Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Pasco,
Mwisho mimi sijapatapo kumbeza Nyerere siwezi kukosa adabu kiasi hicho
na kama una ushahidi wa hili ulete hapa barzani watu wote waushuhudie.
 
Pasco,
Mwisho mimi sijapatapo kumbeza Nyerere siwezi kukosa adabu kiasi hicho
na kama una ushahidi wa hili ulete hapa barzani watu wote waushuhudie.
 
Hiyo picha inaonyesha huo ukoo wa kina Sykes ulikuwa na fedha sana mwaka 1942 Ally amevaa suti na tai!

Na ni watunzaji wazuri wa nyaraka na picha.
Kitulo,
Kwa bahati nzuri leo nimeiona hii picha katika archive yangu.

Picha hii ilipigwa mwaka wa 1958 nyumbani kwa Nyerere Magomeni.

 
Pasco,
Mwisho mimi sijapatapo kumbeza Nyerere siwezi kukosa adabu kiasi hicho
na kama una ushahidi wa hili ulete hapa barzani watu wote waushuhudie.
 
Kitulo,
Kwa bahati nzuri leo nimeiona hii picha katika archive yangu.

Picha hii ilipigwa mwaka wa 1958 nyumbani kwa Nyerere Magomeni.

Shukran,inabidi sasa itengenezwe nyumba ya makumbusho ya Abdulwahid&Ally Sykes.

Kama nyaraka na baadhi ya vitu ukoo wao na jamaa zao wanavyo .
 
Pasco..kwani ukikaa kimya utapunguwa nini?
Ww ulitegemea hao masheikh uliosema uliongea nao ulitegemea wakujibu nini ulidhani wanamapungufu ya akili kama ww?
Ivi hufaham mpaka mtu kufikia kuwa sheikh ni mtu mwenye elimu busra hekima upeo kiasi gani?
Utoke utokako huko sijui bariadi au ngudu ukamulize sheikh Kasim au Nurdin kuhusu Mwl Nyerere unadhani watakujibu nini kama sio yale unayo yapenda ww?
Unajaribu kijitutumua kujenga upinzani na mzee MS wakati sio marika yako mzee MS anajenga hoja na anambatanisha na vielelezo ww unaleta porojo zisizo na hoja wala viambatanisho.
Pasco.. hunahoja na sidhani kama hata hao masheikh uliosema uliongea nao kama kweli uliongea nao hassa sheikh Kassim bin Juma allah amreh huko aliko.
 

Kitulo na Sahimtz,
Pasco
kanighadhibisha sana kuniita mimi muongo.
Nimerudi nimuonyeshe ni kiasi gani mimi naunganika na hiki niandikacho:

KUTOKA JF: ALLY SYKES, PETER COLMORE NA JIM BAILEY
Kitulo said:
Shukran,inabidi sasa itengenezwe nyumba ya makumbusho ya Abdulwahid&Ally Sykes.

Kama nyaraka na baadhi ya vitu ukoo wao na jamaa zao wanavyo .​

Kitulo,

Katika moja ya vitu nikimuhusudu Bwana Ally Sykes ni jinsi alivyokuwa hodari
wa kutunza nyaraka na kumbukumbu.


Alikuwa na tabia ya kuweka katika jalada chochote atakachokuandikia au wewe
utakachompelekea katika maandishi.


Nyaraka zote za TAA na TANU alikuwa akiziweka kwenye ''safe,'' na zile za kawaida
akizihifadhi katika ''filling cabinet'' na akijua majalada yake kwa majina.

Utasikia akimwambia secretary wake Bi. Zainab, ''Hebu nipe ''file,'' la fulani.''


Nina hisi hata mimi amenifungulia jalada ingawa sikupata kuliona kwani iko siku
alinitolea ''notes'' niilizochukua katika mazungumzo tuliyofanya miaka 20 iliyopita.


Nilipigwa na butwaa.

Bwana Ally alikuwa na picha nyingi sana za wakati wa kupigania uhuru na
akizitunza kama nembo ya jicho.


Katika moja ya vitu nikizozana na Bwana Ally Sykes ni nyaraka zenye taarifa
za taifa hili yeye kukataa kuzikabidhisha kwa Tanzania National Archive (TNA).


Bwana Ally alikuwa na kisa na sababu za kuamua kukaanazo mwenyewe
nyaraka zake.


