Leo nimesikia audio ikitembea mitandaoni inayodaiwa kuwa imerekodiwa na Manara akimtuhumu kwa mambo mengi Barbara.Inaonekana hawa watu wana mgogoro wa mda mrefu na hawawezi kufanya kazi tena pamoja. Wewe kama mwanasoka unadhani nini kifanyike? Au ni madhara ya Mo kujimilikisha timu kifamilia?🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Kwenye audio hyo Manara kaenda mbali zaidi na kumtishia Barabara sijui Barnaba sorry Barbana,duuh Barbara kwamba ataiacha timu kama alivyoikuta.Sasa hapo sijui nani anaondoka nani anabaki.
Povu ruksa nina nguo chafu hapa.
Najaribu kuapload audio husika hapa inazingua
=====
Afisa Habari wa Simba Haji Manara ameamua kumtolea uvivu Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo Barbara Gonzalez.
Haji anadai Mtendaji huyo amekuwa akimuandama sana na kumnyima raha muda wote toka ameshika majukumu hayo.
====== Hajj Manara mwisho wake ni leo, Gsm poleni sana yuda iskarioti is out, Ezekiel ni kama vile anapewa miezi miwili ya transition ili kuendeshwa kitofauti na kusafisha u snitch ulisababishwa na tamaa za kuchukua mahela ya kuishi kifahari mjini. ===== BAADA ya maneno mengi bila vitendo...
Hapo umbumbumbuni shida ipo yaani hakuna proffesionalism. Na Manara atambue kuwa msimamo wa Barbara ndo huo huo msimamo wa Muddy maana ni chombo yake ndo mana kaionga uCEO
Manara uswahili unamdanganya, Manara hana uwezo wa kumtoa simba Babra wala Mo.. ila Babra na Mo wana uwezo wa kumtoa Simba Manara..
Mwenye pesa sio mwenzako.. hao kina chama na konde boy unawaona sababu ya kina babra na Mo hapo.. hizo robo fainali za klabu bingwa unaziona sababu ya kina Barbara na Mo.
Je Manara ana uwezo wa kulipa mshahara hata wa Zimbwe tu?
Halafu akumbuke soka siku hizi alichezwi mdomoni ila ni uwekezaji wa ndani ya pitch, hizo porojo zake sio muhimu sana hasa ukiangalia katika Club bora barani Afrika kama Al Ahly, Wydad, Je, wana watu kama hao kwenye timu zao, lazima tubadilike katika soka letu. Naungana na Barbra Gonzalez katika hili