Haki Tanzania na 4R za Samia, Ni Mabadiliko ya Kweli au ni Kiinimacho?. Watanzania Waelimishwe Haki Zao, 4R Zisiwe Maneno Matupu, Tuombe Vitendo au?

Haki Tanzania na 4R za Samia, Ni Mabadiliko ya Kweli au ni Kiinimacho?. Watanzania Waelimishwe Haki Zao, 4R Zisiwe Maneno Matupu, Tuombe Vitendo au?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi
Hii ni makala yangu ya Kwa Maslahi ya Taifa kwenye Gazeti la NIPASHE la Jumapili ya leo
Screenshot_20240915-064641_Rifaly.jpg

Kama kawa kila siku za Jumapili hutiririka na makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa
zenye swali hoja majibu utayatoa wewe msomaji mwenyewe.

Swali la leo ni kuhusu haki nchini Tanzania na falsafa ya 4R za Rais Samia。

Rais Samia alipotwaa nchi, ameibuka na falsafa mpya ya 4R ambayo utekelezaji wake kikamilifu utaibadili kabisa Tanzania kuwa ni nchi ya Haki, Upendo, Ustawi, Mapatano, Maelewano na Maendeleo Endelevu, sasa je hizi 4R za Samia zinaleta mabadiliko ya kweli au 4R ni mahubiri tuu lakini tukija kwenye utekelezaji ni utekelezaji kiinimacho?.

Watanzania waelimishwe haki zao, 4R za Rais Samia zisiwe ni maneno matupu, jee sasa umefika wakati Watanzania tuombe kuona utekelezaji kwa vitendo wa hizi 4R au tuendelee kuridhika na haya maneno maneno na utekelezaji viini macho?.

Tumefundishwa kuwa na shukrani, hivyo naianza makala ya leo kwa pongezi na shukrani kwa Rais Samia kwa falsafa yake ya 4R na mahubiri yake mazuri kuhusu haki.

4R ni kifupisho cha maneno ya Kiingereza Reconciliation (Maridhiano), Resilience (Ustahimilivu), Reform (Mabadiliko) na Rebuiding (Kujenga upya).

Makala hii inajikita kwenye R moja tuu ya Mabadiliko, tunataka mabadiliko ya kweli na sio mabadiliko kiinimacho!.

Tunawaomba watendaji waitafsiri kwa vitendo falsafa hiyo ya 4R, kwa kutenda kile kinachohubiriwa yasibaki kuwa maneno tuu ya mahubiri ya 4R lakini vitendo ni tofauti!.

Hakuna mashaka kabisa kuhusu nia ya dhati ya Rais kutaka Watanzania kutendewa haki, ana nia njema ya dhati na thabiti Watanzania wapate, haki zao, lakini anakwamishwa na baadhi ya Watendaji wake ndio wanao mwangusha!.

Haki hailetwi kwenye kisahani cha chai, haki ni stahili na stahiki inayopaswa kutolewa bila wewe kuiomba, na ikitokea haki haikutolewa au haikutendeka, haki haiombwi, bali inapaswa kudaiwa, sasa ukiwa mtu hujui haki yako, huwezi kudai kitu usichokijua!,ndio maana akina sisi,tumejitolea kuwaelimisha Watanzania haki zao。

Nikimuangalia na kusikiliza kauli zake kuhusu haki, kusema la ukweli kabisa, Rais Samia, ana nia njema ya dhati kutoka moyoni mwake kuhakikisha Watanzania wanatendewa haki haya mambo ya ajabu ajabu yanayotokea ni uzembe na udhaifu wa baadhi ya watendaji wake, tunamshauri Rais Samia awe mkali kama Nyerere, kwenye ukiukwaji wa haki, ahakikishe hakuna Mswalie Mtume.

Nimekumbushia haki kufuatia kilichotokea hadi kifo cha huyu Mzee Kibao wa Chadema, ameuliwa kwasababu wananchi hawajui haki zao!. Kama Watanzania wangekuwa wanajua haki zao Mzee Kibao asingekubali kukamatwa na watu ambao hawatambuliki.

1. Kama Watanzania wangekuwa wanajua haki zao, dereva wa basi la Tashrif asinge kubali kusimamishwa na watu wasiotambulika.

