Hakukuwa na sababu ya Profesa Mkenda kuzungumza aliyoyazungumza hadharani. Kiongozi ni kuwa na Kifua na Uvumilivu

Hakukuwa na sababu ya Profesa Mkenda kuzungumza aliyoyazungumza hadharani. Kiongozi ni kuwa na Kifua na Uvumilivu

Ndugu zangu Watanzania,

Sote tumeyasikia maneno na kauli za Waziri wa Elimu Mheshimiwa Profesa Adolph Mkenda akilalamika kuwa alizungushwa kupata nafasi ya kuonana na Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Mimi Mwashambwa nimejiuliza maswali ya je kulikuwa na sababu zipi za kuyaongea hayo masuala hadharani? Yalikuwa na umuhimu upi na sababu zipi? Alishindwa nini kuyaongea faragha alipopata nafasi ya kuongea na kuonana na Mheshimiwa Rais?

Je waziri hana njia nyingine za kuwasiliana na kufikisha ujumbe wake kwa Rais? Je waziri hawezi kuwasilisha jambo hilo kwenye kikao cha Baraza la mawaziri na kutoa dukuduku lake na kero yake ili mambo yazungumzwe na kuonyana humo humo badala ya kuleta hadharani?

Pia soma:
Juu ya Waziri Wa Elimu kuna Naibu Waziri Mkuu, Waziri Mkuu ,Makamu wa Rais kabla ya kumfikia Rais Mwenyewe. Sasa kwanini asingemtumia hata mmoja wapo kati ya hao kupeleka jambo lake na kero yake hiyo?

Hata alipopelekewa kikaratasi mezani kwake kwanini na kulikuwa na sababu gani ya kujibu kwa jeuri kuwa yale aliyokuwa anayaongea yalikuwa ni Sehemu ya hotuba yake? Kwanini alikuwa anaonyesha kana kwamba yupo kwenye mgogoro na wasaidizi wa Rais na sasa anataka kuwachongea na kutunishiana misuli hadharani? Yalikuwa na sababu gani hadi ya kusema kuwa tuliambiwa tuongee kwa saa mbili tu?

Kwanini Waziri ambaye ni Profesa kabisa anakosa kifua na uvumilivu pamoja na subira ya mambo madogo kama hayo? Kama jambo dogo kama hilo linamshinda kuvumilia na kukaa kimya bila kuonyesha hasira zake hadharani,anaweza vipi vumilia mambo makubwa na kukaa nayo mpaka anaingia kaburini? Unapokuwa kiongozi mkubwa ni pamoja na kubeba maumivu na kutunza siri kwa gharama kubwa na Maumivu.

Hivi kama Rais Samia Mama yetu kipenzi asingekuwa na kifua na uvumilivu na kuamua kuzungumza kila kitu hadharani. Unafikiri angezungumza mangapi mazito baada ya kuapishwa kwake kuwa Rais? Au mmesahau ni nini Mkuu wa Majeshi wetu mstaafu Mheshimiwa Jenerali Venance Mabeyo alichokisema na kilichotokea baada ya kifo cha Hayati Mwalimu Daktari John Pombe Joseph Magufuli?

Mmesahau Kauli ya Jenerali Mabeyo kuwa kuna watu walisahau katiba inasema nini na kwamba akawakumbusha Matakwa ya Katiba mara baada ya kufa kwa Rais? Hivi mnaichukuliaje kauli hiyo? Mnaelewa Maana yake? Mnataka niwafungulie mabano ili muelewe?

Je mnafikiri watu hao waliosahau matakwa ya katiba Hawapo hai? Mnafikiri hawapo Tanzania? Mnafikiri hawapo serikalini?? Mnafikiri Mama yetu Mpendwa hawafahamu? Mnafikiri Mama yetu kipenzi hafahamu kilichotokea baada ya kifo cha Hayati? Au mnafikiri amekaa kimya kwa sababu hajui kitu?

Jibu ni kuwa anafahamu kila kitu na ameamua kukaa kimya na kuendelea na kazi kwa sababu anajua maana ya uongozi. anajua maana ya kutunza siri. Anajua Ukubwa ni jalala. Anajua jambo gani linapaswa kuzungumzwa hadharani na lipi halipaswi kuzungumzwa hadharani. Anajua kuna mambo yanapaswa kukaa kifuani na kubakia kama siri mpaka Kifo.

Na huo ndio uongozi. Ndio Ukubwa.Ndio uongozi unavyotaka hivyo kwa kiongozi wa juu kuwa na kifua ,kutunza siri,kuwa na subira, uvumilivu na kujizuia kuongea vitu kwa msukumo wa hasira,jazba, mihemuko na kukurupuka. Kama Rais Samia angetaka kuongea kila kitu hadharani basi Nchi ingesimama. Nasema tena kuwa NCHI ingesimama hii.

