Hakuna nadharia yoyote ya Kisayansi inayoelezea kikamilifu chanzo cha ulimwengu

Hakuna nadharia yoyote ya Kisayansi inayoelezea kikamilifu chanzo cha ulimwengu

Tafsiri ya kusema imani ni kujua kitu kwa hakika ni tafsiri potofu.

Imani ni kuamini kitu bila kuwa na uthibitisho
Nimesema kwenye maelezo yangu kwamba tatizo kubwa ni uelewa wa mambo na elimu ya vitu.

Kuhusu tafsiri yako juu ya imani, huu si ufahamu bali ni hisia, hisia zako binafsi.

Imani maana yake ni "kujua na kuwa na hakika ya mambo.
 
Nimesema kwenye maelezo yangu kwamba tatizo kubwa ni uelewa wa mambo na elimu ya vitu.

Kuhusu tafsiri yako juu ya imani, huu si ufahamu bali ni hisia, hisia zako binafsi.

Imani maana yake ni "kujua na kuwa na hakika ya mambo.
Sawa basi tutumie vyanzo vya kuaminika katika hizo tafsiri ili kuepusha maoni binafsi

Nipe chanzo chako cha hiyo tafsiri
 
Sayansi kuna vitu huwa inakubali haijui na haina majibu yake na bado inachunguza, dini zinajinadi kujua na kuwa na majibu ya kila kitu!
 
1. Sayansi kuna vitu huwa inakubali haijui na haina majibu yake na bado inachunguza

2. Dini zinajinadi kujua na kuwa na majibu ya kila kitu!

1. Kweli

2. Uongo

[emoji6]
 
The creator,the one who is there alpha and omega,the dark matter,,the dark matter theory
 
Kwanza kwa nini unadhani ulimwengu lazima uwe na chanzo?

Umewezaje kuamini Mungu usiyemjua Hana chanzo ila una lazimisha ulimwenguni uwe na chanzo?

Kama Mungu huyo ameweza kuwepo bila chanzo, Inashindikana vipi kwa ulimwengu kuwepo bila chanzo?

Kama Mungu ndio chanzo cha ulimwengu, Chanzo cha Mungu ni nini?

Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe na chanzo. Basi hata Mungu lazima awe na chanzo,Na chanzo cha Mungu kiwe na chanzo, Na chanzo cha chanzo cha Mungu kiwe na chanzo mpaka infinity hukooo...

Pasiwepo kitu chochote kile kilicho jitokeza chenyewe pasipo chanzo maana kitavuruga muundo mzima wa "ULAZIMA AWEPO CHANZO"
The universe is infite hiyo yaweza kuwa sahihi
 
Kuna pande kuu mbili,

Kuna wanaoamini uwepo wa Mungu na wale wasioamini uwepo wa Mungu.

Wasioamini uwepo wa Mungu wanasema, Kila kitu kinacho-exist,uwepo wake lazima uelezewe kisayansi. Swali, kisayansi Ulimwengu ulianzia wapi?

Kundi la pili ni la wale wanaoamini uwepo wa Mungu. Hawa Imani yao inasema si mambo yote yanaweza kuelezewa Kwa akili ya binadamu. Kwaiyo ukimuuliza muumini nini chanzo cha baadhi ya mambo, hawezi kukupa jibu kwasababu msingi wa Imani yake ni kuwa si kila kitu kinaweza kuelezewa na binadamu. Huo ndio Msingi.

Tunapowauliza kuhusu chanzo cha Ulimwengu, na vitu vingine inabidi mtuonyeshe kwasababu msingi wa imani yenu ni kuwa Kila kitu hutokea kisayansi.

Mkituuliza Mungu alianzia wapi, sie jibu letu ni fupi tu kuwa yeye Hana chanzo wala mwisho. Na mkisema hili linawezekana vipi, basi tutasema msingi wa tunachoamini ni kuwa Kuna baadhi ya mambo yana limit.

