake ya taabu akajaribu kutuliwaza kwa kutusimuliwa hadithi za watu waliopatwa na mambo kama haya yaliyotupata sisi, na namna walivyookoka mwishoni.


Na alipoona hadithi zile haziwezi kutuliwaza akatwambia kuwa ni lazima watu wote wafe siku moja, basi sisi tumepungukiwa siku zetu kidogo tu. Alijaribu kwa kila namna kutuliwaza.

Alikuwa mtu mpole na mtaratibu wala hana makuu, lakini alikuwa mtu imara.
Basi mchana nao ulipita kama ulivyopita usiku, tukatazama saa tena tukaona kuwa ni saa moja, na tena tukala kidogo tukanywa, na tulipokuwa tunakula nikapata wazo nikasema, ‘Je, imekuwaje kuwa hewa iliyomo katika chumba hiki ni nzuri? Kweli ni nzito kidogo, lakini ni safi kabisa.’


Bwana Good akashtuka akasema, ‘Kweli! Sikufikiri hivyo. Hewa haiweze kuingia kwa mlangoni, maana pamezibwa kabisa,. Ingelikuwa hewa haingii siku zote, tulipoingia tungalihisi hewa mbaya. Tutazame.’


Basi ikawa ajabu namna tulivyochangamka kwa kupata cheche hizo za tamaa. Na mara sote watatu tulianza kutambaa chini na kupapasa kila mahali tupate kutafuta hata dalili ya hewa.

Kwa muda wa saa nzima na zaidi tulifanya hivi mpaka Bwana Henry na mimi tulikata tamaa tena, maana tuliumia mara nyingi kwa kujigonga na zile pembe na yale makasha, lakini Bwana Good hakukubali kushindwa, akasema afadhali kufanya hivi kuliko kukaa bure.

Baadaye kidogo akatuita, na mara tukamwendea, akasema, ‘Haya, Quatermain, weka mkono wako ulipowangu. Je, unaona kitu?’

Nikajibu, ‘Nadhani nasikia kitu. Nadhani nasikia kama baridi inaingia.’
Akasema, ‘Basi, sasa sikiliza.’ Akasimama akakanyaga chini kwa mguu mmoja, na mara ile tamaa yetu ndogo ikageuka na kuwa tamaa nyingi zilizotujaa maana palilia wazi.
 
nadhani ni vinjia vya mashimo yale ya kuchimbulia almasi.

Baadaye kidogo Niliwasha kibiriti kwa vidole vilivyotetemeka. Maana tulibakiwa na mishale mitatu tu, nikaona tupo katika pembe ya chumba

Kibiriti kilipoangaza nikatazama chini, nikaona kama ufa chini, na tena, Alhamdulilahi! Pale chini juu ya sakafu nikaona pete la mawe limefungwa chini. Hatukusema neno, mioyo zilitupiga kama nini sijui.

Bwana Good alitoa kisu chake akaanza kuchokoa pale penye pete, na baada ya kufanya kazi kwa taratibu na subira nyingi, akaweza kuliinua lile pete, akalisimamisha

Sasa alilishika kwa nguvu akajaribu kulivuta juu lakini hapana kilichojongea hata kidogo.
Basi sasa mimi nikaanza kuwa na hamasa, nikasema, ‘Haya na mimi nijaribu.’ Nikashika lile pete nikalivuta juu. Hakuna kilichonyanyuka. Bwana Henry vile vile akajaribu, na yeye vile vile alishindwa.

Basi Bwana Good akaanza tena kuchokoa pale katika ufa, pale tulipoona baridi inaingia, akasema, ‘Haya sasa Bwana Henry, jaribu kwa nguvu zako zote, wewe una nguvu za watu wawili.’

Akavua kitambaa alichofunga shingoni, akakipitisha katika pete lile, akampa Bwana Henry mkononi, akaniambia nimshike Bwana Henry kiunoni na sote tukavuta kwa nguvu zetu zote.

Bwana Henry akasema kwa sauti kubwa, ‘Haya! Vuteni! Vuteni! Inalegea!’
Nikasikia mishipa yake ikidata kwa nguvu alizotumia.

