Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Niliaminigi maneno ya Wanyakyusa nikaenda huko 2009 nilikutana vumbi kama poda kipindi hiki watu wanakula nondo za utosi, saa moja jioni wote ndani ukitaka kwenda hata dukani inabidi uvae helmet kulinda fuvu.
 
Mbeya old cbd
20221125_083948.jpg
 
Niliaminigi maneno ya wanyakyusa nikaenda uko 2009 nilikutana vumbi kama poda kipindi hichi watu wanakula nondo za utosi saa moja jioni wote ndani ukitaka kwenda hata dukani inabidi uvae helmet kulinda fuvu
Karibu tena Mkuu maendeleo ni hatua vumbi limepungua

 
Ingekuwa Vijana wanaoanza maisha ya Utumishi ingekuwa wanaruhisiwa kuchagua Mkoa, ningewashauri waanze na huo.

Maisha ni Cheap sana Mbeya, mara ya kwanza nafika nakutana na Chips za shilingi 500 ambazo nilishindwa kuzimaliza

Ukiwa na shilingi laki 1 inatosha kula Mwezi Mzima
 
Not that bad

Huu mji umechoka inabidi uvunjwe ujengwe upya. Ni mji mkubwa ila sio mzuri kimpangolio isipokuwa sehemu kadhaa. Mbeya ingepangwa mji ungekuwa mzuri no 1. Geographically ni no 1.

Mwanza itaendelea kuiacha Mbeya daima kwa sababu Mbeya wanaendelea kujenga holela sasa sijii kwa nini Serikali haingilii kati na kuzuia kujenga holela.

Wanyakyusa na ndugu zao wasafwa hawazingatii mpango mji japo ni watu wanaojenga sana pengine kuliko makabila mengi.
 
Huu mji umechoka inabidi uvunjwe ujengwe upya. Ni mji mkubwa ila sio mzuri kimpangolio ispokuwa sehemu kadhaa.
Mbeya ingepangwa mji ungekuwa mzuri no 1.
Geographically ni no1.
Mwanza itaendelea kuiacha Mbeya daima kwa sababu Mbeya wanaendelea kujenga holela sasa sijii kwa nini serikali haingilii kati na kuzuia kujenga holela.
Wanyakyusa na ndugu zao wasafwa hawazingatii mpango mji japo ni watu wanaojenga sana pengine kuliko makabila mengi.
Mkuu rangi za kutu za bati zisikutishe
that_mbeya_guy_1679744755128476.jpg
that_mbeya_guy_1679744711793100.jpg
 
Ingekuwa Vijana wanaoanza maisha ya Utumishi ingekuwa wanaruhisiwa kuchagua Mkoa, ningewashauri waanze na huo.

Maisha ni Cheap sana Mbeya, mara ya kwanza nafika nakutana na Chips za shilingi 500 ambazo nilishindwa kuzimaliza

Ukiwa na shilingi laki 1 unatoa kula Mwezi Mzima
Msipende sana mikoa yenye chakula kingi, hsina nxunguko wa hela. Mbeya, Songea, Rukwa, Kigoma, Kagera,Kilimanjaro.

Hio mikoa utashiba ila hela za maana hutashika. Mkoa unaopta ndizi 4 kwa mia mbili utatoboa hapo. Ili utoboe hio mikia inakubidi ulime usafirishe mikoa mingine.

Napingana na ushauri wako. Maisha sio chakuka bali ni hela, ukiwa na hela utanunua chochote.. Ili upate elfu 10 itabifi uuze sahani ngapi za chips au chane ngapi za nduzi!
 
Mkoa wenyewe imejengwa hovyo hovyo hasa Mbeya mjini kuliko mkoa mwingine wowote hapa Tanzania.
Miundo Mbinu mibovu kuliko mkoa mwingine wowote.
Mbeya mjini wameharibu jiografia kwa kujenga hovyo hadi kwenye vimilima kama kile cha Ilemi, cha Simike! Skwataz everywhere.ipo
Ipo hivi watu wa Mbeya moja ya kitu wanafikiria sana ni kujenga ....... yani wewe ukiwa Mbeya haijalishi una pesa kiasi gani haijalishi unatembelea gari ya bei juu kiasi kuanzia benzi, BMW and the like ...

