Hakuna mwanasiasa/Rais aliweza kupambana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na akashinda!

Hakuna mwanasiasa/Rais aliweza kupambana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na akashinda!

Usahihi kamili wa hoja yako ni huu:

"Hakuna serikali yoyote ya kidunia (ikiwemo ya Tanzania) inaweza kupambana na kupingana na KANISA LA MUNGU na serikali hiyo ikaendelea kuwepo na kusimama..!"

TEC ni sehemu (kipande tu cha kanisa la Mungu). Lakini ukweli mkuu ni kuwa wapo watu wengi (jeshi la Mungu aliye hai hapa Tanzania) kote nchini (ukiacha TEC ambao wametoa official statement ya kukataa mpango huu wa Rais samia) ambao wanafunga na kuomba mchana na usiku kuhakikisha kuwa Mungu anaiponya nchi hii toka Kwa hayawani hawa..

Na mfano ulio dhahiri wa kuwa KANISA LA MUNGU liko kazini ni Mch. Mbarikiwa Mwakipesile na wafuasi wake huko Mbeya wanaomba usiku na mchana wakisema kwa uwazi bila kificho wala kumung'unya maneno kuwa Mungu aiangushe na kuipoteza CCM na serikali yake huku matangazo ya ibada zake yakirushwa live katika channel yake YouTube...

But all in all, huu ulioandika kwa ujumla wake ndiyo ukweli na wote wanaopingana na KANISA LA MUNGU wanajisumbua na kujipaka kinyesi tu...

Na ni kweli hii 👇👇👇 statement ya TEC ndiyo iliyomaliza na kuua kila kitu kabisa..!!

".....Hivyo tukiwajibika kimaadili, tunaona ni jukumu la serikali kusikiliza wananchi wanaotaka mkataba huu ufutwe. Kwa kuwa tumeonesha kuwa Tanzania tumeshawekeza na kuendeleza bandari, reli na bandari za nchi kavu; niwajibu miradi hii tuiendeshe Watanzania wenyewe huku tukikaribisha ubia tunaoudhibiti wenyewe. Hiki ndicho wananchi wanachokililia kusudi tujenge uwezo wetu wenyewe. Kwa vile tumegundua mapungufu yetu ya uendeshaji wa bandari, tunaweza kujizatiti kurekebisha mapungufu hayo wakati njia za kiuchumi zikibaki mikononi mwetu. Kwa sababu hizo na maelezo yote ya hapo juu, sisi Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania hatuungi mkono Mkataba huu”.

This is bold and most importantly authoritative statement. No any other authority will surpass this!!
Mkuu unaweza nipa link nikayaone hayo maombi?
 
Acha Kuwa na Upeo Mfupi..., TEC wanaungwa mkono na wataungwa mkono kama wanachopambania / wanachokieleza at any given time kina manufaa kwa Taifa; Kwahio leo wakisema nchi iwe ya Imani yao, au wapate vitu kwa manufaa yao binafsi unadhani watashinda au kuna atakayewasikiliza ?!!!

Nyie ndio mnaoamisha struggle za kitaifa na kuzipeleka kuwa struggle za kidini / kiimani - na kwa kufanya hivyo hamjengi bali mnabomoa
Punguza hasira na siku zote TEC hawajawahi kuishinikiza au kuitaka serikali juu ya mambo yasiyokua ya manufaa kitaifa in favor ya mambo ya kanisa. Siku zote wamekua wakiadress national issues. na hata katika waraka wao hakuna jambo lolote au statement yoyote iwe kwa uficho au kwa uwazi imejielekeza kwenye maslahi au mahitaji ya kanisa.
 
Acha Kuwa na Upeo Mfupi..., TEC wanaungwa mkono na wataungwa mkono kama wanachopambania / wanachokieleza at any given time kina manufaa kwa Taifa; Kwahio leo wakisema nchi iwe ya Imani yao, au wapate vitu kwa manufaa yao binafsi unadhani watashinda au kuna atakayewasikiliza ?!!!

Nyie ndio mnaoamisha struggle za kitaifa na kuzipeleka kuwa struggle za kidini / kiimani - na kwa kufanya hivyo hamjengi bali mnabomoa

Mkuu, ninachokiona katika hoja zako ni personal incredulity fallacy!

Yaani kwa fikra zako unadhani TEC kwa historia yake nchini wanaweza kupambania suala ambalo halina maslahi kwa taifa?

Nadhani wewe ndiye unayedhani hoja za TEC niza kidini.
 
Hao jamaa wana siri zenu kibao na huwa mnarekodiwa pale mnapo ungama kwaiyo wale pedophiles kwa akili zako wako juu ya serikali na waislamu wote na walutheri
 
Nashauri TEC ndio liwe Bunge letu.
Maana wanaiwezo wa kusoma na kuitahadharisha Serikali mambo ya msingi kama mikataba ya Kimangungo.
Nawashangaa sana wanaoipinga TEC.
TEC imeishauri vizuri Serikali dhidi ya Hila Za Waarabu na Vibaraka wao wa humu nchini wanao waona Waarabu kama Miungu yao.
Huku Bunge likipiga makofi pwa pwa pwa na kushangilia bila hata ya kuusoma na kuuelewa huo Mkataba.

TEC ndio liwe Bunge letu.
Hao wabunge waache wakutane Dodoma na kula ruzuku ya Serikali maana ndicho wanancho kipigania.
Ikiwezekana libinafsishwe kwa DP World.
 
hapo vipi 👇👇👇👇👇👇👇
 
Kwani ni uongo nyie hamuendi kutubu na kuomba binadamu mwenzako akusamehe dhambi 😁
Yakobo 5:16 Kwa hiyo ungamianeni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana ili mpate kuponywa. Maombi ya mwenye haki yana nguvu tena yanafaa sana.
Matayo 18:18 Kwa hiyo ungamianeni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana ili mpate kuponywa. Maombi ya mwenye haki yana nguvu tena yanafaa sana.

ndio maana ya falsafa elimu ya elimu zote na ndo mana ya theology elimu ya dini sio kukariri hata usivyovijua/
 
Mithali 26: 4-12: Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Asije akawa mwenye hekima machoni pake. Apelekaye ujumbe kwa mkono wa mpumbavu Hujikata miguu, na kunywa hasara.
Mmedanganywa na kukuzwa na Nyerere wapumbavu hamna mnalojua...Kama sio Nyerere msingkuwa na sauti .
 
Mkuu kwanza karibu,
Ni kitambo sana kukuona humu,mara ya mwisho ni GE 2020 ambapo wewe ulikuwa ni timu JPM miye timu ENL

Tulitofautiana Kwa mengi,ila Leo tunaongea lugha moja

Mkuu, shukrani sana!

Kutofautiana kimsimamo sio jambo baya kama halileti chuki binafsi.

Kukubali kutokubaliana ni moja ya msingi wa nafsi kwa binadamu.

Tuko pamoja!
 
Back
Top Bottom