Hapa ni Gbadolite, Kijijini kwa dikiteta Mobutu Sesseko Kuku Wazabanga, nyumba zimegeuka Magofu na mahame

Hapa ni Gbadolite, Kijijini kwa dikiteta Mobutu Sesseko Kuku Wazabanga, nyumba zimegeuka Magofu na mahame

Sehemu kama Chato ziko ngapi nchini, ngapi zimeizidi Chato kwa vivutio na kuweza kuwa na uchumi mkubwa zaidi, na kwa nini Chato ipewe kipaumbele (kiasi cha kujengewa uwanja wa ndege unaowezesha ndege kubwa kutua) zaidi ya pengine panapoweza kuwa na ukuaji mkubwa zaidi wa kiuchumi?

Tuangalie kanuni za uchumi za utilitarianism.

Unachosema ni kweli, kua Chato inazdiwa na sehemu kadhaa kwa vivutio na fursa mbalimbali.

Je, tatzo ni Chato kupendelewa na sio sehemu zingne? Na kwa nn sehemu duni kama Chato kujengwa miundombinu mikubwa kama miji mingine?

Lkn kwenye hoja za msingi za maendeleo ya kiuchumi lazma maeneo duni kuimarishwa ili kuleta unafuu wa maisha na kuondoa uchumi kutoka kutegmea sekta moja"economic diversification"

Sasa basi kama tutaendelea kujenga tu Dar, Mwanza, Mbeya n.k ni lini basi maeneo maskini kama Chato, Songea, Rukwa n.k nayo yataboreshwa?

Je ww wasemaje kwa hili?
 
Unachosema ni kweli, kua Chato inazdiwa na sehemu kadhaa kwa vivutio na fursa mbalimbali.

Je, tatzo ni Chato kupendelewa na sio sehemu zingne? Na kwa nn sehemu duni kama Chato kujengwa miundombinu mikubwa kama miji mingine?

Lkn kwenye hoja za msingi za maendeleo ya kiuchumi lazma maeneo duni kuimarishwa ili kuleta unafuu wa maisha na kuondoa uchumi kutoka kutegmea sekta moja"economic diversification"

Sasa basi kama tutaendelea kujenga tu Dar, Mwanza, Mbeya n.k ni lini basi maeneo maskini kama Chato, Songea, Rukwa n.k nayo yataboreshwa?

Je ww wasemaje kwa hili?
Jana kuna mtu alizungumzia habari kama yako.

Walielezea Nyerere alivyokataa kujenga barabara ya lami kwenda Butiama, kwa kuuliza "Butiama kuna zao gani?".

Uchumi ni somo la kujua kupanga mambo ili kutumia rasilimali vizuri kabisa.

Kila sehemu ya Tanzania inastahili kuendelezwa.

Lakini, kuna sehemu nyingine zinastahili kupewa kipaumbele kwanza, kwa sababu, ukiziendeleza hizo, zinaleta kitu kinaitwa "multiplier effect".

Kwa mfano, ukiwa na sehemu ina machimbo ya dhahabu, na sehemu nyingine ina mihogo tu, under ceteris paribus, ina make sense kuanza kujenga barabara ya lami kwenda kwenye machimbo ya dhahabu.

Ukipeleka lami kwanza kwenye machimbo ya dhahabu, hiyo lami inaweza kuzalisha na kukuwezesha kuweka lami sehemu kumi zinazolima mihogo.

Ukijenga kwanza kwenye mihogo, ukaacha kwenye dhahabu, hiyo hela haitarudishwa, mihogo haina multiplier effect.

Wananchi wote wanastahili kupelekewa maendeleo. Tatizo, kwa nchi yenye bajeti finyu na macho mengi yanayoiangalia bajeti hiyo finyu, utaanza kujenga wapi ili ujenzi wako uwe na manufaa mengi zaidi kwa watu wengi zaidi? This is the utilitarianism I was talking about. The greater good for the greater number of people.

Ndiyo maana Nyerere alipoambiwa apeleke lami Butiama, aliyliza, Butiama kuna zao gani?