2. Kama Watanzania wangekuwa wanajua haki zao, dereva wa Tashrif angekuwa anajua ile tiketi ya abiria, ni mkataba wa kisheria wa kumshusha abiria wake kituo alicholipia, dereva ana wajibu wa kisheria, duty of care, kuhakikisha usalama wa abiria wake na mali zake kwenye butt ya gari yake!. Mali pekee ambayo ni responsibility ya abiria ni mzigo wake wa mkononi, hand luggage anaoingia nao ndani ya basi, ndio "abiria chunga mzigo wako" lakini jukumu la abiria kufika salama anapokwenda, dereva wa basi ana wajibu wa kisheria kumfikisha salama.

3. Watanzania wangekuwa wanajua haki zao, abiria tuu wa kawaida akiwemo abiria aliyekaa seat no. 1 ya basi hilo ambaye ni traffic police, alikuwa na uwezo wa kuwabaini majambazi hao kuwa sio askari polisi wa kweli na kuwahamasisha abiria wengine wote wasikubali abiria mwenzao atekwe!.

4. Watanzania wangezijua haki zao, wangejua Polisi haruhusiwi kumkamata mtu yoyote bila kwanza kujitambulisha yeye ni nani na ametokea kituo gani kwa kuonyesha kitambulisho cha polisi.

5. Watanzania wangejua haki zao, wangejua mtu anayekamatwa ana haki ya kusoma number ya kitambulisho na kuihakiki number ya askari police kwenye mfuko wa kushoto wa nguo ya polisi.

6. Wakija polisi ambao ni askari kanzu, hawa hawana uniform hivyo hawavai numbers, hawaruhusiwi kumkamata mtuhumiwa bila kuandamana na polisi wenye uniforms!.

7. Mtu yeyote kabla hajakamatwa lazima awe na arrest warrant na lazima aripoti ofisi ya serikali ya mtaa husika!, aonyeshe arrest warrant atasibdikizwa na mtendaji wa mtaa kuja kukukamata.

8. Baada ya polisi kujitambulisha kwa kuonyesha kitambulisho, kitu cha pili ni kuonyesha arrest warrant na kukumbia unakamatwa kwa kutuhumiwa kwa kosa gani?.

9. Polisi kabla hajamkama mtu anatakiwa kumweza haki zake ikiwemo

haki ya kunyamaza kimya, chochote utakachosema kinaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na haki ya kuwakilishwa na mwanasheria.

10. Kisha polisi hao watawaeleza hao mashuhuda wanakupeleka kituo gani ili ndugu zako wakufuatilie!.

Na ukifikishwa kituoni kabla hujaandikishwa maelezo unaaelezwa haki zako ikiwemo haki ya legal representation.

Hitimisho
Haki hizi zikifundishwa kwa wananchi, 'wasiojulikana' watapungua, watabaki tuu wale wa pyu pyu kama wa Lissu.

Sote tunajua kwa kauli na matendo, Rais Samia ana nia thabiti na ya dhati watu wapate haki zao, amekuwa akilihubiri hili kwa maneno na vitendo, na kuanzisha vitendo, kikosi kazi, tume ya haki jinai.

Kwenye kikosi kazi, Watanzania walitaka tufanye mabadiliko madogo ya katiba, minimum reforms ili haki zilizoporwa kinyume cha Katiba zirudishwe, hili Rais Samia hajalitendea haki ila abebadili sheria ya uchaguzi na tume ya uchaguzi kwa mabadiliko kiini macho!.

Watanzania wametaka Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, Rais Samia ameibadilisha jina Tume ya Uchaguzi kutoka NEC na kuiita jina jipya la INEC sasa inaitwa Tume Huru ya Uchaguzi, ila tume bado ni ile ile!. Watanzania hawakuomba jina la Tume ya Uchaguzi libadilishwe kutoka kuitwa Tume ya Uchaguzi na sasa kuitwa Tume Huru ya Uchaguzi, Watanzania walitaka Tume ibadilishwe iwe ni Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi na sio kubadilishwa jina lakini Tume bado ni ile ile, watu bado ni wale wale na uchaguzi utaendelea kusimamiwa na wale wale makada kindakindaki wa chama kimoja kwenye kofia za wakurungezi wa Halmashauri!. Mabadiliko haya ni kiini macho!.

