Hamna watu wanaotapelika kirahisi kama waumini wa dini hii

Ukraine waafrika wananyanyapaliwa.wale mapadri?

Afrika wananyanyapaliwa kila kona ya dunia uzunguni,uhindini,arabuni nk.

Wamarekani weusi wanawanyanyapaa waafrika kuona wamarekani weusi ni bora zaid ya waafrika wengine.

Watanzania wenyewewe mnanyanyaliana.
 
🤣😅
 
Wakristo wengine pombe siyo haramu.

Hata hivyo hoja kuu no kudanganyika kirahisi.
 
We Wakala wa shetwani shindwa kwa jina la Yesu.

Hiyo ni damu wala si pombe, usirudie tena kujizima data kichwani mwako.



MATHAYO 26:26-29

"Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu

Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki;
kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu."
 
Wakristo wanapigwa kwenye "miujiza"..ni mtu mjinga tu ndo atataka kuona miujiza
 
Reactions: Tui
IMANI !!!

Utamcheka vipi fulani anatapeliwa kwa kuamini wakati mfumo mzima wa Dini umejengwa katika Imani ?

Chochote kile katika imani kwa macho ya asiyeamini logically kinaweza kuonekana kama utapeli
 
Kuna wale wanaoaminishwa wakijilipua na mabomu na kuua watu wengi,wanaenda peponi na huko peponi watapewa zawadi ya mabinti bikra 70!!!
Wote ni Sawa tu,Swala la kudanganyika halina dini.
 
Yesu alikuwa anagonga mvunyo kama kawaida, ndio maana hata muujiza wake wa kwanza ulikuwa kutengeneza gambe la upako
 
Divai ni tofauti na mvinyo.
Mwanzo 9:20-23
[20]Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
And Noah began to be an husbandman, and he planted a vineyard:
[21]akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
And he drank of the wine, and was drunken; and he was uncovered within his tent.
[22]Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
And Ham, the father of Canaan, saw the nakedness of his father, and told his two brethren without.
[23]Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
And Shem and Japheth took a garment, and laid it upon both their shoulders, and went backward, and covered the nakedness of their father; and their faces were backward, and they saw not their father's nakedness.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…