Harmonize bado yuko chini ya Diamond, ni Mbinu za Kibiashara tu

Mkuu,WCB wamemuua Mavoko kisanii?? Kivipi nieleweshe vizuri,Ninachokijua mimi WCB ndio walimrudisha Mavoko kwenye tasnia baada ya kupotea.
Huyo dada ana chuki mpaka anashindwa kutengeneza point zake vizuri
 
Hakuna kitu kigumu kama kitu kipotee ndani ya nyumba alafu uko peke ako, dirisha halijavunjwa wala mlango, Hapo ubongo unawazaaaa ukikosa jibu baada ya Glucose kushuka chini sana, unaanza kutengeneza majibu yake huku ukiyafanya kama ndio majibu rasmi ili suala hilo la kuibiwa lisiendelee kuumiza kichwa. Tunashkuru Mtoa mada kwa mtizamo wako. #Jihadhari na Corona
 
Nakumbuka kulikuwa na thread tulijadili hii kitu, kwenye kuingia na kutoka.
Kuingia alipatia cos alikuwa teyali amepotea kimziki baada ya kuwa chini ya kingkaka baada ya kusigniwa na WCB ndo akafufuka na anatengeneza hit kibao zilizofanya vizuri Kama ibaki story, kokoro, show me n.k na akapata show nyingi Sana kosa alilolifanya ni kuondoka Wasafi bila kujipanga kuishi maisha bila Wasafi.Sasa hiv Hali yake imekuwa mbaya zaidi na inaonekana akili zimemruka baada ya kupost kwenye insta yake akikojoa kichakani
 

Sawa
 
Mavoko aliingia wcb akiwa anawaka mkampaka mafuta ya mgongo mkidhani mnamng'arisha zaidi kumbe mnamuongezea chunusi. Ni sawa na kumdaka aslay au nandy saiv mje mtambe mmemng'arisha. Mavoko aliweza kusimama peke yake.

Kama wcb inang'arisha wasanii yuko wapi lavalava?mboso tu anahangaika sana
Mkuu,WCB wamemuua Mavoko kisanii?? Kivipi nieleweshe vizuri,Ninachokijua mimi WCB ndio walimrudisha Mavoko kwenye tasnia baada ya kupotea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…