Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Attachments

  • IMG_20241010_154153_210.jpg
    IMG_20241010_154153_210.jpg
    325.8 KB · Views: 2
Siyo kama Mbeya. Wala sina chuki kwa sababu mwenyewe imebidi niwepo Mbeya. Hali ya hewa na tabia ya nchi ya Mbeya ni nzuri. Hilo liko wazi. Lakini watu wa Mbeya mnaharibu kwa kujenga vibaya kila kona.
Wale wote ni wahamiaji wa.Sumbawanga,Songwe,Njombe na Iringa,majengo kule juu ndo origina plan ya mbeya kwenda Block T,Uzunguni pia na Soweto,maeneo mengine ni virugu.
 
Ya nini kujidanganya hali ya mji kama Mbeya? Inahitajika kupangwa upya. Hatupaswi kutegemea uzuri wa asilo wa hali ya hewa. Miji yetu inahitaji uzuri wa kutengenezwa kwa kuweka miundo mbinu ya maana ili iweze kuvutia uwekezaji wa biashara kubwa kubwa.

Imagine mji mnauona mkubwa kama Mbeya lkn haina Supermarket hata moja.
Mkuu watanzania hawapendi super market,zile za Dsm ni za Makaburu,watanzania wanapenda local life.
 
Mbeya inawezekana ndio jiji lenye miondombinu mibovu zaidi na makazi yasipangaliwa na duni pia, kuna nyumba za udongo na vijumba vya ajabu ajabu katika jiji!
Maeneo gani hayo mkuu,siku moja.nenda sinza nyuma ya Vunja bei panda gorofa lolote alafu xhungulia chini,hata mwanza panda
pale makoroboi au maeneo ya nata utaona vibanda umiza.
Vya kutosha.
 
Ila
Mabaya yake...
  • Ukimwi mwingi sana, yani sana.
  • Kila kituo daladala,kuna gesti pembeni
  • Imani za shirki nazo ni nyingi
  • Matukio yake ya uhalifu ni ya kibabe ,,Kupigwa nondo, kuchunwa ngozi,Kutobolewa macho,Kuteka wenye alama M kwenye viganja.
  • Hakuna Usalama mida ya usiku,kuanzia saa 4
  • Ajali nyingi sana
  • Utumizi wa Mikorogo ni mwingi
  • Unywaji wa pembe kali.
  • Sehemu za kwenda kutembea hasa siku za mapumziko ni chache sana.
  • Ujenzi holela, aiseeh.
Siwezi laumu kwenye barabara, kwa maana Jiografia yake Milima sana.
Kutembea panda.mrima.mbeya,tembea uzunguni kwa sugu hotel,nenda Soweto na mama John Kuna vibe huko Ilomba na uyole,ukiona vipi nenda tukuyu na usisahau kwenda vwawa one time,ukiona pia nenda.mbalali Kuna view nzuri sana.
 
Kwa Mbeya mjini hapana mkuu.Danganya wasiofika.
1.Poor Infrastructures,barabara za mitaaniu ni vumbi&giza
Hata taa za mitaani shida..
Soko changamoto
(Sijaona cha maana pale Mwanjelwa,Kabwe & Soweto)
Stand za bus mjini na nanenane ni aibu,hakuna majengo ya maana ya stendi kama zilivyo Msamvu Terminal,Magufuli Terminal,Dodoma(88) Terminal etc
2.Poor housings etc
Labda pembezoni huko.
Vijumba vingiii kuliko nyumba za maana.
Isipokuwa taasisi tu
NB;
Kwa hali ya hewa ni pazuri✓
Utalii wa mandhari asilia✓
Hoteli Nzuri ×
Wingi wa watu✓
Vyakula✓
Nahisi mlivyomkwaza jiwe kipindi kile, aliamua kuwatelekeza kimiundombinu😅😅
Nashauri utembelee mikoa mingine.
Hizo stendi zote zilitamalaki kipindi cha Miaka 17 iliyopita,ni swala la muda na mipango Jiji wataliweka sawa hilo
 