Kama utakuwa hujajenga nyumba hata ya vyumba viwili (hauna nyumba ) basi mbele ya wanambeya huna cha kuwaambia wewe ni masikini kama masikini wengine.

Sasa basi ili kila mwanambeya kukwepa hii aibu basi atajitahidi kujenga kajumba kokote kale hata eneo lisilotakiwa ili kukwepa kudharaulika matokeo yake ndyo huo ujenzi wa olela unaouona hapo Mbeya.
 
Msopende sana mikoa yenye cgakula kingi, hsina nxunguko wa hela.
Mbeta,Songea,Rujwa, Kigoma, Kagera,Kilimanjaro.
Hio mikoa utashiba ika hela za maana hutashika. Mkoa unaoata ndizj 4 kwa miambili utatoboa hapo.
Ili uyoboe hio mikia inakubidi ulime usafirishe mikoa mingine.
Napingana na usgsuri wako. Maisha sio cgakuka vali ni hela ukiwa na hela utanunua chochote..
Ili upate elf 10 itabifi uuze sagani ngspi za chips au chane ngapii za nduzi!
Mkoa wa Mbeya ni namba 3 Kwa pato la Taifa Sasa unasemaje hakuna pesa?

Mbeya ni Mkoa wa pili kuwa na mabasi mengi ya kutoka Dar to Mikoani

Sasa with all that how comes hakuna mzunguko wa pesa? Hizi stori Huwa unahadithiwa na nani bwashee?

 
Ipo hivi watu wa mbeya moja ya kitu wanafikiria sana ni kujenga ....... yani wewe ukiwa mbeya haijarishi unapesa kiasi gani haijarishi unatembelea gari ya bei juu kiasi kuanzia benzi , bmw and the like ...

Kama utakuwa hujajenga nyumba hata ya vyumba viwili ( hauna nyumba ) basi mbele ya wanambeya huna cha kuwaambia wewe ni .masikini kama masikini wengine .

Sasa basi ili kila mwanambeya kukwepa hii aibu basi atajitaidi kujenga kajumba kokote kale hata eneo lisilotakiwa ili kukwepa kudharaulika matokeo yake ndyo huo ujenzi wa olela unaouona hapo mbeya.
Hili lina ukweli. Mwanambeya akikuambia amejenga halafu ukakikuta alichokijenga, ni ajabu
 
Naufahamu mkoa vizuri.
Serikali imezembea kwente kipanga huu mji na bafo wanaendekea kugaribu huko milimani wanajenga miji mioya hovyo hovyo.
Mbeya haijawahi pata kiongozi mahiri wa kusimamia mji.
Mbeya ingekuwa kama ulaya.
Hakuna single Kiongozi anaweza badili Mkoa yeye kama yeye,sera za Nchi Haziruhusu Hilo maana hata ukiongeza uzalishaji Bado mapato yatakuwa ni ya Nchi.
 
Mkoa wa Mbeya ni namba 3 Kwa pato la Taifa Sasa unasemaje hakuna pesa?

Mbeya ni Mkoa wa pili kuwa na mabasi mengi ya kutoka Dar to Mikoani

Sasa with all that how comes hakuna mzunguko wa pesa? Hizi stori Huwa unahadithiwa na nani bwashee?
Pesa zingeonekana. Mwanza huitaji kuitetea kila kitu kinajionesha. Kwa nini mbalali haibadiriki kama watu wanahela.
Mbeya ina watu wengj wenye vishughili shughuli.
 
Ingekuwa Vijana wanaoanza maisha ya Utumishi ingekuwa wanaruhisiwa kuchagua Mkoa, ningewashauri waanze na huo.

Maisha ni Cheap sana Mbeya, mara ya kwanza nafika nakutana na Chips za shilingi 500 ambazo nilishindwa kuzimaliza

Ukiwa na shilingi laki 1 unatoa kula Mwezi Mzima
Upo sahihi mkuu, gharama za maisha za huo mkoa ni kitongaaaa...
 
Hakuna single Kiongozi anaweza badili Mkoa yeye kama yeye,sera za Nchi Haziruhusu Hilo maana hata ukiongeza uzalishaji Bado mapato yatakuwa ni ya Nchi.
Hata mipango mji? Mapato ya halmashsuri mengine si yanabaki. Dodoma yajuzi tu wameweza kupanga mji wao na unakua kwa kasi na itaizidi mbeya si muda mrefu.
Mbeya ilitakiwa iwe zaidi ya hapa ilipo, tuongee ukweli.
Mkurugenzi wa dodona kipindi cha Magu alikuwa mkali sana kwenye mipango miji
Mbeya miji mipya inajengwa holela hafi sasa hivi nenda itewe nk ujionee ni shaghala bagala.
 
