Hapa ndipo utatupenda sisi watu weusi

Kuendelea na mjadala na huu Uzi pia Ni matumizi mabaya ya muda. Ndugu Zangu tufanye kazi, Maendeleo hayana chama. In Magu voice.
 
Usiponde sana mzee, Mbona tumegundua CHUMA ULETE
 
Umezungumza ukweli kabisa

Kuna mengi sana ya kuyakana na kuyaacha kuhusiana na ushabiki...

*Asuejua maana haambiwi maana*
 
Mbona historia zetu tunazifaham vema kila usiku bibi zetu wanatusimulia tukiwa tumezunguka moto kabla ya kulala
 
Mbona historia zetu tunazifaham vema kila usiku bibi zetu wanatusimulia tukiwa tumezunguka moto kabla ya kulala
Mwafrika ni Ndege aina ya Tai aliyelelewa tangu mdogo na kuku na kujichanganya na kuku hata ikafika wakati akahisi amepoteza uwezo wake wa kuruka juu angani.

Na hili likitokea baada ya siku moja kujaribu kuruka na kushindwa hata mmiliki wake kunadi, Tai aliyechanganyika na kulelewa na kuku naye ni kuku.

Ila siku katika masiku atajidhihirisha kwamba "ONCE AN EAGLE, ALWAYS AN EAGLE" ipo siku Afrika itaweza kuruka tena na kuwathibitishia wamiliki wake kwamba "TAI NI TAI HATA AKILELEWA KWENYE BANDA LA KUKU.
 
Lengo la wasemao hivyo ni ili tusijione ni completely Failures, Tupate hope, kwa kuona kuwa kuna ndugu zetu waliwahi kuwa vizuri kichwani ho kumbe na sisi tunaweza. Huwezi kuendelea bila kujua ulipotoka. hata hao wachina tunaowaogopa sasa, wanaheshimu na kuenzi kale zao.
 
Tunapoteza muda mwingi katika hilo na kusahau uhalisia.wazungu walianza lini kuja kututawala? Waliwezaje kuja kututawala ikiwa tayari tulikuwa tume advance?

China wameweza kuadvance baada ya kuamua kupambana siyo kutafuta wa kulaumu.sisi miaka na miaka baada ya uhuru tumefanya nini? Kabla ya kutawaliwa tulifanya nini? Mpaka wazungu kadhaa kutoka kwao kuja kututawala sisk wengi tayari ilikuwa inaonesha tuna udhaifu.

Baada ya miaka mingi ya uhuru nambie tunajitegemea vipi?zile akili tulizokuwa nazo tunazitumia vipi kwa sasa? Uvumbuzi gani tunafanya? Tunashindana vipi kujikwamua? Bado tunategemea wazungu na wachina hao hao tena ktk maisha yetu

 
Tena hapa ndio huwa wananifikirisha Sana nikiangalia picha za misafara ya watumwa,yaani Babu zetu mashababi kabisa Kama thelathini wamekamatwa na waarabu wawil legelege,Sasa najiuliza hivi walikuwa sawa kweli?
Hapa kwenye la utumwa wengi hamjui vema au hamjui kabisa. Kwanza kabisa ufahamu utumwa ulifanikiwa vema kwa sababu ya ushiriki thabiti wa mtu mweusi dhidi ya weusi wenzake. Jamii zenye nguvu zilikamata mateka kutoka jamii dhaifu na kuwauza kwa waarabu(mawakala) wa utumwa. Na kumbuka silaha zilitumika pia.

Jambo lingine, jinsi walivyokua wanatekwa hata ungekua wewe usingeweza. Na ile minyororo ni mizito sana na namna walivyokua wanafungwa no way unaweza kujinasua. Jaribuni kujifunza. Awali nami nilikua mpumbavu kuwaza kama wewe.
 
Kwa hiyo unataka turudi darasani tusimuliane kwamba Babu zetu machief waliexchange mateka weusi wenzao kwa kupewa shanga na migolore na waarabu si ndio??HAISAIDII...Tunarudi palepale kwa nini huyu chief mweusi alikubali kuuza weusi wenzie kwa nini asingewateka waarabu Kama tunavyoambiwa kuwa before colonialism watu weusi tulikuwa mbele kitecholojia iweje leo mseme Tena mwarabu alikuwa na silaha madhubuti???
Halafu nikukumbushe tu msomi anapojibu hoja huwa hapanic Kama unavyopanic brother na kutumia lugha za kejeli na matusi,japo unatumia Id fake isikutoe ustaarabu yaani enzi za utumwa wewe ndio ungekuwa wa Kwanza kwenye ule mstari.
 