Watanzania walitaka sheria mpya ya uchaguzi yenye kutoa haki sawa kwa wote na uwanja sawa wa uchaguzi, kwasababu sheria ikiyokuwepo ilikuwa ni sheria batili inayokwenda kinyume cha Katiba ya JMT, tumeletewa sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule ulioshabatilishwa na Mahakama Kuu ya Tanzania kwa kwenda kinyume na katiba!, hivyo mabadiliko haya ya sheria ya uchaguzi pia ni mabadiliko kiinimacho!.

Rais Samia, Watanzania tunakupenda, tunakukubali, tunakuomba mahubiri yako ya falsafa yako ya 4R, yasiwe ni mahubiri ?ya maneno maneno tuu,? (preaching only), tunaomba wasisitize watendaji wako watekeleze kwa vitendo (put to practice what you preach)

Mungu Akubariki Uyaweze Yote Katika YEYE!.

Mungu Ibariki Tanzania

Nakutakia Jumapili Njema.
Paskali
 
Makala ni ndefu ila haijamtendea haki Muanzishaji wa Dhana ya 4R.Ikumbukwe kuwa wapo wasioipenda na wasioijali..sasa wewe badala ya kuwasema hao umeamua kumsema mwenye dhana.
Nilitegemea umseme Mwenyekiti,makamu mwenyekiti au katibu wa CDM kwa nini wanajiondoa kwenye hizi 4Rs kadri uchaguzi umapokaribia??
yaani umeweka unafiki na mawani ya mbao dhidi ya hulka zilizooneshwa na CDM.
Makala inakosa muunganiko na Dhana ya 4R.
 
Kwanza nikupongeze kwa andiko.lako. Leo hijaweka link 😁
Ni hivi, sijui ni kwa nini hali inapokuwa mbaya ktk nchi, main strem media humtenga Rais na uozo huo. Ila ukiingia kwenye social media kama JF na X utaona tofauti kubwa sana. Utajua tatizo ni mkuu wa nchi. Kwa nini?
Kama mkuu wa nchi kwa mujibu wa katiba ana absolute power, anashindwa nini kuweka mifumo ya haki kiutendaji? Yeye anateua mawazori, wakurugenzi, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa, wilaya, wakuu wa idara na taasisi, n.k. Ni nonsense KABISA kuendelea kumwonea Rais huruma na kumtenga na uovu wowote. Likitokea jema ni Rais. Likitokea ovu, ni watu wasiomtakia Rais mema.

Boniyai aliandika uchambuzi wake makini mno kuhusu huu upepo unaoendelea wa utekaji na msuaji. Shida ni polisi. Lakini shida zaidi ni wakuu wa idara mbalombali za kipolisi ambapo mteuzi ni Rais. X Mayor kaandika vizuri sana. Sasa pale unaanzaje kumtenga Rais na shida hizi?

Shida nyingine ni nyie wanahabari. Mnajiita mhimili wa nne. Hovyo kabisa. Nyie ndio mlipaswa kuwa kisemeo cha wananchi katika kujua haki zao. Yani ukweli bora angalau niisifu TBC yenye kuonyesha vipindi vya kimaemdeleo. Hii ni kutokana na mkurugenzi wake Dr. Ryoba. Anajitahidi. Sasa nguvu iongezwe kwenye awareness.

Tukija vyombo binsfsi ni changamoto sana. Yani asubuhi ni michezo, mchana michezo, usiku michezo na matangazo ya matapeli wa kidini. Lini watakuwa na vipindi vya kielimu kuhusu haki na wajibu wa kiraia?

Tusifanye kosa la kumsafisha Rais na yanayoendelea. Yeye ni kiongozi wa vyanzo vya haya yote unayoyaongelea
 
Makala ni ndefu ila haijamtendea haki Muanzishaji wa Dhana ya 4R.Ikumbukwe kuwa wapo wasioipenda na wasioijali..sasa wewe badala ya kuwasema hao umeamua kumsema mwenye dhana.
Nilitegemea umseme Mwenyekiti,makamu mwenyekiti au katibu wa CDM kwa nini wanajiondoa kwenye hizi 4Rs kadri uchaguzi umapokaribia??
yaani umeweka unafiki na mawani ya mbao dhidi ya hulka zilizooneshwa na CDM.
Makala inakosa muunganiko na Dhana ya 4R.
Mkuu jingalao, kwanza karibu tena kwenye nyuzi zangu, tumepoteana kitambo!, naamini ule muda wa kubadili jina lako kutoka Jingalao kuwa Akililao ndio sasa.
Mimi nyuzi zangu na deal na issues na sio watu, kitendo cha kusema namsema mtu hapa ni uchonganishi nionekane kama namsema mtu!. No!.

