Hakuna nadharia yoyote ya Kisayansi inayoelezea kikamilifu chanzo cha ulimwengu

Hakuna nadharia yoyote ya Kisayansi inayoelezea kikamilifu chanzo cha ulimwengu

Binadamu siku zote ni dhaifu, hivyo hivyo kwa wanasayansi

Si kila kitu kwenye sayansi ni cha ukweli/uhakika

Sayansi hii hii ndio unatufundisha kuwa binadamu alitokana na jamii ya sokwe, je ni kweli??

Sayansi hii hii inatuambia kwamba twiga wa zamani walikuwa na shingo fupi, nyoka walikuwa na miguu nk,. Je ni kweli??


Sayansi inashindwa kuthibitisha imani za kishirikina, je hazipo


Kuna watu wanashindwa kupona magonjwa mahospitalini (kisayansi) ila wanapona kwa waganga, masheikh au wachungaji, ila bado sayansi haikubali


MWISHO

Sayansi inacover eneo lake, dini ina eneo lake
Ni chanzo kipi kilichofanikiwa kutoa majibu ya hayo maswali ambayo sayansi imeshindwa?
 
1. Sayansi haijawahi kusema nadharia zake zimekamilika. Ukisikia mtu anakwambia nadharia ya sayansi imekamilika, ujue huyo hajui sayansi ni nini.

Mwanafalsafa nguli Kurt Godel aliandika "Godel's Incompleteness Theorems" zinazoelezea kwa undani kabisa suala hili.

Nakushauri uzisome na kuzielewa.

2. Kupinga uwepo wa Mungu ni kitu kimoja, nadharia za kisayansi ni kitu kingine. Mtu anaweza kupinga uwepo wa Mungu kwa kutumia mantiki na falsafa tu, bila kuhitaji nadharia yoyote kati ya hizi za kisayansi.

Kwa mfano, proof by contradiction, using the problem of evil, inaweza kupinga uwepo wa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote (kama wa Biblia na Quran) bila kuhitaji nadharia yoyote ya sayansi.

Ni sawa na kuweza kujua kwamba 10 si square root ya 2 bila kujua square root ya 2 ni nini.

Ni kama kujua binti mchanga mwenye umri wa miezi 6 leo hawezi kuwa mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 30 leo, bila hata kumjua mama mzazi wa huyo mwanamme mwenye miaka 30 ni nani.

Ni kama kujua the sum of two even numbers will always give you an even number, without knowing all numbers.

Kitu kikubwa kuelewa ni kwamba, hata katika sayansi, huhitajibsayansi ikamilike, au huhitaji hata kujua jibu sahihi la kisayansi, ili kujua kuwa jibu fulani si sahihi.

Kwa maneno mengine, hata kwenye sayansi, tunaweza kuwa hatujakamilisha jibu la ulimwengu umeanzaje, lakini tukajua kuwa jibu la Mungu yupo na ndiye aliyeumba ulimwengu tukajua si la kweli.

carnage21

1. Sayansi haijawahi kusema nadharia zake zimekamilika. Ukisikia mtu anakwambia nadharia ya sayansi imekamilika, ujue huyo hajui sayansi ni nini.

Mwanafalsafa nguli Kurt Godel aliandika "Godel's Incompleteness Theorems" zinazoelezea kwa undani kabisa suala hili.

Nakushauri uzisome na kuzielewa.

2. Kupinga uwepo wa Mungu ni kitu kimoja, nadharia za kisayansi ni kitu kingine. Mtu anaweza kupinga uwepo wa Mungu kwa kutumia mantiki na falsafa tu, bila kuhitaji nadharia yoyote kati ya hizi za kisayansi.

Kwa mfano, proof by contradiction, using the problem of evil, inaweza kupinga uwepo wa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote (kama wa Biblia na Quran) bila kuhitaji nadharia yoyote ya sayansi.

Ni sawa na kuweza kujua kwamba 10 si square root ya 2 bila kujua square root ya 2 ni nini.

