Hai, Kilimanjaro: Komandoo Adamoo na wenzake wazawadiwa ng’ombe dume kila mmoja

Mungu wa Mbinguni awabariki sana
 
Nadhani 'red brigade' ya Chama fulani imepata wakunaji. Ulinzi na usalama wote nchini ni muhimu sana.
 
Hawa Watu na familia zao walipitia ktk kipindi kigumu sana ila nimeamini mafunzo ya ukamandoo yanafundisha uvumilivu wa hali ya juu sana na utii. Pia ni mshauri Mbowe asiwe na kinyongo hata Kidogo na Luteni Denis Urio,alikuwa na nia nzuri sana kwake ila madhila aliyopitia Amuulize vizuri Ling'wenya ata mutamsimulia.
 
Lakini najiuliza alipo mwenzao anayesemekana alitoweka kininja ninja vile! Sijui anaitwa Lijenje?

Na Denis Urio, je, anajisikiaje? Yule mama wa mbege pale Rau?
Itabidi ianzishwe campaign rasmi ya where is Lijenje tujue alipo na kama alikufa waliomuua wafikishwe mahakamani.
 
mambo mengine yanahitaji busara sana, mashtaka mazito kama yale yanafutwaje kirahisi namna hii. DPP atoe ufanunuzi kwa wananchi
Inabidi upeleke malalamiko yako kwa DPP kwanini amekuumiza roho namna hii kwa kumuachia Mbowe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…