Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Huu mji umechoka inabidi uvunjwe ujengwe upya. Ni mji mkubwa ila sio mzuri kimpangolio ispokuwa sehemu kadhaa.
Mbeya ingepangwa mji ungekuwa mzuri no 1.
Geographically ni no1.
Mwanza itaendelea kuiacha Mbeya daima kwa sababu Mbeya wanaendelea kujenga holela sasa sijii kwa nini serikali haingilii kati na kuzuia kujenga holela.
Wanyakyusa na ndugu zao wasafwa hawazingatii mpango mji japo ni watu wanaojenga sana pengine kuliko makabila mengi.
Mkuu, sioni tofauti kubwa sana ya ujenzi holela baina ya Mbeya na Mwanza.
Kama ilivyo Mbeya, Mwanza ina maeneo mengi ambayo mpangilio wake ni holela.
 
Hata mipango mji? Mapato ya halmashsuri mengine si yanabaki. Dodoma yajuzi tu wameweza kupanga mji wao na unakua kwa kasi na itaizidi mbeya si muda mrefu.
Mbeya ilitakiwa iwe zaidi ya hapa ilipo, tuongee ukweli.
Mkurugenzi wa dodona kipindi cha Magu alikuwa mkali sana kwenye mipango miji
Mbeya miji mipya inajengwa holela hafi sasa hivi nenda itewe nk ujionee ni shaghala bagala.
Vyote hivyo viko centralized,ingekuwa hivyo ungekuta Mikoa yote imepangwa..

Ukisema Mbeya haijapangwa Sasa Mwanza utasemaje? Dar Je?
 
Kila mkoa uko njema sana kwa kuishi hata mbeya fresh punguzeni chuki humu .
 
Bajaji nyingi Sana kule

Hakuna migahawa mizuri mjini hakuna

Watu wa mbeya ni wastaarabu Sana huwezi lala njaa kule labda uamue unaweza anza na mmama mmoja Kansani unaenda kwingine unawasalimia tu 😂😂 utakaribishwa chakula watakupa na ndizi au karanga uende nazo Hafu fresh tu hawana noma

Wadada wa mbeya sura za baba zao ila makalio Sasa aisee 😂😂😁😍😍
 
Pesa zingeonekana. Mwanza huitaji kuitetea kila kitu kinajionesha. Kwa nini mbalali haibadiriki kama watu wanahela.
Mbeya ina watu wengj wenye vishughili shughuli.
Acha mzaha basi,Mbarali ipi ambayo haibadiliki?

Unazungumzia Mwanza,hivi ukiacha Mwanza Mjini Kuna Wilayani gani huko Mwanza inaweza fanana na Wilaya yeyeote ya Mbeya ikiwemo Mbarali?

Kwamba ukienda Kwimba au Ukerewe Kuna mzunguko wa hela? 😁😁😁

Acha vichekesho Mkuu ,tofayya Mbeya na Mwanza ni kwamba maendelea ya Mbeya yamesambaa Wiakaya zote na huko Mwanza Yako hapo Mjini na sababu kubwa ni kwamba Wilaya za Mbeya Zina fursa ya kuvutia watu kuishi huko huko badala ya kukimbilia mjini..

Na hii sifa sio ya Mbeya tuu Bali Mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini unlike Mikoa mingine ambako maendelea Yako concentrated kwenye Miji mikuu Yao..
 
Bajaji nyingi Sana kule

Hakuna migahawa mizuri mjini hakuna

Watu wa mbeya ni wastaarabu Sana huwezi lala njaa kule labda uamue unaweza anza na mmama mmoja Kansani unaenda kwingine unawasalimia tu 😂😂 utakaribishwa chakula watakupa na ndizi au karanga uende nazo Hafu fresh tu hawana noma

Wadada wa mbeya sura za baba zao ila makalio Sasa aisee 😂😂😁😍😍
Kwa Sasa usajili wa Bajaji umesitishwa hivyo zitapungua na kuwa replaced na usafiri wa Umma yaani daladala.
 
