Hakuna mwanasiasa/Rais aliweza kupambana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na akashinda!

Wale maaskofu wale ni Watanzania kweli kweli.

Mungu awalinde Maaskofu, Msheikh, wachungaji, maulamaa, wanazuoni, wainjilisti, waalimu wa dini na watumishi wote wanaotumikia imani zao hapa Tanzania
 
Mbona pamoja na nguvu kubwa waliyowekeza kumfanya Padri Slaa awe Rais 2010 lkn waliangukia pua kwa JK
 
Usitake kuchochea kisichokuwepo.

TEC haishindani na serikali, kile sio chama cha siasa. Hakuna vita yoyote kati ya TEC na serikali isipokuwa kuna raia tusioafiki walakini uliojitokeza katika mkataba wa bandari. TEC ni mjumbe wa raia wakatoliki na tusio wakatoliki. SAUTI YA WATU SAUTI YA MUNGU, siyo sauti ya TEC.
 
Mungu - Yehova muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo katika Yesu Kristo mwokozi wa ulimwengu ukiwemo wewe. Soma👇👇

Yohana 3:16-18 SUV
"
...Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu..."

Kama huamini hayo☝️☝️ maneno hilo ni tatizo lako la kutoamini. Ila siku hiyo utakuja kushangaa kukumbushwa kuwa alitokea mtu kwenye mtandao mmoja wa kijamii uitwao Jamii Forum akakuambia habari zangu lakini hukuamini..


 
Kwa kiwango kikubwa nakubaliana na hoja zako!

Ni mjinga anayeweka maisha yake kwa wanasiasa. Wanasiasa ndio wanatakiwa wayaweke maisha yao ya kisiasa kwa wananchi.

Mkataba wa serikali na DP World ungekuwa hauna matatizo hata mimi ningewaunga mkono!
 
Mkuu, hii dhana ya kuwalaumu "washauri" wa Rais mnaitoa wapi? Kwa hiyo huyu Rais hatumii uwezo wake katika kupambanua mambo?
 
hawa jamaa wameletwa na Mungu, wametufumbua macho, pamoja na kwamba bado kuna watu wapo gizani na wengine macho wanayo ila hawataki kuona.
Kwa kweli wamefanya kazi ya kitume katika tamko lao kuhusu mkataba wa serikali na DP World
 
wamissionari au TEC ni kweli wana nguvu pitia historia yao ndiyo chimbuko la ukoloni Afrika, kukomesha biashara ya utumwa,nchi nyingi kupata uhuru etc they are very influencial
Uhuru wakoloni(corporates) waliamua kuachana na ukoloni wa kale na kuja na ukoloni mamboleo,kwa kuwa walifuata malighafi wakabuni njia mpya ya kupata malighafi zilezile bila ya migongano na makoloni yao, biashara ya utumwa kukoma ni baada ya mapinduzi ya viwanda,siyo kanisa,usiwape credit ziso zao
 
Mbona pamoja na nguvu kubwa waliyowekeza kumfanya Padri Slaa awe Rais 2010 lkn waliangukia pua kwa
Angalia utachekwa sana kwenye huu mjadala unapiga Dana Dana na kuruka ruka! Hata yeye akisoma atakushangaa.
 
Kwa kifupi kabisa, Viongozi wa Serikali yetu hawawezi hata kidogo kushindana na TEC.
TEC hawana tabia ya kuropoka ropoka, lakini wana power kweli kweli.
 
Kojoa ukalale sasa!!
 
Watanzania wengi bado ni wazalendo.

Unaweza kuwachezea watanzania wengi kwa mambo ambayo hayana athari kubwa kitaifa lakini sio kwenye mali za asili na adhimu kama bandari zote za nchi.

Hii ngoma bado ni pevu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…