Haji Manara nakuonya mapema usifanye hiyo Press Conference yako ya Kuwachafua Waandamizi wa Simba SC wiki ijayo

Haji Manara nakuonya mapema usifanye hiyo Press Conference yako ya Kuwachafua Waandamizi wa Simba SC wiki ijayo

Ni wapumbavu kupindukia ..unapoenda mahakamani jaji hua anatoa nafasi kwa mshtaki na mshtakiwa wote kuongea kila mtu kwa nafasi yake , tunataka kusikiliza anachotaka kusema Manara

Mbona alishakisema kwenye voice note ww bwimbi hakuna kipya
 
Hiyo press inatakiwa waandishi wamzilie, halafu ajue anacheza na hisia na imani za wengi. Akibugi itamgharim, simba na yanga ni dini za watu..
ila mjiandae kwa kesi pia maana hayo ya kutrace simu zake na location ni kuingilia faragha ya mtu hivyo yaishie hivyo hvyo sio kupelekana tena mahakamani
 
Msimtishe, Manara, kama mlijua tangu zamani mbona hakukuwa na reaction?
Hakuna cha GPS wala tracking yoyote. Sema amepiga kwenye Mshono tu.

Hapotezi chochote , Simba itawagharimu.
Muguseni muone nani atanuka
Wacha utoto wewe, Manara kaokotwa na Simba SC anazurura kariakoo amepauka vumbi leo ajifanye mjanja zaidi ya Simba?
 
Kwani kuna kitu gani ambacho unahofia atakisema hadi azuiliwe kuto kufanya press? Kuna madudu yanafichwa eeh??

Binafsi niseme tu ni upumbavu mkubwa sana kusema eti Haji anauza timu kwa yanga.

Haji Manara huyuhuyu anaye tukanwa matusi kila siku kwasababu ya Simba ?
Simba ikifungwa yeye ndio wakwanza kushambiliwa mara wamu edit Kama mwanamke mitandaoni mara wamuite Nguruwe.

Haji huyuhuyu anaye gombana na waandishi wa Yanga kina kitenge, Shafii Dauda prisca n.k wanao zusha uongo kila siku dhidi ya Simba.?

Haji huyuhuyu Simba inafungwa analia machozi anakuja mbele ya waadhishi wa habari na tv kuonyesha jinsi wavyo hujumiwa?

Eti leo yeye ndio anaambiwa anaenda kuuza timu.

Haji huyuhuyu Simba inaenda kucheza ndondo kipindi hicho yeye anakaa mlangoni kukusanya viingilio timu ipate pesa leo huyu auze timu huyu.

Tena anaye mtuhumu ni babra aliye kuja juzi tu kwenye timu heti yeye ndio kawa mfia timu kuliko Haji?

Huyu Honspopa huyu si ndio yeye aliye watuhumu kina chama na Zimbwe kuwa wanauza game hadi kulekea Simba kufungwa Leo kageukia kwa Haji??


Wamseme kwa mambo mengine ila si kuuza timu hiyo ni matusi makubwa sana kwa mtu kama haji ?
Umefeli kwenye judgement, Barbara kuja juzi hakumuondolei nafasi yake na mapenzi yake kwa Simba, na wakati huo huo, huyo Manara unaemuamini ndio anaitumia imani uliyonayo kwake kuihujumu Simba, wake up.

Yale madai yake aliyoyatoa jana ni ya kijinga sana, na zaidi kuyatoa kwake wakati huu tukielekea kucheza na Yanga SC mechi ya fainali ya ASFC, wakati ambao Manara ana uhusiano na viongozi wa Yanga SC, na zaidi kwanini hakupeleka madai yake kwa uongozi wa Simba akakimbilia Kitenge Tv ya yule yule mchawi wa Simba?

Manara simuamini tena, ni ndumilakuwili mnafiki, anatumiwa na Yanga kuleta mgogoro Simba SC kwa maslahi ya Yanga SC, kwa ujinga alioufanya jana sitegemei aendelee tena kuwa msemaji wa Simba come next season.
 