Ni kama kujua binti mchanga mwenye umri wa miezi 6 leo hawezi kuwa mama mzazi wa mwanamme mwenye miaka 30 leo, bila hata kumjua mama mzazi wa huyo mwanamme mwenye miaka 30 ni nani.

Ni kama kujua the sum of two even numbers will always give you an even number, without knowing all numbers.

Kitu kikubwa kuelewa ni kwamba, hata katika sayansi, huhitajibsayansi ikamilike, au huhitaji hata kujua jibu sahihi la kisayansi, ili kujua kuwa jibu fulani si sahihi.

Kwa maneno mengine, hata kwenye sayansi, tunaweza kuwa hatujakamilisha jibu la ulimwengu umeanzaje, lakini tukajua kuwa jibu la Mungu yupo na ndiye aliyeumba ulimwengu tukajua si la kweli.

carnage21
Yeah ni kweli udhaifu wa theories hizo hauthibitishi uwepo uwepo wa Mungu, kwasababu hata kabla hazijatungwa watu walikuwa wakiamini katika Mungu.

Swali la msingi, ni yapi maelezo ya sayansi juu ya kuumbwa Kwa Ulimwengu? Je sayansi haina majibu juu ya chanzo cha Ulimwengu?
 
Kuna pande kuu mbili,

Kuna wanaoamini uwepo wa Mungu na wale wasioamini uwepo wa Mungu.

Wasioamini uwepo wa Mungu wanasema, Kila kitu kinacho-exist,uwepo wake lazima uelezewe kisayansi. Swali, kisayansi Ulimwengu ulianzia wapi?

Kundi la pili ni la wale wanaoamini uwepo wa Mungu. Hawa Imani yao inasema si mambo yote yanaweza kuelezewa Kwa akili ya binadamu. Kwaiyo ukimuuliza muumini nini chanzo cha baadhi ya mambo, hawezi kukupa jibu kwasababu msingi wa Imani yake ni kuwa si kila kitu kinaweza kuelezewa na binadamu. Huo ndio Msingi.

Tunapowauliza kuhusu chanzo cha Ulimwengu, na vitu vingine inabidi mtuonyeshe kwasababu msingi wa imani yenu ni kuwa Kila kitu hutokea kisayansi.

Mkituuliza Mungu alianzia wapi, sie jibu letu ni fupi tu kuwa yeye Hana chanzo wala mwisho. Na mkisema hili linawezekana vipi, basi tutasema msingi wa tunachoamini ni kuwa Kuna baadhi ya mambo yana limit.

Nyinyi sasa ambao mnaamini kuwa Kila kitu kinatokea kisayansi mnalo jukumu la kuelezea kila kitu kinachoonekena bila kurukaruka.
Dunia Haina mwanzo wala mwisho.

Hakuna kitu kinachoweza kuwepo from nothing...

Ukisema Dunia ina chanzo lazima ueleze na uthibitishe chanzo hicho cha Dunia kilitokea wapi?

Na huko chanzo cha dunia kilipokuwa, kulitoka wapi?
 
Dunia Haina mwanzo wala mwisho.

Hakuna kitu kinachoweza kuwepo from nothing...

Ukisema Dunia ina chanzo lazima ueleze na uthibitishe chanzo hicho cha Dunia kilitokea wapi?

Na huko chanzo cha dunia kilipokuwa, kulitoka wapi?
Hizi hoja zako umezotoa wapi, ni according to science au ni mawazo yako?

Nina mashaka kama hata unajua tofauti kati ya Dunia na Ulimwengu.
 
Yeah ni kweli udhaifu wa theories hizo hauthibitishi uwepo uwepo wa Mungu, kwasababu hata kabla hazijatungwa watu walikuwa wakiamini katika Mungu.

Swali la msingi, ni yapi maelezo ya sayansi juu ya kuumbwa Kwa Ulimwengu? Je sayansi haina majibu juu ya chanzo cha Ulimwengu?
Kuamini katika Mungu pia hakuthibitishi uwepo wa Mungu.

Kwa nini unafikiri ulimwengu uliumbwa au ni lazima uwe na chanzo?

Unalichukulia hili kama jambo ambalo limeshapitishwa bila mgogoro wala swali, hii si kweli.

