Hakuna Taifa lililoendelea kwa kujipendekeza na kujidharau

Tulifikishwa pale tulipofika kutokana style ya uongozi uliopita. Awamu ya 4 ilifanya hayo yote anayofanya mama lakini tulipata nn? Hii nchi utadhani ina laana.

Sent from my SM-A730F using JamiiForums mobile app
 
Mtoa mada anahitaji kujifunza namna ya kutuma ujumbe kwa haraka kuliko kuandika makala ndefu ambayo mtu kama mimi ningetuma ujumbe huo huo kwa paragraph moja tu yenye sentesi zisozidi sita.

Ila alichosema ni ukweli kabisa; kuishi vizuri na jirani yako siyo lazima umlambe miguu yake, ni kuishi kwa kuheshimiana. Magufuli alikuwa expert sana wa kujua jinsi ya kuishi na majirani. Kenyatta alipofanya mambo mazuri kwa Tanzania na yeye alijibu kwa kufanya mambo mazuri kwa Kenya, na wakati Kenyata alipozuia ndege za Tanzania zisiingie Kenya, naye pia akazuia za Kenya zisiingie Tanzania, na wakati balozi wa Kenya alipofanya vizuri kwenye majukumu yake Magufuli alimsifia hadharani.

Siyo kwamba kuishi na jirani ni lazima ujiweke chini kwa kila kitu; hao wanaomshauri huyu mama, yaani timu Msoga itamuangusha huko mbeleni akianza kukumbana na stagnation pressure. Sera za Kikwete za "nikienda nje narudi na kibaba" kila matu anafurahi ni sera za kipuuzi sana zisizokuwa na vision kwa nchi.
 
Hakuna nchi inayoongoza kwa kujifanya iko chini kama Marekani. Sasa hivi ukiwasoma wamarekani mara zote wanaonesha kama nchi yako inaenda kupitwa na China au inazidiwa na China kwa baadhi ya mambo.
Revisit your source of information.
====
Unatilia mashaka uwezo wa wataalamu wako! Vijana wanabuni vifaa/mitambo ya/vya kusaidia jamii, wasimamizi wa mmasuala ya technologies wanawadhibiti kutoendeleza teknolojia hizo kwa sababu za kifitina na uchoyo!

Hivi kifaa chakugundua kuwa kuna mtu kaingia na simu bila mtu huyu kupitishwa kwenye scana zenye mionzi hatarishi sehemu fulani ambapo haparuhusiwi kuingia na simu kina ubaya gani?

Hivi kiantena kidogo kabisa cha kukuza mawimbi ya simu ambacho unaweza kutembea nacho popote ambapo kunashida ya mtandao kina shida gani?

Lakini tafiti zinazohusisha madodoso ndizo zina pewa kipaumbele! Unaenda kufanya udodosaji eti " unakubali ndege yupi tumtumie kuwinda nyoka na panya kati ya tai, mwewe,na bundi". Halafu eti tulete wataalamu wa nje watusaidie kupiga hatua.

Halafu mnasema tutafurukuta kate 4th revolution in the technological sphere!
===
Hivi serikali imetenga kiasi gani rasmi kwa ajili ya maendeleo ya kiteknolojia katika pato lake kitaifa!?
 
umeandika vema nadhani kuna cha kujifunza hapo, kazi iendeleee.
 
Ni kweli familia ya Kenyatta wanamiliki ardhi kubwa
, lakini sio 70%. Hata 5% haifiki. Gdp (per capita) Kenya wako juu- $4500+, nafasi ya21, wakati Tz ni $2700 nafasi ya 32 barani Africa. Ukiambiwa wameendelea kuliko sisi, ndio maana yake hatakama hutaki.
 
Baada ya kifo cha King JPM, EU walisema"Sasa Tanzania taa imezima ghafla"
TUTAMKUMBUKA.
Kujipendekeza, kujidharau, kujishusha hadhi ni hatari kubwa zaidi kuliko hatari yenyewe.
Ndiyo maana JPM alikuwa akituambia kuwa sisi si maskini, hivyo tunapaswa kujiamini na kutembea kifua mbele.
 
Siku zote lazima ujifunze kwa waliotangulia. Kenya walishatangulia. Lazima tuangalie njia walizopita.
OOooh, Kenya walishatangulia?

Tangulia kwenda wapi?

Wewe unaona Kenya wameendelea? Kwa akili za tope namna hii tutapata shida sana.
 
