Hakuna aliyetaka Kumuua Godbless Lema. Tuambiane Ukweli tu

Wewe ni mmojawapo ya waliotaka kumuua maana unajiita wasiyo julikana
 
Inawezekana ni Siasa kweli,ila inatakiwa tuwe makini sana kujadili hasa linapokuja suala la uhai wa mtu,kama Godbless alipata fununu alichokifanya alikuwa sahihi kuliko angepuuza na kutokea kweli
Wanao beza hatua ya Lema ni wale waliokuwa na mipango hovu juu ya maisha ya mh Lema
 
Hata Lissu alivyolalamika kuwa anawindwa ili auwawe, sina shaka kuwa na wewe ni mmoja ya mliokuwa mnakejeri na kudai, hakuna kitu kama hicho! Hata Ben, naye alilalamika kuhusiana na hilo, bado mkamkejeri kuwa ni muongo!
Haya majitu ni ya kuogopa sana
 
Labda useme hamna mawasiliano mazuri na wenzako kama mumemuua Ben wa saa 8 kwa kuhoji PhD tu mtashindwa kumuua lema aliyekuwa anawatoa kamasi.
 
Hawana uwezo wa kuleta facts maana ni kati ya wahusika wa hayo mambo ya kuumiza watu kisa chuki za kisiasa
 
Hakuna hilo jambo Lema hakuwa katika hatari ya kuuawa.
Mlisema na kukaza shingo kwamba hakukuwa na mtu anataka kumuua/kumteka/kumjeruhi Lissu.Na alitoa taarifa hadharani kuhusu hilo.Ben Saanane vilevile alisema kupokea vitisho vya kuuliwa.Baada ya kutokea yaliyotokea mkabadili simulizi kwamba Lissu amejipiga risasi na ujinga mwingi.Ifike mahali muache ujingaujinga ujinga.Ulikuwa naye kila sehemu aliyoenda?
 
Acha mihemko aya kishamba ile awamu ukipata ujumbe kwamba wanaitaka roho yako sio wa masihara
 
Godbles Lema ni mtu mzima mwenye akili zake timamu. We unahangaika nini. Kwani kuna chako alikichukua? Usituchoshe tafadhali wala usitupikgie kelele, enedlea n amajukumu yako au kama huna jukumu lolote ukajilaze hata kwenye mawe.
 
Eleza na Roma Mkatoriki kulikuwa na umuhimu gani wa kumteka na mitutu ya bunduki na kukaa nae siku zote zile huku huku mateso na mahojiano yote yakijikita kuhusu tungo na mashaili ya nyimbo zake. IKUMBUKWE ROMA ALIVYUNJWA HADI KIDOLE NAALIONYESHA MICHUBUKO MINGI MGONGONI....NA WALICHUKUA VIFAA VYOTE MUHIMU PALE TONGO RECORDS KWA BIN LADEN...ETI ANATESWA KIASI KILE ILI ASEME TU KUWA CHADEMA NDO WANAMTUMA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…