Harmonize akiwa na Boss wake mpya

Harmonize akiwa na Boss wake mpya

Ukiona watu wanaondoka jua kuna kitu si bure, unaweza kuta wanaingia a billion alafu msanii mwenyewe anaishia kuonja 30mil, less than 10% ya anachoingiza (speculation). Ila si bure wasanii wanakuja na kuondoka tu. Tatizo watu wanamuona mond ka mungu wanasahau jamaa binadamu tu na anapenda hela kama wengine. Alitengeneza wcb kupiga hela sio kutoa msaada. Kama konde boy anataka kusema ngoja asepe, ashakua hyuu si mtoto tena.
 
Hata kama ameondoka, issue sio kuondoka bali ameondoka vipi! Kama ameondoka kwa makubaliano, hapana ubaya wowote kwa sababu wanaweza kuendelea kushirikana! Na itakuwa poa zaidi kama anaamini anakoenda ni bora zaidi kwa career yake! Lakini kama ni kweli ameondoka lakini ameondoka kwa kiburi cha Kwangwaru (hapa ndipo taabu ilianzia-- inawezekana Diamond alikuwa anamuonea wkivu au inawezekana Harmonize akajiona yeye ndiye yeye) kuwa na Views +50M, hilo haliwezi kuwa jambo jema kwake kwa sababu ukweli ni kwamba, Sebastian hana historia ya ku-manage wasanii successfully ikiwa hata huko ku-manage kwenyewe amewahi! Asije akafanya kosa ambalo alifanya Ruby ambalo watu tuliongea sana hapa na kuhoji historia ya Majizo na EFM yake katika ku-manage wasanii ambako Ruby ndo alikuwa amejiegesha sana!!

Na hapa tukumbushane jambo moja, inawezekana kabisa kwamba Harmonize ni bonge la mkali (binafsi simkubali kwa sababu namuona ni Clone ya Diamond) kwa sasa, tena pengine kuliko msanii yeyote yule hata barani Afrika! Pamoja na yote hayo, tasnia ya muziki ni very stupid! It's not about unajua kuimba namna gani, manake kuwa mkali wa kuimba ingekuwa ndo hoja, leo hii Diamond asingekuwa hata among top 5 kwa mafanikio hata hapa Tanzania!!

Ukweli mchungu ni kwamba, kuna advantage kubwa sana ya kuwa chini ya WCB kwa sababu, kama ni uchawi, basi huyo Mchawi wa Diamond ana karama ya aina yake! Jamaa ana nyota kali sana, kiasi naweza kuthubutu kusema ana nyota kali kuliko msanii yoyote yule nchi hii!!! Leo hii WCB ikisaini msanii ambae hafahamiki kabisa, halafu kaa wiki moja kisha ita watu 1000 at random halafu waulize wakutajie wasanii walio chini ya WCB na wale walio chini ya label kama King Music!!

Wala usishangae, majority wakapatia kutaja wasanii wote walio WCB including yule aliye kundini ndani ya wiki, lakini wengi wakashindwa kutaja akina Cheed waliopo Kings Music, ingawaje wana miezi kadha hivi sasa!!! Na wala usishangae mtu akishindwa kumtaja hata Abdul Kiba, kiasi kwamba hata ukimwongoza "ina maana humfahamu hata Abdul Kiba"? Ukakuta nae anakuuliza "Abdul Kiba? Au unamaanisha Ali Kiba?"

Na ingawaje ni kweli kuna msaada mkubwa sana wa akina Talle na Sallam, lakini mbali na hao, tangia hapo tu Diamond ana nyota ya kwake peke yake, na ndio maana tangia atusue na Nenda Kamwambie, hajawahi kushuka wakati akina Tale wote hao alikutana nao takribani miaka 3 baadae! Which means, walichukua mtu ambae tayari alikuwa na nyota yake; and it doesn't matter iwe ya kuzaliwa nayo au inayotokana na ulozi!
 