Viongozi wetu jifunzeni kuwa na siri,vifua, uvumilivu na subira. Tumieni busara na hekima katika kuzungumza hadharani na chagueni maneno ya kuzungumza mbele ya hadhira. Na ikiwezekana someni hotuba mlizoandaliwa kuliko kutumia hisia bila mantiki kuzungumza na kujikuta mkiharibu na kuleta taswira mbaya kwa jamii .

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kaonyesha umma wa Wanzania kuwa Rais amekuwa ni wa watu fulani tu.
Ikiwa waziri ni ngumu kumuona, usitegemee raia wa kawaida atakufikiria kwa lolote.
Kama mteule wake anafanyiwa hivyo basi tujue nchi haiko salama.
 
Pale jamaa mwenye elimu ya hapa na pale anapompa lekcha mtu mwenye digrii nne, mwalimu wa vyuo vikuu mbalimbali nchini na nje ya nchi,waziri wa elimu hapa Tanzania.
Kwa hiyo wewe kwa akili yako hiyo hiyo uliyonayo unaamini kuwa mtu akiwa Profesa anakuwa kama Mungu mtu? Anakuwa Alfa na omega? Anakuwa na akili nyingi kupita wote ndani ya Taifa na hata nje? Anakuwa hawezi kukosea? Anakuwa malaika atembeaye Duniani? Anakuwa mtakatifu asiyekosea wala kutakiwa kusahihishwa? Anakuwa wa kuabudiwa na kupewa sifa?
 
..Prof.Mkenda hakukosea ktk kauli yake.

..Nilichogundua ni kwamba Prof ni mmoja kati ya mawaziri wanaopima kauli zao kabla hawajazungumza.

..hebu kaleta hotuba ya Prof ili wasomaji waone kama kuna ulazima wa makelele yote haya.
Kiuongozi alichokifanya Mheshimiwa Waziri siyo sahihi hata kidogo
 
Kiuongozi alichokifanya Mheshimiwa Waziri siyo sahihi hata kidogo

..hakukosea chochote kile.

..nenda kasikilize hotuba yake.

..infact Prof amemzungumzia Rais vizuri sana.

..tatizo CCM mmezoea kupotosha sasa imefika wakati Watanzania wanaamini jambo la uongo kuliko ukweli.

..hili ni tatizo mmelilea CCM sasa imefika mahali Watanzania wamekuwa wagumu kufanya tafakuri za kina, na wepesi mno kupotoshwa.
 
Kati yako wewe na Profesa Mkenda unafikiri akiongea kwenye hadhara nani atasikilizwa?

Profesa kaongea ukweli na ndio hali aliyopitia na huyo mama yako alikuwepo pale kasikiliza hakuongea chochote kama hizi sarakasi unazoleta hapa.

Kwa kukusaidia sio kila kitu kinaongelewa kwenye simu kama unavyodhani, utatoaje wasilisho lenye takwimu ,michoro, jedwali kwenye simu ?

Sasa nashangaa wabeba mabango kama wewe ndio mnaumizwa kwa waziri kuongea ukweli alipozuiliwa kutoa wasilisho lake.

Taaluma na UCHAWA havikai sehemu moja .

Profesa Mkenda apongezwe na mchawa na vidampa wapuuzwe.
 
Najua huna uwezo wa kujibu hoja zangu.
Wewe mpuuzi kweli kweli yaani naianzishe kampuni inayojiendesha kwa faida halafu nisijue maana ya kampuni, na hiyo ndiyo unaita hoja? Nimeshapata jibu kwa nini hupati uteuzi,watu wamekufanyia vetting wakaona hutoshi,kwa akili hizi hata mimi siwezi kukupa ajira.
 
..hakukosea chochote kile.

..nenda kasikilize hotuba yake.

..infact Prof amemzungumzia Rais vizuri sana.

..tatizo CCM mmezoea kupotosha sasa imefika wakati Watanzania wanaamini jambo la uongo kuliko ukweli.

..hili ni tatizo mmelilea CCM sasa imefika mahali Watanzania wamekuwa wagumu kufanya tafakuri za kina, na wepesi mno kupotoshwa.
Uko sahihi kabisa imagine huyu kapuku Lucas Mwashambwa anayejigamba ni msomi wa chuo kikuu lakini ameweza kupotosha kiasi hiki, sasa hao wa form IV iatakuwaje,CCM ina hazina kubwa sana ya wapumbavu na majuha kama huyu mpotoshaji na chawa wa Samia Lucas Mwashambwa.
 
Kiuongozi alichokifanya Mheshimiwa Waziri siyo sahihi hata kidogo
Yuko sahihi 100% ila akili yako ya sisimizi imeshindwa kuelewa alichosema ndiyo umekuja na conclusion ya kijinga hivi. Baba yako hiyo hela aliyokupelekea shule bora angefugia nguruwe ingemlipa.
 
Hata RAIS Samia hufanya hivyo. Kumbuka Hotuba Moja amewahi kueleza namna Mheshimiwa Waziri wa Fedha anavyompigia Simu hadi Usiku kumueleza baadhi ya Mambo ambayo anahisi yangefanyika. Hii ni katika kuonyesha kuwa waziri anaweza kupiga simu kwa Rais na Mama akapokea simu na kusikiliza
Sasa Nini hoja ya huyu Waziri kulalamika kushindwa kumfikia Mama...!