Mara tukasikia sauti ya kukwaruza, mara sote tulianguka nyuma na pande la jiwe kubwa likaruka juu. Nguvu za Bwana Henry zimetuokoa. Akasema, ‘Haya Quatermain, washa kibiriti.’

Tukajizoazoa na kupumzika kidogo; nikawasha kibiriti, na hapo tuliona ngazi ya mawe ya kushukia katika shimo! Bwana Good akauliza, ‘Je, sasa tutafanya nini?’

Nikasema, ‘Na tufuate ngazi. Tubahatishe.’ Lakini Bwana Henry akasema, ‘Ngoja kwanza, afadhali na tuchukue nyama na maji yaliyobaki, huenda tutakuwa na haja nazo.’

Nikatambaa chini niyapate, Tulikuwa tumekwisha sahau zile almasi kwa muda wa saa ishirini na nne; na hatukutaka hata kufikiri almasi kwa jinsi zilivyotuingiza katika taabu na shida; lakini nilifikiri afadhali tuweke kidogo mifukoni mwetu, maana huenda tutajaliwa kutoka katika taabu yetu.


Basi nikajaza almasi mifuko yote ya koti langu, na kwa bahati nilichukua nyingine kutoka katika kasha lenye zile zilizo kubwa.

Nikasema, ‘Haya, jamani, njooni mchukue almasi.
Mimi tayari nimejaza mifuko yangu.’ Bwana Henry akajibu, ‘Almasi nazipotelee mbali, natumai sitaona almasi tena mpaka kufa.’

Bwana Good hakujibu, nadhani alikuwa akimuaga Foulata, ambaye alikuwa akimpenda sana na ambaye alilala pale chini maiti.


Basi Bwana Henry akatuita, akasema kuwa yeye atatangulia kushuka. Nikamwambia, ‘Uangalie sana unapoweka miguu, pengine kuna mashimo.’

Basi tukashuka, na tulipohesabu daraja kumi natano tukaona kama tumefika chini. Sasa tukajiona tumo katika kinjia, tukakifuata, huku tumeelekea mahali inapotoka baridi.

Tulipokuwa tumekwanda kwa kadiri ya robo saa, (tulikuwa tukienda pole pole sana ) tuliona kinjia kinapinda, au kimekatwa na kingine.

Basi vivyo hivyo tukafuata kwa saa sijui ngapi. Vinjia hivi ni vya nini hatukufahamu, lakini tulisimama tumekwisha choka kabisa, tukala nyama iliyobaki na tukanywa maji yote yaliyobaki.

Ikawa kama tumeokoka katika kile chumba ili tupotee katika vinjia. Tulipokuwa tumekaa hivi, tukiwa tumekata tamaa kabisa, nilisikia kama sauti, lakini ikitoka kwa mbali sana, ikawa kama sauti ya maji yanayotiririka.
 
Basi tukajipa moyo; tukaendelea tena tukipapasa kuta zilizo kando ya kinjia. Tulipoendelea sauti ikasikika zaidi, mpaka tukaweza kusikia kama maji yanakwenda kwa nguvu.

Sasa tulikaribia sana, na Bwana Henry akasema, Nendeni pole pole, tunakaribia sana sasa.’

Mara tukasikia kishindo cha maji, na Bwana Good akapiga ukelele. Kumbe, ametumbukia majini! Tukafadhaika sana, tukamwita, akaitika, ‘Mimi nipo salama, kwa bahati nimeshika jabali, lakini washa kibiriti nipate kuona nipo wapi.’


Nikawasha mshale wa mwisho wa kibiriti. Na kwa mwangaza wake nikaona pale pale miguuni petu mto wa maji mengi yanapita kwa nguvu, na pale mbali kidogo Bwana Good ameshika jabali lililotokeza katika maji.


Mara tulisikia kishindo tena, kama anashindana na maji, na mara alitoa mkono na kumshika Bwana Henry, tukamvuta nchi kavu. Akasema huku akitweta, ‘Lo! Bahati yangu! Nisingeliweza kuogelea au kushika mwamba ule, ningalichukuliwa mbali kabisa. Mto huu unakwenda kasi sana.’

