Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Hiyo mikoa maisha mdebwedo sana inawafaa wavivu na wajinga Maana hutumii akíli nyingi kuishi.

Tanzania ni DAR, ARU, MWZ na DDOM tu. Kwingineko tutakuja kutalii tu kipindi cha likizo kupanga natural air.
Sasa mbona huko mnakotumia akili nyingi Kuna maskini wa kutosha shida nini bwashee? Akili zinakuwa zimefikia mwisho au? 😀😀
IMG-20221211-WA0004.jpg
 
Mkoa wa Mbeya umejaaliwa kila kitu unachokijua wewe..

Kwa hapa Tanzania sijaona Mkoa Mzuri wa Kuishi kushinda Mbeya..
Nikweli na naunga mkono hoja
4.Kilimo.

Mbeya Ina Ardhi nzuri ya kulima Kila aina ya zao kuanzia mbogamboga,matunda,nafaka Hadi pareto na chai.
Mchele wa Mbeya, Super Kyela ndio mchele wa grade 1.
Maharage ya Mbeya ndio maharage yanayoongoza kwa ulaini, kuyapika hadi yaive maji ni mara moja tuu!. Tena maharage yenyewe ya Mbeya, sio tuu ni maji mara moja bali pia ni matamu hayo!.
10. Watu .

Aisha watu wake ni Wapambanaji ndio maana huwezi kusikia Mbeya ikitajwa kwenye mambo ya umaskini na shida ndogo ndogo,hawalalamiki kusubiria serikali.

Kiufupi hiyo ni summary ndogo sana Kati ya Mengi mazuri yaliyopo Mbeya,Karibuni sana Mbeya.
Kuna ubaya mmoja wa watu wa Mbeya hukuusema, hawana kabah, as a result watu wasio na kabah wanaitwa Wambeya na wanapenda umbea!.

Na kuna uzuri mmoja wa wanawake wa Mbeya, sio wachoyo, wana roho mzuri na kwenye yale mambo yetu yale, ni kama maharage ya Mbeya, maji mara moja!.

Na kwenye siasa, siasa za Mbeya ni very interesting, kwenye ubunge wa Mbeya mjini, nimewahi kuuliza "Maharage ya Mbeya maji mara moja" ni kauli ya kweli? Ni kwenye maharage tu au hadi kwa wanambeya? Kama kauli huumba, Jibu sahihi ni Oktoba 2020!
P
 
Nikweli na naunga mkono hoja

Mchele wa Mbeya, Super Kyela ndio mchele wa grade 1.
Maharage ya Mbeya ndio maharage yanayoongoza kwa ulaini, kuyapika hadi yaive maji ni mara moja tuu!.

Kuna ubaya mmoja wa watu wa Mbeya hukuusema, hawana kabah, as a result watu wasio na kabah wanaitwa Wambeya na wanapenda umbea!.

Na kuna uzuri mmoja wa wanawake wa Mbeya, sio wachoyo, wana roho mzuri na kwenye yale mambo yetu yale, ni kama maharage ya Mbeya, maji mara moja!.

Na kwenye siasa, siasa za Mbeya ni very interesting, kwenye ubunge wa Mbeya mjini, nimewahi kuuliza "Maharage ya Mbeya maji mara moja" ni kauli ya kweli? Ni kwenye maharage tu au hadi kwa wanambeya? Kama kauli huumba, Jibu sahihi ni Oktoba 2020!
P
Mambo ya mchele wa Mbeya
 
Mkoa wa Mbeya ni Kati ya Mikoa 5. iliyopo Nyanda za Juu Kusini sanjali na Mikoa ya Ruvuma,Iringa,Songwe,Njombe na Rukwa.Mbeya ilianzishwa mwaka 1961.

Mkoa wa Mbeya umejaaliwa kila kitu unachokijua wewe..

Kwa hapa Tanzania sijaona Mkoa Mzuri wa Kuishi kushinda Mbeya..

1.Kiuchumi.

Mbeya ni ya 3 Kwa kuchangia pato la Taifa yaani GDP Tanzania.

Mbeya ni ya 3 Kwa kuwa na Watu wenye kipato kikubwa.

 2.Hali ya Hewa na Mandhari.

Mbeya Ina Hali ya hewa ya majira yote yaani Bariadi na joto na mvua ni uhakika sio tia maji tia maji kama Mikoa mingine.

3.Usafiri

Uwanja wa ndege wa Songwe
Usafiri wa Barabara kutoka Mikoa yote na Nchi jirani Kupitia Barabara kuu ya Tanzam.
Usafiri wa kwenye Maji via Ziwa Nyasa.
Pia Kuna usafiri wa reli nzuri kabisa unakufikisha Zambia kutokea Dar.

4.Kilimo.

Mbeya Ina Ardhi nzuri ya kulima Kila aina ya zao kuanzia mbogamboga,matunda,nafaka Hadi pareto na chai.

5.Madini na Nishati.

Mkoa una Kila aina ya Madini kuanzia Dhahabu za Chunya Hadi Makaa ya Mawe ya Kiwira bila kusahau Madini ya gas asilia ya CO2.
Umeme ni WA uhakika unaozalishwa kutoka migodi ya Kiwira na Geothermal.

6.Elimu.

Mbeya ni Kati ya Mikoa ya Wasomi hapa Tanzania.Mkoa wa Mbeya una vyuo Vikuu zaidi ya 5 mfano MUST,Mzumbe,CuCoM,Udsm,Tumaini,nk.