Kwa Mbeya mjini hapana mkuu.Danganya wasiofika.
1.Poor Infrastructures,barabara za mitaaniu ni vumbi&giza
Hata taa za mitaani shida..
Soko changamoto
(Sijaona cha maana pale Mwanjelwa,Kabwe & Soweto)
Stand za bus mjini na nanenane ni aibu,hakuna majengo ya maana ya stendi kama zilivyo Msamvu Terminal,Magufuli Terminal,Dodoma(88) Terminal etc
2.Poor housings etc
Labda pembezoni huko.
Vijumba vingiii kuliko nyumba za maana.
Isipokuwa taasisi tu
NB;
Kwa hali ya hewa ni pazuri✓
Utalii wa mandhari asilia✓
Hoteli Nzuri ×
Wingi wa watu✓
Vyakula✓
Nahisi mlivyomkwaza jiwe kipindi kile, aliamua kuwatelekeza kimiundombinu😅😅
Nashauri utembelee mikoa mingine.
Kuna vitu vingine mnaongea kama mnachekesha au msiokuwa na akili.Kuna Mji Nchi hii ambao Barabara za Mitaani zote ni vumbi? Kama unadai hakuna hata kidogo nikuoneshe picha za Barabara za Mitaani?

Stendi sio hayo majengo unayodai wewe,kote yalikojengwa yamekaa hayatumiki,Sasa ni mpumbavu tuu ndio anaweza ona ni jambo la kujivunia kumwaga pesa harafu hazizalishi popo wanaishi kuanzia Dodoma, Magufuli, Sumbawanga,Iringa,Mwanza kote huko majengo Yako iddle yanazidi kuzeeka.So Mbeya hawatakiwi kuiga upuuzi huu ,majengo yaje kujengwa pale tuu yanapohitajika.By the way ujenzi wa Stendi Mpya unaendelea Old Airport.

2.Poor housing ni tofauti kabisa na mipango Miji.Poor housing kulinganisha na wapi labda ambako hakuna Vijumba.Wanaoweza kuleta jeuri Kwa Mbeya ni Dodoma mjini tuu,huko Mikoa mingine kuna Vijumba vya mafukara kama wote ikiwemo Dar achilia mbali vimikoa vyenu vingine vya hovyo.

Mwisho Jiwe alijenga miundombinu wapi hapa Tanzania,nitajie nikuoneshe huko kwenu kunavyofanana.
 
Nimesema along the road.
Mbeya hakuna pulling factor ktk mji.
Mwanza kuna ziwa linaloleta utitiri wa watu. Kuna viwanda vya samaki, biashara ipo juu. Ni center ya mikoa ya Shy, Kagera, Mara, Tabora, Singida nk.
Mbeya ipo pembezoni sana watu wa Njombe ndio wamejaa. Mwanza iache tu kama ilivyo mbeya haitakuja kuifikia.
Mbeya asilimia kubwa wanategemea kilimo cha kujikimu, hawana ufugaji mkubwa,wala uvuvi, viwanda vichache sana kulinganisha na majiji mengine.
Wewe hoja zako Zina matege ya mahaba Kwa Mwanza 😂😂

Sasa Kwa taarifa Yako tuu Mwanza Haina tofauti sana na Mbeya na in fact Bora hata Mbeya.

Eti Mbeya hakuna polling factor 😁😁.Unaijua unachoongea lakini? Kwamba mtu anaweza Toka huko Tabora kuja Mwanza Kwa Ajili ya Ziwa?Kwamba Ziwa ndio linampa hela au?

Aliyekudanganya kwamba Mbeya hakuna viwanda ni nani? In fact Mbeya Kuna viwanda ambavyo Mwanza havipo mfano Mbeya Cement,TBL,Viwanda vya Spirits,soft drinks mfano Mohamed Enterprises ana kiwanda Cha soft drinks Mbeya ,Mwanza hakuna nk

Mbeya ndio economic hub ya Nyanda za Juu Kusini,Mikoa ya Njombe,Rukwa,Songwe,Njombe,Ruvuma na kiasi kidogo Iringa vinategemea Mbeya japo Iringa sio sana Kwa sababu ya Dodoma.Kwa taarifa Yako tuu hiyo Njombe unayosema Iko mbali ,75% ya shughuli zao za biashara wanategemea Mbeya.Mbeya itakuja kuipita Mwanza subiria Barabara kuu zote zifunguke na migodi ianze kufanya kazi.

