Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Kwa nyumba sijui ipoje ila kwa kiwanja afadhali
Mi nilijipatia kiwanja kwa namna hiyo
Kilikuwa ubavuni kwangu na mwenyewe hakuwahi kuonekana
Nikaenda ardhi nikawaeleza wakaniambia kasafishe kwanza ukiona kimya weka msingi tulia

Nilifanya hivyo na hakutokea mtu lakini palikuwa ma tofali 12 pale chini
Baada ya mwaka nikaenda ardhi nikawaeleza wakanipa offer/hati na hadi leo napamiliki
Ulitoa hongo wewe si bure, hawawezi kukufanyia kirahisi rahisi hivyo.
 
U know what nilishaona watu wako nje ya nchi wamejenga nyumba zao hapa Tanzania na hawajawashirikisha ndugu zao na hawataki wajue maana ndugu zao walishawatapeli sana ..so mtu anaamini mafundi au mtu baki ikitokea huyu mtu akafariki huko hiyo mali inaweza kosa mwenyewe...yapo kabisa haya sishangai....au mtu amejenga for suprise au siri kwa familia yake mara paa amefariki...

Pia mitaa hapa Dar kuna nyumba majirani wanajua kabisa mtu anayeishi alipewa alinde then huyo aliyejenga hajaonekana miaka mingi sana na inasemekana labda alishafariki au mtu aliyepewa alinde alishafanya ushirikina asije kabisa...
 
Hizi nyumba zione hivi! Hakuna kitu kinachotengenezwa kwa hela ndefu mpaka kukamilika kama nyumba! Ubora na mwonekano wa nyumba na mahali ilipo ndo thamani ya hela iliyotumika kuijenga.

Kwasababu hiyo nyumba haiwezi kukaa tupu! Kama sio watu wanaishi, basi ziko roho zinaishi mule! Mashetani nayo yanataka kuishi kwenye nyumba nzuri! Roho iliyokuwa nyuma ya upatikanaji wa hela na ujenzi wa hiyo nyumba ndo zinaishi mule! Jichanganye uingie uone mziki wake!
Mnamtisha nae aende na roho wa Mungu atafanikisha
 
Kuna nyumba moja ilikua kando ya barabara mitaa fulani ambayo tulikua tukipita tukiwa wadogo. Kipindi hicho hiyo nyumba ilikua ina milango, madirisha ya vioo na kila kitu kama vile kuna watu wanaishi humo, ila hakukua na mtu. Sisi tulikua tukiambiwa nyumba hiyo ina majini, na enzi hizo tulikua tukipita hiyo njia tunarusha mawe juu ya bati na kukimbia!

Juzi nimepita hiyo mitaa, nikakuta ile nyumba imechakaa kabisa, nyasi ndefu zimeota, bati zimeezuliwa, vioo na madirisha yamevunjikavunjika, hakuna milango yaani zimebaki kuta tu zimesimama.. Kwakweli mpaka leo sijajua hii nyumba ilikua ya nani?
Mkuu kwa kuwa sasa ishakuwa mkubwa nakushauri jitwalie hiyo nyumba na kiwanja chake
 
mmh tupe ubuyu bhana ata na id fake kama masai dada , sasa ilikuwaje the bold akamwaga manyanga kwa cheupe wake toto laini Nifah na sasa hivi nani anamiliki jimbo au lipo wazi?
Ungeanza kwa kuuliza kistaarabu ningekujibu vizuri tu, ila kwakuwa ulishavuruga subiri mpaka niwawekee bonge la thread mtajua yote.

Ila, mpira umerudi kwa kipa na kipa hana masihara kaamua kulinda goli lake hafanyi kosa tena.
 
Nyumba za namna hiyo mbona nyingi njia ya kutoka mbezi kwenda mmabwepande mpaka bunju
Niiliwahi kupelekwa kununua kiwanja arround mabwepande ila alokuwa anataka kuniuzia kiwanja akaanza na maneno hichi kiwanja changu niliuziwa na kina kaburi moja katikati lakinj pia huyu jirani yangu tangu ajenge hiki hekalu kubwa hapa hakuwahi kukanyaga tena humu
Anasisitiza, chungulia majani yalivyoota kwenye paving blocks
Niliahirisha kila kitu kwa kumkubalia kila asemacho
Nilitoka hapo hata namba zake niliblock
Maeneo ya Mabwepande, Bunju mpk Bagamoyo huko unauziwa kiwanja halafu ukihurumiwa sana unarogwa kabla ya kujenga. Wakitaka kukukomoa unarogwa baada ya kuwa umejenga.
 
Naona ka waongelea majumba ya mbweni dar es salaam
Hayo majumba ya mbweni huku uswahilini kwetu tunajidanganya kwamba ni ya TISS. Eti wanaoikosoa serikali wakitekwa ndiyo hupelekwa humo kuteswa mpk kufa.
 