Kwa nini unafikiri ulimwengu uliumbwa na ni lazima uwe na mwanzo?

Unajuaje kwamba, tukizama katika ukweli wa ulimwengu halisi ulivyo, suala zima la mwanzo, katika jambo lolote lile, achilia mwanzo wa ulimwengu, ni suala linaloweza kutazamwa kama jambo la uhakika na si suala la tafsiri yetu tu ya ulimwengu kama tunavyouona, lakini kihalisia, si jambo lililopo kiuhakika?

In quantum physics, entanglement, what Einstein called "spooky action at a distance", as well as "quantum causal loop", remove any primacy and certainty on cause and effect.

At that level, you can end up with a cause A, which has the effect B, but also, that very event B being the cause of cause A in a "quantum causal loop".

Yani kama vile, mama yako wewe ni A aliyekuzaa wewe mtoto B, halafu wewe mtoto B pia ni mzazi wa mama yako huyo A.

A kamzaa B na B kamzaa A.

Quantum causal loop.

Hapo utasema nani chanzo?
 
Nisikilize mkuu Ahmet

Tusioamini hatutegemei hoja za sayansi tu, kuna hoja za kimantiki pia.... kutegemea hoja za kisayansi tu haiwezekani kwasababu ni ngumu sana kukariri kanuni zote za sayansi zinazopingana na dini.

Sayansi ni pana mno. Kwahiyo ni kweli kabisa unachokisema. Unavyoona kuna mambo sayansi haiwezi kueleza, pia kuna mambo dini haiwezi kueleza, ndipo tunapoegemea.

Kuthibitisha hilo nitakuuliza maswali kadhaa tu bila mpangilio, ambayo najua hutoweza kujibu moja kwa moja majibu yanayojitosheleza;

1. Kwa mujibu wa dini, kila kitu kina chanzo, chanzo cha Mungu ni nini?

2. Kwanini Mungu ana kanda, yaani anapendelea eneo flani la kijiografia, Allah ametokea uarabuni, kafika Africa kupitia waarabu. Yahweh ana historia ndefu kidogo, ila kafika Africa kupitia wazungu. Kwanini hawakujidhihirisha kabla ya hapo? Ni kama vile Miungu inatengenezwa na watu wa tamaduni flani, kipindi hakuna sayansi Miungu ilitumika kama mbadala. Je waweza bishana na hili?

3. Ni Mungu yupi ndo sahihi, kwanini? na ukijitetea kwamba ni mmoja, kwanini aweke mitazamo tofauti kuhusu yeye kwenye akili za watu?

Kila upande una maswali upande mwingine hauwezi kujibu, tunaamua kuegemea upande fulani kulingana na mapokeo yetu binafsi.
 
Hizi hoja zako umezotoa wapi, ni according to science au ni mawazo yako?
Umesha ambiwa sayansi haina majibu ya kila kitu, ila bado unataka kulazimisha sayansi ieleze chanzo cha ulimwengu.

Sayansi haija thibitisha chanzo cha ulimwengu ni kipi, Sayansi imetoa nadharia (Theories ) mbalimbali tu kujaribu kuonyesha chanzo cha ulimwengu ila Haija fanikisha kuthibitisha nadharia Hizo.
Nina mashaka kama hata unajua tofauti kati ya Dunia na Ulimwengu.
Hebu elezea tofauti ya dunia na ulimwengu.
 
Na bado nadharia zingine zitatokea kwasababu Science haina mipaka na wala haina ukamilifu bali inaendelea nakuendelea...
 
Nadharia zote za kisayansi zinazojaribu kuelezea chanzo cha ulimwengu, ni speculative [science].
Sayansi ishahoji mpaka uhalisia wa dhana nzima ya "chanzo", achilia mbali "chanzo cha ulimwengu".

Between Einstein's Relativity, which tells us time is relative (hence chanzo, which depends on time, is an illussion), and Quantum Physics, whose entanglement renders time irrelevant and whose "quantum causal loop" renders causality obsolete, the concept of "chanzo" as we know it is radically relegated to a parochial experience of our localized universe.

