Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
HahaahHii naiandika yote kwenye daftari, maana unaweza kuamka kesho jf imezimwa
Mkuu nipo jikoni mzigo unatokota!Mkuu alosto inatuua
poa mkuu na mungu akuwezesheMkuu nipo jikoni mzigo unatokota!
sanaBonge la ujumbe Hahaah!
Barikiwa mkuu, tamu sanaBasi tukajipa moyo; tukaendelea tena tukipapasa kuta zilizo kando ya kinjia. Tulipoendelea sauti ikasikika zaidi, mpaka tukaweza kusikia kama maji yanakwenda kwa nguvu.
Sasa tulikaribia sana, na Bwana Henry akasema, Nendeni pole pole, tunakaribia sana sasa.’
Mara tukasikia kishindo cha maji, na Bwana Good akapiga ukelele. Kumbe, ametumbukia majini! Tukafadhaika sana, tukamwita, akaitika, ‘Mimi nipo salama, kwa bahati nimeshika jabali, lakini washa kibiriti nipate kuona nipo wapi.’
Nikawasha mshale wa mwisho wa kibiriti. Na kwa mwangaza wake nikaona pale pale miguuni petu mto wa maji mengi yanapita kwa nguvu, na pale mbali kidogo Bwana Good ameshika jabali lililotokeza katika maji.
Mara tulisikia kishindo tena, kama anashindana na maji, na mara alitoa mkono na kumshika Bwana Henry, tukamvuta nchi kavu. Akasema huku akitweta, ‘Lo! Bahati yangu! Nisingeliweza kuogelea au kushika mwamba ule, ningalichukuliwa mbali kabisa. Mto huu unakwenda kasi sana.’
Tuliogopa kufuata ukingo wa maji tusije tukatumbukia ndani. Basi tulipumzika kidogo, tukanywa maji ya mto, maana yalikuwa matamu, tukajinadhifisha kidogo, tukaburudika. Lakini Bwana Henry akasema, ‘Ya nini kuhangaika, kinjia chochote kitatufaa, maana hatujui viendako wala hatuwezi kujua.’
Basi tukaendelea, na Bwana Henry aliongoza, na mara akasimama ghafla, nasi tuliokuwa tukimfuata tukagongana. Akasema, ‘Tazameni, je, nimeshikwa na kichaa?, au kweli ni mwangaza?’
Tukatazama na kule mbele tukaona mwangaza mdogo sana. Basi tuliingiwa na tamaa ya kuendelea. Baada ya mwendo wa dakika tano tukawa hatuna shaka tena, tuliona kuwa kweli ni mwangaza.
Na baada ya dakika nyingine tuliweza kuhisi upepo unatupiga usoni, tukaenda mbele moja kwa moja
Mara kinjia kikawa chembamba sana kikawa kama shimo la mnyama.
Bwana Henry akatambaa huku kajikunja, naye akatoka, na Bwana Good vile vile, na mimi vile vile, na tulipotupa macho juu tuliona nyota, na pia tukavuta hewa baridi safi kabisa.
Tulikuwa tumesimama hivi, na mara kitu kiliteleza na sote watatu tulianguka tukapinduka pinduka na kubiringika katika majani na vijiti.
Nikawahi kukamata kitu, nikasita kubiringika. Nikapiga kelele, na kwa chini yangu nilisikia Bwana Henry ananiita. Yeye alifika mahali pa sawa, alitulia. Na sasa ikawa kumtafuta Bwana Good, tukamwona karibu, alikuwa amejigonga na mti. Hakuumia sana, naye akaja juu upesi.
Basi sasa tulikaa juu ya majani tumejaa furaha jinsi hali yetu ilivyobadilika kwa ghafla. Kweli tumeongozwa katika kile kinjia ili tuokoke. Na tazama sasa kunaanza kupambazuka, nasi hatukufikiri ya kuwa tutaona tena mapambazuko.
Basi, polepole, jua likapanda na mwangaza wake ukaangaza nchi, tukaona kuwa tumo katika shimo lile kubwa lililo mbele ya pango lile tulimoingia. Na sasa tuliweza kuona yale masanamu matatu yaliyokuwepo ukingoni mwa shimo.
Tukakaa tukangoja mpaka jua likapanda juu zaidi, ndipo tulipoondoka tukaanza kupanda tutoke shimoni. Kwa muda wa saa nzima tulipanda kwa shida, tukajivuta juu kwa kushika majani na miti midogo midogo, mpaka tukafika juu.
Basi tukatoka na kusimama kuelekea yale masanamu matatu, na pale kando ya njia tuliona moto unawaka, na watu wamekaa karibu na moto.
Basi tukajikokota huku tukisaidiana, tukasimama kila hatua mbili tatu. Mara, mmoja katika wale watu alituona, akaanguka chini pale pale huku akipiga kelele kwa hofu.
Tukamwita, ‘Infadus! Infadus! Ni sisi rafiki zako.’ Akaondoka na kutujia. Akatukodolea macho huku akitetemeka. Akasema, ‘Enyi mabwana zangu, ‘kweli ni nyinyi mmefufuka?’ Na yule mzee askari akajitupa mbele yetu, akamshika Bwana Henry magoti, akalia kwa furaha ya kumuona tena.
Mhhsanaaa mzeee....roho imeniuma sana gagulaa aieseee kafarikii
Unaweza tu mkuuMkuu naweza kupata soft yake baadae
Sawa mkuu tutaangalia namnaUnaweza tu mkuu
Poa mkuuSawa mkuu tutaangalia namna