Nyinyi sasa ambao mnaamini kuwa Kila kitu kinatokea kisayansi mnalo jukumu la kuelezea kila kitu kinachoonekena bila kurukaruka.
Ulimwengu wa Mungu unazo Siri kubwa sana hazifahamiki Wala hazitokuja kufahamika kamwe,Sayansi Ina mfululu wa magunduzi na ndani ya mfululu huo tukiwa kama binadamu tunapata maswali mengi kuliko majibu na tunajikuta tuna staajabu uumbaji na uumbaji na uumbaji na uumbaji,,maana kama bing bang existed 13.5 Billions of years ago,,then came the existence discovery of Methuselah which existed 14.5 billion of years ago.
Sayansi Ina maajabu ambayo Mimi naona inatupa raha na msisimko wa ajabu, exploration ya hali ya juu sana.
Imani juu ya uwepo wa Mungu inatupa nguvu kuwa yupo anayejua zaidi yetu,Kuna master wetu,Kuna mamlaka juu yetu,ni ukweli kuwa tupo kwenye matrix ambayo hayuwezi ku escape na njia pekee ya ku flow nayo vyema ni kuwa tu na imani juu ya uwepo wa Mungu,kwa sababu hatuwezi kuthibitisha kisayansi kuwa Mungu yupo au hayupo.
Kuna wale wanaamini na kusadiki hizi hadithi au hakaya za sumerian ancient civilizations,,the stories about Anunnaki as being our masters,,as the human kind creators,but the same question always will rise as in science,how did the Anunnaki exist and who created them,jibu linakuja Tena kwenye Sayansi na theories za dark matter,that everything in the Galaxies started out of the dark matter whereby the light was first created from the dark.
Kwa kifupi Sayansi ifanye kazi yake kwa maendeleo na exploration za wanadamu kwa sababu tunahitaji pia adventures in this life as life is boring in nature so we need explorations and adventures and new challenges.
Tunahitaji Sayansi kutatua changamoto zetu za kifizikia,kibailojia,kikemikali,kijiografia,kiuchumi Kila sekta na nyanja zote za kimaisha zinahitaji Sayansi ili mradi siku ziende vyema.
Lakini ni ukweli usiopingika binadamu ni wanyama katika mfumo wa mtu, we are animals in human form,kwa hivyo baadhi yetu tunahitaji Imani juu ya uwepo wa Mungu ili tuweze kuendelea kuwa salama katika matrix tuliyopo tuishi kwa matumaini na imani,maana Imani ni kama nira ya kuleta utengamano bila Imani sisi ni mahayawani na kawaida ya mahayawani ni kulana,kuchinjana, mwenyewe na nguvu ndio ata survive.
Hayo ni mtazamo wangu tu.
Nayatazama yote ulimwengu kwa mkabala unakwenda namna hii.
 
Habari wapendwa,

Kuna hizi theories zinazoelezea chanzo cha Ulimwengu, kwa uelewa wangu hakuna hata moja inayoelezea kikamilifu chanzo cha huu Ulimwengu, bali nyingi zinaelezea modifications na evolution tu ya Ulimwengu ambapo katika kuelezea huko zinaweza zisiwe sahihi pia.

Tuziangalie kwanza nadharia zenyewe na kivipi zimeshindwa kuelezea chanzo Cha Ulimwengu.

1. Big Bang Theory

Hii ni nadharia maarufu miongoni mwetu, lakini si nadharia pekee inayoelezea chanzo cha Ulimwengu. Kwa mujibu wa big bang, Ulimwengu wote ulianza kama punje ndogo (atom), yenye joto sana, ambayo ilikuwa katika mgandamizo mkubwa usiomithirika (infinitely dense). Kisha punje hii akaanza kutanuka na kutengeneza sehemu na wakati (space and time). Kadri Ulimwengu ulivyotanuka basi ukapoa na kufanya baadhi ya sehemu kuwa ni zenye kukalika na viumbe hai kama ilivyo katika Dunia yetu. Wanasayansi wanadai tulio hili la big bang lilotokea takribani miaka bilioni 13.7 iliyopita.
Wanasayansi wanatumia gunduzi mbili za kisayansi kuthibitisha madai haya.

Kwanza, ugunduzi wa Edwin Hubble miaka ya 1920, ambapo Bw. Hubble kwa kutumia telescope, aligundua kuwa bado Ulimwengu unaendelea kutanuka, ambapo alisema kadri galaxies zipokuwa mbalimbali basi ndio zinazidi kukimbiana (Hubble's law).

Pili, ugunduzi wa Cosmic Microwave Background (CMB). Mnamo miaka ya 1960, wanasayansi waligundua mwanga (radiation) ambao ni wa kale na huo mwanga umetawanyika katika sehemu zote za Ulimwengu. Wanasayansi wanaamini kuwa mwanga huu ulitokana na mlipuko wa big bang na umeendelea kuwepo kwa miaka yote hiyo hadi leo. Inaaminika mwanga huu ni kama mwangi au wimbi la mstuko wa big bang ambalo limeendelea kupoa na hatimae kuonekana katika Microwave domain of electromagnetic spectrum.

