DOKEZO Hali ya Kawe ni mbaya, Serikali ichukue hatua dhidi ya Mwamposa na waumini wake

DOKEZO Hali ya Kawe ni mbaya, Serikali ichukue hatua dhidi ya Mwamposa na waumini wake

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Umepiga picha kwa kuchungulia kiwiziwii sana kupitia senyenge...ulikua unaogopa kumwagiwa chumvi wa upako machoni na kisim chako cha mchina
 
Kama majitu yamerogwa yanalala chini huku yakisubiria kukanyaga mawese wewe inakuuma nini? acha wajinga waangamie kwa kukosa maarifa lile jibwa lenyewe linajenga mahoteli tu, wale nin wakuonea huruma tu na kuwaaacha maana wameamua wenyewe kurogwa
 
Ila Mwamposa anazingua. Kuliko kujenga hotel Mbeya kwanini asingeanza kujenga hostels kwa ajili ya waumini wake kwanza.
Kuna jamaa aliandika "Pastor akihitaji gari, anawaambia waumini wachange, waumini wakiugua hoi wanakosa fedha ya matibabu Pastor anawaambia pray"
 
Nawasalimu wote kwa jina la Upendo. Amani, baraka na neema za Mwenyezi Mungu ziwe pamoja nanyi.

Kwa wakristu, hongereni kwa kuingia nusu ya pili ya mfungo wenu. Pia, nawatakia ndugu zangu waislam mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, mwenyezi Mungu awakirimie Neema na azipokee sala na funga zenu.

Pasipo kuathiri imani na ibada yao kwa Mungu, nataka nitoe maoni yangu kuhusu uzembe uliopo Tanganyika Packers, kwa waumini wanaosali kwa Mtume Mwamposa.

Binafsi, sina shida yoyote na kusali kwao. Isipokuwa, kumekuwepo na tabia ya watu hawa kulala chini, kwenye uwanja wa wazi usiku kucha wakisubiri huduma hii.

Jumatatu moja Mwaka jana mwezi wa 7 wakati naanza kazi kwenye taasisi moja iliyo karibu na maeneo haya, nilishangaa kuona kusanyiko kubwa la watu waliolala chini ambao kwa hesabu ya haraka hawakuwa pungufu ya 500.

Katika kundi hilo, idadi kubwa ya watu walikuwepo ni wazee, wajawazito na wanawake wenye watoto wachanga sana. Hali hii haikuishia siku hiyo, imekuwepo hadi sasa.

View attachment 2562265
Sehemu ndogo ya makundi ya watu waliolala hapo usiku wa kuamkia leo Machi 23, 2023
Mtu yeyote mwenye akili timamu hahitaji elimu ya sayari ya 5 kuona kuwa mazingira haya ni hatari kwa afya ya wahusika.

Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye elimu ya fani fulani ya afya, inayohusika na kushughulikia wagonjwa moja kwa moja, huwa nawaza sana kila ninapoona watu hawa asubuhi. Fikiria hali ya sasa ya mvua, kisha mtazame mzee, au mwanamke mjamzito, mama mwenye mtoto mchanga au mgonjwa wa kisukari, presha au kifafa anayelala hapo usiku kucha kwa siku kadhaa akisubiria huduma.

Kibaya zaidi, sehemu za kujisaidia na kupata huduma muhimu za kibinadamu hazitoshi. Mathalani, ukipita hapo asubuhi utakuta watu wanapiga mswaki hadharani na kutema uchafu barabarani, au hata sehemu ileile ambayo huitumia kulala wakati wa usiku.

Baridi kali na vumbi ni chanzo cha magonjwa mengi hasa kwa watoto na wazee. Badala ya kupata huduma za kiroho, watu hawa wanaweza kuondoka hapo wakiwa na mzigo wa magonjwa mengine makubwa zaidi.

Naomba Serikali itazame suala hili kwa umakini. Kama imeshindwa kabisa kuweka utaratibu mzuri wa kumbana Mwamposa kwa kuwa yeye ndiye kiongozi, basi miundombinu ya eneo hili iboreshwe.

Kuacha hali hii iendelee ikiwa hivi itasababisha maafa makubwa. Uponyaji wa kiroho unapaswa kwenda pamoja na uponyaji wa kimwili.

Naomba kutoa hoja!
Ni miaka kadhaa sasa huduma hii inaendelea hapo, sijapata kusikia hata magonjwa ya mlipuko, why?

Ukiongelea upepo mkali na baridi kali kama chanzo cha magonjwa basi kwa Dar es Salaam utakuwa inasema uongo kwani hali kama hiyo no nadra sana. Huku sio Mbeya wala moshi, kumbuka hilo ili uandike uhalisia.

Nijuavyo mimi hakuna mtu anaruhusiwa kulala kwenye eneo la Kanisa ndio maana hicho kikundi unachokisema (nimepita mara nyingi tu hawafiki hata 200) kinaweka kambi karibu na kituo cha daladala mbali na eneo la Kanisa.