Alipata kunieleza mkasa uliomfika katika siku za mwanzo za uhuru kuhusu hizo
nyaraka hiyo kwake likawa funzo.



Hii picha nilipiga na Bwana Ally Muthaiga Country Club Nairobi tarehe 21 May 1989.

Muthaiga Club ni ''exclusive club,'' ya ''millionaires'' na ni Waafrika
wachache sana utawaona katika club hii.


Bwana Ally alikuwa mwanachama toka mwaka wa 1967.

Nilikuwa kila nikenda Nairobi Peter Colmore akinialika hapo club na
tukizungumza mengi katika historia ya Afrika Mashariki katika miaka ya
1950 hadi 1960.

Ilikuwa kupitia Peter Colmore nikaweza kuandika historia za wanamuziki
mashuhuri kama Frank Humplink, Mwenda Jean Bosco na Eduardo
Masengo.




Peter Colmore akiwa nyumbani kwake Muthaiga

Frank Humplink (1927 - 2007) The Pioneer of East African Sound

Hapo Nairobi ndipo Ally Sykes alipoanza siasa mwaka wa 1947 alipotoka
Burma Vita Pili ya Dunia na ndipo alipojuana na wanasiasa wa wakati ule
hapo mjini kama
Jomo Kenyatta, WW Awori, Tom Mboya na wengineo.

Wakati huu alikuwa kijana mdogo sana wa miaka 20 na alikuwa akihudhuria
mikutano ya siri ya Mau Mau.


Kwa hakika nimesoma mengi kutoka kwa Bwana Ally Sykes na siku zote
akinijulisha kwa watu kama mtoto wake.


Watu wote alionijulisha kwao niliweka kumbukumbu zao katika mazungumzo
yetu.


Alipokufa Peter Colmore February 2004 taazia zilizoandikwa na magazeti ya
Kenya zilikuwa za kurashiarashia.


Taazia niliyoandika mimi kutoka Dar es Salaam ilichapwa na The East African
na walistaajabu imekuwaje mimi nimemjua mtu huyu kwa kiasi kile.


Mimi niliwajibu kuwa Peter Colmore alikuwa baba yangu.

Lakini hata kabla sijakutana na Peter Colmore nikiwa mtu mzima mwaka 1995
Nikimjua toka utoto wangu.

Ofisi yake ilikuwa ilikuwa karibu na nyumba tuliyokuwa tukiishi Mtaa wa Lindi
mwisho karibu na Arab Street (sasa Nkrumah).


Peter Colmore: The Man With the Midas Touch - News

Bwana Ally alinijulisha kwa Jim Bailey.

Jim Bailey
ndiye alikuwa ''owner'' wa gazeti la Drum Magazine likichapwa
Johannesburg.

Afrika Kusini wametengeneza Filamu ya maisha ya Jim Bailey inaitwa ''Drum.''


Nilimsaidia Jim Bailey kupitia mgongo wa Bwana Ally Sykes kuhariri na
kuchapa kitabu cha
Nyerere cha picha: ''Nyerere of Tanzania.''

Nilimshangaza Mzungu kwenye ndege tukielekea Johannesburg ambako yeye
ndiko kwao nilipomwambia kuwa mimi ni rafiki ya
Jim Bailey.

Ikasadifu kuwa wao walikuwa majirani.
Nikamwambia kuwa nataka nimtafute sahib yangu nikifika Johannesburg.


Alinipa pole.
Akanambia
Bailey tumemzika mwezi uliopita.

Bailey ameacha Bailey African History Archive, Johannesburg na ameifanyia
historia ya Afrika hisani kubwa sana.

Huu ni mkusanyo wa picha na makala kuhusu harakati za kudai uhuru wa Afrika
pamoja na mengi katika ukoloni.
 
Pasco..umekimbia au umefuata ushauri wangu maana kimya kimezidi au nondo anazo shusha SHEIKH ULAMAA ALLIM MUHAMED SAID MZEE WA MUJINI zimekuingia hata pakutokea huna?
Muungwana akivuliwa nguo huchuchumaa sijui nyie kina NGOSHA?
NJOO UYAKANUSHE HAYA KWA HOJA MADHUBUTI AU UYAKUBALI KWA MOYO MKUNJUFU...
 
