Hans Poppe wa TATOA amchambua Magufuli

Hans Poppe wa TATOA amchambua Magufuli

Mbn kuna tetesi znasema jamaa kala kona muda tu

Ova

Kwani leo? Ni kitambo sana. Si kwa kesi ya Simba ni issue tofauti. Jiwe alipoingia tu jumba jeupe akaanza kumsulubu nadhani partly kuna uhusiano na issue ya huu uzi. Kuna malori ya jamaa zaidi ya 20 kuna wakati yalikaa border ya Tunduma zaidi ya mwezi eti kodi gani sijui haijalipwa. In the end jamaa akajiongeza akakumbuka ni issue ya makaburi so ikabidi ayauze yote na kampuni yote kwa ujumla akaishia zake. Ila mimi sielewi, hivi hapa duniani tunaishi milele? Vitabu vya dini tunavyoviamini (ninaamini tunaviamini ndio maana kutwa kucha tunaomba tuombewe) vinasema kuna maisha baada ya kifo. Sasa kwanini tunaishi tofauti as if tutaishi milele? Chuki zinatusaidia nini na sisi ni wacha Mungu (sina hakika hii ni kwa mujibu wa yale tuyasemayo majukwaani).
 
Nilimuona huyu jamaa siku ya harambee ya UKAWA wakati wa kampeni mwaka 2015.
 
Uko vizuri Mkuu. Hongera sana. Nakubaliana na yote uliyoyaandika Mkuu.

In a nutshell: Magufuli anaonekana na watanzania kama mtu hodari na mchapakazi, kiuhalisia mimi naona kinyume chake.

Binafsi si msafiishaji wala sina uhusiano wowote na sekta hiyo , lakini ninasafiri sana kwa barabara nchi karibu zote za SADC, Suala la mizani na sheria zake zinazidi Kuwa tight hapa kwetu pengine kuliko nchi nyingine za sadc, na pengine ndo tunaongoza kwa rate ya uharibifu wa barabara kuliko wenzetu kwa sababu ya ubabe wa mtu mmoja tu, MAGUFULI !!!

Uharibifu wa barabara kwa kiasi kikubwa unatokana na sheria mbovu zilizowekwa na kusimamiwa na viongozi husika, kulalamkikia wasafirishaji ni sawa na kuficha ukweli wa tatizo, si kweli kuwa tunabeba mizigo mizito sana. Bali tuna utaratibu mbaya wa kubeba mizigo ndo maana barabara zetu hazidumu.

Kuna mawili huwa nafikiri dhidi ya wizara hii na watendaji wake: Either wananufaika na rushwa kutoka kwa wasafirishaji hivyo wanaopt njia ambazo hazitatui tatizo bali kuiongezea mzigo serikali na mtu wa kawaida au hawajui na hawako serious kuboresha pengne kuondoa kabisa sheria kandamizi zinazopelekea watu kutocomply.

Mfano: Botswana idadi ya juu ya axle ni 9 urefu mwanzo hadi mwisho ni mita 22, hapa kwetu ni axle 7 na urefu hautakiwi kuzidi mita 17!!! Put it simple: napokuwa na axle nyingi ndio unavyozidi kutetea barabara na the opposite is also true,

Ningekuwa mimi ndo Magufuli ningejiuliza swali moja -kwanini South Africa wanabeba mizigo mizito yet road network zao zina lifespan kubwa kuliko zetu na pia hawana idadi kubwa ya mizani kama sisi. Na bado wakifika Tunduma wanaona ni afadhali ku-offload mizigo na kupakia kwenye malori yetu??

Hivi kuna hasara gani TANROADS ikiruhusu axle 9 na urefu ukawa 22 metre! !! Kwanini Trailers za Interlink ambazo zinatuika karibu Africa nzima hapa kwetu ni marufuku? Remember: Australia wanabeba mpaka tani 80 kwa kuongeza idadi ya axle na kuto limit urefu! Na bado barabara zao zinadumu.
 
Akimbie haraka atafia jela mwambieni
Aende wapi wakati tayari washamzunguka?atakuja kuyakumbuka maneno yake ingawa alikuwa sahihi
FB_IMG_1525103633538.jpg
 
Hans Poppe alikuwa na lugha chafu sana kwa msiomfahamu alikuwa anawatukana mpaka mawaziri kwenye serikali ya JK huku akisema kuwa nchi hii Hakuna wa kumfanya lolote......

Alikuwa analalamikiwa na Tanroads kwa kuzidisha uzito kwenye maroli yake na yeye akawa anawajibu watu kuwa yeye haongei na mbwa......

Kwa mhuni fulani mwenye majibu ya kihuni na kejeli iliyochanganyikana na dharau....watu wengi tulijiuliza hii jeuri anaitoa wapi....!!
Sasa kanywea labda MAKONDA atamuokoa maana ni simba mwenzake
FB_IMG_1525103633538.jpg
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mhazini wa TATOA ambacho ni chama cha wenye malori Tanzania amemwita Magufuli ni mtu asiyejua na ambaye ana chuki kubwa kwa transporters na angeweza angewaondoa wote nchini kwa tuhuma za kufikirika kuwa wanaharibu barabara.

Amekwenda mbali zaidi kwa kusema anafikiria kuwa Magufuli anafanya makusudi ili apate mgao wake wa rushwa. Hii ni kwa sababu amewaagiza wafanyakazi wa mizani ya Iringa wawatoze faini wenye malori na kuuliza kwanini faini zinapungua. Hans Poppe anasema faini zinapungua kwa sababu transporters wamekuwa compliant so hawatakiwi kutozwa faini ovyo.

Amesema Magufuli ndio Waziri wa ovyo kuliko wote kwa kuendesha uongozi wa vitisho na amri za ovyo na kwamba mainjia wote wanamwogopa sana na wanasema hivyo.

Anasema ingawa Magufuli si injinia lakini elimu yake inatosha kutoa mwongozo mzuri ila anafanya makusudi.

Amesema amri ya Magufuli kuondoa tolerance ya 5% katika uzito wa mizigo ni kinyume cha sheria kwani hiyo ni sheria au taratibu iliyowekwa tokea zamani wakati Magufuli bado anasoma.

Kwa hitimisho wameamua kusimamisha malori yote kutofanyakazi kuanzia kesho.

Hii imetoka katika mahojiano na ITV 5 minutes ago. Ipo kazi!
Teh teh teh Nimekubali kuna watu wajuzi wa kufukua makaburi
 
Back
Top Bottom