Ni rahisi kusema ashikwe kusaidia upelelezi

Kusaidia upelelezi sio kazi ya raia ni kazi ya jeshi ndio maana tunawalipa

Kusaidia upelelezi ni iwapo watanilipa

Kama hakuna malipo au interests zangu zinakua served basi kazi ya kusaidia wasahau

Ni maajabu watu kudhani kuisaidia serikali kazi zake ni kitu cha maana,sio kitu cha maana ni upumbavu

Serikali ifanye kazi zake yenyewe bila kusaidiwa popote

Pili,kumshika huyu mtu ni rahisi kuongea ila kumshika practically huwezi

Ndio mpaka uende JF uvunje server usome IP yake,na kama likua kwenye VPN,forget it!
Kwa lugha nyingine kusaidia polisi ni kuwa wewe ni mtuhumiwa na unapelekwa kituoni kuhojiwa. Ni ukweli kuna ugumu wa kuwapata wahusika, ila mtoa mada kasema watabainisha vitu walipachika kwenye gari na simu ya Manara ili kunasa mawasiliano yake, akisema hadharani hili ni ikionekana ni ukweli, huyu unasukuma ndani fasta.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Si uje useme uozo wa nyumbani kwako kwanza kabla ya kutaka uozo wa Simba usemwe
Acha kumtisha Haji.

Mimi ni MwanaSimba ila muumini sana wa ukweli. Kama kuna longolongo zinafanyika huko ndani, Haji aeleze ukweli.

Hatuwezi kuyakimbia matatizo kwa kujidanganya kuwa hayapo. Na bora yajulikane na kutatuliwa kwa muda huu, kuliko tuendelee kuyafuga baadae yatuharibie.

Muda pekee wa kuwekwa wazi ni sasa wakati tupo ukingoni mwa mechi za mashindano. Likizo iishe na varangati hili liishe. Tukirudi tupo fresh kabisa.

Kuna matatizo mengi Simba SC, ila kivuli cha kufanya vizuri kinayaficha hayo yaliyopo.

Ukweli ni kuwa, Haji kakosea. Lakini, hatuwezi kumtisha kwa kumzuia kusema uozo uliopo.
 
Unataka Simba ichambane na Manara?
Hii ni Simba siyo utopolo.Simba haiwezi kumjibu manara kama unavyotaka,sisi wapenzi wa Simba ndio tutamjibu
Nyie wanasimba acheni kujitikisa huku mitandaoni mwisho wa siku nyote mnaonekana kina manara tu. Kama mtu ndio tabua yake na hamumchukulii hatua yoyote ina maana mnamuogopa.

Hata kwenye hili ni ajabu mpaka sasa mnabwabwaja tu mitandaoni, hakuna chochote toka kwenu. Hii ishu ni nzito, ikiwa na maana kwamba wanasimba hamwalipi inavyostahili wafanyakazi wenu.

Lakini tuliiii eti wanasubiri kwanza mechi ya j2 ipite, hili jipya sasa huyu anasema sio mechi ipite ila ni mpaka manara aitishe press na waandishi.

SIMBA MNAMUOGOPA MANARA.
 
Semeni yote ila kitendo cha Haji kuvujisha zile clip ni ishara tosha kuwa ni mbinafsi,msaliti,na ana agenda ya kuihujumu Simba.Kama angekuwa anaioenda Simba yote hayo angeyatoa baada ya mechi.

Kutukanwa kwake Simba ikifungwa ni kwa sababu alipenda mwenyewe.Maana yeye naye ana matusi na gubu sana.Si wote tuliyapenda maneno yake ijapo ni wapenzi wa Simba.

Msimtetee Haji ni mnafiki.
Kwani kuna kitu gani ambacho unahofia atakisema hadi azuiliwe kuto kufanya press? Kuna madudu yanafichwa eeh??