It is as parochial and non-fundamental as color.

 
Sayansi ishahoji mpaka uhalisia wa dhana nzima ya "chanzo", achilia mbali "chanzo cha ulimwengu".

Between Einstein's Relativity, which tells us time is relative (hence chanzo, which depends on time, is an illussion), and Quantum Physics, whose entanglement renders time irrelevant and whose "quantum causal loop" renders causality obsolete, the concept of "chanzo" as we know it is radically relegated to a parochial experience of our localized universe.

It is as parochial and non-fundamental as color.

Hahaaa!

That’s why there’s no such thing as ‘settled science’.

I regard science to be a continuum of sorts.

The more you ‘fcuk around’ with it, the more you will ‘find out’.

There’s really no meaningful development without fcuking around and finding out 😀.


View: https://x.com/rogerskaer/status/1576025818182332416?s=20


View: https://youtube.com/shorts/WntjAM2wqF8?si=nfQhALvyblMjhhXF

IMG_3801.jpeg
 
Ni kweli kabisa usemayo and that's what called speculative science.

Lakini ulishajiuliza kwanini imekuwa ngumu sana kupata jibu la chanzo cha Ulimwengu huu? Mambo mengine nadhani yanapaswa kuwa fumbo, ili salama iendelee kuwepo.

Hebu fikiria siku ambayo ikapatikana hakika ya chimbuko hilo, then wanasayansi wachache ndio wakawa wamiliki wa knowledge hiyo, unadhani dunia itaendelea kuwa salama?

Ukishajua chimbuko la jambo fulani, utashindwa kuamua hatma yake?

Siku jibu hili litakalopatikana, itakuwa ndio mwisho wa dunia hii kama tuijuavyo!
 
Nafurahi sana kuona mijadala hii inapamba moto siku za karibuni na watu wengi wanaendelea kujiuliza maswali haya. Zamani zile ilikua ni akina Kiranga na baadhi ya wachache wengine.

Mimi namsubiria Elon na Xai yake tuone kama atakuja na jibu hili la chanzo cha Ulimwengunkama alivyoahidi.
 
Habari wapendwa,

Kuna hizi theories zinazoelezea chanzo cha Ulimwengu, kwa uelewa wangu hakuna hata moja inayoelezea kikamilifu chanzo cha huu Ulimwengu, bali nyingi zinaelezea modifications na evolution tu ya Ulimwengu ambapo katika kuelezea huko zinaweza zisiwe sahihi pia.

Tuziangalie kwanza nadharia zenyewe na kivipi zimeshindwa kuelezea chanzo Cha Ulimwengu.

1. Big Bang Theory

Hii ni nadharia maarufu miongoni mwetu, lakini si nadharia pekee inayoelezea chanzo cha Ulimwengu. Kwa mujibu wa big bang, Ulimwengu wote ulianza kama punje ndogo (atom), yenye joto sana, ambayo ilikuwa katika mgandamizo mkubwa usiomithirika (infinitely dense). Kisha punje hii akaanza kutanuka na kutengeneza sehemu na wakati (space and time). Kadri Ulimwengu ulivyotanuka basi ukapoa na kufanya baadhi ya sehemu kuwa ni zenye kukalika na viumbe hai kama ilivyo katika Dunia yetu. Wanasayansi wanadai tulio hili la big bang lilotokea takribani miaka bilioni 13.7 iliyopita.
Wanasayansi wanatumia gunduzi mbili za kisayansi kuthibitisha madai haya.

Kwanza, ugunduzi wa Edwin Hubble miaka ya 1920, ambapo Bw. Hubble kwa kutumia telescope, aligundua kuwa bado Ulimwengu unaendelea kutanuka, ambapo alisema kadri galaxies zipokuwa mbalimbali basi ndio zinazidi kukimbiana (Hubble's law).

