Hakuna Watu wanapata shida kama bodaboda wa Mafinga nyakati za Usiku

Hakuna Watu wanapata shida kama bodaboda wa Mafinga nyakati za Usiku

Kwema Wakuu!

Nimeshawahi kuishi Mafinga mara kadhaa lakini sijawahi kuona baridi kama ya Juzi jumatatu tarehe 19. Dadeki baridi mpaka ukungu weñye barafu nyepesi ilikuwa inadondoka...
Mwakaleli huko baridi ni balaa!kipindi tunasoma huko kwa mababu zetu kipindi Cha baridi tunaingia darasani saa tatu,hata mwalimu hawezi kuandika ubaoni!
 
Mjifunze hata kujua miezi ya baridi hapa Tanzania ili ubebe hata makoto
. Kuanzi June-August hunipeleki Makambako Njombe,Makete Lushoto na sehemu yoyote inayosifika kwa baridi hapa Tz.
Kama Umeoa huko mna magonjwa au umefiwa!
 
Naelewa hali iliyokukumba.

2018 Nishawahi kukosea step nikajikuta sheli ya CF Mafinga pale Kinyanambo C saa 10 alfajiri. Nilidhani ile restaurant pale ni 24/7 kumbe inafungwa usiku.

Sikuwa na usafiri, hapakuwa na boda, palikuwa na mlinzi tu kwenye vile vibanda wanavyokulaga abiria wa mabasi. Tazama picha
20181125_043951.jpg


Isitoshe, sikuwa na sweta wala koti. Nilivaa mashati yote niliyokuwa nayo kwenye begi, moja juu ya jingine. Palikuwa na ukungu usio wa kawaida, huoni zaidi ya mita 100 mbele. Naweka picha japo sidhani kama itatenda haki
20181125_043930.jpg


Kibanda kilikuwa na umeme. Nilichomeka laptop, nikawasha, nikaandika kaprogram ka kuifanya CPU iwe busy sana, hivyo kuzalisha joto jingi ambalo likawa linapulizwa na feni ya laptop.

Nikaitega laptop kwenye yale matundu ya hewa iwe karibu na pua yangu, ili niweze kupumua hewa ya joto inayotoka kwenye laptop, nisipate baridi ndani ya mwili. Masaa yakapita, asubuhi ikafika, nikaingia kazini.
 
Kwema Wakuu!

Nimeshawahi kuishi Mafinga mara kadhaa lakini sijawahi kuona baridi kama ya Juzi jumatatu tarehe 19. Dadeki baridi mpaka ukungu weñye barafu nyepesi ilikuwa inadondoka.

Nimefika Saa nane Usiku nikitokea Dsm. Nilitamani nirudi kwèñye Basi, Aiseeh! Pale Stendi nikaona makundi mawili ya Vijana yakiwa yamezunguka Moto wakiwa wanaota.
Nikavaa sweta Mbili, koti Moja lakini Wapi, nikaona sina namna Hapa Acha Nani nikaote Moto.

Wenyeji wakawa wananishangaa huku wakijaribu kutaka kunijua kama ninahitaji msaada gàni au nahitaji Usafiri WA bodaboda kwani wôte pale niligundua nu bodaboda, Mimi sikujali Wala nini, sikutaka kusalimu kwa sauti kûbwa, nikamsalimia aliyekaribu yàngu Kwa sauti ya chini. Nao wakanipuuza wakaendelea na Stori zào.

Nami nikaanza kutafakari nitaanzaje harakati zangu Siku ya Kesho Asûbuhi hasa kile kilichonipeleka. Saa yàngu mkononi ikinionyesha NI Saa Nane narobo.

Najua Baadhi ya Lodge nzuri zilizopo Hapa Mafinga, hivyo nikawa natafakari niende Ipi iliyokaribu, Mara ñàona bodaboda mmoja anakoswakoswa na Lori pale Barabarani. Vijana wanapiga Milunzi huku wakishangilia, Wengine wakipiga kelele la shangwe.

