Hali ya kiuchumi Arusha inazidi kushuka kila uchwao

Hali ya kiuchumi Arusha inazidi kushuka kila uchwao

Poker

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2016
Posts
5,445
Reaction score
14,828
Hili jiji la arusha ambalo linasifika kwa utalii na ambalo lina historia nzuri ya kutoa wasanii, waigizaji na watangazaji maarufu, sifa zake kwa nje ni nyingi na nzuri sana. Ila kwa uhalisia ukifika ndani ya jiji hilo ni shida tupu.

Biashara ndani ya jiji hilo ni ngumu sana, watu wanafanya biashara kwa kujuana sana. Kiufupi mzunguko ni mdogo sana si soko la kilombero wala soko kuu.

Ukipita mitaa ya makao mapya utakuta nyumba self contained ya vyumba 3 shs 150,000/= na wanataka kodi ya hata mwezi. Ukienda huko ngarenaro mitaa ya shauri moyo unakuta wali wa kuku 1000.

Mbaya zaidi hili jiji mitaa mingi ni michafu sana kama sekei, sombetini, mbauda na huko mianzini. Biashara kubwa katika hili jiji ni biashara ya shule, biashara ya nyama aina zote na biashara ya bia.

Japo wanachuga hupenda kulitetea hili jiji, ila kiuhalia arusha ilipaswa kuwa mji kama miji mingine. Yaani saivi hata kahama kuna mzunguko wa hela kuliko arusha.

Hili ndio jiji ambalo matajiri wake wote hawapo top 100 ya matajiri Tanzania.

Hili pia ndio jiji linaloongoza kwa kuvaa mitumba wazee wa krokon na memorio.

Hili ndio jiji ambalo wakazi wake wengi ni lialia wakija kwenye biashara yako watataka uwapunguzie hata kitu cha mia.

Hili ndilo jiji ambalo ukikaa mwaka mmoja unaweza wafahamu wakazi wote wa hapo. Hapo utapata picha udogo wa jiji.

Imagine jiji uwanja wa ndege hauna taa za kuongozea ndege usiku.
images.jpeg
 
Arusha wamebaki na WADUDU Tu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Makonda ataliinua ki uchumi hilo jiji , Shida Watu wa Arusha wamejaa Dar es salaam wametelekeza mji wao , Mchaga wa Arusha utamkuta kajenga bonge la nyumba Goba ila Arusha anakiwanja kina Msingi kwa miaka kumi mfululizo akiambiwa auze anakuuliza kabila lako kwanza.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Makonda ataliinua ki uchumi hilo jiji , Shida Watu wa Arusha wamejaa Dar es salaam wametelekeza mji wao , Mchaga wa Arusha utamkuta kajenga bonge la nyumba Goba ila Arusha anakiwanja kina Msingi kwa miaka kumi mfululizo akiambiwa auze anakuuliza kabila lako kwanza.
Arusha ni promo za serikali tu , ule mji baada ya kuwa jiji na kupewa hadhi ya utalii na ile makao makuu ya East Africa basi ...Ila wenyeji starehe za kishamba , wachache tena wale wakimya ndio wanakula pesa , mashamba ya maua wanamiliki wazungu , wabongo kazi kuvaa mitumba .
 
Umeongea uongo mwingi sana, kwamba mji wenye wakazi zaidi ya Million 1.5 biashara ifanyike kwa kujuana tu, labda inategemea na biashara unayofanya mkuu, kuhusu uchafu, Kuna mji mchafu kama dar?
Uhalisia wa mambo ndio ulivyo na ndio maana wengi wenu mmekimbilia dar. Ukikuta palangyo ana duka la spare basi tegemea kuwaona akina ayo, na ukikuta mushi asenga ana bar basi tegemea kuwaona akina laswai.
Jiji la arusha kwa uchafu linaongoza na ni kwa maeneo mengi hata uko njiro ambapo ndio ushuani walienda weka dampo huko. 🤦‍♂️
 
Umeongea uongo mwingi sana, kwamba mji wenye wakazi zaidi ya Million 1.5 biashara ifanyike kwa kujuana tu, labda inategemea na biashara unayofanya mkuu, kuhusu uchafu, Kuna mji mchafu kama dar?
Jamaa yupo sahihi , Arusha kibiashara kutoboa ni kazi kwelikweli , Kheri ukafanye biashara Dodoma kuliko Arusha.

Mji una watu wachache eneo kubwa lakini uchafu kibao , Dar kuwa chafu ni kawaida kuyokana na wingi wa watu.
 
Back
Top Bottom