Watu wanataka mabadiliko ya kweli, unapowaita watu mezani mkajadiliana, mkakubaliana, lakini kwenye utekelezaji ukawaletea viini macho, lazima wataondoka kwenye meza ya majadiliano na kurejea mtaani. 4R zisiwe maneno maneno, ziwe vitendo!.
Watu wameomba mabadiliko ya katiba ili kufanya mabadiliko ya sheria, wewe unawaletea mabadiliko ya sheria kiinimacho!.

Watu walitaka mabadiliko ya Tume ya Uchaguzi NEC kuwa Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, wewe unawabadilishia jina kutoka NEC kuwa INEC, tume ile ile, watu wale wale, wasimamizi ni wale wale makada kindakindaki wa chama kimoja chama kubwa kile kile!, hata ungekuwa wewe!, ungefanyaje?. Ungeendelea tuu kukaa mezani?. Msikilize huyu hiki anachosema
View: https://youtu.be/Qa59DIQs2yI jee kina mantiki?.
Huyo ni VC wa chama, baada ya kauli kama hii, Mwenyekiti kiti wake atathubutu kurejea mezani kwenye mazungumzo?.
P
 
Makala ni ndefu ila haijamtendea haki Muanzishaji wa Dhana ya 4R.Ikumbukwe kuwa wapo wasioipenda na wasioijali..sasa wewe badala ya kuwasema hao umeamua kumsema mwenye dhana.
Nilitegemea umseme Mwenyekiti,makamu mwenyekiti au katibu wa CDM kwa nini wanajiondoa kwenye hizi 4Rs kadri uchaguzi umapokaribia??
yaani umeweka unafiki na mawani ya mbao dhidi ya hulka zilizooneshwa na CDM.
Makala inakosa muunganiko na Dhana ya 4R.
4R initiater said once! The noise of abductions are drama! What do you expect? Did Ali Kombo commit suicede?
 
Mr Pascal i can assure you…people will not be happy to read this article especially those who are expected to implement the called 4R!
 
Mkuu jingalao, kwanza karibu tena kwenye nyuzi zangu, tumepoteana kitambo!, naamini ule muda wa kubadili jina lako kutoka Jingalao kuwa Akililao ndio sasa.
Mimi nyuzi zangu na deal na issues na sio watu, kitendo cha kusema namsema mtu hapa ni uchonganishi nionekane kama namsema mtu!. No!.

Watu wanataka mabadiliko ya kweli, unapowaita watu mezani mkajadiliana, mkakubaliana, lakini kwenye utekelezaji ukawaletea viini macho, lazima wataondoka kwenye meza ya majadiliano na kurejea mtaani. 4R zisiwe maneno maneno, ziwe vitendo!.
Watu wameomba mabadiliko ya katiba ili kufanya mabadiliko ya sheria, wewe unawaletea mabadiliko ya sheria kiinimacho!.

Watu walitaka mabadiliko ya Tume ya Uchaguzi NEC kuwa Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, wewe unawabadilishia jina kutoka NEC kuwa INEC, tume ile ile, watu wale wale, wasimamizi ni wale wale makada kindakindaki wa chama kimoja chama kubwa kile kile!, hata ungekuwa wewe!, ungefanyaje?. Ungeendelea tuu kukaa mezani?. Msikilize huyu hiki anachosema
View: https://youtu.be/Qa59DIQs2yI jee kina mantiki?.
Huyo ni VC wa chama, baada ya kauli kama hii, Mwenyekiti kiti wake atathubutu kurejea mezani kwenye mazungumzo?.
P

Narejea maoni yangu kwamba hata kama Mh.Rais Hajatimiza kwa asilimia 90 ya kile kilichotarajiwa sio sahihi kurudi kwenye mifarakano bali ni busara kuendelea na mazungumzo hadi maelewano yapatikane.
Kurejea kwenye maandamano hakutaleta katiba mpya.
 
