HAKI ya kuchagua, iende sambamba na HAKI ya kumfuta KAZI kiongozi niliyemchagua, nawezaje kumfuta KAZI mbunge wangu?

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam, Shalom!!

Tulipoitwa katika mikutano ya Kutoa maoni kuhusu Katiba mpya Awamu ya nne, Ndugu Samia SH, alikuwa mjumbe wa Tume hiyo.

Moja kati ya maoni muhimu ya wananchi ,tulitaka ipatikane namna ya kuwafuta KAZI wabunge wetu wasio na uwezo kuongoza, tulitaka pia uwepo ukomo wa ubunge iwe Awamu Moja tu.

Swali; Nawezaje kumfuta KAZI mbunge wangu ambaye haonekani bungeni, Wala jimboni haonekani, amehamishia makazi mjini, anatamba kuwa akija na pesa atachaguliwa tu, tupende tusipende?

Karibuni.
 
Katiba yetu hii ya sasa haina check & balance - na ndiyo maana Rais wetu anakopa atakavyo sisi wanachi hatuwezi kumfanya lolote same as wabunge na madiwani.

Na ndiyo maana katiba mpya inahitajika leo, watanganyika amkeni acheni u CCM nchi inaondoka hii mtashtuka yamebaki mabua.
 
Rasimu aliyosimamia Judge Warioba irudi mezani, yafanyike marekebisho kidogo, hatimaye tupate tume HURU ya UCHAGUZI na KATIBA mpya kabla ya Uchaguzi wowote.
Ccm kamwe hawawezi kukubali kwa hiari pendekezo hili. Kwasabb wanajua wataondoka asubuhi na mapema.
 
Tunataka ipatikane namna kikatiba hata Rais afukuzwe KAZI ikitokea ameshindwa kutimiza WAJIBU wake ipasavyo.
 
Ccm kamwe hawawezi kukubali kwa hiari pendekezo hili. Kwasabb wanajua wataondoka asubuhi na mapema.
Sisi ndio bosses wao, tusimame katika nafasi yetu na kujitambua.

Inawezekana kupata Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote.
 
Rasimu ya judge Warioba ilitoa mwanya huo adhimu wa kumfuta KAZI mbunge akiwa ndani ya utumishi.

Sasa kwanini wanakalia maoni ya wananchi?

Si sawa kukalia Rasimu ya Katiba ya wananchi ilhali viti vyenye sponge murua vipo!!
 
Rasimu ya judge Warioba ilitoa mwanya huo adhimu wa kumfuta KAZI mbunge akiwa ndani ya utumishi.

Sasa kwanini wanakalia maoni ya wananchi?

Si sawa kukalia Rasimu ya Katiba ya wananchi ilhali viti vyenye sponge murua vipo!!
Mwanasiasa yupo pale kuhakikisha anabaki madarakani.
 
Tunalima pia mkuu
Kuna Rafiki yangu Huwa nashauri aachane na utapeli huu hanielewwi,

Yeye ni mwalimu by profession, Mimi ni kiongozi wa Biashara Kwa profession, nikimwambia Afanye vitu halisi haelewi,

Ameshapigwa vya kutosha, saiz ananiambia Eti ana Maarifa ya kutosha, nimpe pesa azalishe.

Nikimuuliza wewe kwanini zako huzalishi ukawa bilionea, anasema nina dharau.
 
Kuna mambo mengine unaachana nayo. Ushasikia nchi gani duniani Mbunge anaondolewa Ubunge kisa hachangii Bungeni? Acheni ushamba!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…