Mkoa wa Mbeya ni Kati ya Mikoa 5. iliyopo Nyanda za Juu Kusini sanjali na Mikoa ya Ruvuma,Iringa,Songwe,Njombe na Rukwa.Mbeya ilianzishwa mwaka 1961.

Mkoa wa Mbeya umejaaliwa kila kitu unachokijua wewe..

Kwa hapa Tanzania sijaona Mkoa Mzuri wa Kuishi kushinda Mbeya..

1.Kiuchumi.

Mbeya ni ya 3 Kwa kuchangia pato la Taifa yaani GDP Tanzania.

Mbeya ni ya 3 Kwa kuwa na Watu wenye kipato kikubwa.

 2.Hali ya Hewa na Mandhari.

Mbeya Ina Hali ya hewa ya majira yote yaani Bariadi na joto na mvua ni uhakika sio tia maji tia maji kama Mikoa mingine.

3.Usafiri

Uwanja wa ndege wa Songwe
Usafiri wa Barabara kutoka Mikoa yote na Nchi jirani Kupitia Barabara kuu ya Tanzam.
Usafiri wa kwenye Maji via Ziwa Nyasa.
Pia Kuna usafiri wa reli nzuri kabisa unakufikisha Zambia kutokea Dar.

4.Kilimo.

Mbeya Ina Ardhi nzuri ya kulima Kila aina ya zao kuanzia mbogamboga,matunda,nafaka Hadi pareto na chai.

5.Madini na Nishati.

Mkoa una Kila aina ya Madini kuanzia Dhahabu za Chunya Hadi Makaa ya Mawe ya Kiwira bila kusahau Madini ya gas asilia ya CO2.
Umeme ni WA uhakika unaozalishwa kutoka migodi ya Kiwira na Geothermal.

6.Elimu.

Mbeya ni Kati ya Mikoa ya Wasomi hapa Tanzania.Mkoa wa Mbeya una vyuo Vikuu zaidi ya 5 mfano MUST,Mzumbe,CuCoM,Udsm,Tumaini,nk.

Mkoa una mamia ya vyuo vya kati na shule za kutosha eg St.Francis hivyo ni ideal pia Kwa issues za Elimu.


7.Utalii

Hapa kwenye Utalii ndio Kuna fursa nyingi maana sehemu kubwa ni underdeveloped.

Kuna Milima ya kawetere,bwawa la Mungu,Hifadhi ya Kitulo na pia unafika Kwa urahusi Ruaha au Katavi NP kutokea Mbeya.

8.Viwanda na Biashara.
Kuna viwanda vya aina mbalimbali kama Saruji,vinywaji vikali na laini kama soda,bia,wine nk.
Kuna viwanda vya magodoro,vifaa vya ujenzi,home appliances nk.

Aisha kama unataka kujenga viwanda Kuna maeneo ya kutosha yametengwa Kwa Ajili hiyo.

Mbeya ndio Kitovu Cha Uchumi wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

9.Makazi na Accomodations.

Kuna fursa kubwa Bado ya ujenzi wa hoteli za kitalii na hoteli za kawaida maana ni Mkoa wa Biashara hivyo itakulipa.

Pia Hapa ni wewe tuu maana ujenzi wa Mbeya sio costful kama Mikoa mingine,unachagua ijengee tofauti au blocks au hata tofari mbichi udongo una nata vizuri kabisa..

10. Watu .

Mbeya Ina idadi ya watu zaidi ya mil.2.3 Kwa Mkoa mzima wanaokuhakikishia soko.

Aisha watu wake ni Wapambanaji ndio maana huwezi kusikia Mbeya ikitajwa kwenye mambo ya umaskini na shida ndogo ndogo,hawalalamiki kusubiria serikali.

Kiufupi hiyo ni summary ndogo sana Kati ya Mengi mazuri yaliyopo Mbeya,Karibuni sana Mbeya.



View attachment 2565116View attachment 2565117


Kwenye umeme hapana, labda bwawa likiisha, umeme ni tia maji tia maji sana.
 
Back
Top Bottom