Hamas tumieni mbinu hii kumshinda Israel

Hamas tumieni mbinu hii kumshinda Israel

Soma historia vizuri wewe... Muarabu ndio aliyepora ardhi ya Israel baada ya waisraeli kupelekwa utumwani na wengine kukimbia utumwa... Muarabu kapora ardhi kuanzia Israel kuja mpaka Misri hadi Morocco ambayo Afrika Kaskazini yote ilikuwa ardhi ya Waafrika weusi, ila wao wamejimilikisha hadi leo.... Zanzibar pia ilibaki kidogo iwe mali ya kina Sultan kutoka uarabuni... Muarabu anajulikana kwa kuiba ardhi
Zile ni adithi ukiwa mtu mzima tafakari sana hivi ina kuwaje majirani zako wote ni waarabu halafu we ni mzungu
 
Ushauri wako ni mzuri sana na ni sawa sawa unavyosema haitakiwi kuua au kuteka raia.

Lakini hebu angalia juzi tu hapo mwezi wa Mei mwaka huu wa 2023 wao Waisrael walifanyaje wakati wanawapiga wapalestina? ni juzi tu hapo hao watu wala hawajasahau maumivu

Kama wewe hutaki watoto wako wasiuliwe au wasitekwe basi na wewe usiuwe wa mwenzako. Usifikiri hao wapalestina wao ndio hawana damu au wao hawaumii ndugu zao na watoto wao kuuliwa. Au mtoto wa familia za Israel ni bora kuliko mtoto wa familia za palestina?

Hawa wote wanachofanya sio sahihi kwa hivyo hata hao wazungu ni wabaguzi mbona Israel ilivyoua watoto na wanawake wa palestina hawajasema chochote? na mbona hawasemi Israel ni magaidi? yani wewe ukilipiza kisasi ulichofanyiwa juzi tu hapa wewe ndio gaidi lakini aliyeua mwezi Mei juzi hapo yeye sio gaidi?

Hakuna haki kwa kupendelea upande mmoja haki iwe kwa watu wote wakikosea wote wachukuliwe hatua na sio kumnanga palestina mwenyewe as if isarel yeye haui wanawake na watoto..
 
Shida ni kugeuza hekalu la suleman,kuwa msikiti wa Alaqsa. Sulemani hakujenga msikiti bali hekalu. Israel haiweziachia maneno yake ya kihistoria kisa wahuni wa Hamasi.Ifike mahali hamas wajitambue, umeme,maji pamojana huduma zingine kama chakula n.k wanapata Israel. Bado unataka uitawale Israel na kupora Jerusalem. Huu ni ujinga kabisa. Hamas wanachofanya ni ujinga. Hamas walipaswa kutumia uhuru waliopewa wakuabudu ndani ya Nchi nyingine vizuri. Huwezi jifanya unaenda Alaqsa kumbe unaenda kufanya uhalifu. Condolences to all civilians who passed away.
 
Jukwaa letu hoee Jf safiii
Nitoe shukran za dhati kwa Uongozi wa Jf ukiongozwa na mkurugenzi Maxence Melo
Napenda kutoa pongezi kwa Jf kwenda kimataifa ikiwemo pande za gaza hususani Kikundi cha Hamas kwa kulifufuatilia Jukwaa letu pendwa na kuchukuwa ushauri unaotolewa na wanajukwaa na kuufanyia kazi pia
Kazi nzuri inafanyika nyie wenyewe mnajionea tunavyochanja mbuga Kwa kasi ile ile yenye uvutani sawa na royal tuwa
 
Zile ni adithi ukiwa mtu mzima tafakari sana hivi ina kuwaje majirani zako wote ni waarabu halafu we ni mzungu
Ukiwa na Akili utajiuliza kwa nini waarabu wana nchi barani Afrika wakati Afrika ilikuwa ya watu weusi, angalia Zanzibar wamejaa waarabu, angalia Misri, Algeria, Morocco, Tunisia, Libya... Haya Maeneo ni kwamba waarabu walianza kutateka na kujimilikisha ukitizama ramani ya dunia vizuri utaona walikuwa wakitoka uarabuni wakipitia Israel, na kuingia Misri na kusambaa jangwa lote la sahara hadi huko Morocco... Haya maneno yote waliyopita walijimilikisha na kuyafanya yao mpaka leo...

Hilo swali lako limejibiwa hapo, Israel haikuwa ya waarabu, Misri sio ya waarabu
 
Nawaza tu, hivi hatuna makomando wetu wa kwenda gaza kuokoa raia wetu kama wako mateka mikononi mwa hamas kama ile operation entebe? Au hiyo kazi itafanywa na makomando wa kiisrael kuokoa mateka hao? Kama vipi israel ishirikishe makomando wetu kwenye opesheni ya kuokoa mateka hao.
Sio kukimbizana na CHADEMA....!!!