Tuliogopa kufuata ukingo wa maji tusije tukatumbukia ndani. Basi tulipumzika kidogo, tukanywa maji ya mto, maana yalikuwa matamu, tukajinadhifisha kidogo, tukaburudika. Lakini Bwana Henry akasema, ‘Ya nini kuhangaika, kinjia chochote kitatufaa, maana hatujui viendako wala hatuwezi kujua.’


Basi tukaendelea, na Bwana Henry aliongoza, na mara akasimama ghafla, nasi tuliokuwa tukimfuata tukagongana. Akasema, ‘Tazameni, je, nimeshikwa na kichaa?, au kweli ni mwangaza?’

Tukatazama na kule mbele tukaona mwangaza mdogo sana. Basi tuliingiwa na tamaa ya kuendelea. Baada ya mwendo wa dakika tano tukawa hatuna shaka tena, tuliona kuwa kweli ni mwangaza.


Na baada ya dakika nyingine tuliweza kuhisi upepo unatupiga usoni, tukaenda mbele moja kwa moja

Mara kinjia kikawa chembamba sana kikawa kama shimo la mnyama.
Bwana Henry akatambaa huku kajikunja, naye akatoka, na Bwana Good vile vile, na mimi vile vile, na tulipotupa macho juu tuliona nyota, na pia tukavuta hewa baridi safi kabisa.

Tulikuwa tumesimama hivi, na mara kitu kiliteleza na sote watatu tulianguka tukapinduka pinduka na kubiringika katika majani na vijiti.

Nikawahi kukamata kitu, nikasita kubiringika. Nikapiga kelele, na kwa chini yangu nilisikia Bwana Henry ananiita. Yeye alifika mahali pa sawa, alitulia. Na sasa ikawa kumtafuta Bwana Good, tukamwona karibu, alikuwa amejigonga na mti. Hakuumia sana, naye akaja juu upesi.


Basi sasa tulikaa juu ya majani tumejaa furaha jinsi hali yetu ilivyobadilika kwa ghafla. Kweli tumeongozwa katika kile kinjia ili tuokoke. Na tazama sasa kunaanza kupambazuka, nasi hatukufikiri ya kuwa tutaona tena mapambazuko.


Basi, polepole, jua likapanda na mwangaza wake ukaangaza nchi, tukaona kuwa tumo katika shimo lile kubwa lililo mbele ya pango lile tulimoingia. Na sasa tuliweza kuona yale masanamu matatu yaliyokuwepo ukingoni mwa shimo.

Tukakaa tukangoja mpaka jua likapanda juu zaidi, ndipo tulipoondoka tukaanza kupanda tutoke shimoni. Kwa muda wa saa nzima tulipanda kwa shida, tukajivuta juu kwa kushika majani na miti midogo midogo, mpaka tukafika juu.


Basi tukatoka na kusimama kuelekea yale masanamu matatu, na pale kando ya njia tuliona moto unawaka, na watu wamekaa karibu na moto.


Basi tukajikokota huku tukisaidiana, tukasimama kila hatua mbili tatu. Mara, mmoja katika wale watu alituona, akaanguka chini pale pale huku akipiga kelele kwa hofu.

Tukamwita, ‘Infadus! Infadus! Ni sisi rafiki zako.’ Akaondoka na kutujia. Akatukodolea macho huku akitetemeka. Akasema, ‘Enyi mabwana zangu, ‘kweli ni nyinyi mmefufuka?’ Na yule mzee askari akajitupa mbele yetu, akamshika Bwana Henry magoti, akalia kwa furaha ya kumuona tena.
 
Basi tukajipa moyo; tukaendelea tena tukipapasa kuta zilizo kando ya kinjia. Tulipoendelea sauti ikasikika zaidi, mpaka tukaweza kusikia kama maji yanakwenda kwa nguvu.

Sasa tulikaribia sana, na Bwana Henry akasema, Nendeni pole pole, tunakaribia sana sasa.’

Mara tukasikia kishindo cha maji, na Bwana Good akapiga ukelele. Kumbe, ametumbukia majini! Tukafadhaika sana, tukamwita, akaitika, ‘Mimi nipo salama, kwa bahati nimeshika jabali, lakini washa kibiriti nipate kuona nipo wapi.’


