Hakukuwa na sababu ya Profesa Mkenda kuzungumza aliyoyazungumza hadharani. Kiongozi ni kuwa na Kifua na Uvumilivu

Hakukuwa na sababu ya Profesa Mkenda kuzungumza aliyoyazungumza hadharani. Kiongozi ni kuwa na Kifua na Uvumilivu

Mimi ni akili kubwa ambazo ni sawa na ukoo wako wote kwa pamoja na bado hamnifikii.
mind is infinite potential, huwezi kuunganisha akili za watu wawili alafu ukawa sawa, ndio maana nakwambia wewe ni kichaa, kuna jamaa hapo juu kakwambia hao unaowasifia wakitaka kuwekwa utasema utiwe wewe na ndio unachifanyiwa
 
Vipi mbona na wewe hukupaswa kuyasema haya??
Au wayaona tu ya wenzako kwenye mapambano yao??
 
mind is infinite potential, huwezi kuunganisha akili za watu wawili alafu ukawa sawa, ndio maana nakwambia wewe ni kichaa, kuna jamaa hapo juu kakwambia hao unaowasifia wakitaka kuwekwa utasema utiwe wewe na ndio unachifanyiwa
Ukoo wako wote na upeo wako wote hamuwezi kunifikia mimi mmoja.
 
Tangia lini machizi nao wakawa na uwezo wa kumiliki makampuni?
Na ndiyo maana mimi siyo chawa kama wewe maisha yamekushinda umeona njia ya kujikimu ni kuwa chawa. Kampuni yangu naajiri watu wanaotumia akili kufikiri ungekuwa na sifa hizo ningekustiri uachanane na huo ujuha unaofanya kumsifia mtu ambaye hata ukipita mbele yake anakutema mate. Unatumika kiboya sana.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Sote tumeyasikia maneno na kauli za Waziri wa Elimu Mheshimiwa Profesa Adolph Mkenda akilalamika kuwa alizungushwa kupata nafasi ya kuonana na Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Mimi Mwashambwa nimejiuliza maswali ya je kulikuwa na sababu zipi za kuyaongea hayo masuala hadharani? Yalikuwa na umuhimu upi na sababu zipi? Alishindwa nini kuyaongea faragha alipopata nafasi ya kuongea na kuonana na Mheshimiwa Rais?

Je waziri hana njia nyingine za kuwasiliana na kufikisha ujumbe wake kwa Rais? Je waziri hawezi kuwasilisha jambo hilo kwenye kikao cha Baraza la mawaziri na kutoa dukuduku lake na kero yake ili mambo yazungumzwe na kuonyana humo humo badala ya kuleta hadharani?

Juu ya Waziri Wa Elimu kuna Naibu Waziri Mkuu, Waziri Mkuu ,Makamu wa Rais kabla ya kumfikia Rais Mwenyewe. Sasa kwanini asingemtumia hata mmoja wapo kati ya hao kupeleka jambo lake na kero yake hiyo?

Hata alipopelekewa kikaratasi mezani kwake kwanini na kulikuwa na sababu gani ya kujibu kwa jeuri kuwa yale aliyokuwa anayaongea yalikuwa ni Sehemu ya hotuba yake? Kwanini alikuwa anaonyesha kana kwamba yupo kwenye mgogoro na wasaidizi wa Rais na sasa anataka kuwachongea na kutunishiana misuli hadharani? Yalikuwa na sababu gani hadi ya kusema kuwa tuliambiwa tuongee kwa saa mbili tu?

Kwanini Waziri ambaye ni Profesa kabisa anakosa kifua na uvumilivu pamoja na subira ya mambo madogo kama hayo? Kama jambo dogo kama hilo linamshinda kuvumilia na kukaa kimya bila kuonyesha hasira zake hadharani,anaweza vipi vumilia mambo makubwa na kukaa nayo mpaka anaingia kaburini? Unapokuwa kiongozi mkubwa ni pamoja na kubeba maumivu na kutunza siri kwa gharama kubwa na Maumivu.

Hivi kama Rais Samia Mama yetu kipenzi asingekuwa na kifua na uvumilivu na kuamua kuzungumza kila kitu hadharani. Unafikiri angezungumza mangapi mazito baada ya kuapishwa kwake kuwa Rais? Au mmesahau ni nini Mkuu wa Majeshi wetu mstaafu Mheshimiwa Jenerali Venance Mabeyo alichokisema na kilichotokea baada ya kifo cha Hayati Mwalimu Daktari John Pombe Joseph Magufuli?

