Hapa ndio ninapokuwa na walakini na uwepo wa Mungu

Haya yana uthibitisho. Vitabu kama biblia na kurani ni uthibitisho wa watu waliojifanya mungu kaongea nao.
Labda nikuulize kipi kinakufanya ukatae kuwa Mungu/miungu haijawahi kuongea na binaadamu?
 
Sasa kila mtu akimueleza Mungu tofauti na mwengine na kila mtu akisema ndio alivyomuelewa yeye Mungu hapo inakuwa na tofauti gani na dini?
 
Mkuu ni nakubaliana na wewe kupinga hoja hii kwamba binadamu wanaweza kuwa wasemaji na watetezi wa Mungu.

Pia nakubaliana na hoja yako ya kutafakarisha kinyume na mtazamo ya wengi kuhusu hoja ya Mungu kuumba binadamu dhaifu, ili baadaye aje amfanye mkamilifu iwapo binadamu atamuabudu, atamsujudia, ataonyesha utii na unyenyekevu kwake. Haingi akilini kabisa!!!

Mkuu ninachopingana na wewe ni kwamba viumbe hai pamoja na binadamu wamajitokea tu.

Kwa kuwa wewe ni mchunguzi mwenye fikra huru pamoja na wengine, nawaalika kutandawaa kwa kina kuhusu undani wa elimu na maarifa kuhusu anga za juu zaidi.

Mkuu ni kweli na hakika kuwa kuna matabaka ya uumbaji/uundaji kutokana na utofauti wa maarifa, ujuzi, uwezo, nishati na nyakati.

Karibu tuelimishane pamoja.
 
Wote ni wa Mungu , kila mmoja anayo haki ya kupitia chungu na tamu , maisha yako hivyo
 
Labda nikuulize kipi kinakufanya ukatae kuwa Mungu/miungu haijawahi kuongea na binaadamu?
1. Watu waliodai kuzungumza nayo walishindwa kuthibitisha hilo. Wakademand watu waamini tu blindly, wakisema hiyo ndiyo faith.
2. Binadamu Wana tabia ya kuattribute kila kitu kizuri kwa Mungu. Ni mazoea tu.
3. Mungu anapewa sifa za kibinadamu sana ambayo yanaendana na dhana za kibinadamu zunazoprevail wakati husika. Mfano Lord of lords au king of kings, lords na kings ni obsolete concept mwaka 2024, ila enzi hizo walikuwa na nguvu isiyomithilika so watunzi wakatumia kuonesha ukuu wa mungu. Leo hii, who cares about a lord or a king? Unaona wazi yale ni maandishi ya watu tu.
3. Contradictions kwenye mitazamo iliyoandikwa na watunzi wa misahafu inakuonesha haikutoka chanzo kimoja kama wanavyodai.
4. Jamii zote zenye maendeleo ya kibinadamu kwa sasa zilikuwa na watu waliojidai wametokewa na kuongea mungu na wameoewa kazi ya kusambaza matakwa yake duniani. Mbona Mungu asingeitokea miafrika pia tukasambaze neno lake duniani?
5. The so called neno la Mungu limejaa mambo ya fantasy ambayo mwanadamu mwenye akili timamu unapaswa kuburudika nayo tu ukiwa mtoto, na kuelewa mara moja kwamba hizo ni hadithi ti za kutunga pale unapokuwa mtu mzima.
Mifano ni mingi:
Wanyama kuongea, binadamu kusimamisha jua lisizame watu wapigane, mtu kupasua bahari, jiwe kukimbia na nguo za Musa, n.k
Hizi ni fantasies, legends na fables tupu. Hata watoto wanaosoma literature can tell.
 
1) Hii ya kwamba walishindwa kuthibitisha kuongea kwao na Mungu umeipata vp? Kwa sababu wakati huo walikutana na upinzani pia maana watu walikuwa na imani zao zengine sasa utaanzaje kuwaambia watu waache kuamini wanachoamini wakati huo na kuamini unachosema wewe bila kitu cha kuwashawishi kufanya hivyo?
 
Wa
Wataka kujua kama Mungu yupo au hayupo nenda Spitali ya Muhimbili jibu utalipata huko .
 
Nimeandika vitu vitano, umejibu kimoja.
Jibu vyote, ndipo tuendelee na mjadala. La sivyo, unanipotezea muda.
 
Sasa ndio huwa unajiingiza kwenye hizi blah blah ili iweje ikiwa hutaki blah blah? Unataka Mungu mwenyewe ajitokeze kama yupo hautaki blah blah sasa unajiingiza kwenye blah blah za nini?
Ni maamuzi yangu.
 
Sasa unavyokuja hapa kwenye majadiliano na kusema Mungu mwenyewe ajitojeze na sio sisi kupiga blah blah unataka sie tufanyaje tuache kujadili maana ni blah blah na tukakuitie Mungu? Au unaongea tu bila kufikiri?
Nawakosoa.

Ndio maana nipo hapa.
 
Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe na muumbaji wake, Hata muumbaji wa kila kitu lazima awe na muumbaji wake mwingine.

Pasiwepo kitu chochote kile kilicho jitokeza chenyewe pasipo muumbaji, Maana kitazua maswali ya kiliwezaje ku exist chenyewe tu bila muumbaji.

Hata huyo Muumbaji hawezi ku exist mwenyewe tu from nowhere.

Na kama si lazima kwamba kila kitu kilichopo kina muumbaji, Hata Ulimwengu na vyote vilivyomo except man-made things Havina na havihitaji muumbaji.
 
Kama unasoma Biblia. Unajua aliyoyapata Ayubu? Je, alikuwa na dhambi?
 
Nimeandika vitu vitano, umejibu kimoja.
Jibu vyote, ndipo tuendelee na mjadala. La sivyo, unanipotezea muda.
Nimegusa hilo moja kwa sababu ndio nimeona kitu kipya kwangu tofauti na hayo mengine ambayo tushaona yakielezwa sana humu, ila kama unaona nalazimika kukujibu yote kwa wakati mmoja kinyume na hivyo nakuwa nakupotezea muda basi acha nisipoteze muda wako mkuu.
 
Ukiwa na imani kubwa na Mungu lazima ujaribiwe ndugu ili kuthibitisha imani yako kwake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…