Sent from my Infinix X6517 using JamiiForums mobile app
 
Kupigwa ni kupigwa tu,haijalishi umepigwa wapi.Israel wamepigwa na wanamgambo,sio wanajeshi.
Swala ni kupiga raia... Haijalishi ni wanamgambo au wamasai wenye mishale.
 
Baada ya andiko lako hili, vipi mshahara wako umeongezeka kiasi gani hapo kibaruani kwako?
Waafrika tupunguze ujuaji kwa mambo yasiyotuhusu.
 
Wacha Israel nao ione machungu ya kuwau watoto wa Palestina.
Wewe unaongea jambo husilolijua... Israel imepigana sana vita na waarabu tangu 1948 huko, ndio ije kuona machungu leo... Soma historia Vizuri ndugu. Israel sasa hivi ina mpango wa kuchukua ardhi yote ya Gaza kuwa miliki yao... Wapale-stina wamejichanganya kwa mandonga mtu kazi, ulikuwa ni mtego tu
 
Hawa Hamas,wanawaita wanamgambo,au husikii vyombo vya habari wanavyowaita.Wanamgambo wao ni kudeal na raia,sio wanajeshi.
Ndio maana wanaitwa Magaidi "Terrorists"
 
Vita hii ikiendelea kwa miez 2 sijui kitatokea nn kwa Ukraine, Maana support na Misaada mingi itaenda israeli
Ukrein nae ndio ataendelea kula kwenzi kutoka kwa Kaka yake Urusi... Urusi nae kaona hii ni faida kwake kwa sababu dunia nzima macho yapo israel
 
Kitu pekee kinachofanya Makundi ya Palestina yaonekana ya Kigaidi hususani kwenye umoja wa mataifa na nchi za magharibi ni namna yanavyofanya mashambulio.

Kundi la Hamas lilipaswa kupiga kambi za jeshi na maneno yenye dhana za kijeshi ili kujiwekea uhalali wa kufanya mashambulizi. Kitendo cha Hamas kupiga risasi raia na kuwaua, na wengine kuteka nyara na mashambulizi mengine ya moja kwa moja kwa raia ni kosa la kigaidi, hivyo na kupelekea kundi hili kupewa jina la kigaidi.

Hotuba ya waziri mkuu wa uingereza amesema hawa jamaa sio freedom fighters au wapigania haki bali ni terrorists kutokana na matukio ya kushambulia raia. Nchi ya Marekani nayo imesema Hamas ni magaidi kutokana na namna wanavyoua raia.

Israel yeye katumia Akili sana hili asiitwe gaidi na maadui zake, badala yake wengi wanampongeza kwa kujitetea. Mfano, kabla hajafanya mashambulizi makubwa huko Gaza, aliwaonya na kutoa taarifa kwa raia yeyote aliyeko Gaza kuama eneo hilo, yani hakutaka kufanya mashambulizi ya moja kwa moja kwa Raia, jambo ambalo wengi wanaona ni la kiungwana kwa sababu vita ya Israel anapigana na Hamas na si raia wa palestina. Tofauti na kundi la Hamas ambalo lenyewe linalenga moja kwa moja raia.

Popote pale Duniani uwezi kupata support ya 100% kama unapiga raia moja kwa moja, ndio maana hata nchi za uarabuni zinashindwa kuingilia vita kwa sababu za Hamas kupiga moja kwa moja raia ambayo ni kinyume na sheria za Dunia.

USHAURI: Hamas kuishinda Israel mnapaswa kutumia Akili na si kupiga piga hovyo na kuwateka raia, mkifanya hivyo mtafanya mataifa mengine yazidi kuiunga mkono Israel na mwisho wa siku Israel itazidi kuwa na nguvu zaidi na ushawishi. Ikumbukwe nchi ya Israel inaruhusu uraia pacha, hivyo raia wa Israel wengi mnaowaua na kuwateka pia ni raia wa nchi nyingine, hivyo mtakuwa mnazipa morali nchi nyingine nazo kuiunga mkono Israel. Mfano raia wa Tanzania wawili hawajulikani walipo, hiyo ni go ahead moja kwa moja ya Tanzania kuiunga mkono Israel kwa sababu Hamas wameteka au kuua watanzania, japo Bongo nyoso haiwezi kutoa kauli. Hivyo hivyo nchi nyingine nazo mkiua raia wake. Israel hapa alijitoa kwenye kuua raia, yeye hasa hasa anatungua magorofa matupu yani safisha mji na kambi za Hamas tu, jambo linalompa mashiko.
Mkuu hata wafanyaje wao wataonejana magaidi tu kwa sababu wana resist acha waendelee kupigania ardhi yao kwa kutumia any means poaaible, when u want to kill a dog you give it a bad name, saddam alinyongwa kwa kisingizio ana silaha za mass destruction, gaddafi aliuliwa na hao magharibi kwa visingizio vya ajabu yote ni magharibi watimize lengo lao , acha hamas wapambane kuhusu kuitwa magaidi acha wawaite tu kwa sababu wao ndio wanaoutunga hayo majina kwa wenzao
 