Umenena sawa ila Uanaondoka vipi ndio swala linalozungumziwa apa...,Mbona kama anaondoka kwa Shari..Hajaaga tunaona vitendo tu this is not Gud...nakwambia Utaona Chonde Boy kanyea kambi atayazoa tu
Simshangai kwa sababu amekua kisanaa na kiakili pia siku zote mtoto akikua kiakili anahama nyumbani kwa baba yake anakwenda kutengeneza mji wake anajenga familia yake ila akidumaa atafika miaka 40 nakuolea nyumbani anabakia kusubiri baba afe arithi nyumba na mali

Binafsi nnampongeza harmonize sababu ana akili ameweza kujitambua mapema kutengeneza ngome yake ili na yeye awape vijana wengine ajira

Domo kama ni mwerevu na ana roho safi kama anavyo jionesha kwa jamii alitakiwa ampongeze tena amuongezee na mtaji kisha afanye sherehe kuthibitisha kwamba kijana wake amekua na anaweza kujitegemea nadhani hiyo ndio itakua fahari kwake zaidi
 
Mtoto ukikua unaaga kwa baba kuwa sasa nahama hapa home nimepata kazi, nimepata mchumba, kisha mzee anakupa mabaraka yake unasepa. Sasa huyu mtoto kakua tumuombee atusue lakini aondoke home kwa amani zote.
Acha udwanz Mbona hajaaga?
 
Katika maisha nyakati nyingine inahitajika u take risk ili uweze kufanikiwa,tumuache kijana ajaribu karata nyingine,saa nyingine kashaona upepo kwa upande wake kuendelea kuwepo Wasafi ni sawa na kupoteza na hatujui wamemtenda nini mpaka aondoke kwa style hii...
 
Hebu fafanua kidogo Mkuu,mkataba unambana vipi mavoko
Mavoko aliondoka ndani ya mkataba ndo maana alikuwa analia BASATA wamsaidie kwani mkataba mgumu. Kwa sasa Mavoko hawezi fanya kitu mkataba unambana.

Harmonize mkataba umeisha akaweka terms zake WCB wakakataa yeye akakaa nje. Inatakiwa iwe win win situation
 
Fikra za kimasikini. Kusaga hana utajiri huo unaofikiria wa kummiliki kila mtu. Kwa taarifa yako Mondi kwa hatua aliyofikia kiuchumi anakaa dawati moja na huyo tajiri wako.
Duuuuu hiii mitandao hii unatania au unasema kweli?
 
Huku uongozi wa WCB kupitia Said Fella ukisisitiza hautabembeleza Harmonize kutumbuiza Wasafi festival na Kama Harmonize anataka kuondoka aage kwa amani.
Harmonize amekuwa akionekana na boss wake mpya Jembe Ni Jembe wakipanga mikakati mbalimbaliView attachment 1186225View attachment 1186226
KUNA VITU VINGINE VYA KIPUMBAVU KABISA KUVIZUNGUMZA UKIWA NA AKILI TIMAMU, MTU MZIMA MWENYE VICHWA VIWILI KABISA NA MIDEVU KILA SEHEMU YA MWILI ANAKAA ANAUMIA NA KUMUWAZIA MTU FULANI KWANINI ANAONDOKA SEHEMU FULANI KWENDA SEHEMU NYINGINE, UNABAKI UNAMUANGALIA ANAYEJIULIZA HIVI JE ANAFAIDIKA AU ANAUMIA NA NINI AKIONA MTU HUYO ANAONDOKA AU KUHAMA, HUJUI KULA YAKE, HUMSAIDII MAJUKUMU YA FAMILIA YAKE, HANA EFFECT KTK MFUMO WA MAISHA YAKO ILA YEYE ANAWAZA HARAKATI ZAKE WEWE UNABAKI UNAMUWAZIA YEYE, WENGINE WENYE DUA CHAFU NA CHUKI ZISIZO NA MSINGI UTADHANI ALIIBA MKEO AU ALIWAHI KUKUKOSEA, MTU ANAKUWA JAJI HODARI WA MAISHA YA WATU ILA MAWAKILI IMARA WA WA MAPUNGUFU YAKE, ACHENI MAISHA YAENDELEE KAMA MTU ANA HUSTLE KWA AJILI YA UGALI WAKE KIMPANGO WAKE NA WEWE ANGALIA UGALI WAKO KIMPANGO WAKO, UTAKUJA STUKA UNASINDIKIZA WENZIO KWENYE MAFANIKIO KWA MACHO TU KISA TU UNATUMIA AKILI KUBWA NA NDOGO KUMJADILI WAKATI YEYE HANA TIME NA WEWE, HAKUJUI WALA HAKUFAHAMU WALA HAJAWAHI KUKUPA CHOCHOTE KTK MAISHA YAKO CHENYE KUONGEZA KIPATO AU KUKWAMISHA KIPATO KWAKO.
 