Ukikubali kwamba Chato haipo nafasi ya kwanza kiuchumi kujenga airport, umekubali kwamba kujenga airport hapo si uamuzi mzuri kiuchumi.
 
Charity begins at home! Uzuri ni kuwa chato ipo Tanzania! Kama malalamiko yanayoelekezwa kwa Mkuu yanalenga kutuaminisha kuwa Chato hapana hadhi katika Tanzania, ama basi yaliyofanywa huko yalipaswa kufanyika kaskazini tu itakuwa ni kumuonea mkuu.
Usitetee ujinga Angeliona aibu kidogo akafanya hayo Geita makao makuu ya mkoa
Kiserikali
 
Usimfananishe Mtukufu Rais na mambo yako yakipumbavu..

Hii ni Tanzania sio kongo wewe kilaza, kama unapapenda kongo hamia huko
Mtukufu ni Mungu Mwenyezi pekee magufuli ni wakala wa shetani na nyie ndo misukule yake iliyokatwa ulimi
 
Wa Afrika mnalana akili Zero kwanini wasingeigeuza kuwa hotel na uyo uwanja ukatumiwa kwa Mambo mengine kama Mali ya selikari
 
Ukaangalia comments nyingi kwa umakini utagundua wachangiaji ni watu kutoka kasikazini,,,,, imagine rais angetoka kaskazini nini kingetokea???? Na hatuna mpango wa kuwakabidhi nchi nyie watu mpaka baadaye sana kwasababu tunawajua vizuri, nani asiyewajua??
Ukabila ndio umasikini wako.
 
Charity begins at home! Uzuri ni kuwa chato ipo Tanzania! Kama malalamiko yanayoelekezwa kwa Mkuu yanalenga kutuaminisha kuwa Chato hapana hadhi katika Tanzania, ama basi yaliyofanywa huko yalipaswa kufanyika kaskazini tu itakuwa ni kumuonea mkuu.

Hata huo uwanja wa ndege kijijini kwa Mobutu ilikuwa ni Zaire pia.
 
Fizibiliti study bongo hii!! Rejea lile bwawa la DART jangwani, kulihitajika PhD kujua pale hapafai! Nachokuhakikishia hapa bongo wanaopinga progress za JPM nao wakipata nafasi watakuwa na madudu Yale yale tu! Sisi ni wabinafsi kwa hulka tu, lakini pia yeye sio mtakatifu hadi tuseme hautendei wema utakatifu huo. Hujawasikia wabunge pamoja na vipato vilivyonona bado walishindwa kutoa pesa binafsi kwenda kushangilia Taifa Stars, wakaomba pesa za umma!! Mpumzisheni Mkuu asee.

Kwani hicho kitendo cha wabunge kutumia pesa za umma kwenda kushangilia timu ya taifa kimesifiwa, mpaka uone hicho kitendo cha ubinafsi wa rais ndio kinapigiwa kelele tu?
 
Dah aisee. Ni roho ngumu sana tena kuvaa uso wa mbuzi kupora mali za watu na kujenga mahekalu porini.

Mbinguni Waafrica hawaendi. Wallah kabisa.

Naanza kuamini ile inayosemwa kua sisi ni kizazi cha laana.

Africa kua kama ulaya ni ndoto za mchana.

Lkn wakongoman walishindwa nn kuendeleza hayo makazi ?

Ufafanuzi mwenye kufahamu plz.

Hua naamini waafrika tukibebwa kama tulivyo tukapelekwa US na US wakabebwa kama walivyo wakaletwa africa haitapita mwezi tutakuja kuomba msaada Africa tena msaada wa tech mpya kutoka Africa manake hizo za tutakazokuta kule tutaua ndani ya mwezi
 
Heshima kwako mkuu.

Umechambua vizuri sana. Na hivi ndivyo twapaswa kuelezea mambo kuonesha pros and cons za miradi, na sio kishabiki kam wengi tunavyokua tunafanya. Kwamba kisa mm nimezaliwa Mbeya nikijenga Mbeya nimepapendelea.


