Hapa ndio ninapokuwa na walakini na uwepo wa Mungu

Huyo Mungu wapi alikwambia ukimuamini utaishi maisha ya raha mustarehe hapa duniani?
 
 
Mkuu kwa pole kwa changamoto ulizopitia ila inaonekana zimepita.

Kwa mtu anayefikiri kwa uhuru ni lazima apitie mtanziko kama unaopitia kwa sababu tunakuzwa katika imani sio kwa fikra huru.

Mkuu ukianza kuwa na fikra huru kwenye ulimwengu wa imani unaonekana kuwa unakufuru (Kama Infropreneur na wengine wengi Hapa Jf) na hapa ndipo mtanziko unapoanzia.

Kwa kutumia nadharia ya uchunguzi (observation theory) kwa kina kuna facts zifuatazo utaziona:

1. Viumbe vyote hai na visivyo hai havikujitokea tu! Muda , nishati, nafasi na mifumo vyote hivi viliumbwa/viliundwa.

2. Kila kimoja wapo ni mkusanyiko wa vumbuzi mbali mbali kwa kutumia michakato kadhaa kwa kipindi cha muda mrefu.

3. Kila kiumbe kwa asili yake kimepitia mikononi mwa waumbaji/waundaji wengi hadi kufikia kama kinavyooneka na kinavyojiendesha sasa hivi.

4. Kwa kuzingatia fact namba 1, 2 na 3 hapo juu kuna uhakika kuwa kuna waumbaji/waundaji (Miungu).

5. Kwa kuzingatia fact namba 4 hapo juu ni wazi kwamba kwenye mchakato mzima wa upatikanaji wa kiumbe, Miungu msingi imehusika kwa nyakati tofauti tofauti. Kwa hiyo kuna Miungu mingi sio mmoja.

6. Kila kiumbe kimeumbwa kwa sura tofauti na kusudi maalum tofauti na inavyoelezwa kwenye ulimwengu wa imani kuwa ni kwa kusudi la kuabudu na kusujudu. Kusudi kubwa la kuumbwa binadamu ni kuwezesha mawasiliano ya uhakika kati ya binadamu na Miungu hiyo kutoka hapa duniani kwenda kwa hao Miungu.

Kwa kuzingatia nadharia hii ya uchunguzi ni wazi kuwa Miungu wapo. Dhambi ni dhana ya kukiuka taratibu, kanuni sheria na miiko ya jamii fulani.
 
Huyu atakuwa shabiki wa Yanga
 
Mungu anaadhibu watu wake ikiwa chanzo kikuu ni yeye.

Infact Mungu ni mjuzi wa Yote.

Hivyo alimuumba shetani huku akijua kwamba kuna watu watakwenda kuteseka.

Mateso haya yote duniani, Chanzo chake ni Mungu mjuzi wa yote ajuaye Mwisho kabla ya mwanzo maana haya yote alishayajua kabla.
 
hizo relations za matabaka ya kimaisha sizan kama znatosha kuthibitisha kuhusu uwepo wa Mungu
 
Ebu soma hili andiko kwanza then ukae ujifikilie:



Dunia hii imepitia uongo/utapeli/propaganda kubwa sana na zikapita lakini uongo pekee ulio dumu kwa muda mrefu ni huu

Hebu fikiria unaambiwa kuna MUNGU muweza wa yote yupo sahihi na hajawahi kukosea

Ameumba dunia kwaajili yetu na ataiangamiza dunia kwaajili yetu
Alijua ataiangamiza dunia kabla hata hajaiumba lakini aliiumba hivyo hivyo ili aje kuiangamiza,
Ameumba moto wa jehanamu kwakuwa ametuumba tukosee ili atuchome moto japo alikua na UWEZO wakutuumba tusiwe wakosefu ili atuumbie Pepo tu tukale bata

Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyo taka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje

Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani(magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani
Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake

Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair

Mungu muweza wa yote hayupo WAZI PASI NA SHAKA kwa watu wote kujua huyu ndio MUNGU badala yake Mungu ndio amekua sehemu kubwa ya mgawanyiko wa watu na kusababisha kuwa na imani za MIUNGU zaidi ya milioni dunia nzima
Na kibaya zaidi unatakiwa to blindly believe him, usihoji wala kuwa na shaka juu ya uwepo wake(ni laana na kufuru) vinginevyo moto wa milele unakuhusu

Yaani kuna Fundi Kapenta mmoja huko Galilaya eti kafa kwaajili ya dhambi za watu wote duniani.... seriously ?
Akaitwa Mungu lakini Mungu huyu akajaribiwa na shetani
Fundi kampenta huyu hakuandika kitabu chochote ila wahuni walio kuwa wanampinga ndio wakaja kuandika vitabu kuhusu fundi huyu na vinaitwa “Bibilia Neno la Mungu takatifu”
Mabilioni ya watu dunia kote wanakesha makanisani wakimlilia na kumuomba awape uponyaji, mali, waume/wake nk

Hebu fikiria huko Arabia kuna Maamuma mmoja hajui kusoma wala kuandika alidai anashushiwa maagizo na Mungu kukata vichwa watu wote watakao pinga na kutokutii maagizo yake, “akashushiwa” aya za vitisho na neema kwa watakao tii, yaani ukifa unampigania Mungu unakwenda kupewa mbikra 72 kazi yako ni kuzagamua tu
Mabilioni ya watu duniani wanasujudu mara 5 kwa siku na kushinda njaa mwezi kila mwaka ili wakale naye bata Peponi

Kwamba maisha yako hapa duniani ni ya mpito tu maisha yako yapo baada ya kufa
Unachotakiwa kufanya ni kumuamini na kufanya aliyoa agiza ili ukale bata sana baada ya kufa
 
Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hatakaa awepo.

The fact that an almighty God and all powerful God needs humans to speak for him and defend him, It's a prove that he doesn't exist.

Huyo Mungu kama yupo ajitokeze hadharani mwenyewe ajidhihirishe na kujitetea mwenyewe, Kama ana huo uwezo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…