Binafsi niseme tu ni upumbavu mkubwa sana kusema eti Haji anauza timu kwa yanga.

Haji Manara huyuhuyu anaye tukanwa matusi kila siku kwasababu ya Simba ?
Simba ikifungwa yeye ndio wakwanza kushambiliwa mara wamu edit Kama mwanamke mitandaoni mara wamuite Nguruwe.

Haji huyuhuyu anaye gombana na waandishi wa Yanga kina kitenge, Shafii Dauda prisca n.k wanao zusha uongo kila siku dhidi ya Simba.?

Haji huyuhuyu Simba inafungwa analia machozi anakuja mbele ya waadhishi wa habari na tv kuonyesha jinsi wavyo hujumiwa?

Eti leo yeye ndio anaambiwa anaenda kuuza timu.

Haji huyuhuyu Simba inaenda kucheza ndondo kipindi hicho yeye anakaa mlangoni kukusanya viingilio timu ipate pesa leo huyu auze timu huyu.

Tena anaye mtuhumu ni babra aliye kuja juzi tu kwenye timu heti yeye ndio kawa mfia timu kuliko Haji?

Huyu Honspopa huyu si ndio yeye aliye watuhumu kina chama na Zimbwe kuwa wanauza game hadi kulekea Simba kufungwa Leo kageukia kwa Haji??


Wamseme kwa mambo mengine ila si kuuza timu hiyo ni matusi makubwa sana kwa mtu kama haji ?
 
Hiyo press inatakiwa waandishi wamzilie, halafu ajue anacheza na hisia na imani za wengi. Akibugi itamgharim, simba na yanga ni dini za watu..
Wandishi wakatae kwenda?wakati hiyo ni habari?!!Yaani mechi ya YANGA, na SIMBA inavyokuzwa utadhani kuna mpira basi kumbe ni butua butua tu! Yaani mtu anaweza kuhisi ni bonge la mechi kama la brazil na argentina miaka hiyo ya 90!!
Waafrika bwana, kwa hiyo haji kosa lake ni kuonekana na watu wa yanga, na kufanya nao biashara?kwanza msemaji wa timu na kuihujumu timu wapi na wapi?au mimi ndio sielewi yaani anawezaje kufanya hadi timu ikafungwa?
 
Unataka Simba ichambane na Manara?
Hii ni Simba siyo utopolo.Simba haiwezi kumjibu manara kama unavyotaka,sisi wapenzi wa Simba ndio tutamjibu
Kwani kawaatack wapenzi wa simba au viongozi wa simba!? Na sio mara moja anaaibisha brand yenu ila anakaliwa kimya tu. Nyie mashabiki mtamuandama mitandaoni lakini hamuwezi kutoa uamuzi wowote juu ya hatma yake.

Mo akisema na abaki/aende hakuna wa kumpinga kati yenu, kwahiyo kelele zenu hazina impact sana. Tumsubiri Mo tu
 
Hapo ndo mtajua kuwa manara ni mkubwa kuliko mkia FC
 
Na utakuwa mpumbavu sana kuamini Manara ana nia njema na Simba kwa kuvujisha clip zile kabla ya derby
Ile ni attitude ya Manara ambayo mashabiki wa Simba mmekuwa mkiipraise kila siku kwamba "Semaji La Dunia Limesema"..mara ngapi amekuwa akitukana na kudhalilisha watu? Waandishi? Etc na mishabiki ya Simba mmekuwa upande wake na kumtetea? Tulieni dawa iwaingie sasa, endeleeni kumtetea.
 
Kama una uozo wake basi kuwa mpole akisema ukweli kuhusu uozo wa wakubwa wa simba na wewe umripue sasa iwe bila bila,sio kuanza kumtisha .....hii ni vita na kwenye vita hakuna huruma akimwaga mboga nawe mwaga ugali kijana.
 
Back
Top Bottom