Hali mtaani ni mbaya sana cha ajabu viongozi wapo kimya kama hawaoni

Hali mtaani ni mbaya sana cha ajabu viongozi wapo kimya kama hawaoni

Kazanazo

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2023
Posts
2,582
Reaction score
4,554
Ni siku nyingine tena, nawasalimu

Hapa simaanishi hali ya kiuchumi bali hali ya kimaadili mitaa imechafuka sana ila tunaowaita viongozi wapo kimya sijui maana ya uongozi ni nini?

Wanawake wanadhalilika sana wengine kwa kupenda wengine kwa kutokupenda. Wanawake ndio kioo cha maadili, hali ya kupuuza na kuacha wajiuze, watembee uchi kama bidhaa, watukanwe matusi ya nguoni kama wafanyavyo wasanii na watu wengine mtaani na udhalilishaji mwingine ni kukididimiza kizazi na jamii kwa ujumla

Uongozi ni kuonesha dira njema katika taifa katika nyanja zote kiuchumi na kijamii, kitendo cha viongozi kukalia kimya suala hili la udhalilishaji wa wanawake ni kukwepa uwajibikaji nashauri mamlaka ziangalie suala hili kwa undani na wachukue hatua stahiki

Wanawake ni mama zetu, dada zetu na ndugu zetu kumdhalilisha mwanamke yeyote ni sawa na kumdhalilisha mama yako au dada yako jamii ilitazame hili

Ahsanteni
 
Hilo ni jukumu la jamii nzima kwahiyo usijifiche kwenye kichaka cha Viongozi wakati wewe hakuna ulichofanya kutatua tatizo.

Uko hapa keyboard warrior usikute hata watoto wako hawakusalimii na unaogopa kuwatia adabu
Ni kweli ni jukumu langu lakini hata ulinzi na usalama ni jukumu la jamii ila kuna majeshi na askari wanalipwa kwa ajili ya jukum hilo
 
Mkuu kuna wale wanajifanya kutetea haki za hao wanawake cjui kama hata akili zimo wale jamaa wanawake wanadhalilika na kudhalilishwa mtaan huko wao wanaenda kudili na yule dada aliekaambiwa akaze sauti na makonda, halaf muda mwingine wanawake wanafanya mambo ya kujidhalilisha ila ukinyanyua mdomo tu kukemea utaambiwa mfumo dume, mara 50/50 mara unyanyasaji wa kijinsia, we jaribu tu utaona
 
Mikopo kausha damu chupi mkononi inawadharirisha sana wanawake.
Inaitwa chupi mkononi kwa sababu mwanamke hana kipato cha uhakika anachukua mkopo unategemea nini zaidi ya kuvua chupi ili akalipe mkopo asichukuliwe vitu vyake
Serikali haiwezi kukwepa hili jukumu hao wanaofanywa hivyo ni mama zetu sote hata kama sio ndugu wa damu bado wana jukumu la kuwalinda
 
Back
Top Bottom