Tatizo sio viongozi ni waafrica wenyewe......kwasababu hao viongozi hawatoki nje ya africa ni wenzetu......na hata wewe ukawa leo kiongozi sitoshangaa ukafanya kama hao wengine.....

Shida kubwa ni mindset ya waafrica!
Huu ndiyo ukweli sasa. Kimsingi naomba nitoe shuhuda mimi nipo katika moja ya mashirika makubwa ya usafirishaji ya serekali.

Kwendana na technology ya vyombo vya usafiri vilivyopo vinahitaji mara kwa mara kufuatilia na kuvichunguza mno maana inafikia hatua ikitokea hitilafu huleta changamoto kutokana na kuwa ni very advanced technology .

Sasa wapo watendaji kazi baadhi huwa wanajitahidi sana kujisomea kufanya research n.k ila walio wengi miongoni mwao naweza sema 90% huwa wanasema "tazama fulani yani shuleni alisoma kwa bidii mpaka huku kazini anasoma anahangaika utazani anataka kuwa wa kwanza mpaka kazini?".

Furaha yao ni pale inapokuja ngozi nyeupe toka huko ndo wanakwambia wanaume wamekuja sasa mbaya zaidi hawawi invoved katika kazi itakayofanywa na hao wanaume waliowaita wao. Sasa hapo tatizo ni UONGOZI??
 
Kwa maelezo yako kwanza yanaonyesha sisi sio waisrael sababu waisrael walikuwa hawashirikian na watu wengine, najisi kwao, na wao kujiona bora, asa sisi kumbe tuliuzana wenyew kwa wenyew kwa waarabu, pia inaonyesha tatizo lipo kwa muafrika mwenyew wala sio kwa wazungu, pia nchi nying zimefanywa utumwa ila Afrika maendeleo bado hadi sasa tunabaki tunalaumu tu, km vile tulifanyw peke yetu watumwa, chengine embu angalia wafrika waarabu(kaskazini) walivyotuacha kimaendeleo, ndo tujue ngozi nyeusi ni tatizo na tatizo linazidi sababu hatukubali udhaifu wetu ili tutoke hapa tulipo ila tunaujengea sababu zisizo na mashiko.
 
Sijui hata kama umenielewa little kid? Sipo kwenye mada mliyoianzisha. Nime-chip in kukueleza in few paragraph kuhusu ukweli juu ya utumwa ambao vijana wa kileo wengi wenu hamuujui. Siwezi kujadili mada yenu. It is too cheap for me. Nimesoma na kupita zangu. Nilichokujibu hakina uhusiano na mada yenu ambayo kimsingi imejikita kwenye 'intelligence' kati ya waafrika na the rest of races.
 
Kama ilikuwa too cheap kwako usingejibu Tena kwa papara ulizotumia,na Bado umerudi kujibu Tena kuonyesha madam imekuvutia,acha kujitia we ndio msomii na kudhani wanadiscuss hapa hawana shule....halafu una kale kakasumba kakuona ukichanganya na lugha ya kigeni ndio tutakuona msomi.Pole kijana wa zamani
 
Sikusoma username yako. Kumbe ni mdada. Samahani binti mzuri. Ngoja nikuweke sawa kwa jambo moja.

Nimekunukuu kwa sababu umeandika kauli yenye kudhihaki watumwa; kimsingi mababu na mabibi zetu. Hujui madhila makubwa waliyopitia na kuteseka. Tujadili upumbavu wetu kama waafrika bila kuwadhihaki watumwa ndugu zetu.

Una hoja kimsingi juu ya namna waafrika tulivyo wapuuzi mpaka sasa. Nami naudhika na kuchukizwa na ujingaunjinga unaoendelea kwenye jamiii zetu waafrika weusi. Usingetia neno juu ya kuwadhihaki watumwa (mababu zetu) wala nisingejisumbua kukunukuu. Nadhani sasa umeelewa vema!
 
Wanataka kuwekwa Mambo sawa kwa maana wametukanwa kwa century nyingi Sana wakiambiwa Kila kitu Chao ni Cha kishenzi na hao mazeluzelu πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚!
Hiyo iliwafanya wasijiamini! Wazungu walitumia Vita hiyo ya kisaikologia na wakashindwa kwa hiyo ili kurudisha status ya mwafrica lazima kurudi kwa mzingi wa yote!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…