Uchaguzi 2020 Hali ya maisha mtaani ni ngumu mno

Uchaguzi 2020 Hali ya maisha mtaani ni ngumu mno

Mimi kwa siku napangua mizinga (vibomu ) vya kuombwa hela na wadada zaidi ya 6 wengine hata sio wapenz wangu ila bas tu ukionesha kumzoea anaomba hela. Kunasiku nlikua naandika nikakuta mpaka jioni inasoma 350,000 za kuombwa tu huyu kaomba 15, huyu kaomba 30, yule 20 in total ilisoma 350 nikasema what if ningetoa? Na kesho unaamka na request zingine . Maisha yamekaza sana
Yaani ukikenua meno tu unapigwa mzinga. Kula mzigo ni juu yako lakini elfu walau 10 umpe. Taifa la kudanga.
 
Ccm yenyewe kwenye kampeni zake inadanga kwa serikali. Ni fedha za umma. Mtoaji mtoto wa Dada. La sivyo tungepeana shikamoo mitaani .
 
Kuna watu watatu walienda kukopa mahali, kila mtu kamaliza shida zake hawajapeleka rejesho hata moja mmojawapo ni ndugu wa karibu ananipigia simu nimpe pesa ana issue ya haraka kabla ya saa 9 jana hela iwe imepatikana, nikamwambia hata mimi sina amesononeka sana. Leo hapa nimeshatumiwa namba za simu nitume rambirambi ,. Nawaza mie shida zangu nipeleke wapi? bora kusingekuwa kunakucha.
 
maisha hayajawai kua rahisi, kama yamekaza ni kwako, kama ni magumu ni kwako pekee
 
Ok, so kiongozi alikuwa nani chini ya chama gani?

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Usimfananishe Magufuli na viongozi wa chama chako chenye umri wa miaka 28 na miezi4 na makao makuu ya chama kama haya. Tembea mjini na vijijini wananchi wakuambie Magufuli ni nani na amewafanyia nini
images.jpeg
 
Yani hapa tu nmetoka kuandika comment sim inaingia mtu ananiomba laki kweli??
 
Mjini mnatafuta nini wajameni? Acha kuishi mjini kwa kubangaiza mtu anatembeza mikanda 3 ya suruali, key holder kuanzia jua linachomoza hadi giza linaingia eti naye anasema vyuma vimekaza! Njoo huku kijijini maisha raha na hivi tumepatiwa umeme wa REA, barabara za lami na treni za umeme zinakaribia kuja, nk maziwa, viazi, mahindi, misosi ya kumwaga!

Nje ya mada: Kumbe Trump wa Marekani Tangu awe rais amelipa kodi ya US$ 750 tu? Urais ni dili!!
Maraisi wa nchi huwa wanakuwa na "Tax exemption"
 
Sasa ni dhahiri kuwa hali ya maisha Tanzania inakatisha tamaa. Ni ngumu mno kiwango cha juu kinachokera na kuumiza.

Pamoja na ulofa mtu aliokuwa nao lakini tangu aamke asubuhi mpaka jioni atakuwa amefuatwa na watu wasiopungua 5 waliomfuata wakiomba mkopo huku yeye mwenyewe pia akiwa katika msako wa mkopo.

Yaani kila mmoja anamfikiria mwenzake labda ana unafuu fulani, kumbe siyo.

Wote tupo kwenye msoto mkali. Miaka 5 ya utawala huu imetufikisha hapa! Sasa wanakuja tena kuomba kura eti wamenunua ndege!

Tuna JAMBO LETU 28/10/2020.

Kwa kweli umepiga ngumi ya uso, kama vile unanisema mimi hapa, nimeandamwa na watu kama 7 hivi kila mtu ananiliia hali mbaya, wakati na mimi nahangaika nitoke vipi.
 
Lini hali ya maisha iliwahi kuwa RAHISI ? Kwa mifumo na utamaduni wa waafrika kuuondoa umasikini kwa watu wengi itachukua muda sana.Iwezo wetu wa kufikiri unatia shaka.
Lissu anakuja kumfanya kila mtu tajiri na hakuna kulipa kodi wala sheria kumbana mtu unaishi utakavyo.
 
Nakuuliza tuu Nani MATAGA !?

Wanaishi Duniani
Nikufafanulie nilichotaka ufahamu Mimi binafsi nikiingia Mitandaoni (JF na Twitter) Asilimia Kubwa ndipo napokutana na watu wanao mkashifu MAGUFULI Ni mara chache Sanaaa Huku mtaani kuona mtu/watu wamekaa wana mkashifu Magufuli Sio kwnye Daladala, Sokoni,Madukani nk
Zaidi Utaskia tuu Magufuri jembe, Mzee hataki mchez Safi Sana, Jamaa kanyoosha nchi na mengineyo

Huo Ni mtazamo wang Mimi Kama unao wako wa tofaut I won't mess with it [emoji276][emoji276]
Wanaogopa kupewa kesi ya utakatishsji pesa Ila ukweli tar 28 oct..alaf kaa ukijua wanaojitambua utawakuta Twitter na jamiiforum tuu..huko insta na Facebook ni wasiojitambua ndio wapo
 
Tunaposema mtaani hali ngumu, CCM matawi ya juu huwa hawaelewi, maana wao wanajitumbulia tu watakavyo. Ukimwambia nenda kajiajiri wanaanza kulia lia kama yule mkuu wa Mkoa aliyetumbuliwa akasema hana pa kushika
 
Tunapaswa kuingia mtaani na kufanya chochote hadi haki ipatikane, tusitegemee tume ya uchaguzi hakuna kitu pale.
Tuoneshe mfano. Anza kwa kurekodi ka video tu ukihamasisha tuingie mtaani kufanya chochote.
 
Ili kumuongoza mjinga mfanye kuwa mjinga zaidi,jawabu lipo 28/10 mnalialia nini?fanyeni mabadiliko sasa
 
Sasa ni dhahiri kuwa hali ya maisha Tanzania inakatisha tamaa. Ni ngumu mno kiwango cha juu kinachokera na kuumiza.

Pamoja na ulofa mtu aliokuwa nao lakini tangu aamke asubuhi mpaka jioni atakuwa amefuatwa na watu wasiopungua 5 waliomfuata wakiomba mkopo huku yeye mwenyewe pia akiwa katika msako wa mkopo.

Yaani kila mmoja anamfikiria mwenzake labda ana unafuu fulani, kumbe siyo.

Wote tupo kwenye msoto mkali. Miaka 5 ya utawala huu imetufikisha hapa! Sasa wanakuja tena kuomba kura eti wamenunua ndege!

Tuna JAMBO LETU 28/10/2020.
vip wewe bado huna uchumi wa katikati
 
Tuoneshe mfano. Anza kwa kurekodi ka video tu ukihamasisha tuingie mtaani kufanya chochote.
Usiwakatishe watu tamaa kwa woga wako, sio mara ya kwanza wala si jambo la ajabu kwa watanzania kuingia mtaani wakidai haki zao. Haki yetu ikiminywa tutaingia mtaani.
 
Njoo ununue vitunguu huku vimejaa hakuna wanunuzi. Wanunuzi walikuwa Wakenya, bwana yule kagombana na Uhuru Kenyatta biashara imeota mbawa. Vitunguu vinaozea shambani. Tunapokuambia hali ni ngumu ujue ni ngumu kwelikweli.
leta gunia nitanunua 90elf, soko liko na vinauzika, acha kufuata upepo, bambana kivyako kwa manufaa yako na familia yako,
waache hao wanao shida vijiweni wapoteze muda
 
Back
Top Bottom