Hai: DED aagiza walimu wote kwenda kumpokea Rais Samia uwanja wa KIA

Hai: DED aagiza walimu wote kwenda kumpokea Rais Samia uwanja wa KIA

Siyo Rais, ni watumishi waokuza matukio yanayomhusu mkuu wa nchi kwa kujipendekeza.
Unaweza kukumbuka, wakati wa msiba wa hayati Rais Magufuli, kwa sababu ya ujinga na kujipendekeza, baadhi ya viongozi walikuwa wanahamasisha wananchi waende kwa wingi uwanja wa taifa, bila kujali usalama na matokeo yake watu walikufa na hakuna aliyejali wala kuwajibishwa.
Kwa matukio yanayomhusu viongozi wakuu wa nchi, waende wawakilishi tu, huku shughuli nyingine za ujenzi wa taifa zikiendelea, kama kufundisha shuleni, huduma za afya, biashara, kilimo,....
Hili la kulazimisha kwenda kuaga mwili wa Magufuli hoja yapo imefeli vibaya sn.

Hivi inawezekana hata wale wanainchi waliokuwa wanalia kwa uchungu pia walilazimishwa kulia?
 
Hata hizi protical za awapo Rais,
1. Makamu
2. Waziri Mkuu yupo.
Ifike mahala itumike protocol mbadala, kiusalama na ulinzi inatugharimu sana na nirisik kwa wanausalama wetu.
 
Ujumbe wenyewe huo hapo

Habari za jioni, napenda kuwataarifu kuwa kesho kutakuwa na ujio wa Mhe. Rais , hivyo watumishi wote tunatakiwa tufike uwanja wa ndege wa KIA saa kumi na mbili kamili asubuhi.
Ni walimu tu ndio huendeshwa kama tambara la kudekia kwenye hii nchi. Lakini cha kustaajabisha zaidi ni kuwa wanaowaendesha puta ni wanafunzi wao. Na pia utashangaa zaidi hao hao walimu watasaidia kuwaibia kura watesi wao. Walimu sijui kuna nini kimewakuta kwenye hii nchi.
 
Walimu ni kamyagio la wanasiasa..acha wateseke mana wao ndio mawakala wa uchaguzi feki.

#MaendeleoHayanaChama
 
T

Tangu tupate uhuru wanawake hawajawahi kushindwa kupika maandazi kwa kukosa mafuta ya kula.
Kama huko kwenu mnazalisha mafuta,kazaneni kuzalisha yasikoseakane,maana Indonesia mzalishaji mkubwa wa mafuta nako yamepanda Bei,kazuwia kuuza nje,kwa hiyo yatapanda zaidi
 
Ujumbe wenyewe huo hapo

Habari za jioni, napenda kuwataarifu kuwa kesho kutakuwa na ujio wa Mhe. Rais , hivyo watumishi wote tunatakiwa tufike uwanja wa ndege wa KIA saa kumi na mbili kamili asubuhi.
kuna shule moja Arusha iligoma kupeleka watoto meko akaifunga
 
T

Tangu tupate uhuru wanawake hawajawahi kushindwa kupika maandazi kwa kukosa mafuta ya kula.
Umezaliwa lini wewe?

Nchi hii imepitia mengi kabla na baada ya vita vya Kagera.Bidhaa zilikuwa hamna madukani.Watu wanapikia chai kwa pipi nyeupe. Ma shelf yalikuwa tupu.Kibali cha sukari,unga na mafuta unapata kwa RDD.

Magari yalikuwa
hayaruhusiwi kutembea Jumapili kwa ukosefu wa petroli miaka ya 1970.

Ukikutwa na sabuni ya Imperial au dawa ya meno ya Colgate kutoka Kenya unakamatwa kama mhujumu uchumi.Tulikuwa tunavaa nguo karibu za aina moja kama wafungwa.

Wewe umezaliwa mwaka gani mpaka uje na madai kama haya?
Umedeka sana kwa kutopitia tabu walizopitia wenzako. Uliza wazazi wako if they are old enough to remember.
 
Kuhamasisha watu sio kuwalazimisha
Hapo ni kuhamasisha? "Watumishi wote tunatakakiwa kufika" hapo ni kuwalazimisha. Lakini pia wanaenda kumpokea uwanja wa ndege ili iweje? Si kuna viongozi wapo huko watampokea?
 
Hili la kulazimisha kwenda kuaga mwili wa Magufuli hoja yapo imefeli vibaya sn.

Hivi inawezekana hata wale wanainchi waliokuwa wanalia kwa uchungu pia walilazimishwa kulia?
Sijaandika walilazimishwa, ila kulikuwepo uhamasishaji usiokuwa wa lazima.
Kukiwa na tukio, hata kama ni la hatari, watu wa mitaani hupenda kwenda kushuhudia.
Ni wajibu wa viongozi na yombo vya usalama kuhakikisha kuwa wanapunguza idadi ya watu kwenye mikusanyiko ili kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza.
 
Ujumbe wenyewe huo hapo

Habari za jioni, napenda kuwataarifu kuwa kesho kutakuwa na ujio wa Mhe. Rais , hivyo watumishi wote tunatakiwa tufike uwanja wa ndege wa KIA saa kumi na mbili kamili asubuhi.
Rais Yuko ziara ya kikazi na wengine waachwe waendeleee na kazi sehemu zao za kazi huu upuuzi kuendekeza ukada kila mahali unatugharimu Sana ccm kwa Nini hamkui ????!!!
 
Haina faida yoyote
Bado kuna imani ya kuwa ukiwa umefika mahali watu wajae inaonyesha unapendwa zaidi

Hii ni akili ya viongozi wa Africa tu na nchi maskini za kidikteta
Kwani akishuka akaenda kwake kuna tatizo gani ?
Kuna ulazima wa kuongea siku hiyo hiyo?
Ili iweje
Acheni kusumbua watu
Bado mnatukumbusha kuokota vitambaa kwa mafundi cherehani
 
Back
Top Bottom