Taikon nashusha pumzi kutuliza kihoro kilichokuwa kimenianza kutokana na kuona tukio lile.

Yule bodaboda Manusura akaja pale nikawa namsahili, Hofu yake ilikuwa dhahiri usoni licha ya kuwa alikuwa anaongea na wenzake waliokuwa wanamtania Tania.

Anasema Mikono ilikuwa imeshika ganzi kutokana na baridi Kali kiasi kwamba alishindwa kukata Kona Hali iliyosababishwa akoswekoswe na lile Lori.

Basi Stori ikawa baridi jinsi inavyowapa changamoto. Kîla mmoja akieleza baridi ilivyosababisha hatari ya waô kupata ajali kama mjuavyo Vijana.

Wàpo wateja pale ambao walikuwa wanaenda maeneo ya chini Kabisa àmbapo wanadai Huko kûna baridi la kufa Mtu hivyo waliwakataa kuwabeba.

Kuangalia saa inaniambia Saa tisa. Mpaka asûbuhi yalibaki masaa matatu tuu. Nikaona sina haja ya kuchukua Lodge. Nikaamua kukesha na wale Vijana kupata uzoefu mpya.

Aiseeh! Maisha haya, ukiona unapata chàkula na unaishi Vizuri Mshukuru Sana Mungu. Kûna Watu wanahangaika na wanafanya Kazi katika mazîngira Magumu hasa ikiwemo hawa bodaboda wa Mafinga.

Niligundua pia Vijana wa bodaboda wa Mafinga wanajitambua na kuelewa mambo ya kitaifa kama mambo ya Katiba, mambo ya Haki za kiraia na mambo ya Kisiasa ya Chadema na ccm.
Ingawaje wamekata TAMAA na Maisha, wanafanya mambo ilimradi.

Zaidi, niliwapenda Kwa Sababu licha ya Hali ngumu ya Kazi Yao lakini haikuwaondolea Ûtu na ukarimu Kwa Wageni àmbao tulifika pale Stendi.

Tofauti na maeneo mengine ya nchi niliyowahu kufika Kama Kahama Mjini, Mwanza mjini, Arusha Mjini, Mbeya Mjini, Moshi Mjini, Morogoro Mjini, na Dsm. Àmbapo Miji hiyo ukifika utakutana na usumbufu wa bodaboda au wapiga debe wakikung'ang'ania kama Mpira wa Kona.

Mafinga majira ya usiku ukishuka bodaboda watakuja lakini hawatakusumbua.

Pia suala la utapeli WA nauli Mahali unapoenda nimegundua Hawana TAMAA ndogondogo,
Nakumbuka Wakati fulani nilifika Arusha Saa saba Kasoro Usiku, kuuliza bajaji Ilipo hoteli àmbayo najua Kabisa Ipo upande wa Nyuma Kwa umbali usiozidi kilomita Moja, lakini Baadhi ya madereva wengi wa Arusha wanatamaa, hizô nauli walizokuwa wanataja utabaki kuwaonea huruma, na wewe hata kama unapajua jifanye upajui ili upime uaminifu wao.

Vijana uaminifu ni Jambo kûbwa Sana. Eleweni Siku hizi Mtu hawezi kwenda sehemu pasipo kuwa na ABC za muhimu za Eneo àmbalo anaenda.

Lazima Mtu aulize nauli ya Eneo analoenda Kabla hajafika Hapo Stendi, ajue bei ya hoteli au lodge atakayoenda Kulala, na umbali WA lodge au hoteli hiyo kutokea Stendi.

