Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Dunia hii ina Sayansi kubwa.

Jichanganye uone.

Humo watu wanaishi wengi tu tena raha mstarehe.

Au ukute kuna Mama yake anaishi humo
 
Nyumba za namna hiyo mbona nyingi njia ya kutoka mbezi kwenda mmabwepande mpaka bunju
Niiliwahi kupelekwa kununua kiwanja arround mabwepande ila alokuwa anataka kuniuzia kiwanja akaanza na maneno hichi kiwanja changu niliuziwa na kina kaburi moja katikati lakinj pia huyu jirani yangu tangu ajenge hiki hekalu kubwa hapa hakuwahi kukanyaga tena humu
Anasisitiza, chungulia majani yalivyoota kwenye paving blocks
Niliahirisha kila kitu kwa kumkubalia kila asemacho
Nilitoka hapo hata namba zake niliblock
 
Haya mambo yapo kuna jamaa angu ni fundi alikabidhiwa nyumba ikakamilika ,mmiliki akamwambia aishi kwa muda

Yaan mpaka naandika apa bado anaishi hapo na mwenye nyumba hajatokea inakaribia miaka 15 sasa, tujifunze kushirikisha watu wa karibu ona jamaa anakaribia kumiliki mjengo kiulaiiiiiniπŸ˜…
 
Nakushauri usiingie na kukaa kwenye nyumba hiyo, huenda huo ni mtego. Kwanza mwenye nyumba anahesabia nyumba hiyo ni mpya, kwahivyo ukianza kukaa wewe itaanza kuchakaa (depreciate).

Atakuacha ukae hata miaka miwili ili ahalalishe njama zake. Halafu atakuja, anakuambia umlipe fidia, ambapo atakutajia gharama kubwa sana, ambayo atajua utashindwa kuilipa.

Ukishindwa kuilipa atakuambia either uchague akupeleke mahakamani au mkae wote kwenye hiyo nyumba (nadhani unanielewa). Katika options hizo mbili, hakuna iliyo rahisi, lakini utatakiwa uchague moja. Nakusihi usiingie kwenye nyumba hiyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…