Kenya wako juu- $4500+
Wacha uongo. Ingekuwa tarakimu ndiyo hizo, asingekuwa kwenye Lower Middle Income, kama ilivyo Tanzania. Tofauti ya namba hizo kati ya Tanzania na Kenya sio kubwa kiasi hicho.

Pamoja na uongo huo, unashindwa kujua kwamba hata kama ingekuwa ni tarakimu hizo, mtu wa kawaida Kenya hana hela hiyo. Ni matajiri wachache, tena wengi wao watu wa nje ya nchi ndio wanaogawana sehemu kubwa ya utajiri huo. Lakini kwa kuwa kichwa chako kimejaa tope, basi unafikiri maskini pale Uasin Gishu naye ana pato hilo!
 
anacho jaribu kuwakilisha muandishi ni kwamba tusiwe tegemezi. tujikwamue kwa jituhada zetu
Sijapata kusikia taifa lolote lililoendelezwa na watu wengine wenyeji wao wekiwepowepo tu kama masanamu.

Sasa tunawalilia hata wakenya waje watuendeleze?

Kama hii sio laana, sijui tuiite kitu gani.

Mama ziara yake hii ya kwanza kajijengea sura mbaya kabisa. Natumaini yafuatayo atakayoyafanya yataziba kidogo aibu hii aliyoliletea taifa hili.
 
Mkuu Hongera kwa post ndefu nimesoma yote kwa umakini. Mimi binafsi nimeishi sana Kenya na kuna baadhi ya kozi nimesoma huko, Kenya wako juu sana kwenye mambo mengi, raia kujitambua,seriousness, bidii na uwajibikaji, professionalism, mfano wengi wanaofundisha lugha ya kiswahili nchi za Ulaya ni wa Kenya kwa sababu wao wanachukulia lugha ya kiswahili kama lugha ya biashara wakati sisi watu wamelala wanalalamika, ukienda Nairobi leo hii ukiangalia utembeaji wa watu tuu utangundua kwamba tunatakiwa tujifunze kutoka kwao,shule nyingi za binafsi Tanzania wakenya wamejaa na Tanzania hatutaki kujifunza chochote kutoka kwao kwa sababu ya kuamini kuwa kujifunza kutoka kwa mtu ni kujipendekeza. Tulichowazidi wakenya ni ukarimu na Ukubwa wa eneo la nchi vingine wametuzidi sana.
 
Mtahangaika sana mwaka huu, mwisho wa zamaumefika na mwisho wa chato pia
 
Nimezipenda hizo aya.
Apumzike kwa amani hayati Dr John Pombe Magufuli
 
Hivi nchi kuingia makubaliano ya kibiashara au uwekezaji na nchi nyingine ni kujidharau?!!!

Mtoa mada unaelewa kwa dhati kuhusiana na uwekezaji na biashara katika nyanja za kimataifa? Je, unajua rais anapokuwa ziarani na kusaini makubaliano fulani, kinachosainiwa ni roadmap tu au MoU kukaribisha / kuondoa vizingiti vya kibiashara na uwekezaji baina ya hayo mataifa?.

Na pindi muwekezaji anapokuja kuwekeza mkataba halisi wa biashara husika hujadiliwa na wataalamu wa wizara na kwa kuzingatia sera na sheria za nchi ndipo baadae husainiwa na waziri mhusika wa wizara na siyo Rais.

Kulingana na sheria za nchi yetu kuna mikataba ya kiwango fulani haiwezi kuingiwa na wizara hadi iwasilishwe na kupate kibali cha baraza la mawaziri.
 
OOooh, Kenya walishatangulia?

Tangulia kwenda wapi?

Wewe unaona Kenya wameendelea? Kwa akili za tope namna hii tutapata shida sana.

Watanzania tuwe makini sana, tukisha anza kujidharau/kukosa kujiamini TUMEKWISHA, maadui/washindani wetu wakisha nusa weakness yetu ya kutojiamini watatu chezea sana sana - walisha sema wana kitengo maalum cha ujasusi wa kiuchumi,watatuma watu wa kuchunguza baadhi ya Watanzania ambao ni: wabunge, wanasiasa Viongozi wenye ushawishi Serikalini pia na washauri wa karibu wa Madam President yaani wale wote wenye element ya usaliti watatafutwa na kuingizwa kwenye kundi la kufanya lobbing ya hali ya juu ya kumpotosha mama wa watu - sijasema kwamba mama Samia hawezi kufanya mahamuzi on her own, far from it.