Hizo ng'ombe za kizayuni ni magaidi pia ,wameshambulia hospital yote bila kujali Kuna wagonjwa.USA ni mnafiki pamoja na usharika wake.. Chuki ya USA ni dhidi ya uislamu tu hana jipya maana walishasema hawapigani na ugaidi ila wanapigana dhidi ya uislamu.

View: https://youtu.be/mXwh4bBlP1M?si=aJcNDi196kuOUPIJNdege za US ndio zinapiga Gaza na dalili msikie huyu mta gazaji Israel hana silaha za namna hio ni US peke ndio anazo alizutumia Afghanstan.

Yani ndege za Israel zinapiga na za US kwa pamoja pale gaza.


Kuna ndege za US zinatokea kwenye base yake pale Jordan na kwenye ile carrier zina piga pale Gaza.
 
Mkuu hata wafanyaje wao wataonejana magaidi tu kwa sababu wana resist acha waendelee kupigania ardhi yao kwa kutumia any means poaaible, when u want to kill a dog you give it a bad name, saddam alinyongwa kwa kisingizio ana silaha za mass destruction, gaddafi aliuliwa na hao magharibi kwa visingizio vya ajabu yote ni magharibi watimize lengo lao , acha hamas wapambane kuhusu kuitwa magaidi acha wawaite tu kwa sababu wao ndio wanaoutunga hayo majina kwa wenzao
Ardhi yao gani... Waarabu pale hawana ardhi... Ni kama walivyoteka ardhi ya Misri, Algeria, Libya Tunisia, na Morocco ambazo zilikuwa ni ardhi za waafrika weusi... Walitaka kuiba hadi Zanzibar na kuiweka chini ya utawala wa kisultani
 

View: https://youtu.be/mXwh4bBlP1M?si=aJcNDi196kuOUPIJNdege za US ndio zinapiga Gaza na dalili msikie huyu mta gazaji Israel hana silaha za namna hio ni US peke ndio anazo alizutumia Afghanstan.

Yani ndege za Israel zinapiga na za US kwa pamoja pale gaza.


Kuna ndege za US zinatokea kwenye base yake pale Jordan na kwenye ile carrier zina piga pale Gaza.

Hapo US ameamua kutumia zile Silaha za zinazokaribia ku-expire. Anaona makombora yamekaa muda mrefu ngoja yakafanye kazi... Pia kupitia hiyo vita ndio Marekani uwa-train wapiganaji wao wa ndege za kivita 😂
 
Hata Bongo kisheria raia wote wanapaswa kuwa ni askari... Nchi zote zina sheria hii kila raia kupitia jeshi...

Lakini hiyo aimaanishi kuua raia eti kisa wanapitia kozi za kijeshi... Adui ni yule aliyejohami kwa mapambano tu, hutakiwi kumuua au kumdhuru mtu asiyekuwa kwenye mapambano
Ina maana yale maghorofa ambapo israel anapiga kule yote kuna watu wamejihami kwa silaha ila wapo ndani tu wanakunywa chai?
 
Ina maana yale maghorofa ambapo israel anapiga kule yote kuna watu wamejihami kwa silaha ila wapo ndani tu wanakunywa chai?
Upande wote wa Gaza hakuna raia... Raia wote waliambiwa kuondoka...
 
USHAURI: Hamas kuishinda Israel mnapaswa kutumia Akili na si kupiga piga hovyo na kuwateka raia, mkifanya hivyo mtafanya mataifa mengine yazidi kuiunga mkono Israel na mwisho wa siku Israel itazidi kuwa na nguvu zaidi na ushawishi. Ikumbukwe nchi ya Israel inaruhusu uraia pacha, hivyo raia wa Israel wengi mnaowaua na kuwateka pia ni raia wa nchi nyingine, hivyo mtakuwa mnazipa morali nchi nyingine nazo kuiunga mkono Israel.
Umeongea as if kuna member wa Hamas humu😂
 
Back
Top Bottom