Udhaifu wa Nadharia Hii

i. Nadharia hii haielezi chanzo cha hiyo punje ndogo. Yaani hii punje ndogo ilitokea wapi, nini kilipelekea kuundwa kwa hii punje ndogo? Hapa pana maswali mengi ambayo sayansi haiwezi kujibu na itaendelea kusemwa tu kuwa "Ulimwengu ulianza kama punje ndogo". Na kama watasema ulitokana na vitu fulani basi watatakiwa kuonyesha pia hivyo vitu vimetokana na nini.
ii. Nadharia hii haielezi nini kilisababisha mlipuko ambao umeunda Ulimwengu huu.
iii. Je hii punje ndogo ilikuwa katika nini? Je Nadharia inasema nini juu ya uwepo wa mazingira fulani ambayo huweza kubeba kitu? Je hiyo punje ilikuwa ipo yenyewe tu? Je inawezekana kitu fulani kisiwepo juu ya kitu chochote? Nadharia bado haijaeleza.
iv. Hivi karibuni Kuna baadhi ya nyota zimegunduliwa kuwa na umri mkubwa kuliko big bang yenyewe. Mfano, Methuselah ni nyota ambayo inakadiriwa kuwa na miaka bilioni 14.45, yaani hii nyota ilikuwepo kabla ya tukio la big bang.
Kutokana na kutokuwa na majibu juu ya maswali haya, Kuna nadharia nyengine zilitungwa, ambazo zilizidi kuzua maswali mengine.

2. Steady-State Theory

Nadharia inasema kuwa Ulimwengu siku zote unatanuka lakini density (tungamo) ikindelea kubaki vilevile ambapo nyota na galaxies mpya huendelea kutengenezwa kwa kiwango sawa na hupoteaji wa nyota na galaxies za zamani ambazo hupotelea kwenda katika Ulimwengu usioonekana. Watafiti wa nadharia hii wanasema kuwa Ulimwengu hauna mwanzo wala mwisho katika muda, na density na mpangilio wa galaxies ni sawa kwa muda wote.

Katika nadharia hii, tunaona moja kwa moja wameshindwa kuonyesha chanzo cha Ulimwengu.

3. The Plasma Cosmology

Nadharia hii inaamini kuwa evolution ya Ulimwengu kwa wakati uliopita inabidi ielezewe kwa kuangalia matukio yanayotokea katika Ulimwengu kwa sasa. Yaani inasema, matukio yanayotokea katika Ulimwengu sasa ndio hayohayo yalitokea katika Ulimwengu wakati uliopita. Nadharia hii pia inakataa kuwa Ulimwengu haujatokana na chochote kama inavyoaminika na watafiti wa big bang. Watafiti wa Plasma Cosmology wanaamini kwamba kwasababu tunaona Ulimwengu unaobadilika, basi huu Ulimwengu ulikuwepo siku zote and utaendelea kuwepo and kubadilika milele. Kama ilivyo Kwa steady state theory, Nadharia hii pia inakataa Ulimwengu kuwa na chanzo.

4. Big Bounce Theory

Big Bounce inasema kuwa Ulimwengu umekuwa ukitanuka na kuanguka mara kadhaa. Yaani Ulimwengu umetanuka mara kadhaa na ku-collapse mara kadhaa. Huu Ulimwengu tulionao ni zao la Ulimwengu ambao uli-collapse na kutanuka tena na wanatabiri kuwa huu Ulimwengu uta-collapse tena na pengine kutanuka tena. Kwahiyo Kuna series ya 'crunches and bangs' ambapo Ulimwengu unatanuka na kuanguka. Bado nadharia hii haionyeshi chanzo cha Ulimwengu bali huonyesha mabadiliko tu. Chanzo cha huo Ulimwengu ambao unacollapse na kutanuka ni kipi? Nini ilikuwa sababu ya kutanuka na ku-collapse? Bado hatupati majibu.

5. The Ekpyrotic Model

Nadharia hii inaamini kuwa big bang ilitokea kwa sababu ya mgongano wa branes mbili ambazo zilikuwa sambamba. Sina tafsiri sahihi ya neno branes, lakini branes inaweza kuelezewa kama any of the spatially extended mathematical objects of zero or more dimensions used in string theory. Watu wa Quantum mechanics na General relativity wanaweza wakanielewa. Katika mazungumzo haya, tuzichukulie hizo branes kwa mfano wa kamba, hivyo basi hizo kamba mbili sambamba zilisuguana na kupelekea moto ambao ndio ukazaa big bang na hatimae kuunda Ulimwengu. Hapa tunapata swali jengine, je hizi branes zilitoka wapi? Nini kilifanya zisuguane? Hapa pia Kuna maswali mengi.

Hitimisho: tumeona kuwa nadharia nyingi hazijaelezea hasa chanzo cha Ulimwengu, baadhi zinasema kabisa Ulimwengu hauna chanza na hautakuwa na mwisho na nyengine zinasema Ulimwengu ulianzia na kitu fulani, lakini haziwezi kuelezea chanzo cha hicho kitu. Yaani nini kilikuwa chanzo cha hicho ambacho wewe unakiona kuwa ndio kimeleta Ulimwengu?
Je, Kuna nadharia nyengine ambazo zina majibu mazuri zaidi?
Je, wale wanaopinga uwepo Mwenyezi Mungu wanategemea nadharia hizi katika kuelezea chanzo cha Ulimwengu?
6. Biblical fact
Kuwa ulimwengu uliumbwa, na muumbaji wake ni Mungu
 
Back
Top Bottom