Hakuna watu wajinga kama watu wanaoamini habari za kichawi

Huko kwa Kuhani Musa yeye mahubiri yake kila siku ni uchawi tuu na watoto eti hufukua makaburi na kula nyama za watu 🤣
Mwamposya yeye ni uchawi wa paka na watu kurogwa na kunya misumari na maembe
Upumbavu mtupu
 
Zamani na wajinga wengine hata leo wanaamini mabusha yanatokana na uchawi. Kumbe ni minyoo inayoenezwa na mbu.
kuna la kurogwa na lile la mbu aina ya f/anopheles Mosqu....tofauti yake kuna lenye vitu vizito km nyama.. Na ingine maji maji!...kazi kwako....

lkn ndo tabia zenu wachawi mlivyo nawajua fika...ni kutupoteza maboya eti hkn uchwi ili mpete!!! Nasema humpati mtu hapa...ukija na fisi sie tunakuja na ungo tuna kubeba weye na fisi wako......uchawi upo yamkini unao au weye ni gari la wachawi.....paul mtumishi wa Mungu alirogwa na mchawi maarufu "Baayesu".....wewe nani usirogwe??...kawambiye Jf ni wajanja wamekataa....sikia sasa miye binafsi nilikuwa mchawi maarufu wa kurithi.....so naujua kuliko unavodhania...wana jf kataeni huyu mleta mada ni wakala....
 
Baada ya kugundulika yanatokana na mbu ndiyo mmekuja na explanation kuwa yako mawili. La kurogwa na la mbu?!!!! Ni kawaida kwa mtu mwenye imani ya kijinga anapoambiwa ukweli kutetea kwa nguvu zote. Upo kwenye denial.
 
Sina muda wa kumalizia kusoma upuuzi wako, ila niseme tu, wewe ni mtoto mdogo bado, ukikua utajua kua utoto nao pia ni ujinga.
Wewe mliharisha kule porini kwa food poisoning, sijui kipindupindu ukasingizia uchawi. Mara uliua ndugu zako wachawi. Acha ujinga na utapeli mkuu.
 
Daah watu wakisoma na kupata vyeti vya kucopy assignment na ufaulu wa mchongo hujifanya wanajua kila kitu, asee dunia imekutangulia, nikikumbuka tukio alilopigwa mpenzi wngu nachelea kusema ukue kwanza😭😭
 
Ngozi nyeupe ilivyopumbaza akina sisi Hadi kuaminishwa matukio Fulani ni sayansi ila deep down Ni pure occultism.
Unataka kuuona vizuri nenda kwenye Soka,Mziki, Biashara na Siasa.
 
Mhhh. Nadhani ujinga uliokubuhu ni ule wa kuona kwamba wale wanaoamini uwepo wa Uchawi ni wajinga. (yaani wewe unajiona ndo una akili). Hebu jiulize kidogo; Hivi watu weeengi kiasi hicho(wazee,vijana, wasomi, viongozi wa kiimani, misahafu..) waseme uchawi upo halafu wewe mtu mmoja unanga'ngania kusema uchawi haupo na mbaya zaidi kuwaita watu hao ni wajinga inakuwaje? Mm nafikiri ungelitulia kwanza mahali, ukatafakari kwa kina kisha uanze kufuatilia ukweli wa hicho wanachokiamini(Uchawi) na kinatendaje kazi. Fanya marejeo katika vitabu/maandiko (hata kama vikiwemo vile vya dini), ongea au fanya utafiti na watu - wazee kwa vijana(hata kama ni viongozi wa dini au wasomi maarufu) halafu mwisho pitia matukio mbalimbali ya kweli yaliyotokea na visababishi vyake then Uje kutoa mrejesho hapa. Kwa mfano ni sawa na Ukiambiwa kuna simba Serengeti usiseme eti kwa kuwa hujamwona basi hayupo. Kutokuamini kwako hakutaondoa uwepo wa simba Serengeti. Vivyo hivyo kutokuamini kwako kwamba uchawi upo hakutabatilisha uwepo wa uchawi duniani. Siku ukikamatika ndio utajua ulikuwa hujui na hauamini. Hapo ndo itakuwa kusikia kwa kenge ni damu masikioni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…