Shida nyingine ni nyie wanahabari. Mnajiita mhimili wa nne. Hovyo kabisa. Nyie ndio mlipaswa kuwa kisemeo cha wananchi katika kujua haki zao. Yani ukweli bora angalau niisifu TBC yenye kuonyesha vipindi vya kimaemdeleo. Hii ni kutokana na mkurugenzi wake Dr. Ryoba. Anajitahidi. Sasa nguvu iongezwe kwenye awareness.

Tukija vyombo binsfsi ni changamoto sana. Yani asubuhi ni michezo, mchana michezo, usiku michezo na matangazo ya matapeli wa kidini. Lini watakuwa na vipindi vya kielimu kuhusu haki na wajibu wa kiraia?

Tusifanye kosa la kumsafisha Rais na yanayoendelea. Yeye ni kiongozi wa vyanzo vya haya yote unayoyaongelea
Mkuu Raia Fulani, kwanza asante sana kwa objectivity kwenye michango yako humu.
Hili la media nimelipokea na nimelifanyia kazi
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04
P
 
Mr Pascal i can assure you…people will not be happy to read this article especially those who are expected to implement the called 4R!
The media is the Fourth Estate, its function is not to write things that will make leaders happy while the people suffer, but to tell the truth no matter what!.
P
 
4R ni bosheni, kiini macho, hakuna chochote cha maana.

4R lakini wakosoaji wa serikali wanapotea kila siku, sasa hapo kama sio bosheni ni nini?
 
Wanabodi
Hii ni makala yangu ya Kwa Maslahi ya Taifa kwenye Gazeti la NIPASHE la Jumapili ya leo
View attachment 3096028
Kama kawa kila siku za Jumapili hutiririka na makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa
zenye swali hoja majibu utayatoa wewe msomaji mwenyewe.

Swali la leo ni kuhusu haki nchini Tanzania na falsafa ya 4R za Rais Samia, Rais Samia ameibuka na falsafa mpya ya 4R ambayo utekelezaji wake kikamilifu utaidadili kabisa Tanzania kuwa ni nchi ya Haki, Upendo, Ustawi, Mapatano, Maelewano na Maendeleo Endelevu, sasa jee hizi 4R za Samia zinaleta mabadiliko ya kweli au 4R ni mahubiri tuu lakini tukija kwenye utekelezaji ni utekelezaji kiinimacho?.

Watanzania waelimishwe haki zao, 4R za Rais Samia zisiwe ni maneno matupu, jee sasa umefika wakati Watanzania tuombe kuona utekelezaji vitendo au tuendelee kuridhika na haya maneno maneno na utekelezaji viini macho?.

Tumefundishwa kuwa na shukrani, hivyo naianza makala ya leo kwa pongezi na shukrani kwa Rais Samia kwa falsafa yake ya 4R na mahubiri yake mazuri kuhusu haki.

4R ni kifupisho cha maneno ya Kiingereza Reconciliation (Maridhiano), Resilience (Ustahimilivu), Reform (Mabadiliko) na Rebuiding (Kujenga upya).

Makala hii inajikita kwenye R moja tuu ya Mabadiliko, tunataka mabadiliko ya kweli na sio mabadiliko kiinimacho!. Tunawaomba watendaji waitafsiri kwa vitendo falsafa hiyo ya 4R, kwa kutenda kile kinachohubiriwa yasibaki kuwa maneno tuu ya mahubiri ya 4R lakini vitendo ni tofauti!.

Hakuna mashaka kabisa kuhusu nia ya dhati ya Rais kutaka Watanzania kutendewa haki, ana nia njema na thabiti ya dhati Watanzania wapate, haki zao, lakini baadhi ya Watendaji wake ndio wanamuangusha!.

Haki hailetwi kwenye kisahani cha chai, haki ni stahili na stahiki inayopaswa kutolewa bila wewe kuiomba, na ikitokea haki haikutolewa au haikutendeka, haki haiombwi, bali inapaswa kudaiwa, sasa ukiwa mtu hujui haki yako, huwezi kudai kitu usichokijua!