Sahimtz,
Toka awali nilijua Pasco hana pumzi wala ''stamina,'' ya kwenda ''marathon,''
na mimi.

Katika ujana wetu tulijaribu michezo mingi sana kuanzia kucheza mpira
hadi kupiga muziki.

Vyote hivyo nilipitia na ndani yake nilijifunza mengi.

Kwanza uwe na kipaji na pili juu ya kipaji ujifunze kila siku katika kile
ulichoamua kufanya.

Ikiwa ni muziki na unapiga ala sema ''guitar'' basi jifunze ''chromatics,''
yaani kutembea kwenye ''scales,'' za ''guitar,'' lako au ''key board,'' yako.

Ukiwa ni mpira ujufunze ball control (danadana) na ujifunze ''feints.''
Ukiweza hivi utang'ara.

Pasco anataka kuwa msomi bila kusoma.

Huu ni muhali na ndiyo ikawa kila akiandika anachokijua ni ''Mapinduzi
Matukufu.''

Kashika ''slogans,'' za ASP.
Hapo ndipo nikajua huyu hawezi kwenda raundi 15 na mimi ataishia njiani.
 
Mohamed Said
Kuna mambo kadha wa kadha umeyaongelea, ningependa unisaidie kufahamu

1. Kwavile umesema Pasco hajui kitu kuhusu 'mapinduzi matukufu' leo unawaambia nini wazanzibar wanaosherehekea mapinduzi hayo kila January 12 ya kila mwaka?

2. Je, bado unasimama na kauli yako kuwa hujamdharau au kumdhalilisha Nyerere?

3. 'Umhumi wa nyerere haupo tena' sisi kama Taifa tunawezaje kuandika historia ya nchi hii bila kumtaja Mwalimu?

4.Ni nani aliyeandika katiba ya kwanza ya chama cha siasa Tanganyika?

5. Na kwavile umuhimu wa Nyerere haupo, umuhimu upo wapi na kwa nani sasa hivi?

Ningependa tujadiliane katika muktadha huu, na siyo nukuu za vitabu

Nitashukuru ukinisadia kama nukta zilivyo hapo juu na si kuchanganya mambo katika kapu moja

Ahsante
 


Moh, naona kuna kitu hakija kaa sawa - ukiangalia time stamp ya picha ya Bwana Peter Colmore inaonekana ilipigwa 3/11/2007 16:09 HRS lakini kwenye taarifa yako unasema Colmore alifariki February,2004 - hii imekaa vipi tufafanulie tafadhali.
 

JF siku hizi ni jumba la ibada? Au zile links anazoweka Alama Mohamed Said zinakufikisha jumba la ibada la kwenye mtandao?
 
Kweli kila jambo lina tafsiri mbili.
Ingawa maswali yako umeyaelekeza kwa mzee ms lakini maswali yako no 1,2,3 na 5 hajakaa sawa yanaonekana umemuuliza halafu umemjibia.
Nivyema ungemuuliza na ukamuacha ajibu mwenyewe.
 
Kweli kila jambo lina tafsiri mbili.
Ingawa maswali yako umeyaelekeza kwa mzee ms lakini maswali yako no 1,2,3 na 5 hajakaa sawa yanaonekana umemuuliza halafu umemjibia.
Nivyema ungemuuliza na ukamuacha ajibu mwenyewe.

Huyo anaejiita Nguruvi3 wala asikutaabishe, ni mmoja kati ya wanaoungulika moyo na kukatika matumbo kila wanapomsoma Alama Mohamed Said.

Wengineo utawaona tu humu, maradhi yao ya moyo hayafichiki na huzidi kila waonapo maandiko ya Alama.
 
Moh, naona kuna kitu hakija kaa sawa - ukiangalia time stamp ya picha ya Bwana Peter Colmore inaonekana ilipigwa 3/11/2007 16:09 HRS lakini kwenye taarifa yako unasema Colmore alifariki February,2004 - hii imekaa vipi tufafanulie tafadhali.
Bukyanagandi,
Ile picha ya Colmore niliipiga mimi mwaka wa 1995 na camera
zile za kutia film kisha unasafisha (develop) studio.

Baada ya kuwa na digital camera nikawa nazipiga picha zangu
na kuzihifadhi katika computer yangu ndiyo hapo unaona hiyo
tarehe ya digital.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…