Happy Father's Day kwa akina baba wote JF na Dunia kwa ujumla. Una ujumbe gani kwa Baba yako leo?

Happy Father's Day kwa akina baba wote JF na Dunia kwa ujumla. Una ujumbe gani kwa Baba yako leo?

Ahsante sana mkuu kwa niaba ya wababa watarajiwa
 
Nampenda baba yangu japo ni mkali🥰
Bila malezi yake Bora akishirikiana na mama yangu kipenzi, sidhani kama ningekuwa na mafanikio au Hali niliyonayo Sasa.
Licha ya uchumi WA baba yangu kuwa mzuri, lakini hakunijengea tabia ya kuuwaza na kuutegemea kwa maisha yangu ya baadae

Alinijengea tabia ya ku hustle kivyangu Mimi pamoja na ndungu zangu tunajivunia kuwa na baba Bora

Kuelekea ndoa yangu baba kaniahidi mambo mazuri

Nakupenda baba nyamwi♥️♥️♥️♥️
 
Wakuu salama?


Leo 16/6/2024 ni Siku ya akina Baba Duniani/Father's Day (ambayo husheherekewa kila Jumapili ya tatu ya Mwezi Juni). Kwa maoni siku hii hatuwasherekei tu wanaume wenye watoto/wanaoitwa baba na wenye upendo kwa watoto wao bali pia tunawasherekea:

- Wale wote wanaotamani kuwa baba kwa muda mrefu lakini bado hawajafanikiwa (Mungu atawasaidia msikate tamaa),

- Baba zetu waliotangulia mbele za haki (Mungu awalaze pema)

- Kina baba wa kesho (Mjipange kwa malezi, msije kutekeleza watoto wenu)

- Single father's ambao wanahakikisha watoto wao hawakosi kitu katika maisha yao na wanapata upendo wote

- Baba ambao uhusiano na watoto wao una changamoto za hapa na pale (endelea kupambana mambo yatakaa sawa)

- Wanaume waliosimama/wanaosimama kama baba kwenye maisha yetu (Mungu awabariki mmekuwa nguzo kubwa kwetu)

- Wanaume ambao wamepoteza watoto wao (Mungu awatie nguvu na faraja).

Katika siku ya leo, una ujumbe gani kwa baba yako?
Asante sana Cute Wife 🤝
 
Tatizo sisi Waafrika bado tunaishi kwa kutegemea fikra za mzungu kila anachokitunga na kukileta sisi ni wapokeaji na watekelezaji. Valentine Day, Women Day, Mothers Day, Fathers Day, AIDS Day. Tuishi kwa utashi wetu tumpende kila mtu na kuambiana mara kwa mara kwamba tunapendana na kuthaminiana.

Hizi siku zilitengenezwa na wazungu kwa malengo yao ya kibiashara...siku hizi ndipo wafanyabiashara wanauza sana maua, vyakula,na zawadi nyingine mbali mbali
Kama keyboad uliyoitumia kuandika hapa ni ya mzungu, unachoongea hakina maana
 
Namkumbuka kwa kunipa kipondo kizito kila nilipogoma kwenda shule na leo naona faida niliyopata kwa kipigo kile simchukii kabisa nafikiri asingenipa kipondo ingekuwaje leo?
 
Niliposema baba yangu amevuka viwango vya baba bora, nilimaanisha na anastahili wala sikukosea.

Baba yangu sio mbaguzi wa watoto, kwamba ajivunie wa kiume tyuu na wa kike asijivunie hilo kwake halipo, alinilea kwa mapenzi, maadili na makuzi yenye kumpendeza yeye na umma kwa ujumla tena kwa msingi thabiti wa imani na dini ya kikristo na kupitia baadhi ya hatua na sakramenti.

Yess anajua wazi uhalisia wa mwanae, huenda ananaumia km unavyosema but hakuna kilichobadilika kwake juu yangu, kuhusu mabadiliko ya kutoka nilivyo na kuwa utakavyo, hayo ni maamuzi na matakwa yangu, na yatafanywa kwa ridhaa yangu pale nitakapohitaji.

Umesema ni kheri ningekua jambazi, mlevi, mwizi, au mvuta bangi kwani ningekua mrithi na shujaa wake bado, sijui unalenga nn hasa, ila hayo yote ni ubatili sio ktk tamaduni wala maadili.

Baba yangu ana amini ktk uhuru binfasi hasa kwa mtu mzima aliye na umri wa kufanya maamuzi juu yake, hivyo hana shida kabisaa.

Aishi sana baba yanguu. [emoji482][emoji482]
Duh! Na wewe umeshakuwa baba?
 
Wakuu salama?