Nikimuangalia na kusikiliza kauli zake kuhusu haki, kusema la ukweli kabisa, Rais Samia, ana nia njema ya dhati kutoka moyoni mwake kuhakikisha Watanzania wanatendewa haki haya mambo ya ajabu ajabu yanayotokea ni uzembe na udhaifu wa baadhi ya watendaji wake, tunamshauri Rais Samia awe mkali kama Nyerere, kwenye ukiukwaji wa haki, ahakikishe hakuna Mswalie Mtume.

Nimekumbushia haki kufuatia kilichotokea hadi kifo cha huyu Mzee Kibao wa Chadema, ameuliwa kwasababu wananchi hawajui haki zao!. Kama Watanzania wangekuwa wanajua haki zao Mzee Kibao asingekubali kukamatwa na watu ambao hawatambuliki.

1. Kama Watanzania wangekuwa wanajua haki zao, dereva wa basi la Tashrif asinge kubali kusimamishwa na watu wasiotambulika.

2. Kama Watanzania wangekuwa wanajua haki zao, dereva wa Tashrif angekuwa anajua ile tiketi ya abiria, ni mkataba wa kisheria wa kumshusha abiria wake kituo alicholipia, dereva ana wajibu wa kisheria, duty of care, kuhakikisha usalama wa abiria wake na mali zake kwenye butt ya gari yake!. Mali pekee ambayo ni responsibility ya abiria ni mzigo wake wa mkononi, hand luggage anaoingia nao ndani ya basi, ndio "abiria chunga mzigo wako" lakini jukumu la abiria kufika salama anapokwenda, dereva wa basi ana wajibu wa kisheria kumfikisha salama.

3. Watanzania wangekuwa wanajua haki zao, abiria tuu wa kawaida akiwemo abiria aliyekaa seat no. 1 ya basi hilo ambaye ni traffic police, alikuwa na uwezo wa kuwabaini majambazi hao kuwa sio askari polisi wa kweli na kuwahamasisha abiria wengine wote wasikubali abiria mwenzao atekwe!.

4. Watanzania wangezijua haki zao, wangejua Polisi haruhusiwi kumkamata mtu yoyote bila kwanza kujitambulisha yeye ni nani na ametokea kituo gani kwa kuonyesha kitambulisho cha polisi.

5. Watanzania wangejua haki zao, wangejua mtu anayekamatwa ana haki ya kusoma number ya kitambulisho na kuihakiki number ya askari police kwenye mfuko wa kushoto wa nguo ya polisi.

6. Wakija polisi ambao ni askari kanzu, hawa hawana uniform hivyo hawavai numbers, hawaruhusiwi kumkamata mtuhumiwa bila kuandamana na polisi wenye uniforms!.

7. Mtu yeyote kabla hajakamatwa lazima awe na arrest warrant na lazima aripoti ofisi ya serikali ya mtaa husika!, aonyeshe arrest warrant atasibdikizwa na mtendaji wa mtaa kuja kukukamata.

8. Baada ya polisi kujitambulisha kwa kuonyesha kitambulisho, kitu cha pili ni kuonyesha arrest warrant na kukumbia unakamatwa kwa kutuhumiwa kwa kosa gani?.

9. Polisi kabla hajamkama mtu anatakiwa kumweza haki zake ikiwemo

haki ya kunyamaza kimya, chochote utakachosema kinaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na haki ya kuwakilishwa na mwanasheria.

10. Kisha polisi hao watawaeleza hao mashuhuda wanakupeleka kituo gani ili ndugu zako wakufuatilie!.

Na ukifikishwa kituoni kabla hujaandikishwa maelezo unaaelezwa haki zako ikiwemo haki ya legal representation.

Hitimisho
Haki hizi zikifundishwa kwa wananchi, 'wasiojulikana' watapungua, watabaki tuu wale wa pyu pyu kama wa Lissu.

Sote tunajua kwa kauli na matendo, Rais Samia ana nia thabiti na ya dhati watu wapate haki zao, amekuwa akilihubiri hili kwa maneno na vitendo, na kuanzisha vitendo, kikosi kazi, tume ya haki jinai.