Ikumbukwe kwamba sio jukumu la makanisa kujenga hosteli za kufikia waumini labda kama kuna huduma zinazohitaji waumini waweke kambi. Mwamposa huendesha ibada zake kwa siku na Waumini kurejea makwao. Hivyo basi mimi wajibu wa kila muumini anayekuja kuhudhuria ibada (hasa wanaotoka mikoani) kuhakikisha kwamba wanazo sehemu za uhakika za kufikia ili kupata malazi katika kipindi chote watakachokuwapo mahali hapo.

Ikumbukwe kuwa mambo ya kiimani huhesabiwa kuwa ni UPUMBAVU kwa wenye elimu kama yako, maandiko yanasema hivyo. Sasa Mungu ameyachagua mambo hayo yanayodharauliwa ili kuwaaibisha wakubwa na wenye nguvu, wasomi, nk!!

1 Wakorintho 1 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
²⁷ bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;
²⁸ tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko;
²⁹ mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.
 
"Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa". Ni heri upungukiwe na pesa kuliko upungukiwe na akili.
 
Nawasalimu wote kwa jina la Upendo. Amani, baraka na neema za Mwenyezi Mungu ziwe pamoja nanyi.

Kwa wakristu, hongereni kwa kuingia nusu ya pili ya mfungo wenu. Pia, nawatakia ndugu zangu waislam mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, mwenyezi Mungu awakirimie Neema na azipokee sala na funga zenu.

Pasipo kuathiri imani na ibada yao kwa Mungu, nataka nitoe maoni yangu kuhusu uzembe uliopo Tanganyika Packers, kwa waumini wanaosali kwa Mtume Mwamposa.

Binafsi, sina shida yoyote na kusali kwao. Isipokuwa, kumekuwepo na tabia ya watu hawa kulala chini, kwenye uwanja wa wazi usiku kucha wakisubiri huduma hii.

Jumatatu moja Mwaka jana mwezi wa 7 wakati naanza kazi kwenye taasisi moja iliyo karibu na maeneo haya, nilishangaa kuona kusanyiko kubwa la watu waliolala chini ambao kwa hesabu ya haraka hawakuwa pungufu ya 500.

Katika kundi hilo, idadi kubwa ya watu walikuwepo ni wazee, wajawazito na wanawake wenye watoto wachanga sana. Hali hii haikuishia siku hiyo, imekuwepo hadi sasa.

View attachment 2562265
Sehemu ndogo ya makundi ya watu waliolala hapo usiku wa kuamkia leo Machi 23, 2023
Mtu yeyote mwenye akili timamu hahitaji elimu ya sayari ya 5 kuona kuwa mazingira haya ni hatari kwa afya ya wahusika.

Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye elimu ya fani fulani ya afya, inayohusika na kushughulikia wagonjwa moja kwa moja, huwa nawaza sana kila ninapoona watu hawa asubuhi. Fikiria hali ya sasa ya mvua, kisha mtazame mzee, au mwanamke mjamzito, mama mwenye mtoto mchanga au mgonjwa wa kisukari, presha au kifafa anayelala hapo usiku kucha kwa siku kadhaa akisubiria huduma.

Kibaya zaidi, sehemu za kujisaidia na kupata huduma muhimu za kibinadamu hazitoshi. Mathalani, ukipita hapo asubuhi utakuta watu wanapiga mswaki hadharani na kutema uchafu barabarani, au hata sehemu ileile ambayo huitumia kulala wakati wa usiku.

Baridi kali na vumbi ni chanzo cha magonjwa mengi hasa kwa watoto na wazee. Badala ya kupata huduma za kiroho, watu hawa wanaweza kuondoka hapo wakiwa na mzigo wa magonjwa mengine makubwa zaidi.

Naomba Serikali itazame suala hili kwa umakini. Kama imeshindwa kabisa kuweka utaratibu mzuri wa kumbana Mwamposa kwa kuwa yeye ndiye kiongozi, basi miundombinu ya eneo hili iboreshwe.

Kuacha hali hii iendelee ikiwa hivi itasababisha maafa makubwa. Uponyaji wa kiroho unapaswa kwenda pamoja na uponyaji wa kimwili.

Naomba kutoa hoja!
umeongea ukweli mtupu.. makanisa mengi ya Tanzania haya ubora wa huduma sio kimwili sio kiroho, mambo ni vurugu varaga as long as wanaingiza sadaka kwao hawajali watu wanaowapa sadaka hizo
 
Mbona kila siku wanatangaziwa kwamba hapo sio mahali pa kulaa,watu wamekuja na shida zao hawana ndugu na hawana mahali pa kufikia wameamua kulala hapo unafanyaje?
 
Actually wajukuu zetu wanakua imara kwasababu wazazi wao watateseka sana

Jamii yetu ya sasa itazaa wajukuu wenye hasira sana na sisi

Watatuchukia na kukojolea makaburi yetu
Hata wakikojolea sisi hatujali maji yetu mwaposa wetu mbele kwa mbele nyuma mwiko
 
Back
Top Bottom