Nikawasha mshale wa mwisho wa kibiriti. Na kwa mwangaza wake nikaona pale pale miguuni petu mto wa maji mengi yanapita kwa nguvu, na pale mbali kidogo Bwana Good ameshika jabali lililotokeza katika maji.


Mara tulisikia kishindo tena, kama anashindana na maji, na mara alitoa mkono na kumshika Bwana Henry, tukamvuta nchi kavu. Akasema huku akitweta, ‘Lo! Bahati yangu! Nisingeliweza kuogelea au kushika mwamba ule, ningalichukuliwa mbali kabisa. Mto huu unakwenda kasi sana.’

Tuliogopa kufuata ukingo wa maji tusije tukatumbukia ndani. Basi tulipumzika kidogo, tukanywa maji ya mto, maana yalikuwa matamu, tukajinadhifisha kidogo, tukaburudika. Lakini Bwana Henry akasema, ‘Ya nini kuhangaika, kinjia chochote kitatufaa, maana hatujui viendako wala hatuwezi kujua.’


Basi tukaendelea, na Bwana Henry aliongoza, na mara akasimama ghafla, nasi tuliokuwa tukimfuata tukagongana. Akasema, ‘Tazameni, je, nimeshikwa na kichaa?, au kweli ni mwangaza?’

Tukatazama na kule mbele tukaona mwangaza mdogo sana. Basi tuliingiwa na tamaa ya kuendelea. Baada ya mwendo wa dakika tano tukawa hatuna shaka tena, tuliona kuwa kweli ni mwangaza.


Na baada ya dakika nyingine tuliweza kuhisi upepo unatupiga usoni, tukaenda mbele moja kwa moja

Mara kinjia kikawa chembamba sana kikawa kama shimo la mnyama.
Bwana Henry akatambaa huku kajikunja, naye akatoka, na Bwana Good vile vile, na mimi vile vile, na tulipotupa macho juu tuliona nyota, na pia tukavuta hewa baridi safi kabisa.

Tulikuwa tumesimama hivi, na mara kitu kiliteleza na sote watatu tulianguka tukapinduka pinduka na kubiringika katika majani na vijiti.

Nikawahi kukamata kitu, nikasita kubiringika. Nikapiga kelele, na kwa chini yangu nilisikia Bwana Henry ananiita. Yeye alifika mahali pa sawa, alitulia. Na sasa ikawa kumtafuta Bwana Good, tukamwona karibu, alikuwa amejigonga na mti. Hakuumia sana, naye akaja juu upesi.


Basi sasa tulikaa juu ya majani tumejaa furaha jinsi hali yetu ilivyobadilika kwa ghafla. Kweli tumeongozwa katika kile kinjia ili tuokoke. Na tazama sasa kunaanza kupambazuka, nasi hatukufikiri ya kuwa tutaona tena mapambazuko.


Basi, polepole, jua likapanda na mwangaza wake ukaangaza nchi, tukaona kuwa tumo katika shimo lile kubwa lililo mbele ya pango lile tulimoingia. Na sasa tuliweza kuona yale masanamu matatu yaliyokuwepo ukingoni mwa shimo.

Tukakaa tukangoja mpaka jua likapanda juu zaidi, ndipo tulipoondoka tukaanza kupanda tutoke shimoni. Kwa muda wa saa nzima tulipanda kwa shida, tukajivuta juu kwa kushika majani na miti midogo midogo, mpaka tukafika juu.


Basi tukatoka na kusimama kuelekea yale masanamu matatu, na pale kando ya njia tuliona moto unawaka, na watu wamekaa karibu na moto.


Basi tukajikokota huku tukisaidiana, tukasimama kila hatua mbili tatu. Mara, mmoja katika wale watu alituona, akaanguka chini pale pale huku akipiga kelele kwa hofu.

Tukamwita, ‘Infadus! Infadus! Ni sisi rafiki zako.’ Akaondoka na kutujia. Akatukodolea macho huku akitetemeka. Akasema, ‘Enyi mabwana zangu, ‘kweli ni nyinyi mmefufuka?’ Na yule mzee askari akajitupa mbele yetu, akamshika Bwana Henry magoti, akalia kwa furaha ya kumuona tena.
Barikiwa mkuu, tamu sana
 
Back
Top Bottom