Kwenye kikosi kazi, Watanzania walitaka tufanye mabadiliko madogo ya katiba, minimum reforms ili haki zilizoporwa kinyume cha Katiba zirudishwe, hili Rais Samia hajalitendea haki ila abebadili sheria ya uchaguzi na tume ya uchaguzi kwa mabadiliko kiini macho!.

Watanzania wametaka Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, Rais Samia ameibadilisha jina Tume ya Uchaguzi kutoka NEC na kuiita jina jipya la INEC sasa inaitwa Tume Huru ya Uchaguzi, ila tume bado ni ile ile!. Watanzania hawakuomba jina la Tume ya Uchaguzi libadilishwe kutoka kuitwa Tume ya Uchaguzi na sasa kuitwa Tume Huru ya Uchaguzi, Watanzania walitaka Tume ibadilishwe iwe ni Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi na sio kubadilishwa jina lakini Tume bado ni ile ile, watu bado ni wale wale na uchaguzi utaendelea kusimamiwa na wale wale makada kindakindaki wa chama kimoja kwenye kofia za wakurungezi wa Halmashauri!. Mabadiliko haya ni kiini macho!.

Watanzania walitaka sheria mpya ya uchaguzi yenye kutoa haki sawa kwa wote na uwanja sawa wa uchaguzi, kwasababu sheria ikiyokuwepo ilikuwa ni sheria batili inayokwenda kinyume cha Katiba ya JMT, tumeletewa sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule ulioshabatilishwa na Mahakama Kuu ya Tanzania kwa kwenda kinyume na katiba!, hivyo mabadiliko haya ya sheria ya uchaguzi pia ni mabadiliko kiinimacho!.

Rais Samia, Watanzania tunakupenda, tunakukubali, tunakuomba mahubiri yako ya falsafa yako ya 4R, yasiwe ni mahubiri ?ya maneno maneno tuu,? (preaching only), tunaomba wasisitize watendaji wako watekeleze kwa vitendo (put to practice what you preach)

Mungu Akubariki Uyaweze Yote Katika YEYE!.

Mungu Ibariki Tanzania

Nakutakia Jumapili Njema.
Paskali

Pascal, unataka kusema nini haswa?
 
4R ni kifupisho cha maneno ya Kiingereza Reconciliation (Maridhiano), Resilience (Ustahimilivu), Reform (Mabadiliko) na Rebuiding (Kujenga upya).
Hivi hizi 4R zilenga watendaji wa Serikali, za wanasiasa, za wakulima, za wafanyakazi sekta binafsi, wananchi ?

Au hizi 4R ni za watumishi wa Umma dhidi ya viongozi wa Umma, ama hizi ni za wanachama wa vyama vya siasa dhidi ya viongozi wa vyama hivyo vya siasa, ama za wakulima dhidi ya viongozi wa vyama vyao vya ushirika(Amcos), ama ni za wafanyakazi sekta binafsi dhidi ya viongozi wa sektA hiyo binafsi, ama ni za wananchi dhidi ya serikali?

Au hizi 4R ni za baina ya kati ya Chama cha siasa na Chama kingine, ama ni za baina ya Chama cha siasa na serikali, ama ni baina ya wafanyabiashara na TRA na walaji wa bidhaa za soko.... nakadhalika nakadhalika???

Maswali yangu haya, binafsi, nayaona ni muhimu Sana kujibiwa ili tuweke sawa mjadala wa kujua kama 4R hizi ni mabadiliko ya kweli ama kiini macho.

Asante sana kwa kunielewa kama ufanyavyo siku zote
 
Narejea maoni yangu kwamba hata kama Mh.Rais Hajatimiza kwa asilimia 90 ya kile kilichotarajiwa sio sahihi kurudi kwenye mifarakano bali ni busara kuendelea na mazungumzo hadi maelewano yapatikane.
Kurejea kwenye maandamano hakutaleta katiba mpya.
Siku zote madajiliano ya mazungumzo ya maridhiano yanakuwa based on trust, truthfulness and the spirit of reconciliation with give and take, a win win situation.

Serikali ya CCM ndio the winner who took it all, na wapinzani are the loosers standing small.