Unavyozungumzia Kilimo Cha Kisasa hapa Tanzania basi Mbeya wapo,watu wanalima commercial farming hawajikimu ,eg Mbeya ndio inaongoza Kwa fertilizer consumption hapa Tanzania wewe hujui kitu.

Mwisho Mkoa wa Mbeya ni WA Kimkakati hatutegemei sekta chache unategemea sekta lukuki kuanzia Kilimo Hadi Madini ya Chunya.Takwimu za Uchumi (GDP) hazidanganyi 👇👇
Screenshot_20240903-203253.jpg
 
Daraja zuri lakini angalia background hapo hizo nyumba za tope kila mahali, na hapo ndio maeneo yenu ya kula bata, kutwa nzima kukesha kwenye makanisa na mambo ya kishirikina na kupiga umbeya kama jina la mkoa wenu.
Onyesha hiyo nyumba ya tope.Unajua Hilo daraja liliko kwanza?
 
Mbeya.Mbeya itakuja kuipita Mwanza subiria Barabara kuu zote zifunguke na migodi ianze kufanya kazi.
Wewe una mahaba na mbeya.
Kwa hio hivyo ulivyotaja ndio viwanda ? Umewahi fanya kazi au ingia pale TBL. Malighafi gani inauzwa na watu wa mbeya mle kiwandani ? Kiwanda cha bia fully automation hakuna mamia ya waajiliwa pale wala hakuna value chain, ngano inatoka nje. Pale c4ment mnauza miamba ya kusagia cement ?
Mwanza fish industry inatosha kuzipita huto tuviwanda tote twa mbeya. Ykisikia nchi za maziwa makuu ujue Vi toria ndio baba yao.
Mbeya haitakaa iipite Mwanza kamwe labda wakati tumezeeka au tumerudi kwa maulana.
Mbeya ni mkoa wa wachuuuzi. Hakuna mzunguko wa hela pale. Mbeya ndio mkoa unaongoza kwa subsistence farming ukiondoa mbalali watu wanalima tu portion portion sasa utatajirika kwa kulima chini ya heka 100. Kumkuta ntu anamiliki heka 100 za avocado ni hadithi ya abunuwasi wenzenu Njombe wapo wanaomiliki mpeka heka 700 nawajua trna ni watu wabkawaida hawanw title. Mbeya Shsmba kubwa ni Rungwe Avo ado ambao wana heka 800.
Ukija sekta ya viazi mviringo yaani ni majanga na aibu bora hata nisiseme.
Tukiandika humu usidhani hatujaishi huko. Ukianzia mbalizi mpaka kule juu umalila ni wapi utaona mtu katandika mkeka wa kueleweka ? Njoo uyole mpaka kyela kuna shamba gani kubwa zaidi ya tu plot plot kama viwanja vya mjini. Njoo ukanda wa mwakaleli na busokelo wapi kuna mahekta ya kilimo ? Unaweza ona kidogo chai ukanda wa ushirika, tena nayo ni dead industry.
Ndizi ndio zao la walala hoi. Sijawahi ona mtu katajirika kwa ndizi kama ilivyo chai. Unataka kuniambia chai ni pulling factor kama pamba ?
Zaidi ya bonde la mbalali mbeya hakuna pulling factor inayoweza kuita watu wawekeze zaidi ya dwellers. Mtu mwenye akili zaKe ni bora akawekeze kilimo Songea, katavi, moro, Njombe.
Mbeya ni mkoa wa kuganga njaa na ndio maana wanachelewa kuamka na wanawahi kulala.
Mpaka SGR kupelekwa mwanza sio jambo dogo.
 
Back
Top Bottom