Pili, ugunduzi wa Cosmic Microwave Background (CMB). Mnamo miaka ya 1960, wanasayansi waligundua mwanga (radiation) ambao ni wa kale na huo mwanga umetawanyika katika sehemu zote za Ulimwengu. Wanasayansi wanaamini kuwa mwanga huu ulitokana na mlipuko wa big bang na umeendelea kuwepo kwa miaka yote hiyo hadi leo. Inaaminika mwanga huu ni kama mwangi au wimbi la mstuko wa big bang ambalo limeendelea kupoa na hatimae kuonekana katika Microwave domain of electromagnetic spectrum.

Udhaifu wa Nadharia Hii

i. Nadharia hii haielezi chanzo cha hiyo punje ndogo. Yaani hii punje ndogo ilitokea wapi, nini kilipelekea kuundwa kwa hii punje ndogo? Hapa pana maswali mengi ambayo sayansi haiwezi kujibu na itaendelea kusemwa tu kuwa "Ulimwengu ulianza kama punje ndogo". Na kama watasema ulitokana na vitu fulani basi watatakiwa kuonyesha pia hivyo vitu vimetokana na nini.
ii. Nadharia hii haielezi nini kilisababisha mlipuko ambao umeunda Ulimwengu huu.
iii. Je hii punje ndogo ilikuwa katika nini? Je Nadharia inasema nini juu ya uwepo wa mazingira fulani ambayo huweza kubeba kitu? Je hiyo punje ilikuwa ipo yenyewe tu? Je inawezekana kitu fulani kisiwepo juu ya kitu chochote? Nadharia bado haijaeleza.
iv. Hivi karibuni Kuna baadhi ya nyota zimegunduliwa kuwa na umri mkubwa kuliko big bang yenyewe. Mfano, Methuselah ni nyota ambayo inakadiriwa kuwa na miaka bilioni 14.45, yaani hii nyota ilikuwepo kabla ya tukio la big bang.
Kutokana na kutokuwa na majibu juu ya maswali haya, Kuna nadharia nyengine zilitungwa, ambazo zilizidi kuzua maswali mengine.

2. Steady-State Theory

Nadharia inasema kuwa Ulimwengu siku zote unatanuka lakini density (tungamo) ikindelea kubaki vilevile ambapo nyota na galaxies mpya huendelea kutengenezwa kwa kiwango sawa na hupoteaji wa nyota na galaxies za zamani ambazo hupotelea kwenda katika Ulimwengu usioonekana. Watafiti wa nadharia hii wanasema kuwa Ulimwengu hauna mwanzo wala mwisho katika muda, na density na mpangilio wa galaxies ni sawa kwa muda wote.

Katika nadharia hii, tunaona moja kwa moja wameshindwa kuonyesha chanzo cha Ulimwengu.

3. The Plasma Cosmology

Nadharia hii inaamini kuwa evolution ya Ulimwengu kwa wakati uliopita inabidi ielezewe kwa kuangalia matukio yanayotokea katika Ulimwengu kwa sasa. Yaani inasema, matukio yanayotokea katika Ulimwengu sasa ndio hayohayo yalitokea katika Ulimwengu wakati uliopita. Nadharia hii pia inakataa kuwa Ulimwengu haujatokana na chochote kama inavyoaminika na watafiti wa big bang. Watafiti wa Plasma Cosmology wanaamini kwamba kwasababu tunaona Ulimwengu unaobadilika, basi huu Ulimwengu ulikuwepo siku zote and utaendelea kuwepo and kubadilika milele. Kama ilivyo Kwa steady state theory, Nadharia hii pia inakataa Ulimwengu kuwa na chanzo.

4. Big Bounce Theory

Big Bounce inasema kuwa Ulimwengu umekuwa ukitanuka na kuanguka mara kadhaa. Yaani Ulimwengu umetanuka mara kadhaa na ku-collapse mara kadhaa. Huu Ulimwengu tulionao ni zao la Ulimwengu ambao uli-collapse na kutanuka tena na wanatabiri kuwa huu Ulimwengu uta-collapse tena na pengine kutanuka tena. Kwahiyo Kuna series ya 'crunches and bangs' ambapo Ulimwengu unatanuka na kuanguka. Bado nadharia hii haionyeshi chanzo cha Ulimwengu bali huonyesha mabadiliko tu. Chanzo cha huo Ulimwengu ambao unacollapse na kutanuka ni kipi? Nini ilikuwa sababu ya kutanuka na ku-collapse? Bado hatupati majibu.