Leo 16/6/2024 ni Siku ya akina Baba Duniani/Father's Day (ambayo husheherekewa kila Jumapili ya tatu ya Mwezi Juni). Kwa maoni siku hii hatuwasherekei tu wanaume wenye watoto/wanaoitwa baba na wenye upendo kwa watoto wao bali pia tunawasherekea:

- Wale wote wanaotamani kuwa baba kwa muda mrefu lakini bado hawajafanikiwa (Mungu atawasaidia msikate tamaa),

- Baba zetu waliotangulia mbele za haki (Mungu awalaze pema)

- Kina baba wa kesho (Mjipange kwa malezi, msije kutekeleza watoto wenu)

- Single father's ambao wanahakikisha watoto wao hawakosi kitu katika maisha yao na wanapata upendo wote

- Baba ambao uhusiano na watoto wao una changamoto za hapa na pale (endelea kupambana mambo yatakaa sawa)

- Wanaume waliosimama/wanaosimama kama baba kwenye maisha yetu (Mungu awabariki mmekuwa nguzo kubwa kwetu)

- Wanaume ambao wamepoteza watoto wao (Mungu awatie nguvu na faraja).

Katika siku ya leo, una ujumbe gani kwa baba yako?
Kina baba ni mihimili muhimu sana ya familia.
Nguzo ya familia ni baba.
Mlinzi wa familia ni baba.
Shifu/master wa familia kujifunza na kuwa imara ni baba.
Namshukuru baba yangu kwa mambo matatu;
1)Amenipambania mpaka sasa na hachoki kunipambania licha kuwa nimekua ila anatamani anilee mpaka nikifa.
2)Alinivumilia licha ya makosa mengi na akanipa nafasi tena na tena mpaka nikawa imara.
3)Amenifunza mengi kimaisha japo kwa njia ngumu nyingine za kutokwa na machozi,ila alikua akinijenga na kweli nimejengeka.
ALLAH AMPE STAHIKI BORA BABANGU KWA JINSI ALIVYOTUKUZA VYEMA.
 
Yaani Baada ya siku ya akinamama duniani kushika hatamu, watu wameona waje na siku ya wanaume! Sisi wanaume hatuhitaji haya mambo!! Ili iweje kwa mfano?? Tuacheni tuishi maisha yetu ya kawaida siku zote ni sawa na tuwajibika kila kukicha!!
Umemaliza kaka.
Tuishi humo.
 
Tatizo sisi Waafrika bado tunaishi kwa kutegemea fikra za mzungu kila anachokitunga na kukileta sisi ni wapokeaji na watekelezaji. Valentine Day, Women Day, Mothers Day, Fathers Day, AIDS Day. Tuishi kwa utashi wetu tumpende kila mtu na kuambiana mara kwa mara kwamba tunapendana na kuthaminiana.

Hizi siku zilitengenezwa na wazungu kwa malengo yao ya kibiashara...siku hizi ndipo wafanyabiashara wanauza sana maua, vyakula,na zawadi nyingine mbali mbali
Mhhh!

Hivi waafrika ni lini tutaacha kuwalaumu wazungu hata kwa vitu visivyoeleweka? Hasa uvivu wa akili zetu. Watu wenyewe kila siku na mabakuli yetu tunawafuata kwao kuwasumbua, tukiwategemea hadi kwa kondomu, na neti!

Wao wakianzisha hizo siku kwa malengo ya kibiashara mbona ni mawazo mazuri ya kukuza uchumi. Na si kwamba maadhimisho na biashara hizo hufanyika Afrika pekee, hata kwao pia. Zaidi, hizo biashara za kuuziana vyakula na maua na zawadi nyinginezo sisi hatuzuiwi kufanya, maana hawasafiri na bidhaa zao kuja kuuza wenyewe. Kwa kiasi kikubwa tunauziana wenyewe huku hivyo hawatupangii vya kuuziana, hata tukiamua tuuziane gongo na wanzuki hawatuzuii. Badala tushukuru wametupa fursa za biashara akili zetu zilikuwa zimeganda zinawaza uzinzi, uchawi na siasa chafu, tunawalaani tena! Kweli shukrani ya punda ni mateke.
 
Namuomba Mwenyezi Mungu amfanyie wepesi Baba yangu aliyetangulia mbele za haki, amuondolee adhabu kaburi, amsamehe madhambi yake na amjalie Pepo InshaAllah.
 
Nimesoma vizuri sana. Ila katika kusoma ndio nikabaini wewe ni mwanaume.

Ndio maana nikakuuliza mwanaume mwenzetu, umeshakuwa baba? Au bado bachela kama Nay wa mitego?
Bachelor km Bob risky [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
”Happy fathers day” ndiyo kitu gani hicho?

Hivi vi-wishes vya ajabu ajabu ndiyo vinasababisha wanaume wa Kiafrika kujisahau na kuanza kulia lia kutunzwa na wake zao,hayo ni mambo ya wazungu hayatuhusu waafrika.
 
Back
Top Bottom