DOKEZO Hali ni mbaya sana kwa walemavu tuliosoma, Si Serikali wala kampuni binafsi ambazo ziko tayari kutuajiri. Tunabaguliwa

DOKEZO Hali ni mbaya sana kwa walemavu tuliosoma, Si Serikali wala kampuni binafsi ambazo ziko tayari kutuajiri. Tunabaguliwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Pole sana mkuu.

Ni swali tu ambalo nahitaji uelewa, hivi kwenye usaili hasa serikalini, swala la ulemavu ni kigezo au ni kipaumbele katika kupata ajira? Naomba kujuzwa.

Kwa sababu kwa hali iliyopo sasa sidhani kama issue ni walemavu vs wasiokuwa walemavu, unless otherwise uwe competent na bado ufanyiwe figisu kutokana na hali yako. Ninachofahamu Issue ya ajira ni janga la kitaifa.

I stand to be corrected.
Hapo kuna unafiki mkubwa sana ndugu yangu, mlemavu lazima apewe kipaumble kwa vile ni special group isipokuwa kutokana na ulemavu wake kuna kazi ni uwongo hawezi kufanya kabisa ...Kwa kazi za serikali 90% walemavu wanaweza kufanya inategemea na ulemavu gani ...Nawafahamu wakuu wa vitengo kama wawili ni walemavu , wako nondo balaa kichwani kuzuri hata matokeo yao ya chuo ni mazuri .

Kuwatenga walemavu ni unafiki kwa vile bado kuna 50/50(wanawake kupewa kipaumbele) , kuna asilimia ya raia wa zanzibar ..Vile vile nchi inapokea pesa kutoka kweny mashirika ya kimataifa ili kukuza usawa wa kijinsia na kusaidia walemavu .

Ukisoma mwongozo kwa taasisi za serikali walemavu wanakula bata kama wanaweza kufanya kazi , wana dis-abled allowance...Wana mda mzuri tu wa kwenda kuangalia ishu zao za afya .

Mtoa mada amasema kwamba wanaonekana watasumbua kwenye kuondoka kila mara kazini ili kufuatilia matibabu , hii ni uongo maana ninajua hata hao wasiokuwa walemavu wana excuses kila mara ni yale yale tu ..Hivi ushawahi kuona usumbufu wa mwanamke mwenye mimba ni kama kazini hayupo , bado akizaa atakaa pending kwa mda .​
 
Afadhari hii mada umeweka hapa.

Hii nchi ina mambo ya Ajabu sijawahi ona, yaan mtu ana ajiriwa hadi kwa kuangaliwa Sexual Orientation yake, huu si upumbavu kabisa.

Kazi haiihitaji sexual affairs, inahusu mambo mengine kabisa, lakini hapo utaangalizwa hadi nani una date nae, km si ulofa n nn?

Li nchi ndo maana haliendelei, kutwaa ubaguzi wa kipumbavu usio na tija, una muacha mtu mwenye vigezo na sifa stahiki kwa kazi husika, kisa mapungufu yake, na una mchukua mwingine hata hajui lolote kisa ana ukamilifu fulani, jamani inaumiza hatariii.

Tupaze sauti, kuondoa sintofahamu hii.
Hizo ni mambo kutoka nje , tunapokopa ndiyo wanataka hivyo ...Kwa sasa hawa madogo wa TRA wajiangalie sana wanawake watachukuliwa kinoma .
 
Niende kwenye mada moja kwa moja!!.

Nimekuwa moja ya wahanga wa hili Tatizo kwa muda mrefu sana

Kati ya watu wanaosoma kwa mateso makubwa sana ni watu wenye ulemavu, kuanzia shule za msingi mpaka sekondari, hii inatokana na miundo mbinu mingi kuwa tofauti na Hali zetu watu wenye ulemavu.

Wakati mtu mwenye ulemavu anapambna akiamini kuwa yeye hawez kulima, kutembeza mitumba, Wala kufanya kazi ngumu za ujenzi akitegemea akili yake tu ya darasani angalau impe mwanga wa maisha.

Baada ya ajira huyu mtu mwenye ulemavu anaanza kuzunguka na baiskeli yake au magongo yake kweny interview mbalimbali, wakati mwingine hufanyika mikoani, au kwenye majengo yasiyo na lift.
Wengi wanaishia kukata tamaa sana.

Kuna sehemu niliwahi kataliwa kabisa kisa mimi ni mlemavu kwamba siwezi kufanya hio kazi kwasababu nitakuwa naenda sana hospitali, yaani trip kazini trip hospitali. Wanahisi labda sisi ni wagonjwa fulani hivi,

Inaumiza sana sana, naongea kwa niaba Yao sana.

Wengi walioajiriwa ni sababu za kisiasa, ili ionekane hawabaguliwi hasa kwenye sekta zinazohusiana na walemavu ndio huko wamejazwa!