Kwa mawazo ya wengi humu nimegundua risk taking is not our thing,Diamond asingekua na mawazo kama ya Harmonize angebaki kwa Ruge
Lini diamond amekuwa anamanagiwa na ruge tuanzie hapo kwanza?au inafuata story za mange kimambi.
 
Simshangai kwa sababu amekua kisanaa na kiakili pia siku zote mtoto akikua kiakili anahama nyumbani kwa baba yake anakwenda kutengeneza mji wake anajenga familia yake ila akidumaa atafika miaka 40 nakuolea nyumbani anabakia kusubiri baba afe arithi nyumba na mali

Binafsi nnampongeza harmonize sababu ana akili ameweza kujitambua mapema kutengeneza ngome yake ili na yeye awape vijana wengine ajira

Domo kama ni mwerevu na ana roho safi kama anavyo jionesha kwa jamii alitakiwa ampongeze tena amuongezee na mtaji kisha afanye sherehe kuthibitisha kwamba kijana wake amekua na anaweza kujitegemea nadhani hiyo ndio itakua fahari kwake zaidi
Muziki hauendi hivyo!! Hakuna ubaya wowote kwa Harmonize kuhama WCB lakini kukua kisanii kisiwe ndio kigezo kwa sababu muziki kama sanaa, na muziki kama tasnia ni vitu viwili tofauti! Unaweza kukua kisanaa lakini haimaanishi umekua na kuifahamu tasnia ya muziki! Hapa pa kuifahamu tasnia ya muziki ndio changamoto kubwa sio Tanzania tu, bali duniani kote! Leo watu wakiwaambia wataje wanamuziki wakali wa kike duniani si ajabu ukatajiwa Rihanna, Beyonce, Nick Minaj, Cardi B, and the like! But trust me, hata ndani ya US yenyewe (let alone duniani kote) kuna mademu wakali kuliko hao akina Rihanna! But WHY Rihanna?! NI kwa sababu wapo kwenye mikono inayofahamu tasnia ya muziki!

Ni kutokana na hilo, ndio maana watu kama akina Rihanna hata baada ya kukua maradufu, bado wapo Def Jam iliyowatoa!! Def Jam na Roc Nation sio tu wanajua muziki bali wanaijua tasnia ya muziki!!

<Let's go back almost 15 years ago wakati Destiny's Child inatamba!! Destiny Child ilikuwa chini ya Matthew Knowles ambae anaijua vema tasnia ya muziki! Baada ya Destiny's Child kusambaratika, ni Beyonce pekee ndie anaendelea ku-shine kwa sababu ni yeye ndie aliendelea kuwa chini ya Matthew Knowles ambae ni baba yake! Michelle sijui kafia wapi! Kelly angalau kajikongoja kongoja, na hivi sasa sijui yupi wapi!!

So, Harmonize atakuwa amefanya jambo la maana sio kwa kigezo cha kukua kisanaa bali ikiwa amepata management na watu wanaoifahamu vizuri tasnia ya muziki! Ni management na hawa watu ndio watakaokuwa wanatafuta opportunities mbalimbali na sio yeye!! Usipokuwa na hawa watu, na ukali wako wote utakuwa unaishia kupiga show maharusini kama akina Kassim Mganga na kuwaambia watu umeamua ku-specialize shows za maharusini!!
 
Back
Top Bottom