Hongereni bodaboda wa Mafinga Kwa kuwakilisha Vijana wenzenu WA Hapo Mafinga. Nimewapa marks 70%.
Hii inaonyesha kama utapata kijana wa huku kûna uwezekano akawa mwaminifu ingawaje haimaanishi Hakuna àmbao siô waaminifu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa, Mafinga
Ndio maana ile kanda inaongoza kwa kale kaugonjwa kakongwe kakuitwa "Juliana" na katakuwepo sana maana hali ya hewa sio rafiki.
 
Naelewa hali iliyokukumba.

2018 Nishawahi kukosea step nikajikuta sheli ya CF Mafinga pale Kinyanambo C saa 10 alfajiri. Nilidhani ile restaurant pale ni 24/7 kumbe inafungwa usiku.

Sikuwa na usafiri, hapakuwa na boda, palikuwa na mlinzi tu kwenye vile vibanda wanavyokulaga abiria wa mabasi. Tazama picha View attachment 3075901

Isitoshe, sikuwa na sweta wala koti. Nilivaa mashati yote niliyokuwa nayo kwenye begi, moja juu ya jingine. Palikuwa na ukungu usio wa kawaida, huoni zaidi ya mita 100 mbele. Naweka picha japo sidhani kama itatenda haki View attachment 3075903

Kibanda kilikuwa na umeme. Nilichomeka laptop, nikawasha, nikaandika kaprogram ka kuifanya CPU iwe busy sana, hivyo kuzalisha joto jingi ambalo likawa linapulizwa na feni ya laptop.

Nikaitega laptop kwenye yale matundu ya hewa iwe karibu na pua yangu, ili niweze kupumua hewa ya joto inayotoka kwenye laptop, nisipate baridi ndani ya mwili. Masaa yakapita, asubuhi ikafika, nikaingia kazini.

Basi wewe ndio ungetakiwa uanzishe huu Uzi maana Moto uliokupata ni zaidi. Unaelewa hali hii zaidi na zaidi.

Yaani bila moto Kila kitu ulichovaa kinafreeze na baridi inaukuta mwili,mateso yanaanza kama Kawa.

Yaani usiombe ukajichanganya ukafika Maeneo ya Mafinga au njombe kama huna miundombinu ya kujikinga na baridi na umgeni unaweza ukafa
 
jitahidi sehemu za baridi mbali na sweta usikose kipisi cha bhang na pakiti ya fegi. HILI SITAKUSHAURI TENA
 
Asûbuhi imefika, napanda boda dadeki, mishipa ya kichwa inauma Kwa kupulizwa na Upepo, Lips za midomo inauma na ukisema uachie mdomo meno yanagongana na unaweza kujing'ata.
Huku siô poa
Leo utakunywa chai ukirudi home mdomo utakuwa umeungua, utasimulia maana hapo bado hujasema!
 
Nenda Njombe ukashuhudie baridi..mafinga cha mtoto mbona..
Bahati mzuri nazijuwa sehemu zote mbili.

Mafinga kuna season yake jua linawaka na baridi inapiga.

Sasa ukienda Njomba nyumba nyingi kuna fire place kama nyumba za ulaya kwa ajili ya kuchoma kuni za kuleta joto ndani.

My last experience Njombe nilikaa wiki moja hotelini na kuna maji moto lakini nilioga siku mbili tu, siku tano nilikuwa naoga kizulu narowesha kitaulo kwenye maji moto na kujifuta ukishavaa nguo unapiga pafyumu yako imeisha hiyo.

Kwa kifupi Mafinga na Njombe ni kama National na Panasonic hata Makambako ni walewale tu hakuna Pub za nje ni Pub za ndani.
 
Makambako baridi kavu emu nenda uje ufungue uzi
MAkambako baridi la kawaida Sana ngoja tukuelekeze tunao jua maeneo ambayo ni hatari kwa baridi 1 makete kitulo 2 mbeya isyonje 3 njombe town 4 mafinga haya maeneo ni hatari ukipita lazima mwili usisimuke ikifika Saa Tisa inashuka kama mvua na huwa inachoma hadi parachichi
 
Back
Top Bottom