Nina watu nawajua ni walemavu, wanapitia kipindi kigumu sana lakini wakiwa na elimu Yao kichwani! Yaani huu unyanyapaa huwezi ona kwa jicho la kawaida! Ni dhamira za watu.

Kitanda usicholalia huwezi jua kunguni wake!! We feel pain sana sana

Natimiza mwaka wa saba(7) tangu nimalize digrii yangu ya usimamizi wa fedha..

Serikali haitujali tena, zaidi ya kutulazimisha tukope pesa tuu.

Wadau wapo kimaslahi na kisiasa zaidi wapate attention wakati wanatoa misaada.

Hata vyama vya walemavu sasa hawana la kusema baada ya kulamba sukari

Sisi tukimbilie wapi zaidi yenu wadau wa hapa JF, tusaidieni kupaza sauti sisi walemavu tuliopambana kusoma kwa bidii, tunatamani kubeba tofali angalau tupate mkate wa kila siku lakini Hali zetu hazituruhusu.

Tuliamini katika elimu nayo imetusaliti, nchi imetutenga, tuna hari mbaya sana
Dah nmejisikia vibaya sana kwa kweli mungu awatangulie lakn unaposikia fursa kama bajaj za mikopo kwa walemavu please changamkia fursa siku ukipata ajira unaendelea na Career yako usikae tu kusubiria ajira
 
Mtu am-tag mama Doroth anaweza akalifikisha hili mbali.
 
Dah nmejisikia vibaya sana kwa kweli mungu awatangulie lakn unaposikia fursa kama bajaj za mikopo kwa walemavu please changamkia fursa siku ukipata ajira unaendelea na Career yako usikae tu kusubiria ajira
Bajaji za mkopo kiukweli zinasaidia sana!! C wote ambao wanauwezo wa kuendesha bajaji, Kuna ndug wengi hawana uwezo wa kusikia, wengine wanauono hafifu.. ni serikali ukae chini iunde namna ya kuwa recruit tu wanapotoka vyuo vikuu
 
Hapo kuna unafiki mkubwa sana ndugu yangu, mlemavu lazima apewe kipaumble kwa vile ni special group isipokuwa kutokana na ulemavu wake kuna kazi ni uwongo hawezi kufanya kabisa ...Kwa kazi za serikali 90% walemavu wanaweza kufanya inategemea na ulemavu gani ...Nawafahamu wakuu wa vitengo kama wawili ni walemavu , wako nondo balaa kichwani kuzuri hata matokeo yao ya chuo ni mazuri .

Kuwatenga walemavu ni unafiki kwa vile bado kuna 50/50(wanawake kupewa kipaumbele) , kuna asilimia ya raia wa zanzibar ..Vile vile nchi inapokea pesa kutoka kweny mashirika ya kimataifa ili kukuza usawa wa kijinsia na kusaidia walemavu .

Ukisoma mwongozo kwa taasisi za serikali walemavu wanakula bata kama wanaweza kufanya kazi , wana dis-abled allowance...Wana mda mzuri tu wa kwenda kuangalia ishu zao za afya .

Mtoa mada amasema kwamba wanaonekana watasumbua kwenye kuondoka kila mara kazini ili kufuatilia matibabu , hii ni uongo maana ninajua hata hao wasiokuwa walemavu wana excuses kila mara ni yale yale tu ..Hivi ushawahi kuona usumbufu wa mwanamke mwenye mimba ni kama kazini hayupo , bado akizaa atakaa pending kwa mda .​
Asant kiongozi umenena vyema sana!! Lakn hoja yangu kuu. Ni Walemavu kupata fursa za ajira hapo ndo lilipo ombi langu!! Maisha baada ya kuwa amepata ajira nafikiri inategemea na mtu..

Ombi langu serikali isikie kilio chetu, Kuna marafiki nawafaham Wana miaka mpka kumi wapo tu nyumban!!
 
Niende kwenye mada moja kwa moja!!.

Nimekuwa moja ya wahanga wa hili Tatizo kwa muda mrefu sana

Kati ya watu wanaosoma kwa mateso makubwa sana ni watu wenye ulemavu, kuanzia shule za msingi mpaka sekondari, hii inatokana na miundo mbinu mingi kuwa tofauti na Hali zetu watu wenye ulemavu.

Wakati mtu mwenye ulemavu anapambna akiamini kuwa yeye hawez kulima, kutembeza mitumba, Wala kufanya kazi ngumu za ujenzi akitegemea akili yake tu ya darasani angalau impe mwanga wa maisha.

Baada ya ajira huyu mtu mwenye ulemavu anaanza kuzunguka na baiskeli yake au magongo yake kweny interview mbalimbali, wakati mwingine hufanyika mikoani, au kwenye majengo yasiyo na lift.
Wengi wanaishia kukata tamaa sana.

