Hakuna mchawi anayechanja chale watu usiku, acheni kulalia vitanda vichafu.

Hakuna mchawi anayechanja chale watu usiku, acheni kulalia vitanda vichafu.

Ila jamani kwani uchawi si umezungumziwa kwenye vitabu vya dini? Sasa kama unaamini hivyo vitabu kwanini usiamini na huo uchawi pia, [emoji1]
Unakuta kabisa mtu anasema hakuna uchawi ni imani za kiafrika na masimulizi ya zamani halafu anaamini kuhusu hadithi za Yesu na Muhammad [emoji848]
Jamii zote duniani zimepitia hizi imani za kichawi. Ni mambo yasiyofanya chochote. Lakini kwa vile watu walikuwa wakiyafanya, ndiyo maana yameandikwa.
 
Mmae leo nakupiga chale kwenye kalio uamke nazo kesho halafu ulete thread kesho
 
Ufu 22:15

Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
Wachawi na waabudu sanamu hawana tofauti. Pilika zao hazizai matunda yoyote. Unaamini mtu anaweza zindikwa risasi isimpenye?
 
Hypnostic therapy-- hiyo hutumiwa kutibu wagonjwa wa akili nk,

Kitendo cha mtu kuweza kuitawala akili yako bila wewe mwenyewe kujitambua au kuitawala akili yako hiyo ni miongoni mwa elimu za "Hypnotism", yaani kuna vitu kutoka kwa wanyama (all animals + human beings) na kutoka kwenye aina fulani ya mimea, vitu hivyo vichanganywa "kitaalamu" hapo unaweza kupata "hypnostic stuff", hiyo stuff ndiyo hutumika katika kulaza watu , kufanya watu wasijitambue, kuwafanya watu wawe mentally ecstatic nk, kifupi ni kwamba; Hypnotism has got to do with mental, it affects mental either positive or negative, wachawi hutumia negatively ndio maana uchawi unaitwa Dark science.

It is Hypnosis to be precise.😀😀
Yaani unaelezea mpaka raha bila magumashi🙏🔥🔥
 
Uchawi ni sayansi, ni elimu, mfano mtu anafanya kamba ionekane kama nyoka, ni jinsi gani hiyo kama inaonekana kama nyoka mbele ya watazamaji??, hapo ndipo science ya Optics inapohusika, sasa ili mtu aione hiyo kamba kama nyoka kunatakiwa kuwepo na nyenzo za kufanya kazi hiyo hizo nyenzo ndizo zinaitwa uchawi, hizo nyenzo zinapatikanaje??, hapo ndipo uchawi unapoitwa dark "science".

Mchawi anapoingia nyumbani kwako anatumia elimu ya sayansi inayoitwa Hypnosis (I mistaken with hypnotism), nayo inavyo vifaa vyake (magical tools) ambavyo hupatikana katika njia za giza na ndio maana uchawi unaitwa Dark science na aghlabu ni sayansi inayohusisha unyama na ushetani.
We ni kichwa sana👽👽
 
Mm nilikuwa siamini mambo ya kishirikina ila yaliyo nitokea Mwaka Juzi nikiwa Moshi niliamini uchawi upo Hadi Leo Huwa nashindwa kuelewa Kila nikikumbuka sinywi pombe Wala kuvuta bangi ila niliyo yaona Bado Huwa nikikumbuka naweweseka
 
Jamii zote duniani zimepitia hizi imani za kichawi. Ni mambo yasiyofanya chochote. Lakini kwa vile watu walikuwa wakiyafanya, ndiyo maana yameandikwa.
Sijakuelewa?
Kwa kua watu waliyafanya ndio maana yameandikwa kwa hiyo yapo au hayapo?

Kuna kifungu kinasema mchawi auliwe katika biblia hapo imekaaje?
 
Halafu nikupe siri, wengi wanaosema "hakuna uchawi" ni wachawi kuntu magwiji wa ushirikina na giza.

Hawa wanachofanya ni kutumia MBINU ya kisaikolojia ya kuhadaa watu na kupoteza maboya ili uache kuamini uwepo wao kisha wakunyooshe kimya kimya taratibu.

Hamna mtu MNAFIQ kama MCHAWI. [emoji851]
Aisee kumbe wana mbinu kali hivi [emoji1787]
Mtoa mada aje ajitetee hapa
 
Sijakuelewa?
Kwa kua watu waliyafanya ndio maana yameandikwa kwa hiyo yapo au hayapo?

Kuna kifungu kinasema mchawi auliwe katika biblia hapo imekaaje?
Hata walioabudu Baali waliuwawa, Lakini ibada yao ilikuwa na matokeo yoyote? So aliyefanya uchawi aliuwawa lakini uchawi wake haukuwa kitu chochote. Ni ujinga tu. Leo hii watanzania wengi wanaamini nyongo ya mamba ni sumu. Lakini si kweli hata kidogo. Ndivyo imani juu ya uchawi ipo hivyo. Inatokana na ujinga
 
Back
Top Bottom