Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Kwa nyumba sijui ipoje ila kwa kiwanja afadhali
Mi nilijipatia kiwanja kwa namna hiyo
Kilikuwa ubavuni kwangu na mwenyewe hakuwahi kuonekana
Nikaenda ardhi nikawaeleza wakaniambia kasafishe kwanza ukiona kimya weka msingi tulia

Nilifanya hivyo na hakutokea mtu lakini palikuwa ma tofali 12 pale chini
Baada ya mwaka nikaenda ardhi nikawaeleza wakanipa offer/hati na hadi leo napamiliki
Yaani hivyo tu ukamiliki ardhi?
Hii scenario nimeiona sio mbali sana na nilipo, jamaa amekuwa akilima hicho kiwanja, anapanda mihogo nk na vile amepakana na hicho kiwanja, naona kabisa akikimiliki kiulaini kabisa.
 
Kuna nyumba moja ilikua kando ya barabara mitaa fulani ambayo tulikua tukipita tukiwa wadogo. Kipindi hicho hiyo nyumba ilikua ina milango, madirisha ya vioo na kila kitu kama vile kuna watu wanaishi humo, ila hakukua na mtu. Sisi tulikua tukiambiwa nyumba hiyo ina majini, na enzi hizo tulikua tukipita hiyo njia tunarusha mawe juu ya bati na kukimbia!

Juzi nimepita hiyo mitaa, nikakuta ile nyumba imechakaa kabisa, nyasi ndefu zimeota, bati zimeezuliwa, vioo na madirisha yamevunjikavunjika, hakuna milango yaani zimebaki kuta tu zimesimama.. Kwakweli mpaka leo sijajua hii nyumba ilikua ya nani?
 
Kuna nadharia mbili hapa.

1. Yawezekana mmiliki alikuwa anamjengea mchepuko. Ili siku moja aje amfanyie surprise. Lkn kabla ya surprise jamaa akapata ugonjwa ama ajali na kufariki. Kwahiyo si mchepuko wala familia waijuao nyumba hii.

2. Mmiliki alipoikamilisha alipigwa kifungo cha miaka 30 au zaidi jela.

Je, nijitwale hii nyumba? Vipi kama nadharia ya 2 ndiyo sahihi? Akitoka jela na kurudi uraiani itakuwaje? Ingawa kuna usemi wa kiswahili unanipa moyo "cha kuokota siyo cha kuiba, mwenye mali mpumbavu".
Unajifunza utapeli! Acha hizo, tafuta hela kijana wangu! Acha tamaa.
 
Back
Top Bottom