Hans Poppe wa TATOA amchambua Magufuli

Hans Poppe wa TATOA amchambua Magufuli

Mhazini wa TATOA ambacho ni chama cha wenye malori Tanzania amemwita Magufuli ni mtu asiyejua na ambaye ana chuki kubwa kwa transporters na angeweza angewaondoa wote nchini kwa tuhuma za kufikirika kuwa wanaharibu barabara.

Amekwenda mbali zaidi kwa kusema anafikiria kuwa Magufuli anafanya makusudi ili apate mgao wake wa rushwa. Hii ni kwa sababu amewaagiza wafanyakazi wa mizani ya Iringa wawatoze faini wenye malori na kuuliza kwanini faini zinapungua. Hans Poppe anasema faini zinapungua kwa sababu transporters wamekuwa compliant so hawatakiwi kutozwa faini ovyo.

Amesema Magufuli ndio Waziri wa ovyo kuliko wote kwa kuendesha uongozi wa vitisho na amri za ovyo na kwamba mainjia wote wanamwogopa sana na wanasema hivyo.

Anasema ingawa Magufuli si injinia lakini elimu yake inatosha kutoa mwongozo mzuri ila anafanya makusudi.

Amesema amri ya Magufuli kuondoa tolerance ya 5% katika uzito wa mizigo ni kinyume cha sheria kwani hiyo ni sheria au taratibu iliyowekwa tokea zamani wakati Magufuli bado anasoma.

Kwa hitimisho wameamua kusimamisha malori yote kutofanyakazi kuanzia kesho.

Hii imetoka katika mahojiano na ITV 5 minutes ago. Ipo kazi!
Hiki kisasi anacho sasa ndiyo kawaamuru Takukuru walazimishe kumwingiza kwenye kesi ya Rais wa simba na makamu wake kaburu
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kwani leo? Ni kitambo sana. Si kwa kesi ya Simba ni issue tofauti. Jiwe alipoingia tu jumba jeupe akaanza kumsulubu nadhani partly kuna uhusiano na issue ya huu uzi. Kuna malori ya jamaa zaidi ya 20 kuna wakati yalikaa border ya Tunduma zaidi ya mwezi eti kodi gani sijui haijalipwa. In the end jamaa akajiongeza akakumbuka ni issue ya makaburi so ikabidi ayauze yote na kampuni yote kwa ujumla akaishia zake. Ila mimi sielewi, hivi hapa duniani tunaishi milele? Vitabu vya dini tunavyoviamini (ninaamini tunaviamini ndio maana kutwa kucha tunaomba tuombewe) vinasema kuna maisha baada ya kifo. Sasa kwanini tunaishi tofauti as if tutaishi milele? Chuki zinatusaidia nini na sisi ni wacha Mungu (sina hakika hii ni kwa mujibu wa yale tuyasemayo majukwaani).
ipo List ndefu ya kukomolewa na Mtukufu malaika toka chato hataki kusikia wale waliokuwa wakimpinga wapo Uraiani wanatembea, kaamua kuwa Rais mpenda kesi kesi kutwa kuwabambikia kesi Wapinzani na sasa wafanyabiashara kama alivyomnyanyasa Manji na wengineo kimya kimya wakiwemo akina Dewji baba yake MO Mohamed Dewji na wenzao.
 
Mie nilishangaa sana Mkuu huyu jamaa ujasiri wa kumnanga hivi dhalimu anaupata wapi? Kumbe ni kaburi la miaka mitano iliyopita.

Watu wanafukua makaburi kudhihirisha maandiko kwamba lazima yatimie
 
ipo List ndefu ya kukomolewa na Mtukufu malaika toka chato hataki kusikia wale waliokuwa wakimpinga wapo Uraiani wanatembea, kaamua kuwa Rais mpenda kesi kesi kutwa kuwabambikia kesi Wapinzani na sasa wafanyabiashara kama alivyomnyanyasa Manji na wengineo kimya kimya wakiwemo akina Dewji baba yake MO Mohamed Dewji na wenzao.
Bado yule mwenye kampuni ya ukandarasi wa barabara aliyerudia kipande cha mtongani mpaka mzunguko wa Kona ya bandari kilwa road nimeisahau jina naye yupo kama ndege cha moto anakiona
 
Mie nilishangaa sana Mkuu huyu jamaa ujasiri wa kumnanga hivi dhalimu anaupata wapi? Kumbe ni kaburi la miaka mitano iliyopita.
hahaha kiroba kingemhusu, ila kwa sasa tra, uhamiaji, tanroads, pccb ndo watahangaika nae mpaka aombe po!
 
Back
Top Bottom