Kwahiyo kumbe unafanya comparison Kati ya Mwanza na Mbeya?
Nimeishi Dar, Sumbawanga,Singida,Arusha,Babati,Songea,Mwanza,Mpanda,Mbeya,Njombe nk..hapo sijataja sehemu nilizofika na kuishi Kwa mda mfupi kama wiki au Kupita tuu.
 
Naunga mkono hoja. Pia watu wake wana utu na ni waaminifu. Wanawake wa Mbeya ni kivutio kikubwa zaidi kisichotajwa sana... wamejaliwa makalio ya dunia nzima. Mimi niko mbioni kuweka makazi huko. Mbeya hakuna stress. Kuna unafuu na kibiashara pamekaa poa sana kutokana na connection yake na Malawi & Zambia.
 
Tanzania yote ni nchi nzuri sana duniani kama ulikuwa hujui, tembea kila mkoa, nchi takatifu sana hii, ina kila kitu, Mungu katupendelea sana.
Upo sahihi kila ukanda una jambo zuri.
Ila climatically mbeya ni ni 1.
Watanzania wengi hatujajua kutumia fursa adimu walizoziona mababu zetu.
Huwa naamini kuwa a Bantu man was very intelligent man whenn it come to land, they were very selective. A father of Bantu was geneous! walituchagulia maeneo mazuri sana ya kuishi tofauti na Nilotics, Kush, Khoi walichagua kuishi jJangwani na kwenye nyika.
Wabantu ndio wanamiliki maziwa makuu ya Afrika na Dunia, wanaishi ktk mabonde mazuri na mito mikubwa, waluweza kimiliki wanyama wa pori na wa kufugwa.
Tukumbuke kuwaenzi babu zetu wametuachia urithi mkubwa sana.
 
Nimeishi Dar, Sumbawanga,Singida,Arusha,Babati,Songea,Mwanza,Mpanda,Mbeya,Njombe nk..hapo sijataja sehemu nilizofika na kuishi Kwa mda mfupi kama wiki au Kupita tuu.
Okay


Kwahiyo ukaona Mbeya ni Bora kuliko kote
 
Vyote hivyo viko centralized,ingekuwa hivyo ungekuta Mikoa yote imepangwa..

Ukisema Mbeya haijapangwa Sasa Mwanza utasemaje? Dar Je?
Sijasema Dar, akileta mtu stori ya Dar tutoa mapungufu yao. Dar pamoja na mapungufu yao ila ule mji angalau unamuonekano wa jiji. Mwanza vilevile pesa inaonekana inafanya kazi. Mbeya ni jiji kubwa ila hakuna wenye pesa ndefu wakuweza kulifanta jiji liwe kama mwanza. Arusha dijawahi fika sipajui.
 
20221226_173917.jpg
20221226_173716.jpg
 
Mkoa wa Mbeya ni Kati ya Mikoa 5. iliyopo Nyanda za Juu Kusini sanjali na Mikoa ya Ruvuma,Iringa,Songwe,Njombe na Rukwa.Mbeya ilianzishwa mwaka 1961.

Mkoa wa Mbeya umejaaliwa kila kitu unachokijua wewe..

Kwa hapa Tanzania sijaona Mkoa Mzuri wa Kuishi kushinda Mbeya..

1.Kiuchumi.

Mbeya ni ya 3 Kwa kuchangia pato la Taifa yaani GDP Tanzania.

Mbeya ni ya 3 Kwa kuwa na Watu wenye kipato kikubwa.

 2.Hali ya Hewa na Mandhari.

Mbeya Ina Hali ya hewa ya majira yote yaani Bariadi na joto na mvua ni uhakika sio tia maji tia maji kama Mikoa mingine.

