Joke of the thread!
Kuna jamaa alienda hospitalini,
Akakaa kwenye foleni ya kusubiri kuingia chumba cha daktari.
Sasa kila ikifika zamu yake anampisha mtu, kafanya hivyo weee lakini hatimaye ikafika zamu yake maana wagonjwa wote kwenye ile foleni walishaingia...
Daktari: Karibu
Mgonjwa: Ahsante
Daktari: Enhe, una shida gani?
Mgonjwa: Dokta nina shida, lakini usinicheke!
Daktari: Mimi ni Daktari, nitakuchekaje?!
Mgonjwa: Kweli nina tatizo lakini usicheke! (Alisistiza)
Daktari sura ikaanza kuonesha kuhamanika na kusema...
Daktari: Nimeshakwambia sicheki, we niambie una shida gani!
Mgonjwa: Ngoja nifunge mlango na funguo kwanza.
Yule mgonjwa akamsogelea daktari kisha akavua suruali na chupi, akashika kidushe chake yani kidogo mno, yani very tiny kama inchi moja kasoro hivi!
Daktari wacha aanze kucheka
Alicheka sana hadi machozi ya kucheka yakawa yanamtoka...
Yule mgonjwa akawa yupo kimya
Daktari akamaliza kucheka kisha akamgemgeukia mgonjwa na kumuuliza
Daktari: Sasa tatizo lako ni nini?!!
Mgonjwa: Hii imevimba tangia juzi...
Datari wacha aangue kicheko tena.
_______