Walielezea Nyerere alivyokataa kujenga barabara ya lami kwenda Butiama, kwa kuuliza "Butiama kuna zao gani?".

Nyerere katika kipindi chake na mazingira ya nchi yetu ilikua tofauti sana.
1. Miundombinu ilikua mibovu na duni sana i.e barabara za mikoa na miko, wilaya na wilaya n.k, umeme, maji, hospital.

2. Elimu kwa watz; majority walikua hawana elimu. Ndo maana Nyerere alijikita sana kueneza elimu kufuta ujinga.
3. Uwezekaji ulikua mdogo sana na wengi walikua kwenye "Subsistence economy"

Kwa hiyo ni vigumu sana kufananisha mazingira ya nyerere na hali ya sasa.
Lakini, kuna sehemu nyingine zinastahili kupewa kipaumbele kwanza, kwa sababu, ukiziendeleza hizo, zinaleta kitu kinaitwa "multiplier effect".

Miji kama Mwanza, Geita na nchi ya Rwanda ni fursa kubwa kwa maeneo mingine ya jiran kibiashara. Hiyo miji ina watu wengi na ili kuendeleza biashara ndani ya hii miji inahitajika iwepo miji mingine maeneo jirani ya kibiashara ili uchumi wa ukanda husika uweze kua na "Multiplier effect....la sivyo biashara itajikuta ni Mwanza na Dsm,Mbeya, n.k
Ingawa mhe.alitakiwa pia aiangalie miji kama Musoma, Ngara, Biharamulo, Sirari, Shinyanga, Nyamongo, n.k ili kuhamasisha biashara na mji wake wa chato.

Mfano mji wa nyamongo, Geita, n.k una madini mengi sana angeboresha miundombinu na viwanja vya ndege ili kuleta ushindani ktk huo ukanda.



Tatizo, kwa nchi yenye bajeti finyu na macho mengi yanayoiangalia bajeti hiyo finyu, utaanza kujenga wapi ili ujenzi wako uwe na manufaa mengi zaidi kwa watu wengi zaidi? This is the utilitarianism I was talking about. The greater good for the greater number of people.

Kuna mdau humu ndani aliwahi kuleta mada kuhusu maendeleo kikanda akishauri ukanda flani ujitegemee wenyewe kimaendeleo kulingana na maliasili za ukanda husika. Yaani ukusanyaji kodi, allocation of resources etc visimamiwe na mamlaka (halimashauri) za ukanda huo.
Mfano Mwnza, Mara, Kagera, Geita (Ukanda wa ziwa) viwe na mamlaka ya ukusanyaji wa kodimgawanyo wake. Vivyo Hivyo kwa kanda zingne, pia kuwe na fungu la kwenda serikali kuu. serikali kuu ikiwa ni mshauri na pengme kuingila pale panapostahili.

Lkn hili kwa sasa naona linafanyika indirectly kwan kama maeneo duni katka ukanda flan yanajengwa na kuimarisha ni hatua nzuri ya kuelekea point ya maendeleoya ushindani kikanda.

Wito tu sheria na taratibu zifuatwe ktk allocation of Scarce resources we have, na haki itendeke.
 
Mleta mada naona unaendana na ule msemo wa dua la kuku halimpati mwewe.

Huwezi kumlinganisha Mobutu na JPM, ni watu wawili tofauti kabisa katika suala la maono yao.

Andika vitu kwa facts sio unaongea kama upo kijiweni. Huyu mtoa mada ameweka mpaka vielelezo vya picha. Na wewe tupe facts zako
 
Neutral observers kwa kiswahili fasaha tunawaita ni 'wanafiki daraja la kwanza'.
Sisi wengine huwa tunapenda kuwa 'neutral observers' muda mwingi. Nakuomba tu, kwa uzi huu 'specifically', jaribu kulinganisha Gbadolite na Chato ukizingatia 'ACCESSIBILITY', 'POTENTIAL' ya utalii na uchumi kwa ujumla wake, POPULATION ...... etc etc!
 
Back
Top Bottom