Kwa bahati nzuri madam President aliwahi kutamuka mwenyewe kwamba atatilia maanani baadhi ya maoni ya walala hoi na kuyafanyia kazi, basi tunamshauri kwa nia njema kwamba "tusiende mbio, mbio kukimbilia mlio, kumbe tunako kimbilia kuna kilio, tutapatwa na ajali/hatari DUNIA itatushangaa!!" tuwe wakweli hapa - hakuna Mtanzania mwenye uchungu wa kweli wa Taifa hili inataka kurudi tena kwenye zama za uongozi wa awamu ya nne - hakuna.

Magufuli wa watu pamoja na mapungufu yake ya hapa na pale kama binadamu wote tulivyo lakini alikuwa anasema/anasisitiza kila siku kwamba jamani eeh WATANZANIA tutembee kifua MBELE i.e tujiamini,maadui zake walimchukia lakini wali admire ujasiri wake wa kujali maslahi ya Taifa letu ya kulazimisha wawekezaji wote uwekeze kwenye enviroment ya win win situation ambayo haina element ya unyonyaji,wizi na ufisadi.

Kama ni suala la kujifunza mambo kwa nini tusiende kujifunza kwenye Mataifa yaliyo piga astronomical maendeleo in a record time tangu wapate uhuru - mfano mzuri ni: China, Malaysia, Korea Kusini na India - kuna nini cha kujifunza kwenye mataifa ambayo GDP yao haizidi sana ya Tanzania na wao bado wapo kwenye bracket ya mataifa yenye uchumi wa kati kama sisi - wangesema walao South Africa na Misri watu wange elewa kwamba hao at least uchumi wao umepaa, we can learn something worthwhile therefrom.
 
So hiyo kwako ndo kuendelea, Marekani inakipato cha juu kuliko Scandinavia. Lakini Marekani kuna maskini wa kutupwa. Unapoongelea uchumi ni kitu kipana. Na Scandinavian countries zinaongoza kwa huduma za kijamii na uwezi kuta umasikini kama uliopo Marekani japo Marekani inakipato kikubwa.
Jiulize ni kwann wamerekani wengi wanahamia Canada na scandinavia countries japo uchumi ni mkubwa. Vivyo vivyo life style ya maisha kwa Africa mashariki baina ya Kenya na Tanzania.
Rudi kafanye utafiti wako.
 
Siyo peke yako uliyewahi kuishi huko, kama kweli uliwahi kukaa huko.

Uliyoandika hapa ni kama ni mwenyeji wa huko, au umeolea huko, na pengine kuwa na maslahi binafsi na huko.

Ndiyo, yapo waliyofanikiwa kuyafanya vizuri, mfano mzuri ni elimu yao iko imara zaidi, lakini hilo haliifanyi nchi hiyo iwe "...juu sana kwenye mambo mengi," kama unavyodai
"Raia kujitambua," una maana gani? Umefika kule Baringo ukakuta raia wapo tofauti sana na hawa waliopo Liwale katika kujitambua?
Unachukulia tu kakikundi uliko-'interact' nako hapo ulipofanya vikozi vyako ndiyo ukadhani kuna "seriousness, bidii na uwajibikaji, professionalism", ambayo huku Tanzania haipo mahali popote? Umefanya utafiti ukakupa majibu hayo?

Halafu unachekesha kweli: yaani hata "utembeaji" wa watu unauwekea uzito wai kuonyesha tofauti zilizopo kati ya watu walioko Nairobi na hawa , sijui wa Dar es Salaam au Tanzania yote?
Yaani unataka Tanzania twende Nairobi, tukajifunze kutembea kama wao? Hapo hali zetu ndipo zitakapoonekana kuwa nafuu kidogo kama wao?

Ninachohimiza waTanzania tujitahidi kukifanya kwa bidii zaidi kuliko kitu kingine kwa haraka zaidi, ni kuifanya elimu yetu iwe imara. Elimu yetu inaupungufu sana, na ndio maana, kama huyu 'Executive Sister' ni mTanzania kama inavyoonekana anadai yeye, anadiriki kuandika vitu vya ajabu sana kama alivyoandika hapa. Msingi wake wa elimu ulikuwa duni sana, licha ya kwamba hata hivyo vikozi alivyofanya huko Nairobi inaonyesha havikumsaidia kitu, kutokana kuwa na msingi mbovu tokea mwanzo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…