3.Usafiri

Uwanja wa ndege wa Songwe
Usafiri wa Barabara kutoka Mikoa yote na Nchi jirani Kupitia Barabara kuu ya Tanzam.
Usafiri wa kwenye Maji via Ziwa Nyasa.
Pia Kuna usafiri wa reli nzuri kabisa unakufikisha Zambia kutokea Dar.

4.Kilimo.

Mbeya Ina Ardhi nzuri ya kulima Kila aina ya zao kuanzia mbogamboga,matunda,nafaka Hadi pareto na chai.

5.Madini na Nishati.

Mkoa una Kila aina ya Madini kuanzia Dhahabu za Chunya Hadi Makaa ya Mawe ya Kiwira bila kusahau Madini ya gas asilia ya CO2.
Umeme ni WA uhakika unaozalishwa kutoka migodi ya Kiwira na Geothermal.

6.Elimu.

Mbeya ni Kati ya Mikoa ya Wasomi hapa Tanzania.Mkoa wa Mbeya una vyuo Vikuu zaidi ya 5 mfano MUST,Mzumbe,CuCoM,Udsm,Tumaini,nk.

Mkoa una mamia ya vyuo vya kati na shule za kutosha eg St.Francis hivyo ni ideal pia Kwa issues za Elimu.


7.Utalii

Hapa kwenye Utalii ndio Kuna fursa nyingi maana sehemu kubwa ni underdeveloped.

Kuna Milima ya kawetere,bwawa la Mungu,Hifadhi ya Kitulo na pia unafika Kwa urahusi Ruaha au Katavi NP kutokea Mbeya.

8.Viwanda na Biashara.
Kuna viwanda vya aina mbalimbali kama Saruji,vinywaji vikali na laini kama soda,bia,wine nk.
Kuna viwanda vya magodoro,vifaa vya ujenzi,home appliances nk.

Aisha kama unataka kujenga viwanda Kuna maeneo ya kutosha yametengwa Kwa Ajili hiyo.

Mbeya ndio Kitovu Cha Uchumi wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

9.Makazi na Accomodations.

Kuna fursa kubwa Bado ya ujenzi wa hoteli za kitalii na hoteli za kawaida maana ni Mkoa wa Biashara hivyo itakulipa.

Pia Hapa ni wewe tuu maana ujenzi wa Mbeya sio costful kama Mikoa mingine,unachagua ijengee tofauti au blocks au hata tofari mbichi udongo una nata vizuri kabisa..

10. Watu .

Mbeya Ina idadi ya watu zaidi ya mil.2.3 Kwa Mkoa mzima wanaokuhakikishia soko.

Aisha watu wake ni Wapambanaji ndio maana huwezi kusikia Mbeya ikitajwa kwenye mambo ya umaskini na shida ndogo ndogo,hawalalamiki kusubiria serikali.

Kiufupi hiyo ni summary ndogo sana Kati ya Mengi mazuri yaliyopo Mbeya,Karibuni sana Mbeya.




View attachment 2565229

Hiyo mikoa maisha mdebwedo sana inawafaa wavivu na wajinga Maana hutumii akíli nyingi kuishi.

Tanzania ni DAR, ARU, MWZ na DDOM tu. Kwingineko tutakuja kutalii tu kipindi cha likizo kupanga natural air.
 
Sahihi kabisa, nafurahi kuwa hapa, huu mfungo Sasa hakuna shida sijui ya futar, vyakula vyote vinapatikana tena kirahisi, natarajia kubadili kabila ivi karibuni na jina langu jipya nitaitwa Mwaluswaswa!!
 
Sijasema Dar, akileta mtu stori ya Dar tutoa mapungufu yao. Dar pamoja na mapungufu yao ila ule mji angalau unamuonekano wa jiji. Mwanza vilevile pesa inaonekana inafanya kazi. Mbeya ni jiji kubwa ila hakuna wenye pesa ndefu wakuweza kulifanta jiji liwe kama mwanza. Arusha dijawahi fika sipajui.
Kwani Mbeya Haina muonekano wa Mji?
 
Back
Top Bottom