GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda amesema Serikali itagharamia shughuli zote za harusi, ikiwemo kulipia ukumbi mkoani hapo lengo likiwa ni kuvutia zaidi wageni na watalii kufika Arusha na kuwa chachu ya kukuza uchumi.
Makonda amesema masharti ya ndoa hizo ni pamoja na kati ya wawili hao, mmoja wao atoke nje ya mkoa huo, ikiwezekana atoke nje ya nchi akiwa na maana kwamba wale ambao wote ni wakazi wa mkoani hapo fursa hiyo haitawahusu.
"Lengo letu sisi hatutaki kuwa na 'high season' au 'low season', tunataka kutengeneza shughuli na matukio mbalimbali kuhakikisha muda wote uchumi unakuwa na kuendelea, ili mama wa mboga, bodaboda na kila mtu anufaike na ugeni unaofika hapa Arusha," amesema.
Makonda amesema hayo leo Jumatatu Julai 8, 2024 jijini Arusha alipokutana na wadau na mashirika na asasi zisizo za kiserikali.
Chanzo: mwananchi_official
Najua Mademu wengi hapa JamiiForums mnatamani Kuolewa nami haya jitokezeni nimchague twende zetu Arusha.
Makonda amesema masharti ya ndoa hizo ni pamoja na kati ya wawili hao, mmoja wao atoke nje ya mkoa huo, ikiwezekana atoke nje ya nchi akiwa na maana kwamba wale ambao wote ni wakazi wa mkoani hapo fursa hiyo haitawahusu.
"Lengo letu sisi hatutaki kuwa na 'high season' au 'low season', tunataka kutengeneza shughuli na matukio mbalimbali kuhakikisha muda wote uchumi unakuwa na kuendelea, ili mama wa mboga, bodaboda na kila mtu anufaike na ugeni unaofika hapa Arusha," amesema.
Makonda amesema hayo leo Jumatatu Julai 8, 2024 jijini Arusha alipokutana na wadau na mashirika na asasi zisizo za kiserikali.
Chanzo: mwananchi_official
Najua Mademu wengi hapa JamiiForums mnatamani Kuolewa nami haya jitokezeni nimchague twende zetu Arusha.