Kuna sehemu niliwahi kataliwa kabisa kisa mimi ni mlemavu kwamba siwezi kufanya hio kazi kwasababu nitakuwa naenda sana hospitali, yaani trip kazini trip hospitali. Wanahisi labda sisi ni wagonjwa fulani hivi,

Inaumiza sana sana, naongea kwa niaba Yao sana.

Wengi walioajiriwa ni sababu za kisiasa, ili ionekane hawabaguliwi hasa kwenye sekta zinazohusiana na walemavu ndio huko wamejazwa!

Nina watu nawajua ni walemavu, wanapitia kipindi kigumu sana lakini wakiwa na elimu Yao kichwani! Yaani huu unyanyapaa huwezi ona kwa jicho la kawaida! Ni dhamira za watu.

Kitanda usicholalia huwezi jua kunguni wake!! We feel pain sana sana

Natimiza mwaka wa saba(7) tangu nimalize digrii yangu ya usimamizi wa fedha..

Serikali haitujali tena, zaidi ya kutulazimisha tukope pesa tuu.

Wadau wapo kimaslahi na kisiasa zaidi wapate attention wakati wanatoa misaada.

Hata vyama vya walemavu sasa hawana la kusema baada ya kulamba sukari

Sisi tukimbilie wapi zaidi yenu wadau wa hapa JF, tusaidieni kupaza sauti sisi walemavu tuliopambana kusoma kwa bidii, tunatamani kubeba tofali angalau tupate mkate wa kila siku lakini Hali zetu hazituruhusu.

Tuliamini katika elimu nayo imetusaliti, nchi imetutenga, tuna hari mbaya sana
Jitahidini muwe chawa wa mama😆
 
Sasahiv ukienda kweny maofis mengi utakuta wadada wazuri wenye mashepu Yao ndo wamejaa!! Lakn wenye kigezo Cha ueledi wachache!! Mtanisamehe naongea nilichokishuhudia
Ni kweli kabisa mkuu, nashuhudia ki taasisi fulani madem wapo na ni empty set kinyama.

wanacho jua ni kuvaa nguo za hovyo tu, Kisha kukutana migahawani.
 
Walimwengu hawana huruma wakishashiba wao inatosha hawaangalii wengine
 
Ni kweli kabisa mkuu, nashuhudia ki taasisi fulani madem wapo na ni empty set kinyama.

wanacho jua ni kuvaa nguo za hovyo tu, Kisha kukutana migahawani.
Mkuu wengi Tulisoma sana kwasababu hatupendi kudharaulika! Lakn tunakutana na Changamoto nyingine ya kutafuta ajira, kwenda huku na huko! Kiukweli ni mateso...
 
Pole sana Kwa hiyo changamoto Mkuu

Nafikiri watu wanaajiriwa Kwa kuzingatia weledi na tija ambayo unaweza kuongeza kwenye Taasisi husika.

Unaweza kuajiriwa ukiwa ni mlemavu wa ngozi/viungo ama chochote na ukawa na tija kwenye eneo husika.

Tuishi tukijua Kila mtu ni mlemavu mtarajiwa

Unaweza kuwa mzima sasa, lakini Bodaboda utakayopanda kesho ikakupa ulemavu keshokutwa
Tunaelewa bt kuna muda nako huwezi laumu sana. Hata miundombinu mingi ya ofisi zetu si rafiki kwa wenzetu.

Hata katika ujenzi miundombinu ya wenzetu inaongeza gharama sana.

Jiulize tu hata nyumba zetu tunazojenga ni rafiki kwa wenye ulemavu?
 
Tunaelewa bt kuna muda nako huwezi laumu sana. Hata miundombinu mingi ya ofisi zetu si rafiki kwa wenzetu.

Hata katika ujenzi miundombinu ya wenzetu inaongeza gharama sana.

Jiulize tu hata nyumba zetu tunazojenga ni rafiki kwa wenye ulemavu?
ungekuwa mlemavu, ambaye ulisumbuka kusoma kwa bidii, ili angalau ujikwamue;! Halafu mtu akupe sababu Kama hizo

Kwamba hata kuajiri kwasababu hajajenga barabara kwa ajili yako!! Inauma

Sijui Kama unaujua uchungu wa kushinda njaa Hali ukiwa na vyeti kabatin
 
Asant kiongozi umenena vyema sana!! Lakn hoja yangu kuu. Ni Walemavu kupata fursa za ajira hapo ndo lilipo ombi langu!! Maisha baada ya kuwa amepata ajira nafikiri inategemea na mtu..

Ombi langu serikali isikie kilio chetu, Kuna marafiki nawafaham Wana miaka mpka kumi wapo tu nyumban!!
Watu wamekuwa wabinafsi ila nafasi zenu kisheria zipo kabisa...Hii hata bungeni ilitakiwa kuwe na asilimia kwa watu special .
 
Back
Top Bottom