Ungeanza kwa kuuliza kistaarabu ningekujibu vizuri tu, ila kwakuwa ulishavuruga subiri mpaka niwawekee bonge la thread mtajua yote.

Ila, mpira umerudi kwa kipa na kipa hana masihara kaamua kulinda goli lake hafanyi kosa tena.
mie nilikuwa nachangamsha genge tuu,Hongera mwayaa basi mtoto wa mama mkwee ndo afanye kuoa sasa tena nyie muslim lakini mpaka leo bado mpo kwenye uchumba sugu
 
Kuna nadharia mbili hapa.

1. Yawezekana mmiliki alikuwa anamjengea mchepuko. Ili siku moja aje amfanyie surprise. Lkn kabla ya surprise jamaa akapata ugonjwa ama ajali na kufariki. Kwahiyo si mchepuko wala familia waijuao nyumba hii.

2. Mmiliki alipoikamilisha alipigwa kifungo cha miaka 30 au zaidi jela.

Je, nijitwale hii nyumba? Vipi kama nadharia ya 2 ndiyo sahihi? Akitoka jela na kurudi uraiani itakuwaje? Ingawa kuna usemi wa kiswahili unanipa moyo "cha kuokota siyo cha kuiba, mwenye mali mpumbavu".

3. Lishakuwa Pango la Wachawi, hukosi Popo Humo [emoji1783]
 
Kuna nadharia mbili hapa.

1. Yawezekana mmiliki alikuwa anamjengea mchepuko. Ili siku moja aje amfanyie surprise. Lkn kabla ya surprise jamaa akapata ugonjwa ama ajali na kufariki. Kwahiyo si mchepuko wala familia waijuao nyumba hii.

2. Mmiliki alipoikamilisha alipigwa kifungo cha miaka 30 au zaidi jela.

Je, nijitwale hii nyumba? Vipi kama nadharia ya 2 ndiyo sahihi? Akitoka jela na kurudi uraiani itakuwaje? Ingawa kuna usemi wa kiswahili unanipa moyo "cha kuokota siyo cha kuiba, mwenye mali mpumbavu".
Hakikisha Una Kadi ya Chama
 
Ngoja niwape kisa kimoja

Kuna jamaa zangu Mzee wao alifariki akawa amewaachia nyumba za urithi, sasa baada ya miaka mingi kupita Kuna nyumba walikua wanaiuza. Katika kupekua mafaili wakampa mnunuzi document ili ajiridhishe. Yule mnunuzi kaenda ardhi anakuta ile document ni ya nyumba nyingine kabisa tofauti na ile aliyopanga kununua

Akajulisha jamaa wakamtaftia document sahihi wakafanya biashara. Sasa jamaa wakaanza kujiuliza hii document ya mara ya kwanza ni ya wapi mbona hii nyumba hatuijui. Wakafatilia kushirikiana na ardhi mpaka kwenye Hio nyumba, wakamkuta Mzee mmoja anaishi hapo baada ya kumhoji Mzee akadai alipewa Hio nyumba Aishi na Mzee mmoja ila ana miaka mingi hawajawasiliana na hajui hata yupo wapi.

Jamaa wakawa wamepata nyumba nyingine kilaini kabisa na hakuna aliyekua anaijua.
Sio wazee wa kibongo wanaopenda K za mabaamedi
 
Ungeanza kwa kuuliza kistaarabu ningekujibu vizuri tu, ila kwakuwa ulishavuruga subiri mpaka niwawekee bonge la thread mtajua yote.

Ila, mpira umerudi kwa kipa na kipa hana masihara kaamua kulinda goli lake hafanyi kosa tena.
Lakini jamaa mzigo si kala sana tu?
 
Kuna nadharia mbili hapa.

1. Yawezekana mmiliki alikuwa anamjengea mchepuko. Ili siku moja aje amfanyie surprise. Lkn kabla ya surprise jamaa akapata ugonjwa ama ajali na kufariki. Kwahiyo si mchepuko wala familia waijuao nyumba hii.

2. Mmiliki alipoikamilisha alipigwa kifungo cha miaka 30 au zaidi jela.

Je, nijitwale hii nyumba? Vipi kama nadharia ya 2 ndiyo sahihi? Akitoka jela na kurudi uraiani itakuwaje? Ingawa kuna usemi wa kiswahili unanipa moyo "cha kuokota siyo cha kuiba, mwenye mali mpumbavu".
Yule mwanaume aliyekutia mimba akakukimbia vp mmesharudiana nae.?
 
Mkuu watu wanakufa Kila siku,na kama ujuavyo waafrica wengi asset zetu hufanya Siri Ili kuepuka kupigwa na wake au kulogwa na ndugu,so Kuna majumba,na fedha kibao zimetapakaa,mitaa nliyohamia Kuna mjengo naulia taiming Toka nifike hapa sijawahi ona hata mtu anafyeka nyasi,so Hamia Anza maisha mkuu,Bahati mbaya akija utamwambia unamlindia.
 
Back
Top Bottom