Mkoa una mamia ya vyuo vya kati na shule za kutosha eg St.Francis hivyo ni ideal pia Kwa issues za Elimu.


7.Utalii

Hapa kwenye Utalii ndio Kuna fursa nyingi maana sehemu kubwa ni underdeveloped.

Kuna Milima ya kawetere,bwawa la Mungu,Hifadhi ya Kitulo na pia unafika Kwa urahusi Ruaha au Katavi NP kutokea Mbeya.

8.Viwanda na Biashara.
Kuna viwanda vya aina mbalimbali kama Saruji,vinywaji vikali na laini kama soda,bia,wine nk.
Kuna viwanda vya magodoro,vifaa vya ujenzi,home appliances nk.

Aisha kama unataka kujenga viwanda Kuna maeneo ya kutosha yametengwa Kwa Ajili hiyo.

Mbeya ndio Kitovu Cha Uchumi wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

9.Makazi na Accomodations.

Kuna fursa kubwa Bado ya ujenzi wa hoteli za kitalii na hoteli za kawaida maana ni Mkoa wa Biashara hivyo itakulipa.

Pia Hapa ni wewe tuu maana ujenzi wa Mbeya sio costful kama Mikoa mingine,unachagua ijengee tofauti au blocks au hata tofari mbichi udongo una nata vizuri kabisa..

10. Watu .

Mbeya Ina idadi ya watu zaidi ya mil.2.3 Kwa Mkoa mzima wanaokuhakikishia soko.

Aisha watu wake ni Wapambanaji ndio maana huwezi kusikia Mbeya ikitajwa kwenye mambo ya umaskini na shida ndogo ndogo,hawalalamiki kusubiria serikali.

Kiufupi hiyo ni summary ndogo sana Kati ya Mengi mazuri yaliyopo Mbeya,Karibuni sana Mbeya.




View attachment 2565229

Usisahau kuwa Mbeya ni kinara wa ufirauni

 
Tupo wengi ukichukua wastani Lazima tuoneka tupo Chini.

By the way kipenda Roho
hula myama mbichi. Ila Tanzania ni mikoa niliyokutajia Kwa huduma za uhakika
Mko wengi ila mnazalisha kidogo Kwa Lugha rahisi ni kwamba mumeishiwa akili na wavivu.
 
Acha mzaha basi,Mbarali ipi ambayo haibadiliki?

Unazungumzia Mwanza,hivi ukiacha Mwanza Mjini Kuna Wilayani gani huko Mwanza inaweza fanana na Wilaya yeyeote ya Mbeya ikiwemo Mbarali?

Kwamba ukienda Kwimba au Ukerewe Kuna mzunguko wa hela? 😁😁😁

Acha vichekesho Mkuu ,tofayya Mbeya na Mwanza ni kwamba maendelea ya Mbeya yamesambaa Wiakaya zote na huko Mwanza Yako hapo Mjini na sababu kubwa ni kwamba Wilaya za Mbeya Zina fursa ya kuvutia watu kuishi huko huko badala ya kukimbilia mjini..

Na hii sifa sio ya Mbeya tuu Bali Mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini unlike Mikoa mingine ambako maendelea Yako concentrated kwenye Miji mikuu Yao..
Nimesema along the road.
Mbeya hakuna pulling factor ktk mji.
Mwanza kuna ziwa linaloleta utitiri wa watu. Kuna viwanda vya samaki, biashara ipo juu. Ni center ya mikoa ya Shy, Kagera, Mara, Tabora, Singida nk.
Mbeya ipo pembezoni sana watu wa Njombe ndio wamejaa. Mwanza iache tu kama ilivyo mbeya haitakuja kuifikia.
Mbeya asilimia kubwa wanategemea kilimo cha kujikimu, hawana ufugaji mkubwa,wala uvuvi, viwanda vichache sana kulinganisha na majiji mengine.
 
Nimesema along the road.
Mbeya hakuna pulling factor ktk mji.
Mwanza kuna zuwa linsloketa utiyiti wa watu. Kuna viwanda vya samaki, buashara ipo juu. Ni center ya mikoa ya Shy, Kagera, Mara, Tabora, Singida nk.
Mbeya ipo pembezoni sana watu wa Njombe ndio wamejaa. Mwanza iache tu kama ilivyo mbeya haitakuja kuifikia.
Mbeya asilimia kubwa wanategemea kilimo cha kujikimu, hawana ufugaji mkubwa,wala uvuvi, viwanda vichache sana kulinganisha na majiji mengine.
Kigoma,Ukerewe,Bukoba Kuna Ziwa vipi mbona watu hawajakaa? Mtwara na Tanga Kuna bahari Kwa nini pulling factor ya bahari haijawavuta?😁😁

Acha porojo sababu nilizokupa ndio za kitaalamu.
 
Mbeya bana, napapenda sana hasa wilaya ya kyera, vijiji vya kule kwao Prof. Mwandosya hadi kule Mwakaleli -Tukuyu hii.

Hali ya hewa unaweza ukaishi kule usijue kama kuna dasalama, wanakijiji wa huko siyo wachoyo mtu akiwa na ng'ombe au kuku wanahakikisha na wewe unapewa ili ufuge, yaani maziwa na mayai kule ni kama ugali/maharagwe jera au boding skuli.

Pale Mwakaleli muda wa jua kupunga ni saa 5 kwenda saa 6 tena linaonekana kwa 45min ukilikosa hadi kesho.
 
Back
Top Bottom