Hakuna faida ya kumpeleka mtoto English Medium (mabasi ya njano)

Baada ya kuona amejua kuziandika one -twenty (kwa maneno) kwa usahihi nikamwambia aandike kwa kiswahili (moja-ishirini) haikumchukua dakika 20 aliunga herufi akapata zote. Mwambie huyo wa mchepuo wa kiswahili kama atakupa English na Kiswahili.
 
Mentality yako inaamini hayo ndiyo anayoyapata aliyeenda english medium kakini amini kwamba kuna zaidi ya hivyo.
Unafikiri nilicho andika sikifahamu ?
 
Ni vema kueshimu mawazo ya mtu ata km hujui anamaanisha nn au kusudio lake ni nn

Lakin pia weka sababu tujue nn ttzo
Lakin pia kuna utofauti kati ya private school na english medium jifunze kutofautisha
Sio kla private school ni English medium
 
We jamaa leo umeamkia elimu yetu ya private.
Usiiseme vibaya maana sisi ndo imetufanya tuko hapa tulipo na sijui tungekuwa wapi kama tungepita swahili medium.
Mkuu kama haupo pamoja na ma ccm kitengo cha juu kabsa bado una hali mbaya tu labda unakanafuu upo wodini na sio ICU kama kundi kubwa.
 
Baada ya kuona amejua kuziandika one -twenty (kwa maneno) kwa usahihi nikamwambia aandike kwa kiswahili (moja-ishirini) haikumchukua dakika 20 aliunga herufi akapata zote. Mwambie huyo wa mchepuo wa kiswahili kama atakupa English na Kiswahili.
English gani unayoizungumzia wewe ? Unazungumzia ule uchafu wanaoimbishwa hiyo ndio English ya kueleweka ?
 
Ni vema kueshimu mawazo ya mtu ata km hujui anamaanisha nn au kusudio lake ni nn

Lakin pia weka sababu tujue nn ttzo
Lakin pia kuna utofauti kati ya private school na english medium jifunze kutofautisha
Sio kla private school ni English medium
Huyu mkuu mleta uzi anadhani english medium zote ni private hajui kuna shule za serikali ambazo ni english medium pia.
 
Hiyo ndio kazi ya elimu bora ?
 
Bado najaribu kuwaza mleta mada anaenga nini lakini simuelewi bado
 
Huyu mkuu mleta uzi anadhani english medium zote ni private hajui kuna shule za serikali ambazo ni english medium pia.
Ni wapi nimedhani hivyo ?
 
Utofauti upo kwenye malezi na ufuatiliwaji wa wanafunzi, huko changamkeni kundi kubwa la watoto hupotea kimaadili mapema sana kuliko huku kwingine.
 
Mitaala ya Cambridge pesa yake mlima.

Acha watu wapambane na wanapoweza kufikia, elimu ni uwekezaji. Mtaala wetu kama una mada za Chief Mangungo wa Msowero, Kinjekitile Ngwale. Mtoto wa kayumba atasoma kwa kiswahili na English medium kwa English. Mwisho wa siku tofauti itakuwepo aliyepata elimu kwenye sehemu rafiki kujifunza na kawaida
 
Huyu anakula pumba kwa kiswahili kwa uhuru huku huyu akila pumba kwa kingereza kwa kujibana
 
Utofauti upo kwenye malezi na ufuatiliwaji wa wanafunzi, huko changamkeni kundi kubwa la watoto hupotea kimaadili mapema sana kuliko huku kwingine.
Ila private nyoronyoro wakutosha na machoko ?

Tuizungumzie elimu bora malezi hiyo kazi ya mzazi
 
Ni vema kueshimu mawazo ya mtu ata km hujui anamaanisha nn au kusudio lake ni nn

Lakin pia weka sababu tujue nn ttzo
Lakin pia kuna utofauti kati ya private school na english medium jifunze kutofautisha
Sio kla private school ni English medium
Wewe ulivyosoma uzi umeelewa nini ?
 
Ila private nyoronyoro wakutosha na machoko ?

Tuizungumzie elimu bora malezi hiyo kazi ya mzazi
Hii tendency ya kugeneralize huwa haina maana, unaposema Private nyoronyoro ni lazima uje na uthibitisho unaoonyesha kuwa nyoronyoro wote ni waliopita private. Hoja yangu ilijikita kwenye swala la ufuatiliwaji (wa kimasomo, kiusalama, na malezi)

Ni sawa na mtu aseme kuwa , waliosoma changamkeni ndio majizi, majambazi, machangudoa wanaotusumbua huku mtaani, kwa harakaharaka itaonekana ni kweli lakini sikweli.

Kitu kingine cha ajabu ni kuamini kwamba anakoshinda mtoto wako kwa muda wa masaa 8- 10 kwa siku, eti hakuna impact yoyote ya kitabia juu yake. Kusema " Malezi ni kazi ya mzazi" ni sawa lakini ni lazima ujue kuwa muda anaokuwa sehemu usiyokuwepo wewe ni mwingi na una impact ya moja kwa moja kwenye maisha yake.
 
Kayumba kuna changamoto nyingi sana hasa za kimaadili, kama mzazi kipato kinaruhusu ni bora mtoto umpeleke huko kwenye mabasi ya njano
 
Uliposema huko Changamkeni kundi kubwa la watoto hupotea kimaadili ulikuwa umechanganyikiwa ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…