Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Mwisho kuhusu Mbeya ni kwamba udongo wake ni kama Saruji ukichoma zile tofali unapunguza ubora so una option ya kujengea mbichi au blocks..

Mkuu ujenzi wa tofali za kuchoma kwa Mbeya mjini umekuja baadaye sana, mimi mwenyewe nimeishi sana tu kwenye hizo nyumba za tofali tope...

Nonde, Simike,Sinde, Nzovwe, Mbalizi, Makunguru, Ilomba, Uyole na hata miji mipya kama Nsalaga huku kote nyumba zilizopo ni za matofali ya matope yale...

Kuna miaka serikali ya mkoa ilipitisha amri ya ujenzi wa tofali za kuchoma, ndio walau afadhali watu wakaanza choma matanuru ya tofali na kwa waliokuwa na nyumba tayari, wakaambiwa wapige "lipu"...

Mwisho umewahi kuona zimevunjika? Umewahi sikia nyumba zimepotomoka? Acheni kukariri maisha na vitu msivyovijua Kila kitu Kiko determined na nature na huo ndio uzuri na upekee wa Mbeya

Haziwezi vunjika kwa sababu zinajengwa vizuri, isipokuwa zinaharibu muonekano wa mji kwa namna zilivyo...Hazivutii machoni...
 
Huu mji umechoka inabidi uvunjwe ujengwe upya. Ni mji mkubwa ila sio mzuri kimpangolio ispokuwa sehemu kadhaa.
Mbeya ingepangwa mji ungekuwa mzuri no 1.
Geographically ni no1.
Mwanza itaendelea kuiacha Mbeya daima kwa sababu Mbeya wanaendelea kujenga holela sasa sijii kwa nini serikali haingilii kati na kuzuia kujenga holela.
Wanyakyusa na ndugu zao wasafwa hawazingatii mpango mji japo ni watu wanaojenga sana pengine kuliko makabila mengi.
Ujenzi holela umesababishwa na Serikali.

Ilipaswa panga makazi tokea ilipopata uhuru

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Bajaji nyingi Sana kule

Hakuna migahawa mizuri mjini hakuna

Watu wa mbeya ni wastaarabu Sana huwezi lala njaa kule labda uamue unaweza anza na mmama mmoja Kansani unaenda kwingine unawasalimia tu [emoji23][emoji23] utakaribishwa chakula watakupa na ndizi au karanga uende nazo Hafu fresh tu hawana noma

Wadada wa mbeya sura za baba zao ila makalio Sasa aisee [emoji23][emoji23][emoji16][emoji7][emoji7]
Pia wana ukarimu sana dada zao.
Huhitaji maneno mengi kama wataka shinda udiwani.

Upishi wa chakula Mbeya na ukanda wote huo ni 0



Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Mkuu ujenzi wa tofali za kuchoma kwa Mbeya mjini umekuja baadaye sana, mimi mwenyewe nimeishi sana tu kwenye hizo nyumba za tofali tope...

Nonde, Simike,Sinde, Nzovwe, Mbalizi, Makunguru, Ilomba, Uyole na hata miji mipya kama Nsalaga huku kote nyumba zilizopo ni za matofali ya matope yale...

Kuna miaka serikali ya mkoa ilipitisha amri ya ujenzi wa tofali za kuchoma, ndio walau afadhali watu wakaanza choma matanuru ya tofali na kwa waliokuwa na nyumba tayari, wakaambiwa wapige "lipu"...



Haziwezi vunjika kwa sababu zinajengwa vizuri, isipokuwa zinaharibu muonekano wa mji kwa namna zilivyo...Hazivutii machoni...
Baada ya kuishi umeona Zina shida gani? Kama wewe ni WA Mbeya tofali mbichi na zilizochomwa zipi ngumu?
 
Tupo wengi ukichukua wastani Lazima tuoneka tupo Chini.

By the way kipenda Roho
hula myama mbichi. Ila Tanzania ni mikoa niliyokutajia Kwa huduma za uhakika
Kwahiyo mpo wengi kushinda dar ama sielewi. Mbeya pana pesa sana labda kama ulikuja na biashara yako ya kuuza senene.
 