Hana namba yake!?
 
Nimekuwa nasisitiza hili hapa mara kadhaa lakini mtoa maada kajitoa akili.

..Mkuu hii habari imepotoshwa.

..Na tatizo letu vijana hawana muda wa kuhakiki taarifa wanazopewa.

..Mkenda alisema ilikuwa vigumu kwa yeye na timu yake kupata muda wa kwenda kufanya presentation kwa Raisi.

..Na sababu zake ni Raisi kuwa na ratiba ambayo ni tight sio kwamba Raisi hataki kuonana na Waziri.

..Prof pia akaeleza kwamba yeye na timu yake walipangiwa masaa mawili kufanya presentation.

..Lakini walipomueleza Raisi kwamba they have been given two hours, Raisi akasema anawapa siku nzima ya kuwa naye kuwasilisha hoja zao. Na baada ya hapo Raisi aliwapa commitmet kuwa atatekeleza ushauri waliompa.

..Prof hakulaumu wala kumlalamikia yeyote yule katika hotuba yake. In fact alimzungumzia vizuri sana Rais Mama Samia.
 
..Mkuu hii habari imepotoshwa.

..Na tatizo letu vijana hawana muda wa kuhakiki taarifa wanazopewa.

..Mkenda alisema ilikuwa vigumu kwa yeye na timu yake kupata muda wa kwenda kufanya presentation kwa Raisi.

..Na sababu zake ni Raisi kuwa na ratiba ambayo ni tight sio kwamba Raisi hataki kuonana na Waziri.

..Prof pia akaeleza kwamba yeye na timu yake walipangiwa masaa mawili kufanya presentation.

..Lakini walipomueleza Raisi kwamba they have been given two hours, Raisi akasema anawapa siku nzima ya kuwa naye kuwasilisha hoja zao. Na baada ya hapo Raisi aliwapa commitmet kuwa atatekeleza ushauri waliompa.

..Prof hakulaumu wala kumlalamikia yeyote yule katika hotuba yake. In fact alimzungumzia vizuri sana Rais Mama Samia.
Kuna wasaidizi wa rais walikuwa wanamnyima nafasi ya kuongea na rais. Hata alipokuwa anatoa hotuba walimpelekea kimemo kumwambia atoe hotuba asitoe porojo, akasema hii ndiyo hotuba naitoa.

Kuna katibu wa rais (si katibu mkuu kiongozi, katibu wa rais) anamu isolate rais kutoka kwa mawaziri wake na watendaji wwngine wa serikali.

Hii habari inajulikana muda mrefu tu kabla hata ya malalamiko ya Mkenda.
 
Kuna wasaidizi wa rais walikuwa wanamnyima nafasi ya kuongea na rais. Hata alipokuwa anatoa hotuba walimpelekea kimemo kumwambia atoe hotuba asitoe porojo, akasema hii ndiyo hotuba naitoa.

Kuna katibu wa rais (si katibu mkuu kiongozi, katibu wa rais) anamu isolate rais kutoka kwa mawaziri wake na watendaji wwngine wa serikali.

Hii habari inajulikana muda mrefu tu kabla hata ya malalamiko ya Mkenda.
Siyo kweli na acha upotoshaji wako hapa wa kusema katibu wa Rais anamtenga na kumuweka mbali Mheshimiwa Rais na Mawaziri wake.
 
Mm niko upande w prof kwakua yuko kwenye baraza l mawaziri je mtendaji w kijiji uko kilosa au tukuyu anaweza kumuona CHURA? Za ndani nikua tangu mwaka umeanza huu 2025 Baraza la mawaziri hawajaa kaa. TAIFA linajiendea tu.
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Sasa Nini hoja ya huyu Waziri kulalamika kushindwa kumfikia Mama...!

Hana namba yake!?
Ndio Maana nimesema ya kuwa waziri hakuwa na sababu ya kulalamika juu ya juu ya jambo hilo kwa sababu anazo njia nyingi sana za kuwasiliana na Mheshimiwa Rais ili apate nafasi ya kuonana naye moja kwa moja kwa ajili ya kuwasilisha jambo kama hilo alilokuwa analitaka. Lakini pia kuna vikao vya mawaziri huwa vinafanyika mara kwa mara . Na majuzi juzi tu hapo vilifanyika.
 
Mm niko upande w prof kwakua yuko kwenye baraza l mawaziri je mtendaji w kijiji uko kilosa au tukuyu anaweza kumuona CHURA? Za ndani nikua tangu mwaka umeanza huu 2025 Baraza la mawaziri hawajaa kaa. TAIFA linajiendea tu.
KAZI ni kipimo cha UTU
Unafahamu mara ya mwisho lilikaa lini na linatakiwa likae kila baada ya muda gani?
 
Back
Top Bottom