Mmesahau Kauli ya Jenerali Mabeyo kuwa kuna watu walisahau katiba inasema nini na kwamba akawakumbusha Matakwa ya Katiba mara baada ya kufa kwa Rais? Hivi mnaichukuliaje kauli hiyo? Mnaelewa Maana yake? Mnataka niwafungulie mabano ili muelewe?

Je mnafikiri watu hao waliosahau matakwa ya katiba Hawapo hai? Mnafikiri hawapo Tanzania? Mnafikiri hawapo serikalini?? Mnafikiri Mama yetu Mpendwa hawafahamu? Mnafikiri Mama yetu kipenzi hafahamu kilichotokea baada ya kifo cha Hayati? Au mnafikiri amekaa kimya kwa sababu hajui kitu?

Jibu ni kuwa anafahamu kila kitu na ameamua kukaa kimya na kuendelea na kazi kwa sababu anajua maana ya uongozi. anajua maana ya kutunza siri. Anajua Ukubwa ni jalala. Anajua jambo gani linapaswa kuzungumzwa hadharani na lipi halipaswi kuzungumzwa hadharani. Anajua kuna mambo yanapaswa kukaa kifuani na kubakia kama siri mpaka Kifo.

Na huo ndio uongozi. Ndio Ukubwa.Ndio uongozi unavyotaka hivyo kwa kiongozi wa juu kuwa na kifua ,kutunza siri,kuwa na subira, uvumilivu na kujizuia kuongea vitu kwa msukumo wa hasira,jazba, mihemuko na kukurupuka. Kama Rais Samia angetaka kuongea kila kitu hadharani basi Nchi ingesimama. Nasema tena kuwa NCHI ingesimama hii.

Viongozi wetu jifunzeni kuwa na siri,vifua, uvumilivu na subira. Tumieni busara na hekima katika kuzungumza hadharani na chagueni maneno ya kuzungumza mbele ya hadhira. Na ikiwezekana someni hotuba mlizoandaliwa kuliko kutumia hisia bila mantiki kuzungumza na kujikuta mkiharibu na kuleta taswira mbaya kwa jamii .

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
wewe ungekuwa ndugu yangu ningemshauri baba yako abadilishane na paka uko geita watu wakuchimbie madini huna faida kama mwanadamu
 
Ndugu zangu Watanzania,

Sote tumeyasikia maneno na kauli za Waziri wa Elimu Mheshimiwa Profesa Adolph Mkenda akilalamika kuwa alizungushwa kupata nafasi ya kuonana na Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Mimi Mwashambwa nimejiuliza maswali ya je kulikuwa na sababu zipi za kuyaongea hayo masuala hadharani? Yalikuwa na umuhimu upi na sababu zipi? Alishindwa nini kuyaongea faragha alipopata nafasi ya kuongea na kuonana na Mheshimiwa Rais?

Je waziri hana njia nyingine za kuwasiliana na kufikisha ujumbe wake kwa Rais? Je waziri hawezi kuwasilisha jambo hilo kwenye kikao cha Baraza la mawaziri na kutoa dukuduku lake na kero yake ili mambo yazungumzwe na kuonyana humo humo badala ya kuleta hadharani?

Juu ya Waziri Wa Elimu kuna Naibu Waziri Mkuu, Waziri Mkuu ,Makamu wa Rais kabla ya kumfikia Rais Mwenyewe. Sasa kwanini asingemtumia hata mmoja wapo kati ya hao kupeleka jambo lake na kero yake hiyo?

Hata alipopelekewa kikaratasi mezani kwake kwanini na kulikuwa na sababu gani ya kujibu kwa jeuri kuwa yale aliyokuwa anayaongea yalikuwa ni Sehemu ya hotuba yake? Kwanini alikuwa anaonyesha kana kwamba yupo kwenye mgogoro na wasaidizi wa Rais na sasa anataka kuwachongea na kutunishiana misuli hadharani? Yalikuwa na sababu gani hadi ya kusema kuwa tuliambiwa tuongee kwa saa mbili tu?

Kwanini Waziri ambaye ni Profesa kabisa anakosa kifua na uvumilivu pamoja na subira ya mambo madogo kama hayo? Kama jambo dogo kama hilo linamshinda kuvumilia na kukaa kimya bila kuonyesha hasira zake hadharani,anaweza vipi vumilia mambo makubwa na kukaa nayo mpaka anaingia kaburini? Unapokuwa kiongozi mkubwa ni pamoja na kubeba maumivu na kutunza siri kwa gharama kubwa na Maumivu.