5. The Ekpyrotic Model

Nadharia hii inaamini kuwa big bang ilitokea kwa sababu ya mgongano wa branes mbili ambazo zilikuwa sambamba. Sina tafsiri sahihi ya neno branes, lakini branes inaweza kuelezewa kama any of the spatially extended mathematical objects of zero or more dimensions used in string theory. Watu wa Quantum mechanics na General relativity wanaweza wakanielewa. Katika mazungumzo haya, tuzichukulie hizo branes kwa mfano wa kamba, hivyo basi hizo kamba mbili sambamba zilisuguana na kupelekea moto ambao ndio ukazaa big bang na hatimae kuunda Ulimwengu. Hapa tunapata swali jengine, je hizi branes zilitoka wapi? Nini kilifanya zisuguane? Hapa pia Kuna maswali mengi.

Hitimisho: tumeona kuwa nadharia nyingi hazijaelezea hasa chanzo cha Ulimwengu, baadhi zinasema kabisa Ulimwengu hauna chanza na hautakuwa na mwisho na nyengine zinasema Ulimwengu ulianzia na kitu fulani, lakini haziwezi kuelezea chanzo cha hicho kitu. Yaani nini kilikuwa chanzo cha hicho ambacho wewe unakiona kuwa ndio kimeleta Ulimwengu?
Je, Kuna nadharia nyengine ambazo zina majibu mazuri zaidi?
Je, wale wanaopinga uwepo Mwenyezi Mungu wanategemea nadharia hizi katika kuelezea chanzo cha Ulimwengu?
Arm chair thinking converted to Emperical Science
 
Kwanza inabidi ufahamu maana ya nadharia (theory)

Katika sayansi kuna theory, facts, laws, principles, etc

Theory/nadharia huwa haina ushahidi isipokuwa ni mawazo tu ya mtu au watu.
Duh you couldn't be wronger.
Hiyo ambayo Haina ushahidi inaitwa hypothesis.

Theory lazima iwe na proof
 
Nafurahi sana kuona mijadala hii inapamba moto siku za karibuni na watu wengi wanaendelea kujiuliza maswali haya. Zamani zile ilikua ni akina Kiranga na baadhi ya wachache wengine.

Mimi namsubiria Elon na Xai yake tuone kama atakuja na jibu hili la chanzo cha Ulimwengunkama alivyoahidi.
Ulimwengu hauna Chanzo.

Ukianza kuweka ulazima wa kila kitu kiwe na chanzo hata hicho "chanzo" lazima kiwe na chanzo chake to endless.

Pasiwepo kitu chochote kile kilicho jitokeza chenyewe pasipo chanzo maana kitavuruga muundo mzima wa ulazima wa kuwepo chanzo kwa kitu.
 
Ni kweli kabisa usemayo and that's what called speculative science.

Lakini ulishajiuliza kwanini imekuwa ngumu sana kupata jibu la chanzo cha Ulimwengu huu? Mambo mengine nadhani yanapaswa kuwa fumbo, ili salama iendelee kuwepo.

Hebu fikiria siku ambayo ikapatikana hakika ya chimbuko hilo, then wanasayansi wachache ndio wakawa wamiliki wa knowledge hiyo, unadhani dunia itaendelea kuwa salama?

Ukishajua chimbuko la jambo fulani, utashindwa kuamua hatma yake?

Siku jibu hili litakalopatikana, itakuwa ndio mwisho wa dunia hii kama tuijuavyo!
Dunia Haina chanzo.

Kama Dunia lazima iwe na chanzo, Hata hicho "chanzo" cha Dunia lazima kiwe na chanzo chake.

Pasiwepo kitu chochote kile hata hicho chanzo, kitakacho jitokeza chenyewe tu from Nothing...!!!

Maana lazima swali lije, Huko chanzo kilipotokea kulitoka wapi?
 
Back
Top Bottom