Uchaguzi 2020 Hapa ndipo anapokosea Dkt. John P. Magufuli. Kwasasa yeye ni 'mgombea zaidi' kuliko Rais

Uchaguzi 2020 Hapa ndipo anapokosea Dkt. John P. Magufuli. Kwasasa yeye ni 'mgombea zaidi' kuliko Rais

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kila anapopita, hujieleza. Tena ni mambo yaleyale aliyoyahubiri na kuyatajataja kwa miaka yake yote mitano madarakani: ujenzi wa reli, ujenzi wa bwawa la umeme, barabara, zahanati, madaraja na kufuta ada za shule za msingi hadi kidato cha nne. Hana jipya katika sera zake. Hana mipango mipya kuelekea 2025. Ndiyo maana ametamka kuwa miaka mitano hii iliyopita ilikuwa ni onjaonja tu, yenyewe inakuja. Nani, mwenye utimamu wa akili na mwili, ataitaka hali iliyopo iendelee?

Katika kauli zake (mfano ya jana kule Ikungi, Singida), Dr. Magufuli amekuwa akizungumza kana kwamba yeye si mgombea wa Urais ila Rais 'anayeendelea' bila kuzingatia matokeo ya mwisho ya kura za Urais zitakazopigwa Oktoba 28. Kwa mfano alisema eti (Lissu) anagombea Urais ambao hatashinda! Yeye, kama mgombea, anajuaje kama Lissu hatashinda? Yeye, kama mgombea, anamjua mshindi wa uchaguzi huu tayari? Amejuaje?

Dkt. Magufuli anapaswa kuuvaa 'ugombea' zaidi ya Urais. Anapaswa, pamoja na kuwa bado yuko madarakani, kusema amefanya nini; amefanikiwa katika nini; ameshindwa katika nini na atarekebishaje aliposhindwa. Si sawa hata kidogo kuongea kana kwamba LAZIMA ASHINDE. Watanzania wanaweza kumchagua mgombea mwingine kwa kura zao. Wanaweza kuvutiwa na mwingine katika sera hata kama hakuna hela.

Mgombea ajinadi kwa sera zake na si mikwara yake!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kasulu, Kigoma)
 
Watumishi wa Tume ya UCHAGUZI wote ni WATEULE WAKE.

Wasimamizi wa Uchaguzi wote ni WATEULE WAKE.

Viongozi wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, wote ni Wateule wake.

Mishahara anawalipa yeye, magari mazuri amewapa yeye.

Halafu wawatangazie WAPINZANI ushindi!

AMEJIHAKIKISHIA USHINDI.
 
Alafu Sera ya Mgombea urais kusema ataboresha maisha ya watanzania alafu mwisho wa mkutano anaanza kuwaomba wamchangie hela hao hao anaosema ni masikini wameharibiwa maisha na ccm aache kabisa.

Kama ni masikini wa kutupwa hizo hela wanazokuchangia wanatoa wapi.

Lisu acha kupotosha watu
 
Atapigwa na butwaa kubwa pale anapotakiwa kufanya Handover ya ofisi ya urais kwa Mhe.Tundu Lissu.....
Acheni kudanganyika na mikusanyiko mnayoiona.. Katika jiji kama Mza lenye wakazi milioni mbili, watu wazima wakiwa takrabin 1.5M, CHADEMA ikikusanya watu elfu 20, hao ni sawa sawa na 1.5%. Kwa hiyo huwezi isemea 98.5% ambayo haijafika kwenye mkutano wa Lissu ina maamuzi gani.
 
Watumishi wa Tume ya UCHAGUZI wote ni WATEULE WAKE.

Wasimamizi wa Uchaguzi wote ni WATEULE WAKE.

Viongozi wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, wote ni Wateule wake.

Mishahara anawalipa yeye, magari mazuri amewapa yeye.

Halafu wawatangazie WAPINZANI ushindi!!!!!!!!!!!!.

AMEJIHAKIKISHIA USHINDI.
Na hii kauli ndo itafanya tuungwe mkono na jumuiya ya kimataifa pale tutakapoamua kumng'oa madarakani kwa nguvu
 
Ni lazima JPM awaambie watanzania kafanya mambo gani makubwa ya kimaendeleo kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.kama kaweza makubwa madogo hayatomshinda kuyatekeleza endapo wananchi wakimchagua kwa mara ya pili.
 
Kwani Tundu Lissu in Rais Mbona Kila Akikaribishwa Jukwaani anaitwa Mheshimiwa Rais karibu uongee na wananchi wako .....Hlafu inakuwa dhambi kwa mwenye chake kukutumia kwenye Kampeni
 
42 (3) Mtu aliyechaguliwa kuwa Rais atashika kiti cha Rais hadi-
(a) siku ambapo mtu atakayemfuatia katika kushika kiti hicho atakula kiapo cha Rais; au
(b) siku ambapo atafariki dunia akiwa katika madaraka; au
(c) siku atakapojiuzulu; au
(d) atakapoacha kushika kiti cha Rais kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.

Rais_bado_ni_Rais.jpg
 
Back
Top Bottom