Hivi kama Rais Samia Mama yetu kipenzi asingekuwa na kifua na uvumilivu na kuamua kuzungumza kila kitu hadharani. Unafikiri angezungumza mangapi mazito baada ya kuapishwa kwake kuwa Rais? Au mmesahau ni nini Mkuu wa Majeshi wetu mstaafu Mheshimiwa Jenerali Venance Mabeyo alichokisema na kilichotokea baada ya kifo cha Hayati Mwalimu Daktari John Pombe Joseph Magufuli?

Mmesahau Kauli ya Jenerali Mabeyo kuwa kuna watu walisahau katiba inasema nini na kwamba akawakumbusha Matakwa ya Katiba mara baada ya kufa kwa Rais? Hivi mnaichukuliaje kauli hiyo? Mnaelewa Maana yake? Mnataka niwafungulie mabano ili muelewe?

Je mnafikiri watu hao waliosahau matakwa ya katiba Hawapo hai? Mnafikiri hawapo Tanzania? Mnafikiri hawapo serikalini?? Mnafikiri Mama yetu Mpendwa hawafahamu? Mnafikiri Mama yetu kipenzi hafahamu kilichotokea baada ya kifo cha Hayati? Au mnafikiri amekaa kimya kwa sababu hajui kitu?

Jibu ni kuwa anafahamu kila kitu na ameamua kukaa kimya na kuendelea na kazi kwa sababu anajua maana ya uongozi. anajua maana ya kutunza siri. Anajua Ukubwa ni jalala. Anajua jambo gani linapaswa kuzungumzwa hadharani na lipi halipaswi kuzungumzwa hadharani. Anajua kuna mambo yanapaswa kukaa kifuani na kubakia kama siri mpaka Kifo.

Na huo ndio uongozi. Ndio Ukubwa.Ndio uongozi unavyotaka hivyo kwa kiongozi wa juu kuwa na kifua ,kutunza siri,kuwa na subira, uvumilivu na kujizuia kuongea vitu kwa msukumo wa hasira,jazba, mihemuko na kukurupuka. Kama Rais Samia angetaka kuongea kila kitu hadharani basi Nchi ingesimama. Nasema tena kuwa NCHI ingesimama hii.

Viongozi wetu jifunzeni kuwa na siri,vifua, uvumilivu na subira. Tumieni busara na hekima katika kuzungumza hadharani na chagueni maneno ya kuzungumza mbele ya hadhira. Na ikiwezekana someni hotuba mlizoandaliwa kuliko kutumia hisia bila mantiki kuzungumza na kujikuta mkiharibu na kuleta taswira mbaya kwa jamii .

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Hao wote ni walewale tu. Yeye Rais anashindwa nini kuwashughulikia na hata kuwatia kizuizini wahaini waliotaka kumzingira na kumpora madaraka yake ya kikatiba?
 
Siyo kweli. Unakumbuka kuna siku Rais alieleza namna ambavyo Mheshimiwa Waziri wa Fedha alivyokuwa akimpigia simu Mheshimiwa Rais kumueleza baadhi ya mambo? Huoni kuwa hapo inaonyesha wazi kuwa waziri anaweza hata kumpigia simu Mheshimiwa Rais?
This logical fallacy is called non sequitur.

Kwani rais hawezi kuwa anampa priority waziri wa fedha lakini anampotezea Mkenda?

Vyovyote utakavyoliangalia hiki rais ana makosa, hayupo accessibke kwa wqziri wake mpaka waziri kamshitaki kwa wananchi.

Au kama yupo accessible basi kateua waziri mjinga sana ambaye anamshitaki rais kwa wananchi bila sababu.

Yote ni makosa ya rais hayo. Rais wako haepuki lawama hapo.
 
This logical fallacy is called non sequitur.

Kwani rais hawezi kuwa anampa priority waziri wa fedha lakini anampotezea Mkenda?

Vyovyote utakavyoliangalia hiki rais ana makosa, hayupo accessibke kwa wqziri wake mpaka waziri kamshitaki kwa wananchi.

Au kama yupo accessible basi kateua waziri mjinga sana ambaye anamshitaki rais kwa wananchi bila sababu.

Yote ni makosa ya rais hayo. Rais wako haepuki lawama hapo.
Mawaziri wote ni sawa na wana hadhi sawa na wanaweza kuwasiliana na Rais wakati wowote ule.
 
Back
Top Bottom