The role of leadership in such situation is having a vision tunataka kujenga Tanzania gani, hivyo falsafa ya 4R ndio vision ya Rais Samia, mtekelezaji sio yeye ni wasaidizi wake, hivyo hao wasaidizi wanapaswa to implement the vision of their visionary leader.
Rais ameunda kikosi kazi, kimewasikiliza wananchi wanataka nini, kikamletea mapendekezo wananchi wanataka katiba mpya, au mabadiliko madogo ya katiba, minimum reforms, Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi na sheria mpya ya uchaguzi ili uchunguzi uwe huru na wa haki.

Wasaidizi wake wamemtungia sheria batili na kutuletea kiinimacho the Tume Huru ya Uchaguzi!.

Mkikaa na watu mezani mkakubaliana, kisha kwenye utekelezaji ukawabadilikia kwa kuwaletea kitu tofauti, it's a breach of trust, hakuna atakayekubali kurejea mezani!.

A best way forward ni bado hajachelewa to do the right thing!.
P
 
Siku zote madajiliano ya mazungumzo ya maridhiano yanakuwa based on trust, truthfulness and the spirit of reconciliation with give and take, a win win situation.

Serikali ya CCM ndio the winner who took it all, na wapinzani are the loosers standing small.

The role of leadership in such situation is having a vision tunataka kujenga Tanzania gani, hivyo falsafa ya 4R ndio vision ya Rais Samia, mtekelezaji sio yeye ni wasaidizi wake, hivyo hao wasaidizi wanapaswa to implement the vision of their visionary leader.
Rais ameunda kikosi kazi, kimewasikiliza wananchi wanataka nini, kikamletea mapendekezo wananchi wanataka katiba mpya, au mabadiliko madogo ya katiba, minimum reforms, Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi na sheria mpya ya uchaguzi ili uchunguzi uwe huru na wa haki.

Wasaidizi wake wamemtungia sheria batili na kutuletea kiinimacho the Tume Huru ya Uchaguzi!.

Mkikaa na watu mezani mkakubaliana, kisha kwenye utekelezaji ukawabadilikia kwa kuwaletea kitu tofauti, it's a breach of trust, hakuna atakayekubali kurejea mezani!.

A best way forward ni bado hajachelewa to do the right thing!.
P
Inawezekana kikosi kazi kilipata maoni ya wanasiasa na si wananchi haswa.

Bado sio haki kwa wapinzani kushinikiza tena kwa kutumia njia zile zile zilizowahi kutumika miaka yote...yaani kutengeneza kelele na kuzipeleka kwenye senate ya Marekani ili tunyimwe misaada.
 
Makala ni ndefu ila haijamtendea haki Muanzishaji wa Dhana ya 4R.Ikumbukwe kuwa wapo wasioipenda na wasioijali..sasa wewe badala ya kuwasema hao umeamua kumsema mwenye dhana.
Nilitegemea umseme Mwenyekiti,makamu mwenyekiti au katibu wa CDM kwa nini wanajiondoa kwenye hizi 4Rs kadri uchaguzi umapokaribia??
yaani umeweka unafiki na mawani ya mbao dhidi ya hulka zilizooneshwa na CDM.
Makala inakosa muunganiko na Dhana ya 4R.
Samia hana cha 4R, alidhani ataweza kudanganya, Kashindwa kirahisi sana
 
.....yote...yaani kutengeneza kelele na kuzipeleka kwenye senate ya Marekani ili tunyimwe misaada.
Wapinzani wanaamua kuwaadhibu wananchi wakati wa uchaguzi wanakuja kuwaomba kura wawaweke madarakani, halafu wanalalamika eti wameibiwa kura! Hivi wanatuonaje sisi?

Ndiyo, maana wakati najadili kwenye uzi mwingine niliuliza kama vyama hivi vya siasa kwa maana ya Taasisi ya kisiasa iliwahi kuitisha maandamano ya kuwashinikiza serikali ikubali ushauri iliopewa na Taasisi ya kisiasa juu ya masuala ya uchumi, teknolojia diplomasi na kadhalika ambao ushauri huo ungeweza kusaidia wananchi kujikwamua kiuchumi?
====
Kumradhi Ndugu Pascal kwa kutoka Nje ya mada nilitaka tu kujazia point ya Ndugu yetu jingalao. Tuendelee na mjadala uliopo mezani.
 
Back
Top Bottom