Uchaguzi 2020 Halima Mdee apelekwa kupekuliwa nyumbani kwake na Jeshi la Polisi baada ya kwenda kuripoti matukio ya kutishiwa amani

Uchaguzi 2020 Halima Mdee apelekwa kupekuliwa nyumbani kwake na Jeshi la Polisi baada ya kwenda kuripoti matukio ya kutishiwa amani

alafu tunashangaa kwanini watu sio wazalendo kwa nchi yao ?
 
Tumefikaje huku?
Kikwete na Mkapa walimfahamu vizuri sana huyu binadamu ikiwa ni pamoja na jamii yake ya asili lakini waliamua kufumbia macho (funika kombe).Mkapa ameishatangulia mbele ya haki.

Ningeomba Kikwete, Mungu aendelee kumpa afya njema kwa miaka mingine mitano hadi 10 ijayo ashuhudie alichoitendea Tanzania!!! Tuombe uhai.
 
Jeshi la Polisi limemkamata mgombea ubunge wa jimbo la Kawe Dada Halima Mdee na sasa wanakwenda naye kumpekua nyumbani kwake Mbweni.

Halima Mdee alikwenda kuripoti Polisi juu ya Matukio ya kutishiwa Amani lakini cha kushangaza alipofika amewekwa chini ya Ulinzi.

Hao Polisiccm wanaoshiriki vitendo vya hovyo kuwaonea wapinzani kuwabambikia kesi wote mara baada ya uchaguzi watafikishwa ICC The Hague
 
Hii nchi bana ina mambo ya kipuuzi sana! Asa mtu anatishiwa amani anaenda kwa mamlaka za kulinda amani kureport afu jamaa wanamgeuka tena... Daah! Inasikitisha sana hawa policcm ni hovyo kweli!
 
Dada yetu alienda kuripoti polisi juu ya kuhofia usalama wake lakini polisi wakituo cha mbweni wamemweka chini ya ulinzi na wanaenda kupekua nyumban kwake hapo Mbweni...
Polisiccm wote wanaoshiriki vitendo vya hovyo hovyo kuwaonea kuwabambikia kodi watu wajiandae kukabiliana mahakama ya ICC The Hague
 
Back
Top Bottom