Kwahiyo mpo wengi kushinda dar ama sielewi. Mbeya pana pesa sana labda kama ulikuja na biashara yako ya kuuza senene.
Kwanza hao wanaojisemesha ni aidha wanasimuliwa au waliishi miaka hiyo.
sijui inakuaje mtu anashindwa kuelewa kwamba Miji inakua na shughuli zinaongezeka za Kila aina..

Mbeya mjini plus Mbalizi inaleta jumla ya watu 650,000 Hawa watu sio wachache Kwa mjini hapo Bado mawilaya nk.
 
Niliaminigi maneno ya wanyakyusa nikaenda uko 2009 nilikutana vumbi kama poda kipindi hichi watu wanakula nondo za utosi saa moja jioni wote ndani ukitaka kwenda hata dukani inabidi uvae helmet kulinda fuvu
[emoji1787] nimecheka kwenye kulinda fuvu[emoji1787][emoji1787]
 
Sababu za kihistoria.
Mfano Kigoma imezungukwa na nchi zenye vita muda wote nani ataenda kuwekeza? Serikali haikujenga barabara mapema, mkoa upo pembezoni sana. Kutoka tabora mpaka kigoma mapori makubwa sana hakuna mwingiliano.
Kusini haikukuwa na barabara nzuri kama mbeya. Tanga ni jiji hivyo lina hadhi sawa na Mbeya, Tanga inashindwa na Dar na pwani as a pulling factor, kwa sababu ni karibu hivyo Dar inawavuta zaidi kuliko Tanga, Kuna mambo mengi sana ktk kukua kwa miji.
Ni sawa ba kusema lwa nini Tunfuma inakua kuliko Mbalali.
Hivi Mbeya usipolima na kuwa mchuuzi wa mazao utafanya ishu gani nyingine,.
Fursa ya mipaka inatimiwa na wageni zaidi kuliko wenyeji.
Vitu vingi vinasafirishwa kwenda mikoani badala nje ya mipaka, kwa hio Mbeya imekuwa njia panda ya wageni badala uwe fursa kwa wanambeya.
Kaskazini wanajitahifi zaidi kusafirisha mazao kenya kuliko kusini.
Tujadili ktk mtazamo chanya sio hasi maana hii mikoa tunaishi wote, hivyo maendeleo ni ya wote.
Kwahiyo umeamua kutupangia shuguli ya kufanya wanambeya. Haya sasa wanambeya tumeamua kulima tu tunatoa tani na tani kila siku za mazao ya kilimo eheee mwanza mnafanya nini
 
Baridi na HIV ni balaa huko.Sipapendi Mbeya.Pachafu na wale Nguruwe wanaozurura kila kona hapana aisee.Bora nikaishi Kigoma kuliko Mbeya.
Wewe utakua ni mkimbizi tu unatuzuga hakuna mahali pazuri kama mbeya apa nimelala zangu kaubaridi safi niamke niende soweto mchana nikagonge kitimoto
 
Wewe ni mwenyeji wa Mbeya?

Ni jiji gani Tanzania hapa ushawahi ona lina nyumba za udongo kama si Mbeya?
Arusha kimandolu kijenge juu chini ungalimited na kwingineko hata dar kariakoo kuna nyumba za udongo we umezaliwa kahama ukakulia kahama huwezi yajua haya
 
Kwanza hao wanaojisemesha ni aidha wanasimuliwa au waliishi miaka hiyo.
sijui inakuaje mtu anashindwa kuelewa kwamba Miji inakua na shughuli zinaongezeka za Kila aina..

Mbeya mjini plus Mbalizi inaleta jumla ya watu 650,000 Hawa watu sio wachache Kwa mjini hapo Bado mawilaya nk.
Na mbeya inajengwa na wanambeya ukiona magorofa hakuna la muhindi wala mwarabu na ya taasisi za serikari ni machache sana. Hotel za mbeya zinamilikiwa na wanambeya huyo yeye alikuja kua dalali mbeya akapaogopa
 
Mkoa wenyewe imejengwa hovyo hovyo hasa Mbeya mjini kuliko mkoa mwingine wowote hapa Tanzania.
Miundo Mbinu mibovu kuliko mkoa mwingine wowote.
Mbeya mjini wameharibu jiografia kwa kujenga hovyo hadi kwenye vimilima kama kile cha Ilemi, cha Simike! Skwataz everywhere.

Kama vile Manzese,Vingunguti,Buguruni,Kwa Mnyamani au Mbagala??
 
Back
Top Bottom